MGODI WA ACACIA BULYANHULU WALIPA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1 KWA HALMASHAURI YA MSALALA NA NYANG'WALE

Mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyanhulu uliopo katika halmashauri ya Msalala wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga umekabidhi hundi zeny...

Mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyanhulu uliopo katika halmashauri ya Msalala wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga umekabidhi hundi zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni moja kwa ajili ya malipo ya ushuru wa huduma kwa halmashauri ya Msalala iliyopo mkoani Shinyanga na halmashauri ya wilaya ya Nyang’wale mkoani Geita.
Hafla fupi ya kukabidhi hundi hizo imefanyika Alhamis Machi 2,2017,katika ukumbi wa halmashauri ya Msalala wilayani Kahama na kuhudhuriwa na viongozi wa halmashauri na mikoa ya Shinyanga na Geita pamoja na viongozi mbalimbali kutoka mgodi wa Acacia Bulyanhulu. 
Akizungumza wakati wa hafla hiyo,Meneja mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu Graham Crew alisema fedha hizo ni malipo ya ushuru wa huduma kwa ajili ya kipindi cha miezi sita kuanzia mwezi Julai hadi Disemba 2016. 
Alisema fedha hizo ni asilimia 0.3 ya ukokotoaji wa ushuru wa huduma ya mgodi huo kwa kipindi cha miezi sita katika awamu ya pili kuanzia mwezi Julai hadi Disemba 2016. 
“Mgodi umelipa shilingi za kitanzania 1,135,178,526/= na malipo hayo yamegawanyika katika halmashauri mbili kwa mujibu wa makubaliano na serikali ambapo halmashauri ya Msalala imelipwa shilingi milioni 760 sawa na asilimia 67 na Nyang’wale shilingi milioni 374 sawa na asilimia 33”,alisema Crew. 
Aidha alisema mpaka sasa mgodi huo umelipa jumla ya shilingi bilioni 4.3 tangu mwaka 2014 kampuni ya Acacia ilipoanza kutoa malipo ya ushuru wa huduma wa asilimia 0.3 ya mapato ghafi kwa halmashauri husika. 
“Katika kipindi cha miaka hiyo minne halmashauri ya Msalala imelipwa zaidi ya shilingi bilioni 3.7 na Nyang’wale imelipwa shilingi bilioni 1.1”,aliongeza Crew. 
Katika hatua nyingine Crew alisema mgodi huo unaendelea kushirikiana na serikali na wadau wa maendeleo ili kutekeleza miradi mbalimbali kwa ajili ya kuboresha huduma endelevu za kijamii na miundombinu katika jamii hususani katika elimu,barabara,umeme,maji na huduma za afya.
Wakipokea hundi hizo,mkuu wa mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga na Katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela waliushukuru mgodi huo kwa kutimiza wajibu wa kulipa kodi na kuongeza kuwa fedha hizo zitatumika katika shughuli za maendeleo ya wananchi katika halmashauri za Msalala na Nyang'wale.
Mwandishi wetu,Kadama Malunde alikuwepo wakati wa hafla hiyo,ametuletea picha za matukio yaliyojiri,tazama hapa chini 
Wa pili kutoka kulia ni Mtaalamu wa Mawasiliano Mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyanhulu Mary Lupamba akiwakaribisha viongozi wa mkoa wa Shinyanga na Geita wakati wa hafla fupi ya kukabidhi hundi zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni moja kwa ajili ya malipo ya ushuru wa huduma kwa halmashauri ya Msalala na Nyang’wale.Wa kwanza kushoto ni Meneja mkuu wa mgodi wa Bulyanhulu Graham Crew,akifuatiwa na mkuu wa mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga na Katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela 
Meneja mkuu wa mgodi wa Bulyanhulu Graham Crew akiangalia hundi ya shilingi milioni 374 kabla ya kuikabidhi kwa mkuu wa mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga kwa ajili ya halmashauri ya wilaya ya Nyang'wale .Kushoto ni Kiongozi wa Kitengo cha Mahusiano ya Jamii mgodi wa Bulyanhulu Sarah Ezra Teri 
Meneja mkuu wa mgodi wa Bulyanhulu Graham Crew akikabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni 374 kwa mkuu wa mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga kwa ajili ya malipo ya ushuru wa huduma ya mgodi kwa halmashauri ya Nyang'hwale iliyopo mkoani Geita 
Meneja mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu Graham Crew akishikana mkono na mkuu wa mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga wakati akikabidhi hundi ya shilingi milioni 374 
Meneja mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu Graham Crew akizungumza wakati wa kukabidhi hundi zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni moja kwa ajili ya malipo ya ushuru wa huduma kwa halmashauri ya Msalala iliyopo mkoani Shinyanga na halmashauri ya wilaya ya Nyang’wale mkoani Geita. Alisema halmashauri ya Msalala imelipwa shilingi milioni 760, Nyang’wale shilingi milioni 374 
Mkuu wa mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga akikabidhi hundi hiyo ya shilingi milioni 374 kwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Nyang’wale Carlos Gwamagobe 
Mkuu wa mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga akizungumza wakati wa zoezi la makabidhiano ya hundi yenye thamani ya shilingi milioni 374 kwa ajili ya halmashauri ya wilaya ya Nyang’wale ambapo alisema fedha hizo zitatumika katika shughuli za maendeleo ya wananchi katika halmashauri hiyo 
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Nyang’wale Carlos Gwamagobe (kulia) akishikana mkono na Mkuu wa mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga wakati wa makabidhiano ya hundi hiyo 
Mkuu wa wilaya ya Nyang’wale Hamim Gwiyama akishikana mkono na Meneja mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu Graham Crew wakati wa makabidhiano ya hundi ya shilingi milioni 374 
Meneja mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu Graham Crew (kushoto) akizungumza wakati wa kukabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni 760 kwa ajili ya malipo ya ushuru wa huduma ya mgodi kwa halmashauri ya Msalala iliyopo mkoani Shinyanga. Katikati ni katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela akifuatiwa na mbunge wa jimbo la Msalala Ezekiel 
Meneja mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu Graham Crew akishikana mkono na katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela wakati wa kukabidhi hundi ya shilingi milioni 760 kwa ajili ya halmashauri ya wilaya ya Msalala iliyopo wilayani Kahama mkoani Shinyanga 
Meneja mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu Graham Crew akizungumza wakati wa kukabidhi hundi hiyo ambapo alisema halmashauri ya Msalala imelipwa shilingi milioni 760 sawa na asilimia 67 
Meneja mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu Graham Crew akizungumza wakati wa makabidhiano hayo ya hundi ya shilingi milioni 760 
Meneja mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu Graham Crew akishikana mkono na mbunge wa jimbo la Msalala wilayani Kahama Ezekiel Maige 
Katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela akizungumza wakati wa kupokea hundi yenye thamani ya shilingi milioni 760 ambapo alisema aliushukuru mgodi huo wa malipo ya ushuru na kuongeza kuwa tayari fedha hizo zimeshaingizwa kwenye bajeti ya halmashauri ya Msalala kwa ajili ya maendeleo ya halmashauri hiyo. 
Meneja mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu Graham Crew akishikana mkono na Mweka hazina  halmashauri ya Msalala Masatu Mnyolo aliyemwakilisha mkurugenzi wa halmashauri ya Msalala wakati wa kukabidhi hundi hiyo 
Mbunge wa jimbo la Msalala Ezekiel Maige akizungumza wakati wa makabidhiano hayo ambapo aliuomba mgodi huo kuendelea kulipa kodi kama inavyostahili huku akiomba mgodi kuyabana makampuni yanayofanya kazi zake mgodini ili yalipe kodi kwa ajili ya maendeleo ya halmashauri ya Msalala 
Meneja Mkuu wa Mahusiano ya Kampuni ya Uchimbaji ya Acacia na Serikali Mhandisi Asa Mwaipopo akizungumza wakati wa makabidhiano hayo ambapo alisema Acacia imetimiza wajibu wa kulipa ushuru na kufanya tukio la kukabidhi hundi hizo kwa uwazi zaidi ili kuepuka minong'ono kuwa pengine mgodi huwa haulipi kodi 
Meneja Mkuu wa Mahusiano ya Kampuni ya Uchimbaji ya Acacia na Serikali Mhandisi Asa Mwaipopo alisema kodi iliyolipwa imetokana na uzalishaji wa mgodi kwa kipindi cha miezi sita na hiyo ni awamu ya pili,utaratibu wa Acacia ni kulipa kwa miezi 6 na tayari awamu ya kwanza walishalipa na sasa wamemalizia kipindi cha pili katika mwaka 2016 
Meneja Mkuu wa Mahusiano ya Kampuni ya Uchimbaji ya Acacia na Serikali Mhandisi Asa Mwaipopo alisema kampuni ya Acacia imekuwa ikifanya kazi zake kwa kushirikiana na wananchi wanaozunguka migodi yao
Meneja Mkuu wa Mahusiano ya Kampuni ya Uchimbaji ya Acacia na Serikali Mhandisi Asa Mwaipopo akishikana mkono na mbunge wa jimbo la Msalala Ezekiel Maige
Meneja Mkuu wa Mahusiano ya Kampuni ya Uchimbaji ya Acacia na Serikali Mhandisi Asa Mwaipopo akiagana na katibu tawala mkoa wa Shinyanga Albert Msovela.
Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: MGODI WA ACACIA BULYANHULU WALIPA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1 KWA HALMASHAURI YA MSALALA NA NYANG'WALE
MGODI WA ACACIA BULYANHULU WALIPA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1 KWA HALMASHAURI YA MSALALA NA NYANG'WALE
https://3.bp.blogspot.com/-oEu-6Fv344k/WLhRy7ZwclI/AAAAAAAANUY/v73c_47uWoYRgHBhGAo62QT7Nq38L_d2wCEw/s640/UF3A0805.JPG
https://3.bp.blogspot.com/-oEu-6Fv344k/WLhRy7ZwclI/AAAAAAAANUY/v73c_47uWoYRgHBhGAo62QT7Nq38L_d2wCEw/s72-c/UF3A0805.JPG
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2017/03/mgodi-wa-acacia-bulyanhulu-walipa-zaidi.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2017/03/mgodi-wa-acacia-bulyanhulu-walipa-zaidi.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy