SERIKALI KUZIBA PENGO LA WAHADHIRI WAANDAMIZI NCHINI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia kwenye kilele cha Maadhiisho ya miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam  kwenye ukumbi wa Nk...

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia kwenye kilele cha Maadhiisho ya miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam  kwenye ukumbi wa Nkurumah jijini Dar es salaam Oktoba 25, 2016.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


*Waziri Mkuu ataka vyuo viweke utaratibu bayana wa kurithishana kazi

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itaendelea kutafuta fedha
za mafunzo kwa ajili ya wahadhiri wa vyuo vikuu nchini ili kuziba
pengo la wahadhiri waandamizi lililopo hivi sasa lakini pia amevitaka
vyuo hivyo viweke utaratibu wa kuachiana nafasi ama kurithishana kazi
(succession plan).

Amesema yeye binafsi anatambua upungufu uliopo umesababishwa na
masharti ya ajira za mkataba kwa wahadhiri waandamizi kuwa miaka 65 na
maprofesa kuwa miaka 70.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumanne, Oktoba 25, 2016) wakati akifunga
kilele cha maadhimisho ya miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
yaliyoanza jana kwenye ukumbi wa Nkrumah. Kampasi ya Mwalimu J. K.
Nyerere, jijini Dar es Salaam.

“Ninatambua kuwa katika vyuo vya umma kuna upungufu mkubwa wa
wahadhiri waandamizi na maprofesa na hivyo kuathiri hali ya utoaji wa
taaluma kwa fani za ‘Post-Graduates’. Ninajua kuwa pamoja na sababu
nyingine, hali hii inachangiwa pia na masharti ya ajira za mikataba
kwa wahadhiri waandamizi kuwa miaka 65 na maprofesa kuwa miaka 70.
Serikali itaendelea kuweka kipaumbele cha upatikanaji wa fedha za
kutosha kwa ajili ya mafunzo,” amesema.

“Lakini vyuo vya elimu navyo havina budi kuweka taratibu na mipango
endelevu ya kurithishana (kuachiana nafasi) ‘Succession Plan’. Jambo
hii ni muhimu sana kwani bila hivyo, wakati wote kutakuwa na pengo
kubwa katika utoaji wa taaluma,” amesisitiza.

Amesema Serikali itatoa ushirikiano wa kutosha katika utekelezaji wa
mipango hii ya kuwa na watalaamu wa kutosha katika vyuo huku
ikiendelea kutekeleza majukumu ya kuwaajiri wanataaluma na wafanyakazi
wapya pale wanapohitajika.

Akizungumzia kuhusu maslahi ya watumishi wa vyuo hivyo, kikiwemo Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam, Waziri Mkuu amesema Serikali ya awamu ya tano
imedhamiria kuhakikisha inaondoa malimbikizo ya madai kwa watumishi
wote wa umma na hivi sasa inakamilisha uhakiki wa taarifa za
kiutumishi kwa watumishi wa umma ili kubaini watumishi hewa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongozana na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Profesa  Rwekaza Mukandala  (kulia  kwake) kuelekea kwenye ukumbi wa Nkurumah baada ya kuwasili kwenye Chuo Kikuu cha Dar es salaam kuhutubia kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 55 ya Chuo hicho Oktoba 25, 2016. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Ally Happy, kushoto ni Rais wa  Jumuiya ya Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Jaji Joseph Warioba na wapili kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekinoloji, Dkt. Leonard Akwilapo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Rais wa Jumuiya wa Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Jaji Joseph Warioba baada ya kuhutubia kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 55 ya chuo hicho kwenye ukumbi wa Nkurumah jijini Dar es salaam Oktoba 25, 2016.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Kitabu Kiitwacho  From Lumumba  Street to the Hill and Beyond katika kilele cha  Maadhimisho ya Miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es salaa baada ya kuhutubia kwenye ukumbi wa Nkurumah jijini Dar es salaam  Oktoba 25, 2016. Katikati ni Makamu Mkuu wa CHuo Kikuu cha Dar es salaam, Profesa Rwekaza Mukandala  na kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Dkt Leonard Akwilapo.

“Hadi kufikia tarehe 20 Oktoba, 2016 zoezi linaloendelea hivi sasa,
limesaidia kuwabaini watumishi wa umma hewa wapatao 16,500. Baada ya
zoezi hilo, tutarudia uhakiki wa madeni yote yaliyowasilishwa
Serikalini na kisha tutalipa madeni ya watumishi wote,” amesema.

“Ninafahamu kuwa yapo madai mbalimbali ikiwemo malimbikizo ya
mishahara kwa watumishi hususan baada ya kuanza kwa muundo wa pamoja
wa wanataaluma wa vyuo vikuu vya umma. Serikali inaendelea na
maboresho na kuimarisha maslahi kwa watumishi wote wa umma kupitia
bodi ya mishahara na motisha; na mara tutakapokamilisha, tutapanga
upya mishahara na motisha kwa watumishi,” amesema.

Akifafanua kuhusu mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu, Waziri Mkuu
amesema Serikali inaendelea kufanya uhakiki wa taarifa za waombaji wa
mikopo. Ametoa wito kwa wanufaika na waombaji wote wa mikopo
wahakikishe kuwa wanatoa taarifa zilizo sahihi na za uhakika.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema Serikali ilikwishaongeza bajeti ya
mikopo ya elimu ya juu kutoka sh. bilioni 340 mwaka 2015/2016 hadi sh.
bilioni 483 kwa mwaka 2016/2017.

Mapema, akielezea utendaji kazi wa chuo hicho katika miaka yote 55,
Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Rwekaza Mukandala amesema chuo hicho
kinakabliwa na changamoto ya uhaba wa wanataaluma waandamizi wa fani
mbalimbali.

“Chimbuko la changamoto hii ni kusitishwa kwa ajira katika taasisi za
umma kwenye miaka ya 1990. Kutoajiriwa kwa wanataaluma chipukizi kwa
miaka mingi, kulivuruga utaratibu wa miaka mingi wa kurithishana
uzoefu baina ya wanataaluma wanaostaafu na wale ambao wangelichukua
nafasi zao,” amesema.

“Hali hii iko kwenye vyuo vikongwe ambako mamia ya wanataaluma wazoefu
wanastaafu kwa wakati mmoja na wengi wa wanataaluma walioajiriwa hivi
karibuni bado wako masomoni au wangali chipukizi katika taaluma zao na
hivyo hawana uwezo wa kutosha kubeba majukumu ya kufundisha katika
ngazi za digrii za umahiri na uzamivu,” amesema.

Hata hivyo, ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha za kuwadhamini
wahadhiri chipukizi ambao wako sehemu mbalimbali wakipata mafunzo. Pia
amemshukuru Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa uamuzi wake wa kujenga
hosteli yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi zaidi ya 3,800 na hivyo
kutarajiwa kupunguza tatizo la malazi.

Wakati huohuo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na
Teknolojia, Dkt. Leonard Akwilapo alisema wizara hiyo imetenga kiasi
cha sh. bilioni 9 kwa ajili ya kufanya ukarabati wa miundombinu kwenye
chuo hicho zikiwemo maabara.

(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 - DAR ES SALAAM
JUMANNE, OKTOBA 25, 2016.
https://ssl.gstatic.com/ui/v1/icons/mail/images/cleardot.gif

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: SERIKALI KUZIBA PENGO LA WAHADHIRI WAANDAMIZI NCHINI
SERIKALI KUZIBA PENGO LA WAHADHIRI WAANDAMIZI NCHINI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj0hCsrAu1bHhTJK8yo6wqm-BVkEty9tP8mD_qXVoMyh6fL4sJ-bHl4he2t_igWUGBtJaan4qHAmgOkD-4-ULK_26SpSCVZARwhddpkuwgrC5iSt6z53gYaQtWFDEDk_Md2rV6rHdP18GQ/s320/hotubia.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj0hCsrAu1bHhTJK8yo6wqm-BVkEty9tP8mD_qXVoMyh6fL4sJ-bHl4he2t_igWUGBtJaan4qHAmgOkD-4-ULK_26SpSCVZARwhddpkuwgrC5iSt6z53gYaQtWFDEDk_Md2rV6rHdP18GQ/s72-c/hotubia.JPG
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/serikali-kuziba-pengo-la-wahadhiri.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/serikali-kuziba-pengo-la-wahadhiri.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy