MAGUFULI, SMZ, CCM WASIKITISHWA NA KIFO CHA JUMBE

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Jumbe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambiram...



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Jumbe
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na pia Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Aboud Jumbe Mwinyi kilichotokea leo tarehe 14 Agosti, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Mhe. Aboud Jumbe Mwinyi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na pia alikuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia Mwaka 1972 hadi 1984.
Kufuatia kifo hicho Rais Magufuli amesema Taifa limempoteza mtu muhimu ambaye alijitoa kupigania Uhuru, Umoja, Haki na Maendeleo ya Wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla katika kipindi kigumu ambacho Taifa lilikipitia.
"Nimeshitushwa sana na kifo cha Mzee wetu Mhe. Aboud Jumbe, kwa hakika Tanzania imepoteza mtu muhimu ambaye katika kipindi cha uongozi wake alitoa mchango mkubwa wa kuipigania na kuijenga Tanzania tunayoiona leo" Amesema Rais Magufuli.
Dkt. Magufuli ameendelea "Kupitia kwako Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein napenda kuwapa pole familia ya Marehemu, Ndugu, Jamaa na Marafiki wote, Wananchi wa Zanzibar na Watanzania wote kwa ujumla kwa kufikwa na msiba huu mkubwa"
Rais Magufuli amemuombea marehemu Aboud Jumbe Mwinyi apumzike mahali pema peponi.
Nayo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeeleza kusikitishwa kwake na kifo cha aliyekuwa rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Alhaji Aboud Jumbe Mwinyi kilichotokea nyumbani kwake Mji mwema Dar-es-Salaama. 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na waziri wa nchi Ofisi ya Makamo wa pili wa rais Mohamed Aboud , SMZ inaukumbuka mchango mkubwa wa hayati Jumbe katika kipindi cha uongozi wake wa miaka 13. 
'Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesikitishwa na kifo cha hayati Alhaji Aboud Jumbe ambaye alikuwa rais wa Zanzibar kwa muda wa miaka 13 huku mchango wake mkubwa katika kukuza na kuimarisha demokrasia ukibakia kielelezo kwa wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla'alisema. 
Kwa mujibu wa taarifa za kutoka kwa familia ya hayati Jumbe mazishi yake yanatazamiwa kufanyika kesho mchana hapo nyumbani kwake Migombani nje kidogo ya mji wa Zanzibar eneo ambalo watoto wake watatu wamezikwa hapo. 
Jumbe alishika madaraka ya kuongoza Zanzibar katika mwaka 1972 mara baada ya kuuwawa kwa aliyekuwa rais wa kwanza wa Zanzibar hayati Abeid Amani Karume ambapo baraza la mapinduzi kwa kauli moja lilimchaguwa kushika wadhifa huo wa rais wa Zanzibar. 
Kufuatia kuchafuka kwa hali ya kisiasa Zanzibar katika mwaka 1984 Jumbe alilazimika kujiuzulu pamoja na viongozi wengine akiwemo waziri kiongozi Ramadhan Haji Faki na hivyo kupoteza nyadhfa zote ikiwemo makamo wa rais wa muungano na makamo mwenyekiti wa chama cha mapinduzi. 
Alhaji Aoud Jumbe Mwinyi atakumbukwa kwa mambo mengi akiwa ni mmoja ya viongozi walioshirikiana na baba wa taifa mwalimu Nyerere kuzaliwa kwa chama  cha mapinduzi CCM hapo mwaka 1977 katika uwanja wa Amaan Zanzibar. 
Kabla ya kuzaliwa kwa CCM Jumbe alikuwa rais wa chama cha ASP ambapo ushawishi mkubwa wa hayati Jumbe ndiyo uliosababisha kuunganishwa kwa vyama hivyo na kuzaliwa kwa CCM ikiwa ni moja ya juhudi za kuimarisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar. 
Nacho Chama cha Mapinduzi Zanzibar kimearifu kusikitishwa na kifo cha mmoja ya viongozi wake ambaye alikuwa Makamo Mwenyekiti wa kwanza wa chama hicho Aboud Jumbe Mwinyi. 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na naibu katibu mkuu wa chama cha Mapinduzi Zanzibar Vuai Ali Vuai alisema mchango wa hayati Jumbe katika chama cha Mapinduzi hautosahaulika ambapo yeye kwa kushirikiana na baba wa taifa mwalimu Nyerere walihakikisha kinazaliwa chama chenye nguvu katika Jamhuri ya Muungano hapo mwaka 1977. 
'Chama cha mapinduzi kinatoa masikitiko yake makubwa kufuatia msiba mkubwa wa aliyekuwa makamo mwenyekiti wake wa kwanza hayati Aboud Jumbe Mwinyi........mchango wa Jumbe hautosahaulika katika chama cha Mapinduzi'alisema. 
Alisema Jumbe alihakikisha kinazaliwa chama kipya kitakachokuwa na nguvu pamoja na sura ya Muungano kwa ajili ya faida ya wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania'alisema. 
Alisema tangu kuzaliwa kwa chama hicho,kimeendelea kupata mafanikio makubwa ikiwemo kushinda katika chaguzi zote kuanzia za mfumo wa chama kimoja hadi vyama vingi. 
Aidha chama hicho kimeendelea kuwa imara bila ya kuyumba na kuendelea kushika hatamu ya kuongoza dola katika kipindi chote kuanzia mwaka 1977 hadi leo. 
'Mafanikio yote ya chama cha mapinduzi hatuna budi kukumbuka juhudi zilizofanywa na hayati Jumbe kwa sababu ndie aliyekiunganisha chama hicho kutoka ASP na TANU na kuzaliwa CCM'alisem Vuai. 
Aidha Vuai alisema katika kuimarisha demokrasia na sauti za wananchi kusikika,Jumbe alianzisha chombo cha kutunga sheria ambacho alikiita baraza la wawakilishi. 
Baraza la wawakilishi liliasisiwa katika mwaka 1979 kwa kuanzia viongozi kutoka katika wilaya za Unguja na Pemba kwa kuzishirikisha jumuiya za chama ikiwemo umoja wa vijana,wazazi ushirika na Umoja wa wanawake UWT. 
'Huo ndiyo mchango mkubwa wa hayati Jumbe katika kuanzisha chombo cha Baraza la Wawakilishi ambalo aliliita ngome ya wananchi katika kusikiliza maoni yao kusikika'alisema.




COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,301,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,23,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: MAGUFULI, SMZ, CCM WASIKITISHWA NA KIFO CHA JUMBE
MAGUFULI, SMZ, CCM WASIKITISHWA NA KIFO CHA JUMBE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg_ewvX0YyLgPLXd4_yzwLs_9C5489IGfIgsdm87VgN19d9SKBnikClXg5snsWsoDofe6y0kvuEakvXlPfiw_7B82d2YLjP5p9o6_f3iG0p1JZBtKnFmTiztiGyLCeCHzjLuURxyqx4qV4/s1600/jumbe.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg_ewvX0YyLgPLXd4_yzwLs_9C5489IGfIgsdm87VgN19d9SKBnikClXg5snsWsoDofe6y0kvuEakvXlPfiw_7B82d2YLjP5p9o6_f3iG0p1JZBtKnFmTiztiGyLCeCHzjLuURxyqx4qV4/s72-c/jumbe.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/08/magufuli-smz-ccm-wasikitishwa-na-kifo.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/08/magufuli-smz-ccm-wasikitishwa-na-kifo.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy