RAIS, Dk John Magufuli akiongoza kwa mara ya kwanza Sherehe za Miaka 53 ya Mapinduzi tangu aingie madarakani mwishoni mwa mwaka juz...
RAIS, Dk John Magufuli akiongoza kwa mara ya kwanza Sherehe
za Miaka
53 ya Mapinduzi tangu aingie madarakani mwishoni mwa mwaka
juzi,
ameapa kuulinda Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa nguvu
zake
zote, huku akiapa yeyote akayejaribu kuleta chokochoko za
kutaka
kuuvunja, atavunjika yeye kabla ya Muungano.
Akizungumza katika hotuba fupi ya dakika 17 jana kwenye
Uwanja wa
Jamhuri mjini hapa ambako sherehe za Muungano zimefanyika kwa
mara ya
kwanza tangu Uhuru na pia kwa mara ya kwanza tangu Serikali
ihamishie
rasmi makao makuu ya nchi Dodoma kuanzia mwishoni mwa mwaka
jana,
alisema kwa kushirikiana na Rais wa Zanzibar, DK Ali Mohamed
Shein,
watafanya kila linalowezekana kuhakikisha muungano inazidi kuimarika,
badala ya kuvunjikia mikononi mwao.
“Nataka niwahakikishie, mimi na Dk Shein tutaulinda kwa nguvu
zote
Muungano huu, na kamwe asijitokeze mtu yeyote, atakayekaidi au
kujaribu kuvunja Muungano, atavunjika yeye…," alisema.
Alisema kufikisha umri wa miaka 53 ya kuzaliwa kwa taifa la
Tanzania
si jambo dogo, kwani mataifa mengi yamejaribu kufanya hivyo,
lakini
bila ya kufanikiwa, huku akisisitiza kwa kusema,”Hii ni siku
ya
kipekee, ya kihistoria kwa tanzania. Leo ni `Birthday’ (siku
ya
kuzaliwa) ya Tanzania.”
Aliongeza kuwa, si jambo dogo kusherehekea Miaka 53 ya
Muungano,
kwani kazi ya kuulinda Muungano ni ngumu, kwa sababu
hata kulinda
ndoa ni ngumu.
“Hii inathibitisha kuwa suala la kulinda muungano si jambo
rahisi hata
kidogo, hivyo basi hatuna budi kuwapongeza waliofanikisha
nchi yetu
kufikisha miaka 53, tunawapongeza sana.
“Tunafahamu wapo wengi waliotoa mchango wao, lakini kwa leo
nitawataja
wote. Wa kwanza kwa niaba yenu, napenda niwashukuru waasisi wa
Muungano, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Rais wa Kwanza
wa
Zanzibar, Hayati Abeid Amani Karume kwa kuufanikisha na
kuuwezesha
Muungano huu. Hawa ndio waliosaini hati ya Muungano, bahati
nzuri, leo
hii tunao hapa Mama Maria Nyerere na Mama Fatuma Karume,”
alisema.
Aliwapongeza pia viongozi wote wan chi katika awamu zote, Ali
Hassan
Mwinyi aliyeiongoza Serikali ya Awamu ya Pili, Benjamin Mkapa
wa Awamu
ya Tatu na Jakata Kikwete aliyeiongoza Awamu ya Nne, lakini
pia
waasisi mbalimbali. Alirudia kuahidi yeye na Dk Shein,
watafuata nyayo
za kuulinda na kuutetea Muungano huo.
Aidha, alisema wakati Watanzania wakisherehekea kutimiza
miaka 53 ya
kuzaliwa kwa taifa la Tanzania, ni vyema watu kutafakari
walikotoka,
walipo na wanakokwenda.
“Niwaombe pia baada ya kuzaliwa kwa taifa la Tanzania mwaka
1964 na
leo tunatimiza miaka 53, ni ushahidi Watanzania wengi
tunaoishi, ambao
ni asilimia kubwa wamezaliwa baada ya Muungano, kwa hiyo tuna
wajibu
mkubwa, bila kujali makabila wetu, bila kujali vyama vyetu na
bila
kujali maeneo yetu, kuulinda na kuudumisha Muungano huu ili
taifa la
Tanzania liendelee kudumu,” alisema.
Alisema anafahamu kukiwa na mshikamano, itawezekana kuulinda
Muungano,
hivyo kushauri Watanzania wazidi kushikamana ili kuwe na
miaka mingine
mingi zaidi ya kusherehekea Muungano.
Changamoto; za Muungano
Alisema licha ya mafanikio, bado zipo changamoto za Muungano,
lakini
akaahidi kuwa zinashughuliwa kwa kuwa kuna Kamati ya Pamoja
inayoshughulikia masuala ya Muungano ambayo Mwenyekiti wake
ni Makamu
wa Rais, Samia Hassan Suluhu na wajumbe ni pamoja na Waziri
Mkuu,
Kassim Majaliwa, Makamu wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali
Idd,
mawaziri na makatibu wakuu wa Serikali zote mbili.
Alisema kamati hiyo inafanya kazi nzuri, lakini pia haipaswi
kuachwa
ifanye kazi peke yake, hivyo kila Mtanzania awe mshiriki wa
kulinda
Muungano.
Alisema dhamira hiyo inashabihiana na kaulimbiu ya sherehe
za mwaka
huu, inayosema “Miaka 53 ya Muungano; “Tuulinde, Kuuimarisha.
Tupige
Vita Dawa za Kulevya na Kufanya Kazi kwa Bidii,” hivyo kusema
imekuja
kwa wakati mwafaka.
Kuhamia Dodoma
Alisema kufanyika kwa sherehe hizo mkoani Dodoma kwa mara ya
kwanza
katika historia ya Tanzania, ni ishara kuwa Serikali ya Awamu
ya Tano
inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) imedhamiria kwa
dhati
kuhakikisha makao makuu ya Serikali yanahamia Dodoma.
“Na niwahakikishie wakazi wa Dodoma na Watanzania kwa ujumla,
Serikali
sasa imefika Dodoma na hatutarudi nyuma tena. Kama
tulivyoahidi,
kufikia mwaka 2020 serikali yote itakuwa imehamia hapa,”
alisema na
kushangiliwa mno.
Rais Magufuli ambaye mwaka jana alifuta sherehe za miaka 52 ya
Muungano na kupeleka fedha kiasi cha Sh bilioni 2 katika
shughuli ya
upanuzi wa barabara ya Uwanja wa Ndege jijini Mwanza, alisema
katika
kuthibitisha utayari wa kuhamia Dodoma, tayari hatua kadhaa
zimefanyika.
Alizitaja kuwa ni pamoja na mawaziri wote, manaibu waziri,
makatibu
wakuu, manaibu na wakurugenzi mbalimbali wameshahamia Dodoma.
Alisema
zaidi ya watumishi wa umma 3,000 wameshahamia Dodoma.
Lakini pia alisema awamu ya pili na ya tatu ya kuhamia Diodoma
imepangwa kuhamia katika mwaka ujao wa fedha, ambapo serikali
imepanga
kutumia zaidi ya Sh bilioni 200 kwa ujenzi wa ofisi na nyumba
za
viongozi wa Serikali.
Aidha, amesema juhudi za kujenga miundombinu ya usafiri na
usafirishaji, ikiwemo ya upanuzi uwanja wa ndege, lakini pia
ujenzi wa
reli ya kisasa itakapita Dodoma, ujenzi wa barabara
unaendelea sehemu
mbalimbali, upatikanaji umeme, huduma za afya, elimu lakini
pia
maandalizi ya ujenzi wa uwanja mkubwa na wa kisasa wa michezo
utakaojengwa na Serikali ya Morocco.
“Yote haya yanalenga kukidhi mahitaji ya kuwa makao makuu ya
nchi,”
alisema na kuwataka wakazi wa Dodoma na mikoa jirani Singida,
Arusha,
Manyara, iringa na Morogoro, kujipanga kutumia fursa za
Dodoma kuwa
makao makuu ya nchi.
Pamoja na dhamira nzuri ya Serikali ya kutaka kuulinda
Muungano,
alisema hiyo itakuwa kazi bure kama nchi haitakuwa na amani
na kusema
kama waasisi wasingeweza kulinda amani, leo hii Watanzania
wasingekuwa
na chereko za miaka 53 ya Muungano, hivyo kusisitiza kila
mmoja
ashiriki kuilinda amaniya nchi iliyopo.
Faida za Muungano
Alisema licha ya awali kuwapo kwa mwingiliano baina ya watu wa
Tanganyika na Zanzibar, miaka 53 ya Muungano, nchi imekuwa na
faida
nyingi zaidi, mojawapo ikiwa kuwa taifa lenye nguvu, hivyo
kuwezesha
kulinda uhuru, amani na umoja. Alisema nchi imekuwa yenye
amani na
mipaka iko salama.
Aidha, alisema Muungano umewezesha mafanikio makubwa katika
nyanja za
kiuchumi, kisiasa na kijamii.
“Serikali zetu mbili zimefanya jitihada za kiuchumi na pia
kukabiliana
na matatizo ya kimasikini na ukosefu wa ajira. Mambo
mbalimbali
yameimarika, demokrasia pia imeimarika.
Tanzania ya sasa si ile ya mwaka 1964. Lakini pia tunaheshimika
kimataifa.
"Jamani, tusione vyaelea, vimeundwa na kuna watu
wamefanya kazi usiku
na mchana kuhakikisha Muungano huu unadumu,” alisema na
kuongeza kuwa,
nchi imekuwa yenye heshima kubwa kimataifa imekuwa ikisaidia
katika
shughuli za ukombozi na kutafuta amani katika nchi mbalimbali
kikanda
na duniani kwa ujumla.
Source:eric
mkutai habarileo
COMMENTS