Waziri Nape akiwasilisha WADAU wa habari leo wanaanza kuujadili muswada wa sheria ya huduma za habari huku wabunge wakisema ...
Waziri Nape akiwasilisha |
WADAU
wa habari leo wanaanza kuujadili muswada wa sheria ya huduma za
habari huku wabunge wakisema jambo hilo linahitaji
mjadala mrefu ili
kulinda maslahi mapana ya tasnia ya habari na
wanahabari nchini.
Wakizungumza jana mara baada ya Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa
na Michezo, Nape Nnauye kuwasilisha hati ya muswada
huo mbele ya
kamati ya kudumu ya bunge ya huduma na maendeleo
ya Jamii baadhi ya
wabunge walitaka waandishi wa habari kama wadau
muhimu washiriki kutoa
maoni yao kwenye kamati hiyo ya bunge.
Mbunge wa Buyungu ,Kasuku Billago (Chadema),
alisema muswada huo
umekuja kwa wakati muafaka na kuwataka
waandishi wa habari kukomaa
katika suala linalohusu.
“Haki nyingi za waandishi wa habari hazijaelezwa
kwenye muswada huo,
suala lingine la kuhoji ni nani mwenye mamlaka ya
kufuta chombo cha
habari kwani kosa moja linafanya chombo kizima
kifungiwe” alisema
Alisema chombo ni taasisi kinatoa ajira na
adhabu iwe inalenga kwa
aliyetenda kosa.
“ Chombo ni taasisi inayotoa ajira aadhibiwe mtu
sio taasisi ili
kuwezesha taasisi husika kuendelea kuwepo kuna
watu maisha yao
yanakuwa mle mnapofungua hata familia
zinaathirika” alisema
inahitaji linatakiwa kufanyika kwa umakini mkubwa
kwani serikali
imekuja na lengo jema lakini kuna vitu ambavyo
vinatakiwa kujadiliwa
kwa kina ili kuwe na tija kwa kila upande wenye
maslahi.
Mbunge wa Chemba Juma Nkamia alisema unahitajika
mjadala mrefu sio
jambo la kukurupuka.
“Serikali imekuja na lengo jema ila kuna vitu
ambavyo vinatakiwa
kujadiliwa kwa kina “ alisema
Alisema kwa mtazamo wake kama muda hautoshi
haiwezi kuzuia wadua kutoa maoni.
“Sio lazima kitu kiletwe leo na kupita, unaweza
kufutwa pia ukatetwa
tena kwa majadiliano ya kina” alisema
Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe aliwataka
waandishi wa habari
kama wadau muhimu kushiriki kutoa maoni yao.
“Kama mwandishi wa habari ukikatazwa kuingia
kwenye kamati kusikiliza
majadiliano ingia kama mdau ili uweze kutoa maoni
yako, maoni yenu ni
muhimu sana katika muswada huu” alisema
Hoja hizo za wabunge zimekuja baada ya Waziri Nape
kuwasilisha hati ya
muswada huyo kwa kamati ya bunge ya huduma
na maendeleo ya jamii,
alisema lengo la muswada huo ni kuweka masharti ya
kukuza na
kuimarisha taaluma na weledi katika tasnia ya
habari nchini pamoja na
kuundwa kwa bodi ya ithibati ya wanahabari,Baraza
huru la habari
pamoja na kuweka mfumo wa usimamizi wa huduma za
habari.
Nape alisema Muswada wa sheria ya huduma za habari
umeandaliwa ili
kukabiliana na changamoto mbalimbali zilizopo
katika tasnia ya habari
nchini ambazo ni pamoja na upungufu wa sheria
zinazosimamia tasnia ya
habari na mabadiliko ya teknolojia ya habari.
Pia alisema changamoto ya kutokuwepo kwa udhibiti
wa mzuri na
usimamizi madhubuti ya viwango kwenye taaluma ya
habari na utangazaji
kumechangia madhila kwa jamii ikiwemo kuandikwa
habari za
upotoshaji,zinazokiuka maadili na zinazoweza
kusababisha
chuki,machafuko na uvunjifu wa amani.
‘’Hivyo kuifanya serikali na wadau wengi wengine
kuona umuhimu wa kuwa
na sheria kama hii itakayoainisha bayana sifa na
viwango vya kitaaluma
katika tasnia ya habari.kukamilika kwa sheria hii
kutapanua wigo kwa
wananchi kupata haki yao ya kikatiba yak upata
habari’’alisema
Nape alisema kutokana za muingiliano wa teknolojia
mwaka 2003 serikali
iliona kuna umuhimu wa kuunganisha vyombo hivi
viwili Tume ya
Mawasiliano na tume ya Utangazaji ili kuleta
ufanisi wa usimamizi wa
sekta na utoaji wa huduma bora kwa walaji.
‘’Kwa ujumla sekta hii changamoto kubwa ni taaluma
ya habari
kutotambulika kama taaluma kamili inayopaswa
kuheshimiwa,kukosekana
vyombo madhubuti na huru vya usimamizi na
badala yake mambo mengi
kuwa chini ya serikali moja kwa moja’’alisema
Pia alisema changamoto nyingine ni wadau wa habari
kutoshirikishwa
kikamilifu katika utungwaji wa sheria zilizopo
hivyo kutokidhi matakwa
ya wadau katika sekta ya habari.
‘’Sheria hii inaleta mageuzi makubwa katika
usimamizi wa sekta ya
habari hapa nchini ni sheria mabyo inakwenda kwa
mara ya kwanza katika
historia ya nchi yetu,kuifanya rasmi sekta ya
habari kuwa sekta
rasmi’’
Aidha alisema ushahidi uliowazi kwamba waliowengi
wamekuwa waathirika
wa kadhia ya uandishi usiozingatia maadili na
weledi wa taaluma ya
habari na utangazaji kwa kukashifiwa au kuzushiwa
taarifa zisizokuwa
na ukweli wowote.
Alisema mapendekezo yaliyomo katika sheria ya
habari kwa kiasi kikubwa
yamelenga kutatua changamoto ya kuwa na wanahabari
waliosomea kazi yao
na ambao waewekeana wao wenyewe maadili ya kufuata.
Pia alisema changamoto ya kukuwa kwa teknolojia ya
habari na
utangazaji kumefanya sheria zilizokuwa
zikisimamia tasnia ya habari
na utangazaji kupitwa na wakati na kutoendana na
‘’Ni sheria itakayoleta mifumo ya kisasa ya
usimamizi na ni mifumo
ambayo inaweza kugusa au kubadili namna
tutakavyotenda na
tunavyofikiria sasa,niwaombe wanatasnia wenzangu
tuwe tayari kwa
mabadiliko ili taaluma yetu iheshimiwe na
sisi wenyewe tuheshimike
zaidi’’alisema
Nape alisema serikali imeona kwa sasa ni muhimu
kuwa na sheria ambayo
itakidhi pia matakwa ya Matumizi ya Teknolojia
katika sekta ya habari.
‘’Hivi sasa magazeti ambayo yalikuwa yakitolewa
kwa njia ya nakala
ngumu kwa sasa yanaweza kutolewa njia ya mtandao
wa internet na
wananchi wanawe kuyasoma katika mfumo huo’’alisema
Nape alisema mambo muhimu na matokeo ya sheria
inayopendekezwa
kutungwa ni kama kuwepo kwa sheria inayoendana na
sera ya habari na
utangazaji, kuwepo kwa mfumo madhubuti ya kisheria
wenye kukidhi
mahitaji katika eneo la usimamizi na uendeshaji wa
taaluma ya uandishi
wa habari na utangazaji.
Alisema sheria hiyo inaleta mageuzi makubwa katika
usimamizi wa sekta
ya habari hapa nchini.
Ni sheria ambayo inakwenda kwa mara ya nkwanza
katika historia ya nchi
yetu, kuifanya sekta ya habari kuwa taaluma kamili
Source: Sifa Lubasi
COMMENTS