STARTIMES KUWAPAMBANISHA 18 FAINALI ZA SHINDANO LA VIPAJI VYA SAUTI KESHO JIJINI DAR ES SALAAM

Mtengenezaji wa Sauti katika chaneli ya StarTimes Kiswahili, Tracy Luo (katikatio) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) w...


Mtengenezaji wa Sauti katika chaneli ya StarTimes Kiswahili, Tracy Luo (katikatio) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza kufanyika kwa fainali za shindano la vipaji vya sauti litakalofanyika kesho katika ukumbi wa Nkrumah, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kushoto ni mshiriki wa shindano hilo kutoka Zanzibar,  Safiya Ahmed na kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Masoko wa kampuni hiyo, Damien Li. Washiriki 18 kati ya 547 wameingia hatua ya fainali ambapo washindi 10 watajipatia fursa ya kwenda kufanya kazi makao makuu ya StarTimes yaliyopo Beijing, China.

 Mshiriki Safiya Ahmed kutoka Zanzibar (kushoto), akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni Mtengenezaji wa Sauti katika chaneli ya StarTimes Kiswahili, Tracy Luo.
Mshiriki Hilda Malecela kutoka Dar es Salaam (kulia), akizungumza na wanahabari katika mkutano huo.
Mshiriki kutoka mkoani Arusha, Mathew Mgeni (kushoto), akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni mshiriki Hilda Malecela kutoka Dar es Salaam.
Taswira meza kuu kwenye mkutano huo.
Washiriki wa shindano hilo. Kutoka kulia ni Safiya  Ahmed kutoka Zanzibar, Mathew Mgeni kutoka Arusha na Hilda Malecela kutoka Dar es Salaam
Washiriki wa shindano hilo wakiwa kwenye mkutano huo.

Na Dotto Mwaibale

WASHIRIKI 18 waliotinga fainali ya shindano la kusaka vipaji vya sauti linaloendeshwa na kampuni ya StarTimes watapanda jukwaani kesho katika ukumbi wa Nkrumah uliopo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kupigania nafasi kumi za kwenda kufanya kazi jijini Beijing, China.

Washiriki hao ambao walipatikana kwenye usaili uliofanyika katika mikoa ya Arusha (washiriki watano), Zanzibar (washiriki watano) na Dar es Salaam (washiriki nane) watakuwa na kibarua kigumu cha kuwavutia majaji wabobezi katika tasnia ya sanaa za maonyesho ili waweze kuchaguliwa na kula mkataba mnono wa kufanya kazi katika makao makuu ya kampuni hiyo ya matangazo ya dijitali nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi Mtengenezaji wa Sauti katika chaneli ya StarTimes Kiswahili,  Tracy Luo amesema mchakato wa kuwapata washiriki hao waliotinga hatua ya fainali lilikuwa ni gumu sana kwani watanzania takribani 547 walijitokeza na wengi wameonyesha vipaji vya hali ya juu.

“Shindano la kusaka vipaji vya sauti ni la kwanza na aina yake kuwahi kutokea nchini ambalo limewapa fursa watanzania wenye vipaji kujitokeza na kuzitumia katika kuwaingizia kipato. Lakini mwaka 2014 ndiyo yalianza rasmi ambapo matunda yake ni watazamaji waliweza kufurahia vipindi vizuri zaidi. Katika miaka mitatu iliyopita imeonyesha kuwa filamu na tamthiliya zilizoingizwa kwa lugha mbalimbali za kiafrika zilipendwa zaidi. Na hali hiyo imeifanya kampuni ya StarTimes kusaka vipaji vya watu kuingiza sauti ili ziweze kutumika zaidi.” Alisema Luo

“StarTimes kwa kushirikiana na ubalozi wa China hususani idara ya kukuza utamaduni imeamua kuja na mashindano haya baada ya kuona kuna ombwe katika nafasi ya watu wa kuingiza sauti kwenye filamu na tamthiliya za Kichina kwenda lugha ya Kiswahili. 

Tumegundua kuwa watanzania ni wapenzi wakubwa wa tamthiliya na filamu za Kichina zilizoingiziwa sauti za Kiswahili na kupitia washindi watakaopatikana kesho tunaamini kazi nyingi zaidi zitafsiriwa na kuweza kueleweka miongoni mwa watazamaji wengi. Wateja wetu wamekuwa wakifurahia kazi hizo kupitia chaneli za TBC1 pamoja na chaneli mahususi kwa vipindi na madhui ya kwa lugha ya Kiswahili ya StarTimes Kiswahili kama vile Ma Zu, Kutafuta Mapenzi, Ndoa za Familia ya Mi na kadhalika.” alisema Luo 

Mtengenezaji huyo wa sauti wa chaneli ya StarTimes Kiswahili alihitimisha kwa kusema kuwa, “Watanzania inabidi waamke na kuchangamkia fursa zilizokuja pamoja na kuingia kwa matangazo ya dijitali hususani katika kukuza kazi za sanaa. Kwa mfano hivi sasa kuna uhitaji mkubwa wa maudhui ili kuweza kurushwa kwenye chaneli na vipindi vyetu, endapo watu watautumia ubunifu walionao hii itakuwa ni ajira kubwa kwao. 

