Dkt. Kalemani aagiza malipo ya fidia mradi Umeme wa Somanga Fungu – DSM

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani (kulia) akisalimiana na Wawakilishi wa Wananchi watakaopitiwa na mradi wa ...




Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani (kulia) akisalimiana na Wawakilishi wa Wananchi watakaopitiwa na mradi wa kusafirisha umeme wa msongo wa kV 400 kutoka Somanga Fungu hadi jijini Dar es Salaam utakaotekelezwa na Serikali kupitia TANESCO. Wawakilishi hao walifika katika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini ili kujadili ulipaji wa fidia kwa wananchi watakaopisha mradi huo.  Kikao hicho pia kilihudhuriwa na watendaji kutoka TANESCO, Wizara ya Nishati na Madini na  Benki ya Maendeleo ya TIB
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Benki ya Maendeleo ya TIB kuhakikisha kuwa kuanzia Septemba 17 mwaka huu, wanaendelea kuwalipa fidia wananchi watakaopitiwa na mradi wa usafirishaji umeme wa msongo wa kV 400 kutoka Somanga Fungu  wilayani Kilwa hadi Kinyerezi jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri alitoa maagizo hayo jijini Dar es Salaam wakati wa kikao chake na Wawakilishi wa wananchi watakaopitiwa na mradi huo, Watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Benki ya Maendeleo ya TIB.
Kikao hicho kilichofanyika katika Makao Makuu ya Wizara ya Nishati na Madini kililenga katika kuweka utaratibu mzuri wa ulipaji wa fidia hiyo pamoja na kuunda Kamati itakayofuatilia utekelezaji wa malipo kwa wananchi watakaopitiwa na mradi huo unaotekelezwa na Serikali kupitia TANESCO. Hii ni baada ya kuonekana kuwa ulipaji wa malipo hayo ulikuwa ukisuasua na hivyo wananchi kuilalamikia Serikali.
Naibu Waziri alisema kuwa jumla ya fedha inayopaswa kulipwa kwa wananchi hao katika wilaya za Temeke, Mkuranga, Kilwa,  Ilala na Kinondoni ni shilingi bilioni 79 na kwamba mpaka sasa Serikali imeshalipa shilingi bilioni 32.7 na kiasi kilichobaki ni shilingi 46.3.
Hivyo katika kiasi hicho kilichobaki cha shilingi bilioni 46.3, Naibu Waziri aliziagiza TANESCO  na TIB kupunguza deni hilo kwa kuanza kuwalipa shilingi bilioni 7.3, Wananchi wa Kivule na Rufiji ambao watapitiwa na mradi  huo ambapo fedha zitaanza kutolewa kuanzia tarehe 17 mwezi huu na ukomo wake ni tarehe 22 Septemba mwaka huu.
" Hivyo nimewaelekeza TANESCO na TIB kuanza kulipa malipo hayo Tarehe 17 mwezi huu ambapo wataanza kulipa shilingi bilioni 1. 9, hilo ndio elekezo la kwanza na awamu ya kwanza," alisema Dkt. Kalemani.
Alisema kuwa malipo mengine yatafanyika  tarehe 27 mwezi huu ambapo Taasisi hizo zitalipa shilingi bilioni 1.03 kwa wananchi, tarehe 8 mwezi wa 9 mwaka huu Taasisi hizo zitalipa shilingi  bilioni 1.60 na tarehe 15 mwezi wa Tisa zitalipa shilingi  bilioni 1.53 ambapo malipo ya mwisho kufanyika  ni tarehe 22 Septemba mwaka huu pale ambapo Taasisi hizo zitalipa shilingi bilioni 1.2  na hivyo watu wa Kivule na Rufiji watakuwa wamekamilika.
Dkt Kalemani aliongeza kuwa baada ya Awamu ya Kwanza ya malipo kukamilika mwezi Septemba mwaka huu,  malipo hayo ya fidia yataendelea kufanyika katika sehemu nyingine zenye madai hayo huku lengo likiwa ni kumaliza madai husika  mwezi Oktoba mwaka huu.
Kuhusu uundaji wa Kamati ya kufuatilia malipo hayo ya fidia, Dkt. Kalemani alipendekeza Mwenyekiti wa Kamati hiyo atoke upande wa wananchi watakaopitiwa na mradi huo ili kufuatilia kwa karibu malipo hayo kwa wananchi, ambapo pendekezo hilo liliridhiwa na Wawakilishi  wa wananchi pamoja na Watendaji wa Serikali.
 
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani (kulia) akiwa katika kikao na Wawakilishi wa Wananchi watakaopitiwa na mradi wa kusafirisha umeme wa msongo wa kV 400 kutoka Somanga Fungu hadi jijini Dar es Salaam utakaotekelezwa na Serikali kupitia TANESCO
Katika kikao hicho, Wawakilishi hao wa wananchi walimchagua Ndugu Josephat Haule kuwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo huku Katibu wa Kamati akitoka Wizara ya Nishati na Madini. Wajumbe wa Kamati hiyo wanatoka upande wa Wananchi, TANESCO, TIB na Wizara ya Nishati na Madini.
Aidha, Naibu Waziri alitoa angalizo kuwa, mwananchi yeyote atakayewasilisha madai ya uongo au kuweka majina hewa ili alipwe fidia  atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Aidha kwa nyakati tofauti Wawakilishi hao wa wananchi walimpongeza Naibu Waziri kwa kuamua kulivalia njuga suala hilo  ili kuwezesha mradi huo kutekelezeka kwa ufanisi na kuhakikisha wananchi wanapata haki yao.
Kwa upande wake Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia umeme, Mhandisi Innocent Luoga, alisema kuwa,  kukamilika kwa ulipaji wa fidia kwa wananchi hao kutawezesha kuanza kwa ujenzi wa njia hiyo ya kusafirisha umeme wa  msongo wa kV 400.
Alisema kuwa umeme utakaosafirishwa  na miundombinu hiyo utatoka katika mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia itakayojengwa na kampuni ya Kilwa Energy katika eneo la Somanga wilayani Kilwa ambapo mitambo hiyo  itazalisha umeme wa kiasi cha megawati 320.
Vilevile alisema kuwa Serikali ilichukua jukumu la kulipa fidia hiyo kwa wananchi mwaka 2015, hivyo  baada ya tathmini kukamilika,  fedha hizo zimeanza kulipwa na Serikali mwaka huu  kupitia Benki ya Maendeleo ya TIB.

Source: Teresia Mhagama, Dar es Salaam


COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Dkt. Kalemani aagiza malipo ya fidia mradi Umeme wa Somanga Fungu – DSM
Dkt. Kalemani aagiza malipo ya fidia mradi Umeme wa Somanga Fungu – DSM
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjgFOXlWSFtCXrc86ThyphenhyphenIzeGgaB8PdnoqsyATko8Hxx-vl4d3rwmmhNLrSbob0Vc71KZqvjOjJkdYuDv7t3k8_ONCXoYCE4q5PSgy4eS9m0W4HARWwnzecOHVuQvrzYS0cOHTXZatMsK94/s320/PAGE+YANGU.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjgFOXlWSFtCXrc86ThyphenhyphenIzeGgaB8PdnoqsyATko8Hxx-vl4d3rwmmhNLrSbob0Vc71KZqvjOjJkdYuDv7t3k8_ONCXoYCE4q5PSgy4eS9m0W4HARWwnzecOHVuQvrzYS0cOHTXZatMsK94/s72-c/PAGE+YANGU.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/08/dkt-kalemani-aagiza-malipo-ya-fidia.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/08/dkt-kalemani-aagiza-malipo-ya-fidia.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy