Tamko la Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA Kitalu Na. 8, Mtaa wa Luthuli S.L.P 2643, DAR ES SALAAM Simu: +2...


TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA
Kitalu Na. 8, Mtaa wa Luthuli
S.L.P 2643, DAR ES SALAAM
Simu: +255 22 2135747/8; 2137125; 2135222
Faksi: +255 22 2111281
Barua Pepe: chragg@chragg.go.tz
Tovuti: www.chragg.go.tz


Oktoba 01, 2016


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tamko la Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani, Oktoba 1, 2016
                                           
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) inaungana na watu wote duniani katika kuadhimisha siku ya wazee duniani. Wakati dunia inaadhimisha siku hii, Tume inatoa wito kwa jamii yote ya Watanzania kuondoa vitendo vyote vya unyanyasaji dhidi ya wazee ili kuhakikisha kuwa wanaishi katika jamii salama kama sehemu ya utekelezaji wa Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Dunia na kauli mbiu ya taifa inayosema “Ondoa Unyanyasaji kwa Wazee”.

Uzee na kuzeeka, havikwepeki; hivyo ustaarabu wa jamii au nchi yoyote duniani si wingi wa rasilimali na mazingira mazuri bali katika uwekaji wa mifumo madhubuti ya kulinda na kutetea haki za makundi maalumu yanayohitaji ulinzi wa jamii husika. Kwa kulitambua hilo Disemba 14, 1990, Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika Azimio lake Na. 45/106 uliipitisha tarehe 1, Oktoba ya kila mwaka kuwa Siku ya Wazee Duniani. Vipaumbele katika Azimio hilo ni pamoja na suala la uhuru wa wazee, wazee kushiriki na kushirikishwa katika shughuli za maendeleo, kutunzwa na kuheshimiwa.

Hivyo siku hii ya tarehe 1, Oktoba dunia inawapa nafasi wazee kukutana pamoja na kubadilishana mawazo juu ya nini cha kufanya kuhusiana na mustakabali wa haki zao kwa ujumla, zikiwemo haki za kupata huduma za matibabu na mafao yao kwa wakati.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 pamoja na marekebisho yake Ibara ya 12(2) na ibara ya 14 imeeleza juu ya wazee kupewa heshima na kupata hifadhi kutoka katika jamii wanamoishi.
Aidha, Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 ilionesha kuwa idadi ya watanzania wote ni milioni 45; kati yao idadi ya wazee kwa Tanzania Bara ni 2,507,568 (5.6%) - wanaume 1,200,210 (5.5%) na wanawake ni 1,307,358 (5.7%). Tanzania visiwani ina jumla ya wazee 58,311 (4.5%) - wanaume 29,887 (4.7%) na wanawake 28,424 (4.2%). 

Kundi hili la wazee ni kubwa na linahitaji ulinzi na utetezi maalumu wa haki zao kwa kuwa lina wanyonge wengi kulingana na umri wao, hali duni za kiuchumi,  matatizo ya kiafya na kisaikolojia.

Tume kama taasisi ya kitaifa iliyo kitovu cha ukuzaji na ulinzi wa haki za binadamu nchini, imefanya jitihada mbalimbali kuhakikisha kuwa wazee wanapewa haki zao. Jitihada hizo ni pamoja na:-
  • Kutoa elimu ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora, ikiwemo haki za wazee kwa viongozi na watendaji wa ngazi mbalimbali wa taasisi za Serikali na Asasi za Kiraia, na wadau mbalimbali wa haki za binadamu. Kazi hii imefanyika kupitia Mpango-kazi wa Kitaifa wa Haki za Binadamu (National Human Rights Ation Plan) uliozinduliwa rasmi mwaka 2013.

  • Kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kutunga Sheria ya Wazee nchini kwa kutoa maoni yatakayohakikisha kuwa haki za wazee zinalindwa na kuhifadhiwa.

  • Kushughulikia malalamiko yanayohusiana na uvunjwaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora, hasa katika suala la mapunjo na wastaafu kutolipwa pensheni zao stahiki na kwa wakati.

Tume inatambua na kupongeza jitihada mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali katika kujali ustawi wa wazee nchini. Jitihada hizo ni pamoja na kuundwa kwa Sera ya Wazee ya mwaka 2003, kuundwa kwa taasisi mbalimbali zinazoshughulikia masuala ya Wazee, kama vile Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Wanawake, Jinsia na Wazee, na jitihada za kupunguza umaskini kwa kaya maskini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAF).
.
Pamoja na jitihada hizi bado wazee wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali, zikiwemo:-
  • Kutofaidika na mafao mbalimbali ya mifuko ya hifadhi ya jamii (pensheni jamii) licha ya kwamba maendeleo yaliyofikiwa na nchi yetu leo hii ni matokeo ya mchango wa wazee hao kwa kazi zao mbalimbali walizofanya.

  • Kutopata huduma muafaka za afya na matibabu bure licha ya matamko mbalimbali ya viongozi wa Serikali ya kuwapatia matibabu bure na huduma bora za afya kwa wakati muafaka; jambo lililoendelea  kuwa wimbo usio na kibwagizo kwa muda mrefu sasa. Wazee wananyanyasika hasa kwa magonjwa kwa kutopatiwa matibabu sahihi.

  • Kutokuwepo kwa sheria maalum inayoshughulikia masuala mbalimbali ya wazee;

  • Umaskini wa kipato miongoni mwa wazee wengi.

  • Kutokuwa na uwakilishi katika vyombo na ngazi mbalimbali za maamuzi ili kuwapo na utetezi wa haki zao.

  • Usalama mdogo kwa wazee kutokana na ukatili na manyanyaso wanayofanyiwa, hasa vitendo vya unyanyasaji kwa wanawake na walemavu na mauaji ya wazee kutokana na imani potofu.

Kwa mujibu wa taarifa za utafiti uliofanywa na Shirika la Kimataifa la Help Age International (HAI) Tanzania siyo mahali salama kwa wazee kuishi; kwani kuanzia mwaka 2013 hadi 2015 jumla ya wazee 2,866 waliuawa kwa imani za kishirikina katika mikoa mbalimbali ya Tanzania bara, ikiwa ni wastani wa mauaji ya wazee 573 kila mwaka.

Kutokana na changamoto hizo Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, inatoa mapendekezo yafuatayo kwa Serikali, jamii na wadau katika uimarishaji wa upatikanaji wa haki za wazee nchini:-
  1. Elimu ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora itolewe kwa wananchi wote ili kujenga jamii inayoheshimu na kulinda haki za binadmu.

  1. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikamilishe utungaji wa Sheria ya Wazee kwani kupatikana kwa sheria hiyo kutawezesha utekelezaji wa Sera ya Wazee ya mwaka 2003.

  1. Utaratibu wa malipo ya pensheni/hifadhi ya jamii kwa wazee wote bila kujali hadhi zao, yaani bila kuangalia iwapo walikuwa wafanyakazi katika sekta rasmi au siyo rasmi, uwekwe na uharakishwe kutekelezwa.

  1. Huduma za afya ziboreshwe na kutolewa bure kwa wazee, hii ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa huduma maalum za afya, madawa ya kutosha na vyumba maalum kwa ajili ya wazee.

  1. Kwa kupitia mradi wa TASAF wa kunusuru kaya masikini Serikali itoe kipaumbele kwa wazee ili kuwanusuru wazee wote nchini. Kupitia mradi huu itakuwa rahisi kuwafikia wazee walioko vijijini kwa kuwa mradi umeweza kuwakwamua kiuchumi watu wanaoishi katika mazingira magumu.

  1. Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora inatoa wito kwa jamiii kuwatambua wazee kama rasilimali muhimu katika maendeleo ya taifa. Aidha, inawataka wadau wa haki za binadamu kuhamasisha wananchi nchini kote kulinda, kukuza na kutetea haki na ustawi wa wazee nchini ili kuondoa unyanyasaji dhidi yao.

  1. Serikali iweke mikakati endelevu ya kukomesha na kutokomeza mauaji ya wazee yanayochangiwa na imani za kishirikina. Mauaji haya yanavunja haki za binadamu, na yanaitia doa na kuiaibisha nchi yetu.

  1. Pia Serikali kwa kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama iongeze jitihada za kuwasaka na kuwakamata wahusika wa mauaji ya wazee. Aidha, vyombo hivyo viharakishe upelelezi na uendeshaji wa kesi za mauaji ya wazee ili haki ionekane kuwa inatendeka.

  1. Mwisho, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora inatoa wito kwa jamii kuwathamini wazee, kwani ni kundi muhimu linalohitaji upendo, kuthaminiwa na kusaidiwa.

Wazee ni hazina ya taifa tusiwanyanyase!

Imetolewa na:

(SIGNED)

Salma Ali Hassan (Kamishna)

Kny. Mwenyekiti
                                                 
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Oktoba 1, 2016

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Tamko la Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani
Tamko la Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/tamko-la-tume-ya-haki-za-binadamu-na.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/tamko-la-tume-ya-haki-za-binadamu-na.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy