Stiletto:Sinema ya mwaka 2008 lakini naihusudu sana

KUNA baadhi ya sinema ukizitazama ni lazima urejee tena na safari hii nimerejea tena kuangalia Stiletto. Hii sinema ina utamu wake kw...



KUNA baadhi ya sinema ukizitazama ni lazima urejee tena na safari hii nimerejea tena kuangalia Stiletto.
Hii sinema ina utamu wake kwa kuwa ina mambo ambayo huwezi kuamini kwamba huwatokea binadamu.
Mambo hayo ambayo huwa ni sumu kali katika maisha yameoneshwa na kufuatiliwa sana katika sinema hii ambapo staa wake mkubwa ni Tom Berenger na mdada Raina (Stana Katic).
Ndani ya  filamu hii unaanza kwa kuona mauaji katika mkutano wa watu wawili katika sauna.
Mmoja wa hawa anapigwa kisu (stiletto kwa maana halisi)  anapona na kukimbizwa hospitalini na kuamka baadaye akisema kwamba aliyefanya mauaji hayo ni mpenzi wake.
Mpaka unapomaliza sinema hii unakuwa unahema kama wewe si mtu wa kupenda masikhara ya kuona damu au kuona ubamizaji usiokuwa wa kawaida na tabia za uwehu.
 Nini stori yake: Ukianza unaweza kabisa usijue hii ni stori ya aina gani lakini unapomuona Tom Berenger unajua moja kwa moja kwamba hii ni sinema ya gangstar.
Unajua hivi kwa kuwa muziki na aina ya mazungumzo yanagusia ujahili wa aina fulani wa magenge makubwa ya chini kwa chini, magenge ambayo yanashindana katika biashara huku yakiwa na ubabe wa juu kiasi cha kutishia hata mwenendo wa serikali.
Wakati Tom Berenger akicheza kama Virgil Vadalos  akizungumza na tajiri moja la Kigiriki kiongozi wa kundi la mafia anaingia na kumchinja huyu mwingine na kisu na anapojitokeza tunamuona kwamba ni msichana.
Vadalos akizubaa naye anajikuta  akichomwa kisu cha tumbo na mdada huyo huyo ambaye ama hakika alikuwa mpenzi wake.
Mdada Raina aliua na kuondoka lakini Vadalos anaponea tundu la sindano na hapa ndipo picha linapoanza.
Nasema ndipo picha linapoanza kwa kuwa wakati wa upelelezi wanajaribu kujua nani anafanya mauaji ya watu wa magenge,Vadalos anataka mshikaji wake wa zamani Raina atafutwe kwa kuwa yeye ndiye aliyekuwa anahusika na mauaji hayo.


Filamu hii iliyoongozwa na Nick Vallelonga ni moja ya filamu ambayo utapenda kuiangalia kwa kuwa uwongo wake na utamu kolea unakaribia na ukweli kwa wale wanaojua ukweli wa sinema.
Stiletto hii ya mwaka 2008  ambayo ni picha ya kimarekani pamoja na akina Stana na Tom Berenger wapo pia Michael Biehn, William Forsythe, na Tom Sizemore.
Filamu hii ambayo ilionwa kwa mara ya kwanza katika tamasha la sinema la kimataifa la  Newport Beach Aprili 28, 2008 na kuachiwa katika DVD Machi 3,2009 imetengenezwa katika mazingira ambayo raha yake ni kuona kuchachawa kwa Raina, aina yake ya mauaji na jinsi wanaume walivyo viumbe dhaifu.
Virgil  pamoja na kuagiza watu wake pamoja na askari mmoja mpenda rushwa wamsake mdada huyo ambaye aliwaarifu kuwa ni mpenzi wake wa zamani,  alikuwa anashangazwa na kasi ya mauaji ya Raina na sababu zake.
Hakuwa anaua katika kundi lake tu bali aliwachanganya .
Hapakuwepo na maelezo wala akili kwamba kwa nini Raina anaua hovyo kwenye makundi yanayopingana. Pamoja na mambo kuonekana ya hovyo Virgil anajikuta akihamanika kutokana na kupotea kwa dola za Marekani milioni 2.
Wasaidizi wakubwa wawili wa Virgil Lee (Biehn) na  Alex (Forsythe) wanajikuta wanatiliana shaka kuhusu kupotea kwa fedha hizo.
Mauaji ya Raina, baadaye unayagundua kwamba yalikuwa ni kuwashughulikia watu waliomfanyia ndivyo sivyo katika maisha yake.
Anawasaka watu hawa, anaonesha urafiki wa kurudiana na kisha anawaua katika furaha zao. Watu hawa walikuwa wakitoka katika makundi mbalimbali na hivyo kusababisha taharuki kubwa ndani ya makundi hayo wakishindwa kuelewa nani anawapa  wakati mgumu.


Kiukweli wakati anaua mmoja baada ya mwingine mchakato wake wa kwenda kumalizia kazi yaani ya kumuua Virgil ulikuwa unazidi kujisogeza.
Filamu hii unatakiwa kuiangalia vizuri sana kwani  njia nzima utafanyiwa kujua kwamba Raina anafanya vile kwa watu ambao wamemdisi lakini baadaye unaweza kuoanisha mawazo yako na kisasi.
Katika vurugu za kulipiza kisasi cha kuuawa kwa dada yake anagundua  kitu kibaya na ambacho kinamfanya ajiulize kwa nini alikuwa na imani kubwa na shughuli zake alizokuwa akizifanya na kuzitekeleza.
Raina (Stana Katic) kiukweli  alikuwa anampenda sana Virgil Vadalos (Berenger) hadi pale alipogundua kwamba yeye ndiye aliyehusika na kupotea kwa dada yake.
Kuanzia hapo akaamua basi, na kuapa kwamba atawaondoa Virgil na kundi lake  lote.
Akiwa hana kingine zaidi ya kisu na hasira, ndipo Raina anapoingia katika bafu na kufanya mambo yale, kisha taratibu akaingia katika ngazi za juu  za magenge hayo huku akipanda kwa kasi katika namna anavyoua akitumia kisu.
Virgil alijua kwamba si rahisi sana kumkomesha muuaji ambaye anafanya vitu vyake kwa akili akiwa amejiamini sana ndipo alipompa kazi polisi mmoja mpuuzi anayependa vijisenti na kumpa kazi ya kumsaka Raina kwa udi na uvumba.
Polisi huyu Beck ( nafasi iliyochezwa na Paul Sloan) anatakiwa kumsimamisha Raina ambaye alionekana kuwa tishio kubwa na katika saka nikusake ndani ya Los Angeles, Raina na Beck  wanagundua kitu kingine kwamba huwezi kukwepa rushwa inayofanya akili za watu zisiwe sawasawa.


Filamu hii kama utaipata mimi niliiona katika You Tube baada ya muda mrefu ni mbaya kwa maana ina mtetemo wa mauaji usiopendeza, dawa za kulevya na maeneo yasiyotamkika lakini shua ni aksheni kwa kwenda mbele ni advencha na kubwa zaidi inasisimua na inakuacha  ukishindwa kuamua mpaka mwisho wa safari.
Wiki hii kuna mtu anataka nimpe taarifa ya sinema gani ina ukweli wa kutosha kuhusu uvamizi wa Entebe uliofanywa na Waisrael. Nikuhakikishe ndugu yangu naingia katika genge langu la kuchakura na nitakuja kukupa kitu.
Ukitaka zaidi unaweza kunisaka katika ujumbe mfupi 0713176669 au ndani ya msimbebeda @gmail.com

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Stiletto:Sinema ya mwaka 2008 lakini naihusudu sana
Stiletto:Sinema ya mwaka 2008 lakini naihusudu sana
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEggIwvF1zvfJ-B0JSqfUofZjxQxOJSCzO-5RDbxNQQvVo2xQxiL5Xal6xJYF4VJqYm4aw9c71kOZAHmzOJe4A9LnJKsI7Q7PprOLZNQo4HmYlVqS3M9Mi88xPyOzZX5d7iGxkBBJpkdTIw/s320/stiletto.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEggIwvF1zvfJ-B0JSqfUofZjxQxOJSCzO-5RDbxNQQvVo2xQxiL5Xal6xJYF4VJqYm4aw9c71kOZAHmzOJe4A9LnJKsI7Q7PprOLZNQo4HmYlVqS3M9Mi88xPyOzZX5d7iGxkBBJpkdTIw/s72-c/stiletto.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/stilettosinema-ya-mwaka-2008-lakini.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/stilettosinema-ya-mwaka-2008-lakini.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy