Kiwango cha maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi Halmashauri ya Mji Njombe inakadiriwa kuwa ni wastani wa asilimia 14.8% kwa ngazi ya Mk...
Kiwango
cha maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi Halmashauri ya Mji Njombe inakadiriwa kuwa
ni wastani wa asilimia 14.8% kwa ngazi ya Mkoa. Hii ikimaanisha kuwa kwa kila
watu 100, watu 15 wanaishi na VVU.
Akiwasilisha
taarifa ya kiwango cha maambukizi katika Halmashauri ya Mji Njombe Kwa wadau wa
mapambano ya Ukimwi Mkoa wa Njombe, Mratibu wa UKIMWI Katika Halmashauri, Daniel
Mwasongwe amesema kuwa kiwango cha maambukizi ni kibaya.
“Leo
hii tumekutana na ninyi wadau mbalimbali wa mapambano dhidi ya Ukimwi lengo
ikiwa ni kupunguza maambukizi mapya na kuboresha huduma kwa watu wanaoishi na
virusi vya UKIMWI. Tunaamini katika mdahalo huu wa wadau tutatoka na maazimio mazuri
ambayo hayataishia mezani bali tutayapeleka kwenye utendaji ili kuhakikisha
maambukizi mapya hayatakuepo tena, na Halmashauri yetu inaendelea kuwa salama.”
Akifafanua
sababu zinazopelekea kiwango hicho kuendelea Mratibu huyo amesema kuwa sababu
kuu zilizopelekea kiwango hicho kuendelea Ni pamoja Na sababu za Kibaiolojia,
mabadiliko ya kitabia, vichocheo vya Kijamii na masuala ya kiuchumi likihusisha
pia suala la ukosefu wa ajira kwa vijana.
Kwa
upande wake msimamizi wa huduma za wagonjwa nyumbani katika Halmashauri ya Mji
Njombe amesema kuwa kumekuwa na changamoto ya uhaba wa vituo vichache vya
kutolea huduma za dawa jambo ambalo limeleta kero kubwa, kwa watumia dawa
kutokana na kutembea umbali mrefu na kuingia gharama kubwa za usafiri kufuata
vituo vya kutolea dawa na kusababisha kasi ya maambukizi kuendelea na hivyo
wameiomba serikali na wadau kuongeza vituo vya huduma ili kuwezesha upatikanaji
wa dawa maeneo ya karibu.
Ameendelea kusema ipo kasumba ya upande wa
watu waliopima na kugundulika kuwa na maambukizi kutokuwa wafuasi wakubwa wa
dawa na wameitaka jamii kuongeza jitihada za uhamasishaji, utoaji elimu kwa
watumia dawa waendelee kuwa wafuasi wazuri wadawa.
“Wamepima
na wameshaingia kwenye huduma ukweli asilimia kubwa sio wafuasi wazuri wa dawa,
nguvu zote za serikali na hata mdahalo wa wadau wa leo tunawatazama wale ambao
wameshaingia kwenye huduma. Tunataraji kuwa hawa ambao wameshaingia kwenye
huduma wakimeza dawa kwa miongozo mizuri hawatasababisha maambukizi kuhama
kutoka kwa mtu mmoja kwenda mwingine hivyo ni jukumu letu kupitia mdahalo huu
kuongeza jitihada za kuhimiza watu wanaochukua dawa.” Alisema Rustica
Akiwasilisha
salamu za Pongezi kwa serikali Mwenyekiti wa Baraza la watu wanaoishi na
Maambukizi Taifa (NACOPHA) Justine Mwinuka Amesema wanaishukuru serikali ya
Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwani imewapa usahihi na uhalali wa huduma ya
ARV ambao kwao wafuasi wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa.
Aidha
ameendelea kusema kuwa miongoni mwa maazimio ya kitaifa na ambayo halmashauri
imeanza kutekeleza ni pamoja na uundwaji wa baraza la WAVIU ngazi ya
halmashauri lijulikanalo kama KONGA kwa ajili ya utetezi, shuhuda na
uratibisha.
“Tunashukuru
Baraza la Taifa na wenzetu wa TB kwa kuunda mahusiano kutoka ngazi ya Taifa
hadi ngazi ya jamii na ndio maana ndani ya Halmashauri kuna KONGA. Lengo letu
ni kuhakikisha kuwa kila palipo na
mkusanyiko wa kiutendaji wa serikali na sisi sauti ya WAVIU na TB tunakuwepo
ndani yake kwa ajili ya kuisaidia serikali kupanga mipango yake kupitia shuhuda
tulizo nazo sisi tuliosaidiwa lakini pia kuwashawishi wadau mbalimbali ambao
wamekua kwenye mapambano haya.”Alisema Mwinuka.
Mwinuka
alisema kuwa kumekuwa na unyanyapaa mkubwa na ukosefu wa ushirikiano katika
ngazi za vijiji, mitaa na kata na hii husababishwa na pale mabaraza haya
yanapotaka kutoa elimu na shauhuda kwa
umma na amewataka wadau kuendelea kuutoa
elimu kwa jamii ili kuondoa unyanyapaa
uliopo ngazi ya jamii. Wengi wamekuwa na mila potofu kufanya ngono isiyo salama
lakini hii yote inasababishwa na inasababishwa na uduni wa elimu. Hivyo ni
vyema jamii ikaendelea kupatiwa elimu zaidi ya unyanyapaa.
Miongoni
mwa Maazimio ambayo wadau hao waliafikiana kuyatekeleza ni pamoja na
kuhakikisha kunakuwepo na vikao vya wadau mara kwa mara katika kubadilishana
uzoefu juu ya changamoto wanazokabiliana nao, uimarishaji wa Kamati za UKIMWI za
vijiji ili kuhakikisha zinafanya kazi na kufikia malengo ya kufikisha huduma
kwa jamii, na kuhakikisha kuwa elimu ya mabadiliko ya tabia kwa jamii inaendelea
kutolewa katika jamii zetu tunazoziudumia.
Licha
ya kuwa Halmashauri ya Mji Njombe kuendelea kuongoza jitihada mbalimbali
zimekua zikifanyika ikiwa ni pamoja na kuwaleta wadau mbalimbali wa mapambano
dhidi ya UKIMWI kujadili changamoto ili kuhakikisha maambukizi mapya ya VVU
yanapungua na mwishowe kuisha.Wadau waliokutana katika mdahalo huo ni pamoja na
TUNAJALI,JHPIEGO,PSI,SHISO,HIGLANDHOPE,JSI,NJODINGO,KONGA,COCODA,IMO,BAYLOR,URC,MDH,TAASISI
ZA KIDINI NA VYOMBO VYA HABARI.
Imetolewa na,
Hyasinta Kissima
Afisa
Habari-Njombe TC.
COMMENTS