Taarifa kwa vyombo vya habari Agosti 1, 2016 Kuhusu kutenguliwa kwa Mkuruge...
Taarifa kwa vyombo vya habari
Agosti 1, 2016
Agosti 1, 2016
Kuhusu kutenguliwa kwa Mkurugenzi wa
Bagamoyo na uhusiano wa kushindwa
CCM katika majimbo ya Mlimba na Kilombero, mkoani Morogoro 2015.
CCM katika majimbo ya Mlimba na Kilombero, mkoani Morogoro 2015.
Julai 30, mwaka huu, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Dokta John Pombe Magufuli alitengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji
wa Wilaya ya Bagamoyo, Bibi Azimina A. Mbilinyi. Taarifa hiyo
iliyosainiwa na Eng. Musa Iyombe, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, ilisema
Rais alitengua uteuzi huo kwa sababu hakuridhishwa na utendaji kazi wa Bibi
Azimina A. Mbilinyi.
Baada ya taarifa hiyo, wapo watu wanaohusisha kutenguliwa
mkurugenzi huyo na kushindwa kwa CCM katika majimbo ya Mlimba na Kilombero. Kabla
ya kuhamishimiwa Bagamoyo, Bibi Mbilinyi alikuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Kilombero, yenye majimbo mawili ya uchaguzi, ambayo yote wabunge wake ni wa
kambi ya Chadema; Peter Lijualikali-Kilombero na Suzan Kiwanga Mlimba.
NINACHOKIJUA KUHUSU MAJIMBO HAYA
Naandika haya kama mtu ambaye nilishiriki kura za maoni na
niliona kasoro zilizotokea na ndizo zilizosababisha CCM kushindwa, unaweza
kuona hata madiwani tumepata wachache kuliko wenzetu. Nilikuwa kati ya watia
nia katika CCM Jimbo la Mlimba, wengine niliogombea nao ni Dk Frederick
Sagamiko (ambaye sasa ni Mkurugenzi-Maswa), Senorina Kateule, Godwin
Kunambi (ambaye ndiye alipitishwa na chama kugombea), Augustino Kusalika,
George Swevetta, Castor Ligallama, Profesa Jumanne Mhoma, Fred Mwasakilale.
Kwa upande wa Jimbo la Kilombero watia nia walikuwa Kanali
mstaafu Harun Kondo, Vitus Lipagila, Abdullah Lyana, Oscar Mazengo,
Japhet Mswaki, Paul Mfungahema, John Guninita, Abubakari Asenga (ambaye sasa
ni katibu tawala Rombo) na Abdul Mteketa.
MCHAKATO WA KURA ZA MAONI
Katika mchakato wa kumpata mgombea wa Ubunge, hapo ndipo
tatizo lilipoanzia; Kwa mfano katika Jimbo la Mlimba, tangu siku ya kwanza ya
kampeni katika kumsaka mgombea, tukiwa tunatoka makao makuu ya wilaya
(Ifakara), tulipofika hotelini kata ya Mlimba ugomvi uliibuka miongoni mwa
watia nia.
Msingi wa ugomvi huo uliozaa uhasama, ilikuwa mmoja wa watia
nia kumrushia maneno mwingine kiasi cha kutaka kupigana; sababu kubwa ni kwamba
sote tuliwahi kufika katika kambi yaani hoteli ambayo tulitakiwa kuwepo kabla
ya kwenda vijijini kwa wanaCCM wenzetu kujinadi, lakini kuna mtia nia ambaye
alichelewa zaidi ya saa masaa matano kufika tulipotakiwa kuwepo yaani hapo
kwenye kambi, kitendo ambacho kilitafsiriwa kama alikuwa anafanya kampeni.
Aidha mtia nia huyo aliambiwa na mtia nia mwenzake (huyo
waliyekuwa wakigombana) kwamba yeye hakupaswa kugombea Jimbo la Mlimba, kwa
sababu makazi yake ni kata ya Mkamba, ambayo iko katika Jimbo la Kilombero.
Kama hiyo haitoshi, katika kura za maoni kulikuwa na malalamiko
kuwa baadhi ya watia nia ni kama walipandikiza watu, kwamba yuko mtia nia
ambaye kulipokuwa na mkutano wa wana CCM ili kusikia sera za watia nia,
aliposimama yeye alikuwa anashangiliwa sana, na wakati mwingine kama yeye
alikuwa wa kwanza kuzungumza, basi baada ya yeye kuongea, wengi wa wana CCM
walikuwa wakiondoka kwenye mikutano.
OFISI YA CCM WILAYA KUTOCHUKUA HATUA
Licha ya malalamiko hayo kuwasilishwa wilayani, hapakuwa na
hatua za haraka zilizochukuliwa. Kitendo hiki kiliendelea kuimarisha ufa ndani
ya CCM hasa miongoni mwa wagombea (watia nia).
KURA ZA MAONI NA BAADA YA MATOKEO
Baada ya kumaliza kujinadi, uchaguzi ulifanyika katika vituo
mbalimbali huku tukiambiwa tuweke mawakala katika maeneo ya kupigia kura. Wengi
tulifanya hivyo. Kwenye kura za maoni, miujiza ilianza kutokea, kwamba katika
kata fulani, wakala wako anakwambia umepata kura kiasi fulani, wilayani
tulikuwa tukiona kura tofauti. Wengi tulipohoji tuliambiwa tutulie kungekuwa na
vikao kujadili kama kuna kasoro na namna gani twende sawa.
NINI KILITOKEA?
Hadi leo hakuna kikao kilichoitishwa na wilaya kujadili malalamiko ambayo watia nia waliyawasilisha wilayani. Matokeo yake ni nini? Ukweli ni kwamba wapo wanaCCM wengi walijitoa CCM moja kwa moja na kuungana na upinzani, huku wengine walifanya hivyo kwa siri, sababu kubwa ni kwamba waliona ofisi ya Wilaya haikuwatendea haki kwa kutofanya kikao, kitendo ambacho kilitafsiriwa kama walikuwa na mgombea wao waliyemtaka, japo ofisi ya CCM wilaya Kilombero imekuwa ikikanusha hilo.
Hadi leo hakuna kikao kilichoitishwa na wilaya kujadili malalamiko ambayo watia nia waliyawasilisha wilayani. Matokeo yake ni nini? Ukweli ni kwamba wapo wanaCCM wengi walijitoa CCM moja kwa moja na kuungana na upinzani, huku wengine walifanya hivyo kwa siri, sababu kubwa ni kwamba waliona ofisi ya Wilaya haikuwatendea haki kwa kutofanya kikao, kitendo ambacho kilitafsiriwa kama walikuwa na mgombea wao waliyemtaka, japo ofisi ya CCM wilaya Kilombero imekuwa ikikanusha hilo.
Anguko la CCM katika Wilaya ya Kilombero lilitokana na
dharau; baadhi ya viongozi kuamini kwamba wanaweza kwenda mbele hata kama
watawadharau au watayadharau malalamiko ya watia nia wengine.
USHAHIDI WA HILI
Ni mimi, Dismas Lyassa pekee ndiye niliyeshiriki kwenye mikutano
ya kuwanadi wagombea, niliwasha gari yangu kutoka Dar es Salaam hadi Ifakara
kwenye kumnadi Abubakar Assenga. Wengine walikuwa na sababu zao zikiwamo
kutofurahishwa na mchakato mzima wa upatikanaji wa wagombea.
INAWEZEKANAJE
BIBI AZIMINA A. MBILINYI AKATENGULIWA HARAKA HIVI
BAADA YA KUHAMISHIWA BAGAMOYO?
BAADA YA KUHAMISHIWA BAGAMOYO?
Kama nilivyotangulia kusema, natoa taarifa hii kama mtu
ambaye nayajua mazingira ya kushindwa kwa CCM yangu katika uchaguzi, mtu ambaye
najua kwanini CCM tulishindwa mwaka 2015. Huenda wengine waliona tofauti lakini
haya ni kwa namna ninavyoona mimi kama Dismas Lyassa.
Kwa bahati nzuri katiba inaruhusu kila mtu kutoa maoni yake
katika jambo kwa kadri anavyoona yeye, ndivyo ninavyoona mimi kilichotokea
kwenye uchaguzi 2015, wengine wanaweza kuwa na maoni tofauti, nao waheshimiwe
kwa sababu kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni kwa kadri anavyoona yeye.
Katika mitandao ya kijamii, yuko mwanasiasa mmoja maarufu
nchini anahusisha kuanguka CCM eti kwa sababu alishindwa kuisaidia CCM
kushinda. Kwa mazingira niliyoyaeleza wagombea wetu wangewezaje kushinda? Mfano
katika kijiji cha Mofu pekee, zaidi ya viongozi 15 wa matawi na taasisi
mbalimbali walihama CCM na kwenda upinzani, jumatano ya kuelekea jumapili ya uchaguzi.
CCM haijapoteza majimbo ya Mlimba na Kilombero pekee, kwa hiyo sioni mantiki ya
kuhusisha haya ya Azimina na siasa.
Wapo
wanaoweza kusema aaah sasa mbona Rais amechukua maamuzi saa chache baada ya CCM
kushindwa kesi za kupinga matokeo….jambo humtokea mtu wakati wowote, iwe
anatoka usingizini…kazini nk…mtu anaweza kufa hata kama anatoka nyumba ya
ibada…huwezi kusema si angesubiri kwanza.
Bibi Azimina A. Mbilinyi
Akiwa Mkurugenzi Kilombero niliwahi kuwasiliana nae kwa
simu/whatsap kuhusu kijana mmoja aliyesomeshwa na mjane. Kwamba, kijana huyo
alipata ajira katika halmashauri hiyo kama afisa maendeleo, lakini aliporipoti
akaambiwa arudi atatafutwa. Nilimpigia Azimini mara kadhaa kujua juu ya suala
hili na majibu yalikuwa ni kwamba anafanyia kazi, huku kukiwa na utata wa kama
nafasi hiyo ambayo ilikuwa ni kwa mujibu Tume ya Utumishi wa Umma kama ilikuwa
bado au la.
Maana yake ni nini? Ikiwa mimi najua
hili, je wewe ulikuwa unajua? Kumbe ni kwamba sio sahihi kuzungumza mambo
tusiyoyajua. No research, no right to SPEAK. Huyo kijana ambaye
amesomeshwa na mjane, hadi leo hana kazi, anaishi kwa mama yake kwenye nyumba
moja inayotazamana na hoteli ya Landmark Ubungo, Dar es Salaam. Hana ajira,
licha ya kwamba tayari alishaipata, ameambiwa asubiri, leo ni zaidi ya miezi
nane tangu aambiwe asubiri, hakuna jibu lililonyooka.
Ambacho nataka umma ufahamu ni kwamba ukweli kuhusu majimbo
ya Kilombero na Mlimba ni huo, kwamba wapo wana CCM walioshirikiana na vyama
vya upinzani ili tu ishinde kwa sababu waliamini hawakutendewa haki na chama
hasa pale kilipofunga milango ya kuwepo kwa mikutano ya suruhu.
NILIWAHI KUSHAWISHI WANACHAMA NA
VIONGOZI WA CCM KUWAONDOA VIONGOZI WA WILAYA LAKINI NIKAOMBWA NIACHANE NA HILO
ILI LISILETE ATHARI KWA CHAMA
Kama mtakumbuka baada ya uchaguzi mkuu, niliongoza mpango wa
kufufua CCM Kilombero, niliwasiliana na viongozi wa kata zote, matawi na
wanachama; azma ilikuwa kwanza ni kuwaondoa viongozi wa wilaya, hata hivyo
nilishawishiwa na baadhi ya viongozi wa ngazi za juu wa chama kwamba suala hilo
lingeweza kuharibu zaidi, kwa hiyo niwe na utulivu na nifanye mawasiliano na
wote ambao nilishawasiliana nao ili kuahirisha chochote nilichokuwa
nimekipanga.
Nilifanya hivyo, kutokana na kuwatii hasa baada ya kuelezwa
njia nyinginezo ambazo zingeweza kuweka mambo sawa ndani ya chama.
Naomba ulimwengu ufahamu kwamba hayo ndiyo yaliyotokea
katika majimbo ya Mlimba na Kilombero; shida kubwa ni sisi wenyewe tulishindwa
kuungana baada ya kura za maoni, na viongozi hadi leo hawajatuunganisha.
Kwa kuanguka kwa CCM wa kuondolewa ni viongozi wote wakuu wa CCM Wilaya kutokana na sababu 1.Kushindwa kuwa na mkakati wa kuimarisha chama, hasa kutokana na ukweli kwamba hata wakati wa kura za maoni, wapo wanachama walitoa lawama za wazi kwamba viongozi wa wilaya wamekuwa wazito kutembelea kata na matawi ili kuyaimarisha. 2. Pia hawakuona umuhimu wa kuweka suruhu baina ya watia nia 3. Kuna haja ya viongozi wakuu wa chama chetu (CCM) kuomba kibali ili waingilie mawasiliano ya simu ya viongozi wa CCM Wilaya Kilombero, hasa laini za tigo na Airtel, kuanzia Julai 2015 hadi Oktoba 2015. Nafahamu ninachokiongea ndio maana sijataja laini za simu za makampuni mengine.
Kwa kuanguka kwa CCM wa kuondolewa ni viongozi wote wakuu wa CCM Wilaya kutokana na sababu 1.Kushindwa kuwa na mkakati wa kuimarisha chama, hasa kutokana na ukweli kwamba hata wakati wa kura za maoni, wapo wanachama walitoa lawama za wazi kwamba viongozi wa wilaya wamekuwa wazito kutembelea kata na matawi ili kuyaimarisha. 2. Pia hawakuona umuhimu wa kuweka suruhu baina ya watia nia 3. Kuna haja ya viongozi wakuu wa chama chetu (CCM) kuomba kibali ili waingilie mawasiliano ya simu ya viongozi wa CCM Wilaya Kilombero, hasa laini za tigo na Airtel, kuanzia Julai 2015 hadi Oktoba 2015. Nafahamu ninachokiongea ndio maana sijataja laini za simu za makampuni mengine.
TUUNGANE KUIMARISHA NCHI
Kutangaza mambo tofauti ni kupotosha umma bila sababu, tuungane na Rais katika kuimarisha nchi. Miaka mingi tumekuwa tukililia Rais mchapakazi, sasa amepatikana ni vema kumtia moyo.
Kwani hujawahi kuwa na rafiki, halafu ukabini kwamba haikuwa
sahihi kuwa nae?
Ni mambo ya kujitafakari badala ya kulaumu.
Ni mambo ya kujitafakari badala ya kulaumu.
Tanzania kwanza; tuungane kuijenga nchi yetu.
Wako katika ujenzi wa taifa
COMMENTS