UFUNGASHAJI BIDHAA KUWAINGIZA AKINAMAMA KWENYE SOKO LA USHINDANI

Mwezeshaji wa mafunzo ya nembo na vifungashio, Emmanuel Bakashaya, akifundisha akinamama wa Green Voices jinsi nembo na vifungashio vi...


Mwezeshaji wa mafunzo ya nembo na vifungashio, Emmanuel Bakashaya, akifundisha akinamama wa Green Voices jinsi nembo na vifungashio vinavyopaswa kuonekana.


Akinamama wa Green Voices wakiwa katika ofisi  za Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wakijifunza kutoka kwa Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula, Raymond Wigenge, hivi karibuni.

Green Voices katika majadiliano ya vikundi juu ya njia mbali mbali za kutafuta rasilimali wakati wa mafunzo chini ya mwezeshaji Richard Jackson. 

Green Voices wakiangalia bidhaa za ujasiriamali za Mama Rocky (mwenye mtandio wa buluu) katika supermarket. Hii ni baada ya kumtembelea kiwandani kwake katika ofisi za Makao Makuu ya Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) jijini Dar es Salaam.

Dkt. Alicia Cedaba, Meneja wa Mradi wa Green Voices kutoka Hispania, akifundisha akinamama wanaotekeleza mradi huo nchini Tanzania. 

Akinamama wa Green Voices wakiwa katika mafunzo kwa vitendo katika makao makuu ya SIDO jijini Dar es Salaam.
Green Voices baada ya kuhitimu mafunzo. Walioketi kutoka kushoto ni Mratibu wa Green Voices nchini Tanzania, Secelela Balisidya, Mkurugenzi wa taasisi ya IMED iliyotoa mafunzo, Dkt. Donath Olomi na Meneja wa Mradi wa Green Voices kutoka Madrid, Hispania, Dkt. Alicia Cebada.


AKINAMAMA wanaotekeleza mradi wa Green Voices nchini Tanzania sasa wanalenga kuboresha bidhaa za kilimo wanazozalisha ili kuongeza tija ikiwa ni katika azma yao ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi.
Wakizungumza baada ya semina ya wiki moja iliyofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni, akinamama hao walisema elimu waliyoipata imewapa mwanga wa kuendeleza miradi yao na kuhakikisha wanaboresha bidhaa zao ili ziwezi kuingia katika soko la ushindani.
Miradi inayotekelezwa kupitia Green Voices Tanzania ni kilimo cha mihogo, kilimo cha matunda, uyoga, ufugaji wa nyuki, ukaushaji wa mbogamboga na utengenezaji wa majiko rafiki wa mazingira ambayo inatekelezwa katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Kigoma, Mwanza na Kilimanjaro.
“Nilikuwa nimekata tamaa nisijue nitauendelezaje mradi wangu, lakini kwa mafunzo niliyoyapata kutoka kwa wataalam mbalimbali, hakika nimehamasika na kuona kwamba ninaweza kusimama na kusonga mbele,” alisema Farida Makame ambaye anasimamia mradi wa Majiko ya Umeme-Jua mkoani Kilimanjaro.
Farida alisema amehamasishwa zaidi na mafunzo hayo, ambayo yamempatia mbinu mpya zaidi za kuendeleza mradi huo kwa wanawake wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Kwa upande wake, Abiah Magembe anayesimamia mradi wa Usindikaji wa Muhogo na Mtama katika Kijiji cha Kitanga, Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, amesema mafunzo ya jinsi ya kufungasha na kuweka nembo kwenye bidhaa yamempa mwanga mkubwa na kwamba sasa yeye na wenzake watazalisha bidhaa zao kwa kujiamini na kuziingiza kwenye soko la ndani na la kimataifa.
“Tunatengeneza bidhaa nyingi zinazotokana na muhogo na zina viwango vizuri, lakini kwa mafunzo tuliyoyapata, sasa tunaweza kuziboresha kwa kuhusisha taasisi husika kama Shirika la Taifa la Viwango (TBS) na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) ili tuingie kwenye ushindani wa kitaifa na kimataifa,” alisema Bi. Magembe.
Bi. Magembe alisema kwamba, bidhaa wanazozalisha kutokana na zao la muhogo ni unga unaotumika kwa uji na ugali, vitafunwa kama keki, mikate, skonzi, biskuiti, mandazi, sabuni ya unga pamoja na bidhaa nyingine nyingi.
Mazao mengine yanayopatikana katika muhogo ni mzizi wenyewe ambao unatafunwa mbichi au ukiwa umepikwa au kukaangwa, kwenye futari, miti na majani huweza kuzalisha bidhaa anuwai za viwandani kama vifaa vya nguo, karatasi, mafuta, kilevi, dawa za binadamu na plastiki wakati ambapo wanga (starch) hutumika kutengeneza dawa za madoa, gundi katika samani, rangi za awali za ukuta na sukari (sugar syrup).
Takwimu za kilimo cha muhogo duniani zinaonyesha kuwa, Afrika ni bara la tatu duniani kwa kuzalisha zaidi muhogo ambapo huzalisha takriban tani milioni 102.6 kila mwaka.
Tanzania ni nchi ya nne kati ya wazalishaji wakubwa wa muhogo barani Afrika baada ya Nigeria, Ghana na Congo DRC ambapo inaelezwa kwamba karibu ekari 670,000 za ardhi ya kilimo zinatumika kuzalisha muhogo, zao linalochangia karibu asilimia 15 za chakula kwa nchi nzima na karibu kaya 1,213,958 huzalisha muhogo nchini.
Regina Kamuli ambaye anasimamia mradi wa Majiko Banifu wilayani Mkuranga, alisema anashukuru wanakikundi wenzake wamejizatiti na sasa wanapata fursa ya kushiriki katika maonyesho mbalimbali yakiwemo ya kilimo kuonyesha majiko hayo ambayo ni rafiki wa mazingira.
“Hivi sasa baada ya kikundi kusajiliwa akinamama wamenufaika na mikopo nafuu kutoka Halmashauri ya Wilaya na kwa mafunzo haya tutaboresha majiko yetu ili tuyanadi katika maeneo mengi nchini Tanzania kwa sababu yanatumia kuni kidogo, hivyo kuokoa mazingira,” alisema Regina.
Magdalena Bukuku anaongoza kikundi cha akinamama wanaoshiriki Kilimo cha Uyoga huko Bunju jijini Dar es Salaam, ambapo anasema mafunzo ya ufungashaji na uwekaji wa nembo yamempa mwanga mkubwa ili kwenda kuboresha bidhaa zao ziingie kwenye ushindani.
“Tunazalisha uyoga kwa wingi kwa sasa na wateja wameongezeka, hata hivyo, ikiwa tutafungasha vizuri na kupanua kilimo chetu tunaweza kulifikia hata soko la kimataifa,” alisema.
 Mariam Bigambo na Monica Kagya wao wanashiriki ufugaji wa nyuki ambapo mbali ya kuvuna asali, lakini wanasaidia kutunza mazingira na kuongeza tija katika mazao ya kilimo kutokana na uchavushaji.
Wakati Mama Bigambo anaendesha Ufugaji wa Nyuki huko Dakawa, Morogoro, Bi. Monica yeye na akinamama wenzake wana jukumu kubwa la kutunza misitu ya Pugu na Kazimzumbwi wilayani Kisarawe kutokana na Ufugaji wa Nyuki.
“Tunataka tujikite katika kufungasha vizuri asali na kuziwekea nembo ili tuingie kwenye ushindani,” walisema.
Suala la ufungashaji na uwekaji wa nembo nalo limewagusa Esther Muffui, Dkt. Sophia Mlote na Leocadia Vedasto ambao wanashiriki katika kilimo na ukaushaji wa mboga na matunda.
“Tunajihusisha na Ukaushaji wa Mboga na Matunda kule Morogoro, sasa tulikuwa tunashindwa kufungasha vizuri, naamini tumepata mwanga wa namna ya kufungasha bidhaa zetu ili tupate tija zaidi,” alisema Bi. Esther.
Leocadia yeye anashiriki mradi wa Kilimo na Usindikaji wa Viazi Lishe huko Ukerewe mkoani Mwanza wakati Dkt. Mlote anashiriki mradi wa Kilimo Hai cha Nyanya na Mbogamboga Kinyerezi jijini Dar es Salaam.
Naye Evelyn Kahembe ambaye anaendesha Kilimo cha Matunda huko Uvinza, Kigoma, amesema mafunzo hayo yamemuongezea ujasiri wa kuendeleza mradi huo akishirikiana na wanawake wengine huko Kigoma.
Kwa upande wake, Mratibu wa Mradi wa Green Voices Tanzania, Bi. Secelela Balisidya, alisema mafunzo waliyoyapata yametoa mwanga mkubwa kwa washiriki na kuleta mtazamo wa kibiashara zaidi tofauti na hapo mwanzo.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: UFUNGASHAJI BIDHAA KUWAINGIZA AKINAMAMA KWENYE SOKO LA USHINDANI
UFUNGASHAJI BIDHAA KUWAINGIZA AKINAMAMA KWENYE SOKO LA USHINDANI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgE1wVJA_Kzl79S27KKnA9ljlBnHAMQVi2bBrHdQgeAEtcf3f9i1AghgJLyUYnQKC4xJgT1bvcu7WOeHV2OEJ52k0png1m1M0o7MZc7As4mKTCaiU9uJqdVKWlwMVd2mLOXtWaAaQGThyw/s640/G1.jpeg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgE1wVJA_Kzl79S27KKnA9ljlBnHAMQVi2bBrHdQgeAEtcf3f9i1AghgJLyUYnQKC4xJgT1bvcu7WOeHV2OEJ52k0png1m1M0o7MZc7As4mKTCaiU9uJqdVKWlwMVd2mLOXtWaAaQGThyw/s72-c/G1.jpeg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2017/08/ufungashaji-bidhaa-kuwaingiza-akinamama.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2017/08/ufungashaji-bidhaa-kuwaingiza-akinamama.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy