MAMBO TISA YA KUZINGATIA UNAPOTAKA KUUPANDA MLIMA KILIMANJARO

Na Jumia Travel Tanzania Hivi unajua kwamba binti wa miaka nane, Roxy Getter, kutokea Florida nchini Marekani amekuwa ni mwanamke wa...


Na Jumia Travel Tanzania

Hivi unajua kwamba binti wa miaka nane, Roxy Getter, kutokea Florida nchini Marekani amekuwa ni mwanamke wa kwanza mwenye umri mdogo zaidi kupanda mlima Kilimanjaro mpaka kileleni mnamo mwezi Julai mwaka 2017? Kama hiyo haitoshi, Mmarekani Kyle Maynard, ambaye hana mikono wala miguu mwaka 2012 aliweza kuupanda Mlima Kilimanjaro mpaka kileleni mwenyewe bila ya msaada wowote? Licha ya kuupanda mlima huu wengine wamekuwa wakijiwekea nia  ya kufanya mambo mbalimbali kwa mara ya kwanza wakiwa kileleni kama vile kundi la wachezaji wa kike 30 wa mpira wa miguu kutokea mataifa 20 walivyofanikisha azma yao ya kucheza mechi kwa dakika zote 90 kwenye urefu wa mita 4000 mwezi Julai mwaka huu!   
Kuupanda Mlima Kilimanjaro ambao ndio unashikilia rekodi ya kuwa mrefu zaidi barani Afrika ukiwa na urefu wa mita 5,895 (sawa na futi 19,341) na unaoweza kupandika kwa urahisi zaidi duniani ni miongoni mwa malengo wanayojiwekea watu mbalimbali katika maisha yao kutoka kila kona ya dunia.


Yapo mambo mengi ambayo inabidi kuyafahamu kwanza kama una ndoto ya siku moja kuja kuupanda Mlima Kilimanjaro. Jumia Travel ingependa kukushirikisha dondoo zifuatazo ambazo wapandaji wengi huzitumia kabla ya kukata shauri la kufunga safari kwenda kuupanda mlima huo.      
Tafiti kampuni sahihi itakayokusaidia kukuongoza kuupanda Mlima Kilimanjaro. Zoezi la  kuupanda Mlima Kilimanjaro sio jambo rahisi ambalo mtu yeyote anaweza kujiamulia kufanya hivyo. Unahitajika uzoefu na utaalamu wa hali ya juu na ndiyo maana kuna watu na kampuni yenye vibali kujihusisha na shughuli hizo. Hivyo basi ili kufanikisha lengo lako itakuwa ni vema ukawasiliana na makampuni hayo, yapo mengi kwa hapa nchini na kuchagua lipi linafaa zaidi.

Panga bajeti mapema. Kama shughuli nyingine yoyote ile itakulazimu kutumia kiasi cha fedha ili kufanikiwa kuupanda mlima huu. Gharama hizo ni kwa ajili ya kugharamia safari nzima ambayo kwa kawaida huanzia siku tano mpaka kumi, chakula, malazi, mavazi, matibabu nakadhalika. Vyote hivi hushughulikiwa na kampuni utakayoichagua kukuongoza. Kwa hiyo itakubidi kuwasiliana nayo mapema ili ujue itakugharimu kiasi gani.
Tambua majira yapi ni muafaka kwa kuupanda mlima. Kwa sababu Mlima Kilimanjaro upo pale siku zote haimaanishi kwamba unaweza kuupanda muda wowote utakaojisikia wewe. Majira ya mwaka huwa yanabadilika, kuna masika, baridi, kiangazi, upepo na vinginevyo. Ushauri kutoka kwa makampuni yanayofanya kazi ya kuwapandisha watu mlima unahitajika ili kukuhakikishia safari yako itakuwa ni salama na yenye mafanikio. Kwa mujibu wa watu waliokwishaupanda mlima huu wanapendekeza miezi ya kuanzia Januari mpaka Machi na kuanzia Juni mpaka Oktoba. Kati ya miezi ya Januari na Machi hali ya hewa ni nzuri na kunakuwa hakuna watu wengi. Kuanzia Juni mpaka Oktoba, kunakuwa wa watu wengi kutokana na kipindi hiko kugongana na likizo za majira ya kiangazi kwa nchi nyingi za Ulaya na Marekani, lakini hali ya hewa ni nzuri na ya kuvutia. Ni vema kuiepuka miezi yenye mvua nyingi ya Aprili, Mei na Novemba, lakini pia unasisitizwa kubeba nguo za kukukinga na baridi kali linalopatikana kileleni mwa mlima huo kwa kipindi chote cha mwaka.
Chagua njia sahihi na rahisi kuupanda Mlima Kilimanjaro. Zipo njia saba za kuweza kukufanikisha kuukwea mlima huu mpaka kileleni zikiwa zinatofautiana kwa ugumu, msongamano wa watu, na mazingira ya kuvutia, hivyo kuchagua ile iliyo sahihi zaidi ni sehemu muhimu kwako pindi unapofanya maandalizi. Njia tatu za Machame, Umbwe na Marangu zinapatikana upande wa Kusini; mbili za Shira na Lemosho zinapatikana kutokea Magharibi na Rongai kwa upande wa Kaskazini Mashariki. Njia ya saba ni kutokea upande wa Magharibi kuanzia Lemosho kuuzunguka Mlima Kilimanjaro ikiwa imevumbuliwa siku za hivi karibuni. Muda utakaoutumia njiani mpaka kufika kileleni utategemea na njia utakayoichagua, ambapo kwa kawaida ni kuanzia siku tano mpaka kumi. Kwa mujibu wa wataalamu na waliowahi kuupanda mlima wanapendekeza kwamba njia zinazoweza kukufanikisha kumaliza zoezi zima ni zile zinazochukua muda mrefu na kupandwa kwa mwendo mdogo au wa kawaida. Hali hii huwaruhusu wapandaji kuendana na mabadiliko yanayotokana na kukwea miinuko mirefu na mikubwa. Njia ya Marangu ndiyo inayofahamika kama rahisi zaidi lakini Rongai, Lemosho na zile za upande wa Kaskazini zimeonyesha mafanikio kwa kiasi kikubwa.    
Je itanichukua muda gani kukamilisha zoezi zima la upandaji mlima? Mpaka unafanikiwa kuupanda Mlima Kilimanjaro itategemea ni njia ipi utakayoichagua. Lakini kwa kawaida ili kukamilisha zoezi zima itakulazimu kutumia siku kuanzia tano mpaka kumi ukiwa njiani kuelekea kileleni. Wazoefu na wataalamu wanapendekeza muda mwingi utakaotumika kuupanda mlima huo ndio nafasi kubwa ya kufika kileleni huwepo. Na hii ni kutokana na urefu wake, njia ilivyo na mabadiliko ya hali ya hewa kuendana na afya ya mpandaji. Sio watu wote wanaoupanda Mlima Kilimanjaro hufika kileleni, wapo wanaofanikiwa, wengine wanaoishia njiani kwa kuchoka au kwa matatizo ya kiafya na wengine hufariki dunia. Hivyo ni vema kuyajua haya mapema na kujiandaa kukabiliana nayo, cha msingi ni kutokulazimisha kuendelea na safari pale unapoona mwili wako haukuruhusu kufanya hivyo ili kujipanga kwa wakati mwingine.    

Nipande mwenyewe au pamoja na watu wengine? Hakuna sheria inayomlazimu mtu kuwa na watu wengine ili kuupanda Mlima Kilimanjaro. Lakini ni lazima kuwepo kwa waongozaji wenye uzoefu na utaalamu wa shughuli hiyo kwani zipo changamoto kadhaa njiani mpaka kufika kileleni. Ingawa kwa sababu zoezi zima ni kufurahia tukio hilo huwa inapendeza ukiongazana na watu wengine, inaweza kuwa mke, mume, familia, ndugu, jamaa na marafiki.

Vitu gani unahitajika kubeba kwenye begi lako? Wasiliana na kampuni itakayokuongoza kuupanda mlima ili wakupatie maelekezo ya vitu muhimu vya kupakia kwenye begi lako. Wao ndio wenye utaalamu wa vitu vinavyohitajika pamoja na uzito wa mzigo utakaoweza kuumudu mpaka kufika kileleni. Kutokana na umbali wa safari ni vema kubeba vile unavyoshauriwa kuvibeba na vitakavyohitajika njiani ili kujiepusha na usumbufu utakaoweza kujitokeza.

Nawezaje kujiandaa kwa kupanda mlima? Kukwea mwinuko wenye urefu wa mita 5,895 sio jambo rahisi kwani linahitaji maandalizi ya muda mrefu hususani kama sio mtu unayefanya mazoezi mara kwa mara. Kama jambo lingine lolote unalotaka kulifanikisha maandalizi ya mapema yanahitajika. Hivyo basi maandalizi kama vile kufanya mazoezi ya kuuweka mwili wako katika hali nzuri ili kukabiliana na mabadiliko yoyote ni muhimu, muone daktari ili kufanya uchunguzi wa afya yako kama itakuruhusu kupanda mlima lakini pia kwa wenye uwezo hukata na bima ya afya kabisa ili kugharamia matatizo ya kiafya yatakayojitokeza.

Vipi kuhusu matatizo ya kiafya? Ni vema kuchukua tahadhari ya hali ya juu kuhusiana na afya yako kabla, wakati na baada ya kuupanda mlima huu mrefu zaidi barani Afrika. Hakikisha unafanya uchunguzi wa afya yako kabla ya kukata shauri la kufanya hivyo, waweke wazi waongozaji wa safari kuhusu afya yako, hakikisha kampuni utakayoitumia ina vifaa vya kitaalamu kukusaidia pindi matatizo ya kiafya yatakapojitokeza, lakini pia itakuwa ni vema kwenda kufanya uchunguzi wa afya yako baada ya kufanikiwa na zoezi zima la upandaji wa mlima.
Hakuna jambo linaloshindikana chini ya jua, kila kitu kinahitaji dhamira ya dhati, maandalizi ya kutosha na bidii kuhakikisha linafanikiwa. Kwa mbinu hizo chache zilizoshirikishwa na Jumia Travel kwako wewe msomaji, tunaamini kwamba sasa utakuwa umepata mwanga wa kutosha juu ya vitu gani unavyotakiwa kuvifahamu kabla ya kwenda kupanda mlima huu ambao watu mbalimbali wanasafiri maelfu ya kilometa kuja kuupanda.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4811,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: MAMBO TISA YA KUZINGATIA UNAPOTAKA KUUPANDA MLIMA KILIMANJARO
MAMBO TISA YA KUZINGATIA UNAPOTAKA KUUPANDA MLIMA KILIMANJARO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgsmOXHi10hQiwPeOWID9lnBORlocae9mtmcjcCovoKmjcLqVFe_Aa2BOX6BpUqL6Wf-DjsVRIhTPxMJjD7rechJ6-7q0ctrekj1gJNPj1zjylZuZKNAJK6Jz6m4oqyvWmKiX2jIC9Wd0Pd/s640/001.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgsmOXHi10hQiwPeOWID9lnBORlocae9mtmcjcCovoKmjcLqVFe_Aa2BOX6BpUqL6Wf-DjsVRIhTPxMJjD7rechJ6-7q0ctrekj1gJNPj1zjylZuZKNAJK6Jz6m4oqyvWmKiX2jIC9Wd0Pd/s72-c/001.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2017/08/mambo-tisa-ya-kuzingatia-unapotaka.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2017/08/mambo-tisa-ya-kuzingatia-unapotaka.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy