Majaliwa aziagiza halmashauri nchini kuwa na anwani za makazi

Balozi wa Anwani za Makazi Duniani Prof. Anna Tibaijuka akiongea akimkabidhi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe....



Balozi wa Anwani za Makazi Duniani Prof. Anna Tibaijuka akiongea akimkabidhi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa anwani ya makazi wakati wa wa hafla ya uzinduzi wa Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi na Mwogozo wa Postikodi katika ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Mjini Dodoma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameziagiza halmashauri zote nchini kutekeleza mpango kazi wa anwani za Makazi na Postikodi kwa kushirikisha wadau mbalimbali wakiwemo wananchi. 
Waziri Mkuu Majaliwa ametoa agizo hilo leo kabla ya kuzindua Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi na Mwongozo wa Postikodi uliofanyika katika ukumbi wa Pius Msekwa uliopo ndani ya viwanja vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dodoma.

“Nikizingatia hatua ambazo zimechukuliwa na Serikali katika kuweka mazingira ya utekelezaji wa anwani za makazi, naagiza halmashauri zote nchini kuzifanyia kazi changamoto ambazo hazihitaji fedha ama ambazo hazihitaji gharama kubwa” amesema Waziri Mkuu Majaliwa.

Waziri Mkuu amebainisha baadhi ya changamoto ambazo hazihitaji gharama kuwa ni pamoja na kuhakikisha barabara na mitaa yote inakuwa na majina yaliyorasimishwa na wananchi wenyewe, kudhibiti mipango miji dhaifu na ujenzi holela, kuwa na takwimu za idadi ya barabara na mitaa na nyumba katika kila kata na kuwa na taarifa za wakazi katika kila kata.

Changamoto nyingine zisizohitaji gharama kubwa ni kujengea uelewa wadau na wananchi kuujua na kuwa mfumo huo, kuimarisha matumizi ya daftari la wakazi ambapo taarifa za utekelezaji wa kazi hizo Waziri Mkuu ameagiza ziwasilishwe Ofisi ya Rais TAMISEMI kabla ama ifikapo mwezi Desemba, 2016.

Aidha, Waziri Mkuu Majaliwa amesema kuwa kufuatia nia ya Serikali kuhamia Dodoma, manispaa ya Dodoma na halmashauri ya Chamwino zipewe kipaumbele cha utekelezaji ili kuweka mazingira mazuri ya kuishi na kufanya kazi.

“Utekelezaji wa Mpango katika Manispaa ya Dodoma na Halmashauri ya Chamwino ukamilike kabla ama ifikapo mwezi Desemba, 2016 na kuhakikisha utekelezaji huo kukamilika kwa wakati” amesema Waziri Mkuu Majaliwa.

Kwa upande mwingine Waziri Mkuu amezitaka wizara za Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Manispaa ya Dodoma, Halmashauri ya Chamwino, CDA; TCRA na TPC zishirikiane ipasavyo katika kukamilisha mpango wa anwani katika mkoa huo.

Mbali na hayo, Waziri Mkuu amezitaka taasisi za TANROADS, TBA, NHC, Mipango Mji na Mradi wa Kuboresha Miji (TSC) zinapoandaa mipango hususan mipango ya miundombinu na makazi, ziainishe pia anwani za makazi kwa kushirikiana na Halmashauri katika maeneo husika.

Katika kufanikisha hilo, Waziri Mkuu amezitaka Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Wizara ya Unjenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, TCRA na TPC kushiriki ipasavyo katika utekelezaji wa mpango hususan katika kujenga uelewa na uwezo kwa viongozi na watendaji  wa halmashauri ili waweze kutekeleza mpango huo ipasavyo.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa George Simbachawene amesema kuwa Mpango huo umefanyiwa majaribio katika majiji mawili ya Dar es salaam na Arusha pamoja na manispaa za Dodoma na Zanzibar.

Waziri Simbachawene aliongeza kuwa ili kuwa na Tanzania ya kisasa, anwani za makazi ni kigezo muhimu cha kuzingatiwa katika kundeleza majiji, manispaa, halmashauri, kata na hata mitaa ambayo ndio inajenga taswira ya nchi.

Wakati huo huo Waziri Mkuu amesema kuwa Mfumo wa Anwani za Makazi na Postikodi una manufaa mengi ambao utarahisisha ukusanyaji wa mapato kutoka vyanzo mbalimbali nchini.
Waziri Mkuu Majaliwa amesema hayo leo mjini Dodoma wakati alipokuwa akizindua Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi na Mwongozo wa Postikodi ambao utatumika nchi nzima.
“Kama kila mlipa kodi tutamfahamu kwa uhakika anaishi wapi,   tutamutoza kodi stahiki na hili ni jambo muhimu la utawala bora” amefafanua Waziri Mkuu.
Waziri Mkuu Majaliwa amesema kuwa uwepo wa anwani ya makazi nchini utasaidia kurahisisha ukusanyaji wa mapato mbalimbali ikiwa ni jukumu muhimu la utawala bora.
Aidha, amesema kuwa mfumo huo wa anwani za makazi utaiwezesha  Serikali kuwahudumia wananchi wake kirahisi ikiwa ni pamoja na kutoa ulinzi, kurahisisha mawasiliano miongoni mwa wananchi na Serikali.
Vile vile mfumo huo utasaidia kurahisisha na kuongeza ufanisi katika utoaji huduma za kijamii, huduma za kibiashara, huduma za dharura na uokoaji, kurahisisha sensa, kuboresha daftari la wapiga kura, kuboresha huduma za posta na kuwezesha utoaji wa biashara mtandao.
Waziri Mkuu ameongeza kuwa katika nchi nyingi za viwanda na nchi zilizoendelea suala la miundombinu ikiwemo Mfumo wa Anwani za Makazi na Postikodi ni muhimu na linaeleweka kwa kila mtu katika kuanzisha, kukuza na kuendeleza uchumi wa viwanda.
“Kwa kutumia mfumo huu, viwanda viwe vikubwa au vidogo vinatambulika viko wapi kwa anwani zao za makazi na hivyo kuweza  kupima kirahisi ukuaji wa viwanda” alifafanua Waziri Mkuu.
Waziri Mkuu amesisitiza taasisi zote za umma na zile za binafsi zianze kutumia anwani za makazi na postikodi ili kuchochea kasi ya maendeleo ya nchi ikiwa ni pamoja na kutumia katika makusanyo ya mapato.
Waziri Mkuu Majaliwa amewasisistiza wadau wote nchini kuzingatia kuwa na anwani ni haki ya kila mtu na pia kupata huduma za msingi kupitia mfumo huo ni haki ya kila mtu.

Aidha, dhana ya kuwa “dunia ni kijiji” inapaswa kuwa chachu ya kupata huduma zote mahali ulipo, inahitaji juhudi za makusudi za kuhakikisha Tanzania imekuwa sehemu ya kijiji hicho na inakuwa ni moja ya mataifa kinara wa kutoa huduma mbalimbali kwa ufanisi kwa kutumia Mfumo wa Anwani za Makazi na Postikodi.
Kwa upande wake Balozi wa Anwani za Makazi Duniani Prof. Anna Tibaijuka amesema kuwa anajivunia mradi huo kutekelezwa nchini ambao utasaidia kuonesha watu mahali wanapoishi ambapo Tanzania imefanikiwa kuwa na anwani za makazi nchi nzima licha ya changamoto ya  kuwa na miji mingi ambayo haijapangwa.
Zao la anwani za makazi linatokana na Umoja wa Posta Dunia (UPU) iliyopitishwa katika mkutano mkuu wa 25 uliofanyika mjini Doha, Qatar mwaka 2012 ambao ulipitisha azimio la kuzitaka nchi zote duniani kuhakikisha kuwa kila mtu anakuwa na anwani.
Source:Beatrice Lyimo na Eleuteri Mangi, MAELEZO, Dodoma

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,301,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,23,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Majaliwa aziagiza halmashauri nchini kuwa na anwani za makazi
Majaliwa aziagiza halmashauri nchini kuwa na anwani za makazi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiRm3VgYUEHOGayKjiAY1BXUxUWEgYd4S6v1Sk1d-b5UwzAU0jt1UlVKJpog3c7O0e9fb3cfVGUJIK3Fch9v3H_POTPj_hfPGxMbQsX_YoVWpa1G9pgpE_I_32SN69nz7TukhyphenhyphenKKslF_6Y/s320/7.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiRm3VgYUEHOGayKjiAY1BXUxUWEgYd4S6v1Sk1d-b5UwzAU0jt1UlVKJpog3c7O0e9fb3cfVGUJIK3Fch9v3H_POTPj_hfPGxMbQsX_YoVWpa1G9pgpE_I_32SN69nz7TukhyphenhyphenKKslF_6Y/s72-c/7.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/09/majaliwa-aziagiza-halmashauri-nchini.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/09/majaliwa-aziagiza-halmashauri-nchini.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy