Waziri Mkuu akisalimiana na Dk Mary Mgonja viwanja vya Mwakangale . Kwa miaka 10 imetumia dola za Marekani milioni 51 kuendeleza...
Waziri Mkuu akisalimiana na Dk Mary Mgonja viwanja vya Mwakangale |
.
Kwa miaka 10 imetumia dola za Marekani milioni 51 kuendeleza kilimo
TAASISI ya Mapinduzi ya Kijani Barani Afrika (AGRA)
imetoa wito kuwapo kwa matumizi zaidi ya teknolojia kwa wakulima wadogo
ili kuwa na uhakika na usalama wa chakula huku wakiingiza ziada katika soko.
Mtendaji
wa taasisi hiyo nchini Tanzania Dk Mary Mgonja alisema hayo akizungumza na
waandishi wa habari katika maonesho ya wakulima ya nanenane katika viwanja vya
John Mwakangale mjini hapa hivi karibuni.
Katika
mkutano huo taasisi zinazoshirikiana na AGRA katika kuleta mabadiliko kwa
wakulima zipatazo 10 zilikuwapo.
Dk
Mgonja alisema ana matumaini makubwa na hali ya baadae ya kilimo nchini
Tanzania na kuongeza kwamba matumizi zaidi ya teknolojia ndio njia pekee ya
kuwainua mamilioni ya wakulima wadogo kutoka katika lindi la umaskini.
“Tanzania
kuanzia mwaka 2006 imekuwa ikipewa kipaumbele na AGRA na kwamba miradi 96
imepewa ruzuku inayofikia dola za Marekani milioni 51,” alisema.
Kwa mujibu wa Dk Mgonja ruzuku hizo zimetoa mchango mkubwa katika kukabiliana na changamoto za wakulima wadogo katika mnyoror wa thamani wa shughuli zao kuanzia masuala ya mbegu, udongo, soko, sera hadi fedha.
Kwa mujibu wa Dk Mgonja ruzuku hizo zimetoa mchango mkubwa katika kukabiliana na changamoto za wakulima wadogo katika mnyoror wa thamani wa shughuli zao kuanzia masuala ya mbegu, udongo, soko, sera hadi fedha.
Sehemu
ya uwekezaji huo imezaa matunda kwa kupata aina tofauti za mbegu zilizoboreshwa
kukabiliana na hali za maeneo; matumizi sahihi ya mbolea; utunzaji baada ya
mavuno; teknolojia ya hifadhi za nafaka na ubunifu wa upatikanaji wa fedha kwa
ajili ya kuinua kilimo.
“Ninatoa
wito kwa wakulima kukumbatia njia mpya za teknolojia katika kilimo ili kupata
tija zaidi ;kuanzia matumizi ya mbegu bora zilizoboreshwa mashambani hadi
kwenye matumizi ya teknolojia mpya ya kuhifadhi mavuno; Njia hizo kama
zitatumika vyema zitaongeza uzalishaji na kupunguza upotevu wa mavuno. Mambo
hayo ni muhimu ili wakulima wadogo wajinasue kiuchumi,” alisema Dk Mgonja.
Tangu
kuingizwa kwa teknolojia ya mifuko maalumu ya kuhifadhi nafaka na bidhaa jamii
ya mikunde, kampuni tatu zinashughulika na kutengeneza hifadhi hizo, huku
zikiuzwa na kuwafikia mamia kwa maelfu ya wakulima.
Aidha
Dk Mgonja aliipongeza serikali ya Tanzania kwa kupiga hatua kwenye
kuboresha sera ya kilimo yenye lengo la kukabiliana na changamoto za
wadau mbalimbali katika sekta ya kilimo.
“AGRA itaendelea kushirikiana na wizara ya kilimo, mifugo na uvuvi kuhakikisha kwamba shughuli za AGRA nchini zinakwenda sambamba na juhudi za serikali ya Tanzania katika kuboresha kilimo,” alisema Dk Mgonja.
“AGRA itaendelea kushirikiana na wizara ya kilimo, mifugo na uvuvi kuhakikisha kwamba shughuli za AGRA nchini zinakwenda sambamba na juhudi za serikali ya Tanzania katika kuboresha kilimo,” alisema Dk Mgonja.
Aidha
aliongeza kwamba mchango mkubwa wa AGRA umekuwepo katika Matokeo Makubwa sasa
na Kilimo Kwanza.
Alisema
taasisi ambazo zilisaidiana na AGRA kuleta mapinduzi ya kilimo katika kipindi
cha muongo mmoja uliopita ni pamoja na Tanzania Seeds Trade Association
(TASTA), CSDI, Equity Bank, Unyiha Associates, BRITEN, RUDI, AGROZ.
Nyingine ambazo zilikuwa ni taasisi za umma ni pamoja na ARI Uyole,
Chollima AGRO, ARI Mlingano na kituo cha SAGCOT .
Dondoo za Shuhuda
Kwa muda AGRA imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kwamba kunakuwa na mazingira mazuri ya biashara ya mbegu kupitia mradi wa Micro Reforms for African Agribusiness (MIRA) : Mradi huu ulizaa matunda mema kwani kuanzia Juni 2016, kumekuwepo na sera mpya ya mbegu.
Dondoo za Shuhuda
Kwa muda AGRA imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kwamba kunakuwa na mazingira mazuri ya biashara ya mbegu kupitia mradi wa Micro Reforms for African Agribusiness (MIRA) : Mradi huu ulizaa matunda mema kwani kuanzia Juni 2016, kumekuwepo na sera mpya ya mbegu.
Mkurugenzi
Mtendaji Tanzania Seeds Trade Association (TASTA), Bw. Baldwin Shuma.
Alieleza kufurahishwa na Sera hiyo ilitengenezwa kwa namna pekee ambapo
inaruhusu sasa makampuni ya mbegu kuzalisha mbegu ambazo zilifanyiwa utafiti na
taasisi za umma.
Naye
Dk Matilda Kalumuna, wa Taasisi ya utafiti wa kilimo ya Mlingano –Tanga,
amesema kwamba AGRA imesaidia taasisi yake kwa kuipa ruzuku ya dola za Marekani
400,000 kusaidia kuimarisha mifumo yake ya kuangalia ubora wa mbolea.
“Kupitia mradi huu taasisi ilifundisha wakaguzi wa mbolea 100; wachambuzi 15 wauzaji pembejeo wenye uelewa 338 na wadau 8000.
“Kupitia mradi huu taasisi ilifundisha wakaguzi wa mbolea 100; wachambuzi 15 wauzaji pembejeo wenye uelewa 338 na wadau 8000.
Kutokana
na mradi huo makampuni mbalimbali na wauzaji wa pembejeo za kilimo waliamua kwa
hiari yao kujisajiri na TFRA;mbolea iliyoko sokoni inasajiliwa, kukaguliwa na
kuchambuliwa kwa lengo la kuona mbolea zisizokidhi viwango zinajulikana na
kuondolewa sokoni.
“Benki
ya Equity Tanzania imeingia ubia na AGRA kuanzisha mfuko ambao utasaidia
kununuliwa kwa vifaa vya hifadhi ya nafaka. Katika mradi wa majaribio Njombe,
Morogoro na Iringa, tutatoa mikopo ya sh kuanzia milioni 5 hadi 30 ili
kununua mifuko maalumu ya kuhifadhia nafaka; vihenge vya chuma na vifukofuko
(cocoons), kuanzia mwezi huu,“ alisema Mkuu wa biashara ya kilimo wa
benki ya Equity, Enesto Josephat
Mtaalamu wa viazi mviringo Owekisha Kwigizile, kutoka kituo cha utafiti wa
viazi cha SAGCOT katika mazungumzo yake alisema: “hapa nchini Tanzania
tuna aina tatu viazi mviringo zinazotambuliwa kisheria pamoja na kwamba viazi
mviringo ni chakula kikuu nchini. SAGCOT na wadau wengine wa AGRA tunafanya
juhudi kuongeza vipando bora zaidi ambavyo vitatoa tija kubwa na kuongeza
mavuno”
mwisho
COMMENTS