Ninaamini kuwa kupitia teknolojia hii mpya wasanii wanaweza kujulikana zaidi sehemu kubwa ndani ya nchi kwa muda mfupi, kwa mfano StarTimes inapatikana katika nchi takribani 16 barani Afrika na zaidi ya mikoa 17 nchini huku baadhi ya chaneli zetu zikionekana zaidi ya nchi moja kama vile chaneli ya StarTimes Kiswahili inayoonekana nchini Tanzania na Kenya.”

Kwa upande wake mshiriki katika fainali za masindano hayo kutoka Arusha Mahew Mgeni amesema kuwa, “Najisikia mwenye furaha kuwa mmojawapo wa washiriki waliofikia hatua ya fainali kwani hapo awali nilikuwa ni shabiki na mtazamaji wa filamu na tamthiliya za Kichina lakini leo hii ninaweza kuwa naingiza sauti kwenye kazi zijazo siku za usoni. Naipongeza sana kampuni ya StarTimes Tanzania kwa kuja na shindano hili la aina yake ambalo halijawahi kutokea na kusisitiza makampuni mengine kwenye tasnia ya matangazo ya dijitali kufanya hivyo.”

Mshiriki mwingine kutoka visiwani Zanzibar, Safiya Ahmed yeye alielezea matarajio yake endapo atakuwa mmojawapo wa washindi.

“Kwanza, nimefurahi sana kuwepo kwa mashindano haya nchini ambapo wasanii kama sisi wenye vipaji vya kuingiza sauti tunaweza kuonekana na kutambulika. Mimi ninaamini kama mashindano haya yakiendelea basi watu wengi zaidi wataendelea kujitokeza na hivyo kupelekea kazi nyingi zaidi kutengenezwa. Natumaini nitatenda haki kwa hadhira inayotarajia kazi nzui kutoka kwangu endapo nitachaguliwa na kuwa mshindi.” alisema Ahmed

Akizungumzia umuhimu wa mashindano hayo katika kupanua fursa zingine za sanaa nchini Tanzania, mshiriki kutoka Dar es Salaam, Halima Malecela amesema kuwa, “Sanaa ina wigo mpana sana kwani kuna wale ambao wanaopenda kuonekana mbele ya kamera kama vile waigizaji wa filamu na tamthiliya mbalimbali, lakini kuna wengine kama sisi ambao tunapenda kuwa nyuma ya kamera na badala yake tukawasilisha sanaa yetu kupitia sauti. Ni vema sasa wasanii wakaliona hili na kuijitanua zaidi kwa upande wa kazi za sanaa.”

Washiriki waliopatikana na kufanikiwa kuingia hatua ya fainali kwa mkoa wa Arusha ni Mathew Philip Mgeni, Dorcas Francis, Halima Hussein, Janeth N Molely na Hilda Kinabo; Zanzibar ni Safiya Ahmed Said, SaiqKuiuiwa Abdalahh, Rukia Hamdan, Imaiu Obeid Fabian na Mohamed Said Mohamed; na Dar es Salaam ni Hilda Malecela, Abraham Richard, Happines Sianslaus ‘Nyamayao’, Richard Rusasa, Emanuel Landey, Coletha Raymond, Jamila na Maisala Abdul;

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: STARTIMES KUWAPAMBANISHA 18 FAINALI ZA SHINDANO LA VIPAJI VYA SAUTI KESHO JIJINI DAR ES SALAAM
STARTIMES KUWAPAMBANISHA 18 FAINALI ZA SHINDANO LA VIPAJI VYA SAUTI KESHO JIJINI DAR ES SALAAM
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjQuoAC_8wYkPXQZD16h31mShNV1InytWMfe6R4RvSDKgOZlTasbH2vUl2v4bA6_dzXZd924vX0isbC6sDiYMgkp4OOq5rOwpC8wf_qWTV_Nk9m25nnDX6nJ40GrQmkOaI4dI_7g-OWNpSb/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjQuoAC_8wYkPXQZD16h31mShNV1InytWMfe6R4RvSDKgOZlTasbH2vUl2v4bA6_dzXZd924vX0isbC6sDiYMgkp4OOq5rOwpC8wf_qWTV_Nk9m25nnDX6nJ40GrQmkOaI4dI_7g-OWNpSb/s72-c/1.JPG
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/09/startimes-kuwapambanisha-18-fainali-za.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/09/startimes-kuwapambanisha-18-fainali-za.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy