UN YAADHIMISHA MIAKA 71, YAAHIDI KUWEZESHA VIJANA

WAKATI Umoja wa Mataifa (UN) ukiadhimisha miaka 71 tangu kuanzishwa kwake, imeahidi kuwatumia vijana katika utekelezaji wa malengo yake 17 ...

WAKATI Umoja wa Mataifa (UN) ukiadhimisha miaka 71 tangu kuanzishwa kwake, imeahidi kuwatumia vijana katika utekelezaji wa malengo yake 17 ya maendeleo.

Mwakilishi Mkazi wa UN nchini, Alvaro Rodriguez amesema ili kufanikisha hilo, UN pamoja na mashirika mengine itatoa mafunzo ya vitendo kwa vijana zaidi ya 50,000 ifikapo mwaka 2017 ambao wataingizwa katika mpango wa utekelezaji wa malengo hayo.

"UN itaendelea kushirikiana na vijana pia itatoa elimu ya vitendo.Hadi sasa vijana zaidi ya elfu kumi wamepewa mafunzo na wanatambua malengo hayo, na kwamba UN na wadau wengine wanatarajia kufundisha vijana zaidi ya 50, 000 ifikapo mwaka 2017, ili ifikapo 2030 vijana wengi wawe wanajua malengo hayo na namna ya kuyatekeleza," amesema.

Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (wa tatu kulia) akiwasili kwenye viwanja vya Karimjee akiwa ameambatana na mwenyeji wake Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (wa pili kulia) pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Celestine Mushy (kushoto) kwenye sherehe ya kupandisha bendera ya Umoja wa Mataifa katika kuadhimisha miaka 71 ya umoja huo ambapo kila mwaka Oktoba 24 huadhimishwa.(Picha na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

Amesema miongoni mwa mafunzo yatakayotolewa kwa vijana hao ni pamoja na jinsi ya kufanikisha malengo 17 ya maendeleo endelevu ya umoja huo na jinsi ya vijana watakavyoweza kujiajiri.

Aidha, Rodriguez amesema tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana linasababisha umasikini kwa kuwa nguvu kazi hiyo inashindwa kuwajibika katika kuliletea taifa maendeleo.

"Ongezeko la vijana na mahitaji yao ni moja ya changamoto kubwa nchiniTanzania, tunahitaji kuhakikisha kwamba vijana wanawajibika katika kujiendeleza ili kupata maendeleo chanya katika maisha yao, ili kufanikisha hayo vijana wanatakiwa kuwa na ufahamu na taaluma katika kuwezesha mabadiliko ya uchumi nchini Tanzania," alisema Rodriguez na kuongeza: "Vijana wasisahau kuwa wao ni chachu ya amani na maendeleo na UN tutaendelea kushirikiana nao kuhakikisha vijana wanakuwa wadau wa taratibu na kanuni zilizosababisha kuundwa umoja huu, wakijua na kutambua malengo ya dunia," amesema.

Rodriguez amesema UN itaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania katika kuleta maendeleo nchini.
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akitambuliswa kwa Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini Afisa utawala na fedha, Spencer Bokosha (wa pili kulia) na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez katika sherehe za maadhimisho ya miaka 71 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa zilizofanyika katika viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam. 

"UN itashirikiana na serikali ya Tanzania kuleta maendeleo ikiwemo kuboresha utoaji wa huduma za kijamii," amesema.

Kwa upande wa mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Augustine Mahiga amesema serikali inatambua mchango wa umoja huo katika kuleta maendeleo nchini na kwamba itaendelea kushirikiana na umoja huo.

"Serikali ya awamu ya tano tangu kuanza kwake imefanya mambo mengi ili kuleta maendeleo, imedhibiti mianya ya ukwepaji kodi, imefanikiwa kutanua wigo wa ukusanyaji mapato na kuondoa rushwa. Hatuwezi kushinda pekee katika kuleta maendeleo ya wananchi, serikali iko tayari kushirikiana na jumuiya zote duniani," amesema.

Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia wakimbizi nchini (UNHCR), Chansa Kapaya mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Karimjee kwenye sherehe ya kupandisha bendera ya Umoja wa Mataifa katika kuadhimisha miaka 71 ya umoja huo tangu kuanzishwa jana jijini Dar es Salaam.

Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea heshima ya gwaride maalum kwenye sherehe za kupandisha bendera ya Umoja wa Mataifa kuadhimisha miaka 71 ya umoja huo tangu kuanzishwa kwake zilizofanyika katika viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akikagua gwaride la heshima lililoandaliwa kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 71 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake yaliyofanyika katika viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akishuhudia kupandishwa kwa bendera ya Umoja wa Mataifa ikiwa ni ishara ya maadhimisho ya miaka 71 ya umoja huo tangu kuanzishwa kwake yaliyofanyika kwenye viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wakurugenzi wa taasisi mbalimbali, serikali na wafanyakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa wakitoa heshima kwa wimbo wa Taifa wakati wa kupandishwa kwa bendera ya Umoja wa Mataifa kwenye maadhimisho ya miaka 71 ya umoja huo tangu kuanzishwa yaliyofanyika katika viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam.

Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akitoa hotuba kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 71 ya Umoja wa Mataifa zilizofanyika katika viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akimpongeza Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga kwa hotuba nzuri.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akitoa salamu za Umoja wa Mataifa kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 71 ya Umoja huo tangu kuanzishwa kwake zilizofanyika katika viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya mabalozi mbalimbali waliodhuria sherehe za maadhimisho ya miaka 71 ya Umoja wa Mataifa wakiwa jukwaa kuu katika viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam.
Meza kuu, kutoka Kulia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni , Katibu Mkuu wa Asasi ya Umoja wa Tanzania (UNA), Reynald Maeda, Brigadia Jenerali (TPDF), Dominic Mrope, Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez pamoja na Mkuu wa Mabalozi Balozi Prof. Ambrosio Lukoki.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwemo wafanyakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa waliohudhuria sherehe za miaka 71 ya Umoja wa Mataifa zinazofanyika Oktoba 24 kila mwaka ambapo jana zilifanyika kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.


Mshehereshaji wa sherehe za maadhimisho ya miaka 71 ya Umoja wa Mataifa, Bertha Makilagi (kushoto) akijadiliana jambo na Nguse Nyerere (kulia) Afisa mwenzake wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam.
Wanafunzi wa shule msingi Uhuru Mchanganyiko wakitoa burudani wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 71 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika jana katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Jitegemee wakitoa buradani katika sherehe za miaka 71 ya Umoja wa Mataifa zilizofanyika jana jijini Dar es Salaam katika viwanja vya Karimjee.
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga katika picha ya pamoja na waheshimiwa mabalozi na viongozi mbalimbali huku wakiwa na mabango ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) katika sherehe za miaka 71 ya Umoja wa Mataifa zilizofanyika kwenye viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam.
Jukwaa kuu katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule mbalimbali waliohudhuria maadhimisho ya sherehe za miaka 71 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika kwenye viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Celestine Mushy (katikati) wakati akijiandaa kuondoka kwenye viwanja vya Karimjee zilipofanyika sherehe za miaka 71 ya Umoja wa Mataifa jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez.
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiagana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez baada ya kumalizika kwa sherehe za kupandisha bendera ya Umoja wa Mataifa ikiwa ni maadhimisho ya miaka 71 ya umoja huo tangu kuanzishwa kwake zilizofanyika katika viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akiteta jambo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez wakati akijiandaa kuondoka kwenye viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akizungumza jambo na mmoja wa wageni waalikwa kwenye sherehe za kupandisha bendera ya Umoja wa Mataifa ikiwa ni maadhimisho ya miaka 71 ya umoja huo tangu kuanzishwa kwake zilizofanyika katika viwanja vya Karimjee jana jijini Dar es Salaam

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4811,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: UN YAADHIMISHA MIAKA 71, YAAHIDI KUWEZESHA VIJANA
UN YAADHIMISHA MIAKA 71, YAAHIDI KUWEZESHA VIJANA
https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEiwAX1xuRD-MaSFbc4Wci1iJ5QLYfLNdzuU2K_IT44wfXsC4Yk5s9mEJ5ISgWkq8788GhphObE6fXyEJm7_LmJ1npZqd7MNBRBu7Xd-1bUVWhgIYhRG_UAhJBbbUN8BCDqPX5TyueJkHHjJua-1Wvzj1cQxCIwo_Mv8j8wa=
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/un-yaadhimisha-miaka-71-yaahidi.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/10/un-yaadhimisha-miaka-71-yaahidi.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy