MRADI WA GREEN VOICES UMEONYESHA MAFANIKIO, UTAWAKOMBOA WANAWAKE TANZANIA

Makamu wa Rais mstaafu wa Hispania na Rais wa Taasisi ya Women for Africa Foundation, Mama Maria Tereza Fernandez de la Vega, aki...


Makamu wa Rais mstaafu wa Hispania na Rais wa Taasisi ya Women for Africa Foundation, Mama Maria Tereza Fernandez de la Vega, akisalimiana na maofisa wa ulinzi na usalama mara baada ya kuwasili katika bandari ya Nansio, Ukerewe hivi karibuni kuzindua mradi wa kilimo cha viazi lishe unaofadhiliwa na taasisi yake ya inayoshughulikia maendeleo ya Wanawake wa Afrika.
Mama Getrude Mongella (waliosimama katikati mwenye blauzi nyekundu) akifafanua jambo kwa Mkamu wa Rais mstaafu wa Hispania na Rais wa Taasisi ya Women for Africa Foundation, Mama Maria Tereza Fernandez de la Vega, wakati walipotembelea mradi wa kilimo cha viazi lishe wilayani Ukerewe. Kushoto kwa Mama Mongella ni Bi. Leocadia Vedastus, ambaye ni mshiriki kiongozi wa mradi huo.
Makamu wa Rais mstaafu wa Hispania na Rais wa Taasisi ya Women for Africa Foundation, Mama Maria Tereza Fernandez de la Vega, akiangalia bidhaa zilizo mbele yake ambazo zinatokana na viazi lishe katika kuongeza mnyororo wa thamani. Hii ni wakati alipokwenda kuuzindua mradi huo wilayani Ukerewe katika Mkoa wa Mwanza.

MRATIBU wa mradi wa akinamama wapambanao na mazingira wa Green Voices, Alicia Cebada, amesema kwamba wamefarijika na mradi huo kwa kuwa umeonyesha mafanikio makubwa nchini Tanzania.
Akizungumza wakati wa kuhitimisha ziara yao ya kutembelea miradi mitano kati ya 10 inayotekelezwa na wanawake wa Tanzania,hivi karibuni mratibu huyo kutoka taasisi ya Women for Africa Foundation, alisema hawakutegemea kama miradi waliyoianzisha akinamama hao ingeweza kufanikiwa katika kipindi kifupi tangu kuwapatia mafunzo.
“Ni kipindi kifupi tangu wanawake hawa walipopatiwa mafunzo nchini Hispania, lakini kwa hakika miradi waliyoibuni imeonyesha mafanikio, ni endelevu, rafiki wa mazingira na italeta tija kwao na taifa kwa ujumla,” alisema Alicia.
Aidha, alieleza kwamba, changamoto pekee ambayo ipo mbele yao ni kuhakikisha miradi hiyo inasimama na kuwafundisha wanawake wengi kadiri wawezavyo ili kuhakikisha wanajiletea maendeleo katika maeneo yao kiuchumi na kijamii.
“Tumewaona wanawake wa Ukerewe wanavyolima viazi lishe na kuongeza mnyororo wa thamani, tumewaona wanawake wa Kijiji cha Kitanga huko Kisarawe wakiongozwa na ‘Malkia wa Muhogo’ Abia Magembe, tumewatembelea akinamama wanaofuga nyuki kupambana na ukataji wa misitu huko Kisarawe, pia tumewaona wanawake wa Morogoro namna wanavyokausha mboga na kuwa na uhakika wa akiba ya chakula, na hapa (Bunju) tumeshuhudia jinsi kilimo cha uyoga kilivyo na faida, ni miradi mizuri, endelevu na rafiki mkubwa wa mazingira,” alisema.

Alicia Cebada na Anna Salado wakiangalia namna ya mifuko ya kupandikizwa uyoga inavyohifadhiwa kwenye mapipa wakati walipotembelea kilimo cha uyoga Bunju hivi karibuni.

Picha ya pamoja na akinamama wafugaji nyuki katika misitu ya Pugu na Kazimzumbwi wilayani Kisarawe.

Alicia alisema kwamba, taasisi yake inaangalia uwezekano wa kuwaongezea nguvu akinamama wa Green Voices katika awamu ya pili ya mradi baada ya kuridhishwa na mafanikio ya majaribio ili waweze kukabiliana na changamoto walizonazo.
Hata hivyo, aliipongeza serikali ya Tanzania kwa kuunga mkono mradi huo na akasema hiyo inawapa nguvu hata wanawake wanaoshiriki na ni dalili njema kwamba wengi wanaweza kujifunza na kuitekeleza miradi kama hiyo na kubuni mingine yenye manufaa kwa jamii.
“Tumeona jinsi serikali ilivyo bega kwa bega na wanawake hawa katika sehemu zote tulizotembelea, hii inaonyesha kwamba miradi waliyoibuni siyo yao pekee bali ya jamii nzima na itawahamasisha wanawake wengi zaidi kujifunza na kuitekeleza katika maeneo yao,” alisema.
Kauli ya Alicia imekuja muda mfupi baada ya rais wa mfuko huo, Mama Maria Tereza Fernandez de la Vega kuzuru nchini kushiriki uzinduzi wa mradi huo Julai 11, 2016 ambapo ulizinduliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan.
Mama Samia aliahidi wakati wa uzinduzi kwamba serikali yake itahakikisha inakuwa bega kwa bega kusaidia miradi hiyo iwe endelevu ili kuunga mkono juhudi za utunzaji wa mazingira na kupambana na mabadiliko ya tabianchi, kuongeza uhakika wa chakula, kuwakwamua wananchi na umaskini pamoja na kuongeza ajira, hasa kwa wanawake.
Kwa upande wake, Mama Maria Tereza, ambaye ni makamu wa rais mstaafu wa Hispania, alieleza kufurahishwa kwake na jitihada za akinamama wa Tanzania na kusema kwamba taasisi yake inaangalia namna ya kuwasaidia zaidi.
“Tumefarijika sana na jitihada hizi, tumesikia changamoto zinazowakabili na tutaangalia namna gani ya kuwasaidia kuzikabili katika awamu ya pili ya mradi huu wa Green Voices,” aliwaeleza akinamama wa Ukerewe mbele ya wananchi waliokusanyika katika eneo la Shule ya Bukongo.
Mkurugenzi wa ubunifu wa taasisi hiyo, Noellia, aliwapongeza wanawake wanaotekeleza miradi hiyo kupitia Green Voices na kuwataka waendelee kushikamana ili kusonga mbele huku akiwapa moyo kwamba changamoto zilizopo zinaweza kutatuliwa.
Noellia alisema kwamba, kuonekana kwa changamoto ni dalili njema kwamba kumbe miradi hiyo inatekelezeka ikiwa changamoto hizo zitafanyiwa kazi.
“Kama unabaini vikwazo basi ni dalili kwamba kumbe vikifanyiwa kazi unaweza kusonga mbele, msikate tamaa,” alisema wakati alipozungumza na wanawake wafuga nyuki wilayani Kisarawe.
Naye mkurugenzi wa mawasiliano wa taasisi hiyo, Ana Salado, alipongeza namna vyombo vya habari vilivyojitahidi kuripoti mafanikio ya wanawake hao na kusema kwamba hali hiyo imesaidia kuihamasisha jamii kushiriki kutokana na ukweli kwamba miradi yote iliyobuniwa na akinamama hao ina tija kwa taifa zima.
Jumla ya wanawake 15 wa Tanzania walipatiwa mafunzo ya wiki mbili jijini Madrid, Hispania mapema mwaka huu ambapo 10 kati yao walikwenda kuanzisha miradi mbalimbali wakati watano ni wanahabari ambao wamekuwa wakiripoti maendeleo ya miradi hiyo.
Mratibu wa mradi wa Green Voices nchini Tanzania, Bi. Secelela Balisidya, amesema kwamba mradi huo unatekelezwa katika mikoa sita ya Tanzania Bara ambayo ni Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Kigoma, Mwanza na Kilimanjaro.
Anawataja wanawake walioanzisha miradi hiyo – miradi na mikoa watokayo vikiwa kwenye mabano – kuwa ni Regina Kamuli (Mkuranga, Pwani – Majiko Banifu), Abiah Magembe (Kisarawe, Pwani – Usindikaji wa Muhogo na Mtama), Magdalena Bukuku (Kinondoni, Dar es Salaam – Kilimo cha Uyoga), Mariam Bigambo (Dakawa, Morogoro – Ufugaji wa Nyuki), na Esther Muffui (Morogoro – Ukaushaji wa Mboga na Matunda).
Wengine ni Farida Makame (Kilimanjaro – Majiko ya Umeme-Jua), Leocadia Vedastus (Ukerewe, Mwanza – Kilimo na Usindikaji wa Viazi Lishe), Monica Kagya (Kisarawe, Pwani – Ufugaji wa Nyuki), Sophia Mlote (Kinyerezi, Dar es Salaam – Kilimo Hai cha Nyanya na Mbogamboga), na Evelyn Kahembe (Uvinza, Kigoma – Kilimo cha Matunda).
Kupitia miradi hiyo, zaidi ya wanawake 300 wamepatiwa mafunzo mbalimbali huku program nyingine za mafunzo kwa vitendo zikiendelea katika makundi yao.

Anna Salado akifurahi pamoja na akinamama wa Kijiji cha Kitanga wilayani Kisarawe. Wanawake hao wanajihusisha na mradi wa usindikaji wa muhogo na mtama.

Naibu Meya wa Manispaa ya Morogoro, Milikieli Mansweat Mahiku, naye aliongozana na viongozi wa taasisi ya Mfuko wa Wanawake Afrika, Anna Salado (kushoto) na Alicia Cebada (wa pili kulia) kukagua kilimo cha mboga mboga katika Kata ya Mzinga kwenye manispaa hiyo. Wa tatu kushoto ni Mratibu wa Mradi wa Green Voices Tanzania, Secelela Balisidya, na aliyeinama ni mshiriki kiongozi wa mradi wa ukaushaji mboga na matunda wa Mzinga, Esther Muffui.

Kuendelea kwa miradi hiyo kumeonyesha dalili njema hasa baada ya serikali kuahidi kuiendeleza kwa kushirikiana na wanawake hao, ikiwa ni pamoja na kuangalia fedha za maendeleo kupitia mfuko wa wanawake na vijana katika kila halmashauri.
Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Estomih Chang’a, alikwenda mbali zaidi baada ya kuwashauri wananchi wa wilaya hiyo kujikita katika kilimo cha viazi lishe ili kuongeza akiba ya chakula na kukabiliana na baa la njaa.
“Ninashauri wananchi wote wa Ukerewe kulima viazi lishe kwa sababu mbali ya kuongeza akiba ya chakula, lakini vinaongeza pato la familia na taifa hasa vikichakatwa ili kutoa bidhaa mbalimbali,” alisema.
Naye mjumbe wa bodi ya taasisi hiyo, Balozi Getrude Mongella, akizungumza katika uzinduzi huo kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Bukongo mjini Nansio, aliwaomba watendaji wa serikali kusimamia kidete mradi huo ili kuondoa njaa katika visiwa vyote vya wilaya ya Ukerewe.
Alisema kwamba, kuanzishwa kwa mradi huo wilayani humo siyo tu kutawakwamua wanawake na wananchi wote, lakini pia kunaifanya Ukerewe kuwa kiini cha usambazaji wa zao hilo katika maeneo mengine ya Mkoa wa Mwanza.
“Ninawaomba watendaji wa serikali ya wilaya hamasisheni zao hili lilimwe katika visiwa vyote na kama ilivyokuwa zamani ambao mbegu zote za pamba zilitoka Ukerewe, basi tengenezeni na zalisheni mbegu za kutosha msambaze katika wilaya nyingine za Mkoa wa Mwanza.
“Naamini mkoa wote ukilima zao hili njaa haitakuwepo na wanawake wanaweza kutengeneza bidhaa mbalimbali ambazo wakiziuza zitawakwamua kiuchumi,” alisema.
Naye Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mh. Selemani Jaffo, ambaye pia ni Mbunge wa Kisarawe, amesema yuko tayari kushirikiana na wanawake wanaosindika muhogo katika Kijiji cha Kitanga pamoja na wilaya nzima ya Kisarawe kuhakikisha wanajikwamua kiuchumi kutokana na zao hilo.
Aidha, Naibu Meya wa Manispaa ya Morogoro, Milikieli Mansweat Mahiku, alisema atahakikisha anasimamia kwa bidii ili teknolojia ya ukaushaji wa mboga na matunda isambae kwa wanawake wote wa manispaa hiyo.
Aidha, aliahidi kwamba, yeye na madiwani wenzake watahakikisha asilimia 10 ya fedha za maendeleo katika halmashauri wanapatiwa wanawake na vijana wanaofanya miradi endelevu yenye tija na inayolenga kutunza mazingira kama wanavyofanya wanawake hao wa Mzinga.
“Sasa hivi bajeti ya maendeleo ya halmashauri imeongezwa hadi asilimia 60, sasa kati ya fedha hizo, asilimia 10 ni miradi ya wanawake na vijana, ambayo kama tutaisimamia vyema na kuielekeza kwenye miradi endelevu kama hii italeta tija.
“Kama wahisani hawa wamejitokeza na wamekuja kutoka Hispania, sisi kama serikali nasi tunapaswa kuunga mkono jitihada hizi ambazo zina tija kubwa,” alisema Naibu Mstahiki Meya.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: MRADI WA GREEN VOICES UMEONYESHA MAFANIKIO, UTAWAKOMBOA WANAWAKE TANZANIA
MRADI WA GREEN VOICES UMEONYESHA MAFANIKIO, UTAWAKOMBOA WANAWAKE TANZANIA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgPPhOh_NuVVV8T5JV1JSlMsxSin3mwSZ7p_IDQpfEWAokXrdDVFXojL4uOqbSWc31k02FfNje1X3yCgNIK6GxFxYeiDnSftEc1Kd_IqHvHxW2Ko7SqKZz13wZHCNYK9nfmgCVlaGvqbTdh/s640/20160712_124736.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgPPhOh_NuVVV8T5JV1JSlMsxSin3mwSZ7p_IDQpfEWAokXrdDVFXojL4uOqbSWc31k02FfNje1X3yCgNIK6GxFxYeiDnSftEc1Kd_IqHvHxW2Ko7SqKZz13wZHCNYK9nfmgCVlaGvqbTdh/s72-c/20160712_124736.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/mradi-wa-green-voices-umeonyesha.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/mradi-wa-green-voices-umeonyesha.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy