TAMKO LA UMMY MAADHIMISHO YA SIKU YA MALARIA DUNIANI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO TAMKO LA MHE. UMMY   A. MWALIMU (MB) ...



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO

TAMKO LA MHE. UMMY  A. MWALIMU (MB) - WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA MALARIA DUNIANI -
TAREHE 25 APRILI, 2017

Ndugu Wananchi,
Siku ya Malaria Duniani, huadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe 25 mwezi Aprili. Maadhimisho haya yaliridhiwa katika Mkutano wa 60 wa Afya Duniani (World Health Assembly) huko Geneva nchini Uswisi.  

Lengo kuu la maadhimisho haya ni kuielimisha na kuikumbusha jamii ili kutambua athari za ugonjwa wa malaria, jinsi unavyoambukizwa, na namna ya kujikinga. Aidha maadhimisho haya pia hutumika kuihamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kutambua dalili za malaria mapema; kuwahi kituo cha kutolea huduma za afya ili kupima na kuthibitisha uwepo wa vimelea vya malaria kabla ya kuanza kutumia dawa, kutumia dawa sahihi ya kutibu malaria pale itakapothibitika kuwa na vimelea vya malaria na kukamilisha matibabu ya malaria kulingana na maelekezo ya mtoa huduma. Kauli Mbiu ya mwaka huu inasema Shiriki Kutokomeza Malaria Kabisa, kwa Manufaa ya Jamii”.

Ndugu Wananchi,
Takwimu kutoka katika vituo vya kutolea huduma za Afya zinaonesha kuwa, takribani wastani wa  watu million  12 huripotiwa kuwa na ugonjwa wa malaria katika vituo vya kutolea huduma za Afya  kwa mwaka.

Aidha Takwimu za viashiria vya malaria kutoka tafiti zilizofanyika katika kaya zimeonesha kuwa maambukizi ya malaria yalikuwa asilimia 18 mwaka 2008, aslimia 10 mwaka 2012 na asilimia 14.8 kwa mwaka 2015.
Utafiti wa mwaka 2015-2016 unaonesha mikoa mitatu ya; Kagera, Geita na Kigoma ina kiwango kikubwa cha maambukizi ya malaria, (Kagera 41%, Geita 38% na Kigoma 38%). Makundi yanayoathirika zaidi na malaria ni wajawazito na watoto umri chini ya miaka mitano.

Mikakati inayopendekezwa kimataifa ambayo inatekelezwa na Wizara yangu kwa kushirikiana na  wadau wetu ni pamoja na:

  1. Udhibiti wa mbu waenezao malaria; Udhibiti hufanyika kwa kutumia mbinu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na matumizi ya vyandarua vyenye viuatilifu vya muda mrefu (LLINs); unyunyiziaji wa viuatilifu ukoko katika kuta ndani ya nyumba (IRS); kusafisha mazingira na kuua viluwiluwi vya mbu kwa kutumia viuadudu vya kibailojia (LSM) hasa katika maeneo ya mjini.

  1. Uchunguzi na matibabu ya ugonjwa wa malaria; Kwa kuongeza kasi ya upimaji wa ugonjwa wa malaria kwa kutumia kipimo mRDT au hadubini, na kutumia dawa mseto pale mgonjwa anapogundulika kuwa ana vimelea vya malaria; kuwapatia wajawazito vyandarua vyenye viuatilifu na dawa ya Sulphadoxine Pyrimethamine (SP) kwa vipindi maalumu wakati wa ujauzito ili kuwakinga na madhara yanayotokana na malaria.

Ndugu Wananchi,
Nchi yetu imepata mafanikio makubwa ambayo yametokana na utekelezaji wa mikakati na afua za kupambana na ugonjwa wa malaria na ushiriki wa wadau mbalimbali. Miongoni mwa mafanikio hayo ni pamoja na:
  • Kukamilika kwa kampeni: Kampeni ya ugawaji wa Vyandarua vyenye viuatilifu vya muda mrefu (LLINs) katika kaya bila malipo katika mikoa 23 nchini, ambapo jumla ya vyandarua zaidi ya millioni 27 vimegawiwa kwa jamii bila malipo. Lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa kila mwananchi anatumia chandarua kujikinga na ugonjwa huu. Mikoa mitatu ya; Mtwara, Lindi na Ruvuma inapata vyandarua kupitia Mpango wa wanafunzi shuleni unaojulikana kama School Net Program (SNP) toka mwaka 2013.

Chandarua Kliniki: Ili kuhakikisha upatikanaji wa vyandarua unakuwa endelevu hususan kwa makundi yanayopata athari zaidi kwa ugonjwa wa malaria (Wajawazito na Watoto), utaratibu endelevu unaojulikana kama CHANDARUA KLINIKI umeanzishwa ambapo wajawazito na watoto chini ya mwaka mmoja hupewa chandarua wanapohudhuria kliniki kwa huduma mbalimbali. Hadi sasa utaratibu huo unatekelezwa katika Mikoa saba (9) ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Mwanza, Geita, Kagera, Mara, Simiyu na Kigoma.

Ugawaji vyandarua kupitia Shuleni:
Mpango mwingine ni wa ugawaji wa vyandarua kupitia wanafunzi shuleni,  ambapo wanafunzi wanapata chandarua kila mwaka, kama njia ya kufikisha chandarua hicho kwa matumizi ya familia. Mpango huu wa vyandarua shuleni unatekelezwa katika mikoa saba (7) ya; Mtwara, Lindi, Ruvuma, Mwanza, Geita, Kagera na Mara kupitia ufadhili wa PMI.

Upuliziaji viatilifu Ukoko (IRS):
Utekelezaji wa mkakati wa upuliziaji viuatilifu-ukoko katika kuta ndani ya nyumba, unatekelezwa katika Halmashauri za mikoa ya Kanda ya Ziwa yenye maambukizi makubwa ya malaria. Ambapo kwa mwaka huu, zoezi la upuliziaji limefanyika katika mikoa 4 na Halmashauri 10 za Sengerema, Buchosa na Kwimba (Mwanza); Chato na Nyang’wale (Geita) Ngara, Misenyi na Bukoba (V) (Kagera); Musoma (V) na Butiama (Mara). Jumla ya nyumba 487,553 zimepuliziwa viuatilifu-ukoko na takriban wakazi 2,437,760 wamekingwa dhidi ya malaria katika maeneo hayo.

Tiba Sahihi ya Malaria:
Tiba sahihi kwa wagonjwa wa malaria imeendelea kutolewa katika vituo vya kutolea huduma za Afya, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa vipimo vya kutambua uwepo wa vimelea vya malaria kwa kutumia hadubini au mRDTs  vinapatikana katika vituo vya kutolea huduma za afya wakati wote. Aidha, inasisitizwa kuwa dawa zinatolewa kwa wale tu ambao watathibitika kuwa na vimelea vya malaria (confirmed cases).

Serikali imeendelea kuhakikisha kuwa wataalamu wanajengewa uwezo kwa kuwapatia mafunzo mbalimbali ili kufanya kazi kwa ufanisi na weledi. Kwa kupitia juhudi hizi, kumekuwepo na ongezeko la upimaji kufikia asilimia 90 katika vituo hivyo; zaidi ya lengo ambalo Wizara ilijiwekea la asilimia 80.

Kwa upande wa dawa za malaria zimeendelea kupatikana katika vituo vyote vya umma vya kutolea huduma za afya.  



Dawa katika Sekta Binafsi:
Upatikanaji wa Dawa Mseto za malaria kwa bei punguzo kupitia sekta binafsi kupitia mpango  wa  Dawa Mseto kwa bei Punguzo (Co- payment mechanism for subsidized ACTs in the private sector) ambao unajumuisha vituo vya kutolea huduma za afya vya binafsi na maduka ya dawa. Mpango huu, unalenga kuhakikisha kuwa hakuna mwananchi atakayekosa dawa za malaria pale anapougua na kuamua kwenda kutibiwa katika vituo vya serikali au binafsi.

Viuadudu vya Kibailojia (Larvicides):
Serikali kwa kushirikiana na kampuni ya (LABIOFAM) kutoka nchini Cuba, imekamilisha ujenzi wa kiwanda cha kuzalisha viuadudu (biolarvicides) ambavyo vitatumika kuua viluwiluwi vya mbu katika mazalia (madimbwi, mabwawa na sehemu nyingine zinazozalisha mbu). Tayari kiwanda kimeanza uzalishaji wa viuadudu, hivyo natoa wito kwa Halmashauri kutenga bajeti ya kununua viuadudu  hivyo kwa ajili ya utekelezaji wa afua ya kuangamiza viluwiluwi vya mbu kwenye mazalia.

Changamoto:
Pamoja na mafanikio kadhaa yaliyopatikana, bado tuna changamoto katika maeneo yafuatayo:
  • Wanajamii kutotumia vyandarua ipasavyo wakati wote katika kujikinga na ugonjwa wa malaria pamoja na mitazamo potofu juu vyandarua;
  • Hamasa ndogo ya Jamii kupima kabla ya kutumia dawa na kukubali matokeo ya vipimo. Hii huchangia katika matumizi yasiyo sahihi ya dawa za malaria na hivyo kuchangia katika usugu  wa vimelea dhidi ya dawa.
  • Jamii kutoshiriki kikamilifu katika kutunza mazingira na kuharibu mazalia ya mbu kwa kufukia madimbwi, kusafisha mifereji, kuweka mazingira safi na kuharibu mazalia ya mbu kwa kuondoa maji yaliyotuama.
  • Changamoto kubwa ni upatikanaji wa rasilimali kwa ajili ya kuendeleza mafanikio  tuliyoyapata. Kwa mfano misaada iliyokuwa ikitolewa katika nchi za Afrika imepungua kwa kiasi cha dola za kimarekani bilioni 3.6 kwa mwaka, Tanzania ikiwa miongoni mwa nchi hizo.
Ili kupunguza au kuondoa kabisa changamoto zilizopo, Wizara yangu inahakikisha inaendelea kutekeleza ipasavyo mikakati iliyopo ya kupamabana na ugonjwa wa malaria kwa kushirikiana na wadau.

Ujumbe Muhimu kwa jamii
Niwakumbushe kuwa Ugonjwa wa malaria bado ni hatari kwa uhai wetu, maendeleo na ustawi wa Taifa letu. Wakati tunaadhimisha siku ya malaria Duniani, napenda kusisitiza yafuatayo:
  • Wanajamii kushiriki kikamilifu katika kutekeleza na kutumia afua zote za kupambana na malaria.
  • Kila mwanafamilia alale kwenye chandarua chenye viuatilifu kila siku ili kujikinga na malaria. Ni kosa kutumia vyandarua kwa matumizi yasiyo sahihi mf. Kuvulia samaki, kufugia kuku na kuzungushia bustani.
  • Wanajamii kushiriki katika kuharibu mazalia ya mbu kwa kufukia madimbwi, kusafisha mifereji, kuweka mazingira safi na na kuondoa maji yaliyotuama.
  • Kila mwanafamilia  mwenye dalili za malaria ahakikishe anawahi kwenye kituo cha kutolea huduma na kupimwa kabla ya kutumia dawa, na endapo atagundulika kuwa na vimelea ahakikishe anatumia dawa kulingana na maelekezo ya mtoa huduma.
  • Wajawazito kuhakikisha wanahudhuria Kliniki mapema ili kupata huduma zote muhumu ikiwemo kupata tiba ya tahadhari kwa vipindi kwa kutumia SP.
·         Wakurugenzi wa Halmashauri kutenga bajeti ya kununua viuadudu  hivyo kwa ajili ya utekelezaji wa afua ya kuangamiza viluwiluwi vya mbu kwenye mazalia katika Halmashauri zao.

Msisitizo wa Wizara ya Afya, ni kwa wananchi na wadau wote kuendelea kuona umuhimu na kutoa kipaumbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria hususan kwa kutumia fursa zilizopo, kuwekeza katika mapambano dhidi ya malaria na kutekeleza ipasavyo mikakati niliyoitaja hapo juu.



Shukrani:
Napenda nichukue fursa hii kwa niaba ya Serikali, kutoa shukrani zangu za dhati kwa wadau wetu wote waliochangia katika mafanikio tuliyofikia wakiwemo; Mfuko wa Dunia wa kushughulikia ugonjwa wa UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria (The Global Fund), Mfuko wa Rais wa Marekani unaoshughulikia Malaria (PMI), Shirika la Misaada la Uingereza (DFID), Shirika la Maendeleo la Uswisi (SDC), Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la UNITAID, Taasisi zisizo za Kiserikali, Sekta binafsi kupitia Mpango wa Malaria Safe Initiative, Taasisi za Utafiti (NIMR na Ifakara Health Institute) nikitaja kwa uchache; na bila kuwasahau ninyi wanahabari, wananchi na jamii kwa ujumla kwa kuwa tayari kutumia mikakati hiyo kwa kushirikiana na Serikali.

Nimalizie kwa kusisitiza kwamba iwapo tutaitekeleza ipasavyo mikakati niliyoitaja hapo juu, nina imani kabisa, tunaweza kujikinga na ugonjwa wa malaria  na hatimae kuufanya ugonjwa wa malaria kuwa si tatizo kubwa tena katika jamii yetu.

Mwisho kabisa niwakumbushe kuwa zama zimebadilika “Sio kila homa ni Malaria nenda ukapime”, na “lala kwenye chandarua chenye viuatilifu kila siku” ili kujikinga na malaria.   

ASANTENI SANA KWA KUNISIKILIZA.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: TAMKO LA UMMY MAADHIMISHO YA SIKU YA MALARIA DUNIANI
TAMKO LA UMMY MAADHIMISHO YA SIKU YA MALARIA DUNIANI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhsYG4noj4Rc4mgOpBgAFb2jY0rgWP0DUK-WE9XduqUrIgYvsTjdR-NyAJ5kIDEKlHURFWwDHbRkFdqJPWWMY7pq9kHu3nRHKiaWSOpzvfHiAllVgvORFkG4dhCARtH6RDKc6I0YIzKYd8/s320/Ummy-Mwalimu.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhsYG4noj4Rc4mgOpBgAFb2jY0rgWP0DUK-WE9XduqUrIgYvsTjdR-NyAJ5kIDEKlHURFWwDHbRkFdqJPWWMY7pq9kHu3nRHKiaWSOpzvfHiAllVgvORFkG4dhCARtH6RDKc6I0YIzKYd8/s72-c/Ummy-Mwalimu.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2017/04/tamko-la-ummy-maadhimisho-ya-siku-ya.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2017/04/tamko-la-ummy-maadhimisho-ya-siku-ya.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy