VILIO, SIMANZI, MAJONZI VYATAWALA VIFO VYA WATOTO WA MAOFISA WA JESHI LA MAGEREZA

Wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Mtakatifu Therese wakitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa mwanafunzi mwenzao Maria Masal...

Wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Mtakatifu Therese wakitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa mwanafunzi mwenzao Maria Masala wakati wa ibada ya kuuaga mwili huo iliyofanyika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Therese Ukonga Madafu Dar es Salaam jana.
Jeneza lenye mwili wa mtoto huyo likiombewa kabla ya 
kuingizwa kanisani
Wanafunzi wenzake na mtoto huyo wakiwa katika ibada ya kumuaga mwenzao.
Padre aliyekuwa akiendesha ibada hiyo akilinyunyuzia mafuta ya baraka jeneza lenye mwili wa mtoto Maria.
Msemaji wa familia ya ASP Masala akitoa taarifa na historia 
fupi ya marehemu Maria.
Baba wa marehemu, ASP Masala (wa pili kulia aliyevaa shati la kitenge), akiwa na ndugu zake na waumini waombolezaji katika ibada ya kuuaga mwili wa mtoto wake kabla ya kuondoka kwenda nyumbani kwao mkoani Rukwa kwa mazishi.
Padre aliyekuwa akiendesha ibada hiyo akilinyunyuzia mafuta ya baraka jeneza lenye mwili wa mtoto Maria.
Watawa wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Therese wakitoa 
heshima za mwisho.
Waombolezaji wakiwa wamejipanga foleni wakati wakienda 
kutoa heshima za mwisho.
Waombolezaji wakiwa katika foleni ya kutoa heshima za mwisho.
Mtawa wa kanisa hilo akisaidiwa baada ya kushindwa kuvumilia uchungu wa kuondokewa na mpendwa wake mtoto Maria.
Ngugu yake Maria akisaidiwa baada ya kutoa heshima 
zake za mwisho.
Baba ya mtoto huyo ASP Masala akilia kwa uchungu wakati 
akitoa heshima zake za mwisho kwa mwanaye.
Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa mtoto Maria wakati wakitoka katika kanisa hilo.
Jeneza likiingizwa katika gari tayari kwa safari ya kwenda 
mkoani Rukwa kwa mazishi.
Waombolezaji wakiwa wamepigwa na bumbuwazi 
kufuati vifo hivyo.
Ni huzuni na simanzi wakati wa kuuaga mwili wa mtoto huyo.

Na Dotto Mwaibale

WINGU zito vilio majonzi na simanzi vilitanda kutokana na vifo vya watoto wawili wa maofisa wa Jeshi la Magereza waliofariki  dunia kwa kukosa hewa baada ya kujifungia kwenye gari la mmoja wa wazazi wao walimokuwa wakicheza.        

Tukio hilo limetokea juzi jioni katika Kota za Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam, wakati wazazi wao walipokuwa wakitengeneza gari hilo lililogoma kuwaka.

Watoto waliopoteza maisha ni mtoto wa Mrakibu wa Jeshi la Magereza (ASP), Demetrus Masala, aitwaye Maria (6), ambaye alikuwa darasa la kwanza katika Shule ya Mtakatifu Therese Ukonga na Sajini Francis, ambaye ni Esther (4), mwanafunzi wa shule ya awali katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo ambao hawakupenda majina yao yaandikwe kwenye vyombo vya habari kwa sababu si wasemaji wa familia walidai kuwa  watoto hao walipoteza maisha katika gari lenye namba ya usajili T 291 CXR aina ya Toyota Passo ,mali ya ASP Masala.

Mashuhuda hao walidai kuwa siku ya tukio gari hilo liligoma kuwaka na ndipo Masala alipokwenda kumuomba jirani yake ambaye anaishi mlango wa pili Sajini Francis aende kumsaidia kulibusti ambapo alichukua betri katika gari yake ili amsaidie jirani yake huyo.

Ilielezwa kuwa licha ya kuibusti betri ya gari  la ASP Masala haikupokea moto ikiashiria kuwa Alternator ilikuwa ni mbovu kwani ilikuwa haifui umeme.

Baada ya kushindikana kuiwasha gari hilo waliamua kuachana nalo na kushauriana ASP Masala aende kumfuata fundi na ndipo alipolifunga gari lake na kuondoka pasipo kujua watoto wao walikuwa ndani ya gari hilo kwani walipokuwa wakilitengeneza walionekana wakiwa pembeni yake.

Wazazi hao hawakujua watoto hao waliingia saa ngapi ndani ya gari hilo lakini ilidaiwa kuwa awali wakati wakicheza jirani na gari hilo waliwafukuza ambapo baadae waliingia tena bila ya wao kufahamu hasa kutokana na gari hilo kuwa na vioo vya giza isipokuwa cha mbele ambapo walikuwemo ndani ya gari hilo kuanzia saa 7 mchana hadi saa 11 jioni.

Ilidaiwa kuwa baada ya kukaa kwa muda mrefu Francis ambaye ni dereva ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali alibaini watoto hao wawili hawaonekani katika eneo hilo ndipo walipoanza kuwatafuta katika nyumba za jirani bila mafanikio.

Inadaiwa wakati wakiendelea kuwatafuta kuna kijana aliwadokeza kuwa wakati gari hilo likiendelea kutengenezwa watoto hao walikuwa ndani ya gari hilo.

Kauli hiyo inadaiwa ndiyo iliyomshtua Francis na kuamua kuchungulia ndani ya gari hilo ambapo waliwaona watoto hao wakiwa wamekaa siti ya nyuma wamelala fofofo huku mwingine akivuja damu puani.

Hali hiyo ilisababisha Francis na watu wengine waliokuwepo eneo hilo kusogea na kuvunja kioo kidogo cha gari hilo na kuwatoa watoto hao wakiwa katika hali mbaya.

Imedaiwa kwa sababu ya hali waliyokuwa nayo waliamua kuwakimbiza katika Hospitali ya Kardinal Rugambwa Ukonga kwa ajili ya matibabu ya haraka lakini hata hivyo walibaini mtoto Maria tayari alikuwa amekwisha fariki dunia.

Madaktari walijaribu kumpa huduma ya kwanza mtoto Esther kwa kumuongezea Oksjeni na baadaye walimkimbiza Hospitali ya Mkoa wa Ilala ya Amana ambapo naye walibaini kuwa tayari alikuwa amekwisha fariki.

Baadhi ya waumini wa Kanisa Katoliki la Ukonga la Mtakatifu Therese wakizungumza na wanahabari walielezea kusikitishwa na tukio hilo, wakidai mtoto Maria juzi asubuhi walishiriki naye Jumuiya ya Mtakatifu Maria Consolata ambayo ilifanyika nyumbani kwao.

Walisema kwa nyakati tofauti mtoto huyo alishiriki na wazazi wake kupanga viti tayari kwa maandalizi ya jumuiya.

Mkazi mmoja wa eneo hilo alidai, kifo cha watoto hao ni pigo kwa wazazi hao ambao ni majirani na marafiki wa muda mrefu.

Imedaiwa kuwa wazazi hao kila mmoja alikuwa na watoto wawili, wa kwanza wote wakiume na wapili wa kike ambao ndio waliofariki katika tukio hilo la kusikitisha.

“ Kifo hiki kimeacha pengo kwani wote wameondokewa na watoto wao wa pili kuzaliwa na wote ni wa kike wamebaki wakiume tu…inauma sana na ni funzo kwetu kuwa tayari wakati wowote,” ilielezwa.

Mwili wa mtoto Maria ulisafirishwa jana kwenda mkoani Rukwa kwa mazishi ambayo yanatarajia kufanyika kesho.

Hata hivyo inadaiwa mama mzazi wa Maria hayupo jijini Dar es Salaam alisafiri kwenda Rukwa kwa ajili ya sherehe za mwisho wa mwaka na bado yupo huko.

Familia ya Francis inatarajia kufanya mazishi ya mtoto wao Esther leo katika Makaburi ya Segerea, Ukonga.

Padre aliyeongoza ibada ya kuuaga mwili wa mtoto Maria aliwataka wazazi na waumini wa kanisa Katoliki la Mtakatifu Therese kutohusisha tukio hilo na imani potofu na kusema kila binadamu anakuja duniani kwa mpango wa mungu na kuondoka kwa mpango wa mungu ingawa vifo vya watoto hao ni vyakusikitisha hasa ukizingatia umri wao mdogo waliokuwa nao na kuwa kazi ya mungu haina makosa.

Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mwembe Madafu, Deus Nchimbi alisema, kifo cha watoto hao ni pigo kwa familia hizo marafiki. 

“Kikubwa ni kuomba amani na kuwaombea marehemu lakini watoto wamekufa kifo cha uchungu kwa kukosa hewa huenda wangekuwa na wakubwa wangeweza kufungua gari,”alisema Nchimbi.

Alisema kilichobaki ni kuikumbusha jamii kuwa makini na vyombo vya moto na kuwapa uhuru watoto waweze kufahamu aina ya mali zilizopo nyumbani.

Changamoto kubwa iliyoibuka katika tukio hilo ni kwa wazazi wote wa pande mbili kugoma kulizungumzia tukio hilo kwa waandishi wa habari kwa madai kuwa  wanaopaswa kulizungumzia ni Jeshi la Magereza wakati suala hilo ni la kifamilia zaidi na linagusa maisha ya kijamii.

"Tumepewa maagizo kutoka juu kuwa waandishi wa habari hampaswi kuchukua taarifa hii kwani ndugu za marehemu bado wanamajonzi hivyo subirini wakisha zika mje kuwahoji wafiwa hayo ndiyo maagizo na jeshini hatuna kauli nyingi ni moja tu" alisema ofisa mmoja wa jeshi hilo ambaye hakujitambulisha jina lake. 

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,301,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,23,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: VILIO, SIMANZI, MAJONZI VYATAWALA VIFO VYA WATOTO WA MAOFISA WA JESHI LA MAGEREZA
VILIO, SIMANZI, MAJONZI VYATAWALA VIFO VYA WATOTO WA MAOFISA WA JESHI LA MAGEREZA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjUPryBNAKy4DoGJGZs___LbSnUFhBV8b81CSHKPHnKMFlvzHSzNrWDGM_AVjsH6gTKq7py8Hb7fXWP8WqsK6HYGcuzVe4IrXYGLZI0iQaw1OefdK5XdVTeyRI5xN9Zwf7bBIwpKuoHWjyz/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjUPryBNAKy4DoGJGZs___LbSnUFhBV8b81CSHKPHnKMFlvzHSzNrWDGM_AVjsH6gTKq7py8Hb7fXWP8WqsK6HYGcuzVe4IrXYGLZI0iQaw1OefdK5XdVTeyRI5xN9Zwf7bBIwpKuoHWjyz/s72-c/1.JPG
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2017/01/vilio-simanzi-majonzi-vyatawala-vifo.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2017/01/vilio-simanzi-majonzi-vyatawala-vifo.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy