JITIHADA ZA KIMATAIFA ZAHITAJIKA KATIKA KUKABILIANA NA UVUVI HARAMU.

RIPOTI ya shirika la Chakula duniani (FAO) inasema asilimia 15 ya samaki wanaovuliwa duniani ambao ni sawa na tani Milioni 26 wanatokan...


RIPOTI ya shirika la Chakula duniani (FAO) inasema asilimia 15 ya samaki wanaovuliwa duniani ambao ni sawa na tani Milioni 26 wanatokana na uvuvi haramu na hivyo kuleta tishio kwa uendelevu wa rasilimali za bahari na uhakika wa chakula.

Taarifa hiyo inazitaja nchi za Afrika Magharibi ikiwemo Guinea, Siera Leone, Morroco, Mauritania na Angola kuwa ni mataifa yaliyoshamiri vitendo vya uvuvi haramu kukiwa na idadi kubwa ya meli na makampuni yanayojihusisha na uvuvi haramu zinapofanya safari za majini.

Aidha utafiti uliofanywa na chombo cha Umoja wa Ulaya kilichoanzishwa kusaidia nchi za Afrika, Caribbean na Pacific (CTA) unaonyesha kuwa  jumla ya hasara ya sasa inayotokana na uvuvi haramu duniani kote inakadiriwa kuwa kati ya dola bilioni tisa na 24 kwa mwaka.

Nchi zinazoendelea zipo hatarini zaidi kukumbwa na uvuvi haramu, huku jumla ya samaki wanaovuliwa kwa njia haramu katika Afrika Magharibi pekee ikifikia hadi juu ya asilimia 40 kuliko samaki wanaoripotiwa.

Ili kukabiliana na changamoto hiyo mwaka 2016 FAO iliandaa mkataba wa kimataifa kuhusu udhibiti wa uvuvi haramu ambao tayari umeridhiwa na nchi 30 na hivyo kuanza kutumika kisheria, ambapo unalazimisha nchi wanachama kuhakikisha boti zote zinazoingia bandarini nchini mwao zinaheshimu kanuni za uvuvi endelevu.

Tanzania kama zilivyo nchi nyingine zilizopo katika ukanda wa bahari, mito na maziwa imekuwa mstari wa mbele kuunga mkono jitihada za mashirika ya kimataifa katika kupiga vita tatizo la uvuvi haramu, ambao unaendelea kuathiri mazalia ya samaki sambamba na uchafuzi wa mazingira ya bahari.

Uvuvi haramu unatajwa kushamiri zaidi katika maeneo mengi ya pwani kuanzia Dar es Salaam, Mtwara hadi Tanga, hatua inayoisababishia Serikali kukosa mapato ya fedha za kigeni pamoja na kudumaza mchango wa sekta hiyo katika pato la taifa.

Kwa mujibu wa taarifa ya Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi inasema sekta ya uvuvi inachangia asilimia 2.4 yapato la taifa wakati ukuaji wake ni wa kiwango cha asilimia 5.5 kwa mwaka na kutoa ajira ya kudumu kwa wavuvi 185,000.

Pamoja na jitihada zinazofanywa na Serikali katika kuwahimiza wavuvi kuzingatia sharia, kanuni na taratibu zilizopo, baadhi ya wavuvi wamekuwa wakitumia zana na vifaa vya uvuvi zisivyo rasmi ikiwemo nyavu, matumizi ya mabomu ya sumu na hivyo kupelekea tishio la kupotea kwa rasilimali hizo muhimu.

Hivi karibuni Serikali ilitangaza operesheni maalum kwa kuunda kikosi kazi maalum kinachojumuisha Wizara saba ikiwa ni mkakati maalum wa kupambana vikali na wavuvi haramu pamoja na waigizaji, wauzaji na watumiaji wa zana zisizoruhusiwa katika uvuvi.

Kikosi kazi hicho kinahusisha Wizara mbalimbali ikiwemo OfisiyaRais- TAMISEMI, Ofisi ya Makamu waRais-Mazingira, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la KujengaTaifa, Wizara ya Mambo  ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Kilimo,  Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Maliasili na Utalii, na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Akizungumza wakati wa ziara yake ya kutembelea soko la kimataifa la samaki lililopo Feri Jijini Dar es Salaam, Waziri wa Kilimo, Mifugo naUvuvi, Dkt. Charles Tizeba alisema hakuna namna nyingine ya kukabiliana na vitendo hivyo haramu zaidi ya kuweka adhabu kali kwa wanaotiwa hatiani.

“Baadhi ya makosa ya uvuvi haramu kuwa ni uhujumu uchumi au ugaidi wa silaha (terrorism) kwa vile wanatumia milipuko  au mabomu na kumaliza mazalio ya samaki na kutishia wafanyakazi wa Serikali wanaofuatilia masuala hayo” anasema Dkt. Tizeba.

Kwa mujibuwaDkt. Tizeba anasema Serikali imebaini mapungufu yaliopo katika  sheria zilizopo, hivyo imejipanga kuwasilisha mabadiliko Bungeni  ambapo, itaamuliwa  kwa kiasi gani wataweza kuwabana wavuvi walio waharibifu na wavunjaji sheria.

Anasema sekta ya uvuvi nchini inatawaliwa na sheria kuu mbili za Sheria ya Uvuvi ya mwaka 2003 na Sheria ya Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu ya mwaka 2009, ambazo hazimfanyi mtu kuacha uvuvi haramu lakini iwapo adhabu itaongezwa, wengi wataogopa.

Anaongeza kuwa mikakati hiyo ya Serikali imekuja baada ya sheria na kanuni zilizopo kushindwa kupambana kikamilifu na vitendo vya uvuvi haramu vinavyotishia ukuaji wa sekta ya uvuvi nchini.

Aidha anasema Serikali itafanya mabadiliko ya sheria zinazosimamia uvuvi kwa kuyaainisha baadhi ya makosa ya uvuvi haramu kuwa ni ya uhujumu uchumi, ili kuongeza adhabu iwe kali kwa watu wanaotiwa hatiani kwa makosa hayo.

Waziri Tizeba anaongeza kuwa Serikali inaendelea na operesheni zake za kudhibiti uvuvi haramu katika mnyororo wote wa thamani kwa maana kutoka kwa watengenezaji zana haramu, wanaoziingiza nchini, wasafirishaji na wavuvi.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Yohana Budeba anasema Serikali imenunua boti nane za kisasa zenye thamani ya Tsh. Milioini 640 kwa ajili ya kuongeza nguvu ya doria na kupambana na uvuvi haramu katika maeneo mbalimbali ya uvuvi nchini ikiwemo maziwa makuu ya Victoria, Nyasa na Tanganyika.

Dkt. Yohana Budeba anasema boti nne kati ya hizo zimenunuliwa nchini Afrika Kusini na nyingine zinaendelea kutengenezwa hapa nchini katika kituo cha kunduchi ikiwa ni jitihada za Serikali za kukabiliana na Uvuvi haramu ambao umeanza kutishia kutoweka kwa baadhi ya samaki katika Mito, MaziwanaMabwawanchini.

KuhusuuvuviwasamakikatikamajiyabahariKuu, Dkt. Budeba anasema Serikali imeanzisha kituo cha udhibiti wa uvuvi kwenye maji ya kina kirefu cha bahari kuu ambacho kitasaidia nyendo za vyombo vya uvuvi wakiwemo wavuvi wa kimataifa wanaoingia kuvua samaki kinyume cha sharia na taratibu za nchi.

Mazao ya samaki pamoja na kuwa kuchanzo cha kipato kwa watanzania wengine na taifa kwa ujumla, lakini pia samaki wanachangia katika kuwapatia lishe na kwa sababu hiyo matumizi endelevu ya mazao ya bahari na bahari ni jambo muhimu sana.

Usimamizi endelevu na ulinzi wa bahari na mazingira ya pwani na viumbe hai ni jambo muhimu ili kuiepusha jamii na athari mbalimbali ikiwemo mabadiliko ya tabia nchi.
Source: Ismail Ngayonga
MAELEZO

Dar es Salaam.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: JITIHADA ZA KIMATAIFA ZAHITAJIKA KATIKA KUKABILIANA NA UVUVI HARAMU.
JITIHADA ZA KIMATAIFA ZAHITAJIKA KATIKA KUKABILIANA NA UVUVI HARAMU.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhswod3ZTiFi5c-Jqd1WYNRjxgfxljFx-hlQ0-Vh13XdiOwPDyXQ-ru4e5sveWZHuk8Z2zdA6Vn1zAGVU8-Ibo0N22oVRBNYV66_SFEBp0uZ-Rz9CYG7FkFq3QSpyTBRdhYmBbax7otv6I/s320/UVUVI+HARAMU.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhswod3ZTiFi5c-Jqd1WYNRjxgfxljFx-hlQ0-Vh13XdiOwPDyXQ-ru4e5sveWZHuk8Z2zdA6Vn1zAGVU8-Ibo0N22oVRBNYV66_SFEBp0uZ-Rz9CYG7FkFq3QSpyTBRdhYmBbax7otv6I/s72-c/UVUVI+HARAMU.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2017/03/jitihada-za-kimataifa-zahitajika-katika.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2017/03/jitihada-za-kimataifa-zahitajika-katika.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy