RIPOTI ya shirika la Chakula duniani (FAO) inasema asilimia 15 ya samaki wanaovuliwa duniani ambao ni sawa na tani Milioni 26 wanatokan...
RIPOTI ya shirika la Chakula duniani
(FAO) inasema asilimia 15 ya samaki wanaovuliwa duniani ambao ni sawa na tani
Milioni 26 wanatokana na uvuvi haramu na hivyo kuleta tishio kwa uendelevu wa
rasilimali za bahari na uhakika wa chakula.
Taarifa hiyo inazitaja nchi za Afrika
Magharibi ikiwemo Guinea, Siera Leone, Morroco, Mauritania na Angola kuwa ni
mataifa yaliyoshamiri vitendo vya uvuvi haramu kukiwa na idadi kubwa ya meli
na makampuni yanayojihusisha na uvuvi haramu zinapofanya safari za majini.
Aidha utafiti uliofanywa na chombo
cha Umoja wa Ulaya kilichoanzishwa kusaidia nchi za Afrika, Caribbean na
Pacific (CTA) unaonyesha kuwa jumla ya hasara ya sasa inayotokana na
uvuvi haramu duniani kote inakadiriwa kuwa kati ya dola bilioni tisa na 24 kwa
mwaka.
Nchi zinazoendelea zipo hatarini
zaidi kukumbwa na uvuvi haramu, huku jumla ya samaki wanaovuliwa kwa njia
haramu katika Afrika Magharibi pekee ikifikia hadi juu ya asilimia 40 kuliko
samaki wanaoripotiwa.
Ili kukabiliana na changamoto hiyo
mwaka 2016 FAO iliandaa mkataba wa kimataifa kuhusu udhibiti wa uvuvi haramu
ambao tayari umeridhiwa na nchi 30 na hivyo kuanza kutumika kisheria, ambapo
unalazimisha nchi wanachama kuhakikisha boti zote zinazoingia bandarini nchini
mwao zinaheshimu kanuni za uvuvi endelevu.
Tanzania kama zilivyo nchi nyingine
zilizopo katika ukanda wa bahari, mito na maziwa imekuwa mstari wa mbele kuunga
mkono jitihada za mashirika ya kimataifa katika kupiga vita tatizo la uvuvi
haramu, ambao unaendelea kuathiri mazalia ya samaki sambamba na uchafuzi wa
mazingira ya bahari.
Uvuvi haramu unatajwa kushamiri zaidi
katika maeneo mengi ya pwani kuanzia Dar es Salaam, Mtwara hadi Tanga, hatua
inayoisababishia Serikali kukosa mapato ya fedha za kigeni pamoja na kudumaza
mchango wa sekta hiyo katika pato la taifa.
Kwa mujibu wa taarifa ya Serikali
kupitia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi inasema sekta ya uvuvi inachangia
asilimia 2.4 yapato la taifa wakati ukuaji wake ni wa kiwango cha asilimia 5.5
kwa mwaka na kutoa ajira ya kudumu kwa wavuvi 185,000.
Pamoja na jitihada zinazofanywa na
Serikali katika kuwahimiza wavuvi kuzingatia sharia, kanuni na taratibu
zilizopo, baadhi ya wavuvi wamekuwa wakitumia zana na vifaa vya uvuvi zisivyo
rasmi ikiwemo nyavu, matumizi ya mabomu ya sumu na hivyo kupelekea tishio la
kupotea kwa rasilimali hizo muhimu.
Hivi karibuni Serikali ilitangaza
operesheni maalum kwa kuunda kikosi kazi maalum kinachojumuisha Wizara saba
ikiwa ni mkakati maalum wa kupambana vikali na wavuvi haramu pamoja na
waigizaji, wauzaji na watumiaji wa zana zisizoruhusiwa katika uvuvi.
Kikosi kazi hicho kinahusisha Wizara
mbalimbali ikiwemo OfisiyaRais- TAMISEMI, Ofisi ya Makamu waRais-Mazingira,
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la KujengaTaifa, Wizara ya Mambo ya Ndani
ya Nchi, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Maliasili na
Utalii, na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Akizungumza wakati wa ziara yake ya
kutembelea soko la kimataifa la samaki lililopo Feri Jijini Dar es Salaam,
Waziri wa Kilimo, Mifugo naUvuvi, Dkt. Charles Tizeba alisema hakuna namna
nyingine ya kukabiliana na vitendo hivyo haramu zaidi ya kuweka adhabu kali kwa
wanaotiwa hatiani.
“Baadhi ya makosa ya uvuvi haramu
kuwa ni uhujumu uchumi au ugaidi wa silaha (terrorism) kwa vile wanatumia
milipuko au mabomu na kumaliza mazalio ya samaki na kutishia
wafanyakazi wa Serikali wanaofuatilia masuala hayo” anasema Dkt. Tizeba.
Kwa mujibuwaDkt. Tizeba anasema
Serikali imebaini mapungufu yaliopo katika sheria zilizopo, hivyo
imejipanga kuwasilisha mabadiliko Bungeni ambapo, itaamuliwa kwa
kiasi gani wataweza kuwabana wavuvi walio waharibifu na wavunjaji sheria.
Anasema sekta ya uvuvi nchini
inatawaliwa na sheria kuu mbili za Sheria ya Uvuvi ya mwaka 2003 na Sheria ya
Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu ya mwaka 2009, ambazo hazimfanyi mtu kuacha
uvuvi haramu lakini iwapo adhabu itaongezwa, wengi wataogopa.
Anaongeza kuwa mikakati hiyo ya
Serikali imekuja baada ya sheria na kanuni zilizopo kushindwa kupambana
kikamilifu na vitendo vya uvuvi haramu vinavyotishia ukuaji wa sekta ya uvuvi
nchini.
Aidha anasema Serikali itafanya
mabadiliko ya sheria zinazosimamia uvuvi kwa kuyaainisha baadhi ya makosa ya
uvuvi haramu kuwa ni ya uhujumu uchumi, ili kuongeza adhabu iwe kali kwa watu
wanaotiwa hatiani kwa makosa hayo.
Waziri Tizeba anaongeza kuwa Serikali
inaendelea na operesheni zake za kudhibiti uvuvi haramu katika mnyororo wote wa
thamani kwa maana kutoka kwa watengenezaji zana haramu, wanaoziingiza nchini,
wasafirishaji na wavuvi.
Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo,
Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Yohana Budeba anasema Serikali imenunua boti nane
za kisasa zenye thamani ya Tsh. Milioini 640 kwa ajili ya kuongeza nguvu ya
doria na kupambana na uvuvi haramu katika maeneo mbalimbali ya uvuvi nchini
ikiwemo maziwa makuu ya Victoria, Nyasa na Tanganyika.
Dkt. Yohana Budeba anasema boti nne
kati ya hizo zimenunuliwa nchini Afrika Kusini na nyingine zinaendelea
kutengenezwa hapa nchini katika kituo cha kunduchi ikiwa ni jitihada za
Serikali za kukabiliana na Uvuvi haramu ambao umeanza kutishia kutoweka kwa
baadhi ya samaki katika Mito, MaziwanaMabwawanchini.
KuhusuuvuviwasamakikatikamajiyabahariKuu,
Dkt. Budeba anasema Serikali imeanzisha kituo cha udhibiti wa uvuvi kwenye maji
ya kina kirefu cha bahari kuu ambacho kitasaidia nyendo za vyombo vya uvuvi
wakiwemo wavuvi wa kimataifa wanaoingia kuvua samaki kinyume cha sharia na
taratibu za nchi.
Mazao ya samaki pamoja na kuwa
kuchanzo cha kipato kwa watanzania wengine na taifa kwa ujumla, lakini pia
samaki wanachangia katika kuwapatia lishe na kwa sababu hiyo matumizi endelevu
ya mazao ya bahari na bahari ni jambo muhimu sana.
Usimamizi endelevu na ulinzi wa
bahari na mazingira ya pwani na viumbe hai ni jambo muhimu ili kuiepusha jamii
na athari mbalimbali ikiwemo mabadiliko ya tabia nchi.
Source: Ismail Ngayonga
MAELEZO
Dar es Salaam.
COMMENTS