Nimemalizia
mwaka kwa kuangalia filamu za kibongo nne; Nazo ni Father Ezra, Fitina Dhidi
yangu, Nabii Mswahili na Why.
Ukiingalia
filamu ya Father Ezra katika nchi ambayo makanisa mapya yanayochipuka kila
kukicha kwa kasi unaweza kupata fadhaa amabyo mtengeneza sinema hii anayo.
Sinema
hii imegonganisha kwa kiwango kikubwa mawazo ndani ya kitabu husika, kwa
kuonesha watu wanavyokosa subira na kubaki kusubiri kupata muujiza.
Lakini
labda nawe umeiona filamu hii, kwa namna yako nikuulize weye kama mtaalamu wa
kutazama sinema na unayejua falsafa za filamu na maudhui yake katika jamii
inayoamini sana dini zake. Filamu ya Father Ezra umeionaje?
Nimekuuliza
ili urejee katika mahangaiko yako na utambue kwamba kutengeneza shari ni lazima
uwe na sababu na kuitafuta heri ni lazima uwe na sababu.
Simulizi
lake limejikita na kwa namna ambavyo jamii inapotoka na kuamini katika muujiza
na mali na hivyo kuabudu baali badala ya Mungu wa kweli. Hiki ni kizazi cha
nyoka ni kizazi cha Miujiza .
Hili
si swali lakini niulize kuwapo kwa uwingi wa makanisa ya kisasa yanayotangaza
ushuhuda wa mali hili haliwezi kuwa tatizo?
Sina
tatizo nayo kiprofesheno kwani naamini imetengenezwa katika hali ya
kuangalia makandokando ya imani zetu za kisasa kutokana alivyosimulia na
alivyojenga visa vyake akihimiza zaidi kutambua ukweli kwa macho na kupambana
na uwongo wake ka nguvu zote ukitambua kwamba huenda ni wewe peke yako unayejua.
Filamu
hii ina matatizo nya kihariri na hata upigaji picha wake, rangi yake kama
iliyohbabuka inaashiria mengi zaidi. Filamu hii kwenye thieta inaweza isifiti
kabisa.
Pia
namna alivyoingiza wahusika wenye miliki za ajabu katika njia ambayo ni rahisi
mno, kama mtu anayechunguza wakati kam a isivyojulikana mashetani yaliyobeba
sura za binadamu yanatokeas wapi angefanya hivyo lakini si kama anajifunza
wakati yeye ni gwiji.
Pia
namna ambavyo pete yake inatumika unatakiw akuwa maarifa ya kuangalia na kuna
sehemu effects zingetumika zaidi kuonesha nguvu ya pete sivyo mtu wa kawaida
hawezi kuunga maneno na vitendo.
Mbaya
zaidi inaonekana kanisa zima limepegawa na kuvutwa upande wa shetani.
Mbaya
zaidi kama mtu hujaiona hii ni namna vipande vya ubakaji vilivyowekwa, vipande
hivi vinaashiria wazi kwamba sinema hii watoto hawastahili kuiona, fikira
zimepelekwa wazi sana.
Mwanga
na sauti katika sinema hii si sawa ni kama vile mtu kaona sinema za ulaya
zinaozhusu waabuduo miungu na
kuijaribisha akikwepa kukamatwa.
Lakini
inamaliza kwa maneno ya kukuambia na kukuonesha kwamba kanisa hili na wafuasi
wake wanaongezeka kwani kundi lililoibuliwa limepwa nyenzo za kwenda
kutengeneza wafuasi wao wengine si
wanapenda miujiza?
Inaweza
kuwa chungu kumeza kwa watu waliopitiliza imani lakini ndio ukweli unaobeba na
maneno ya maandiko kwamba kizazi cha nyoka kinataka ishara na miujiza badala ya
kweli na subira.
Fitina
dhidi yangu
Sinema
hii ilistahili kubadilishwa jina kwani hili la sasa lina walakini kutokana na
asilimia 75 kuwa gubu la mke kabisa dhidi ya mkwe sasa hii fitina ipo asilimia
ndogo tu na mwisho wake ni mwepesi kwa imani yangu mimi.
Mwepesi
kwa kuwa mambo mazito yamefikiwa conclusion kwa sekunde chache tu tena kirahisi
rahisi kama utamaduni wa kizungu wakati waswahili ni vuta nkuvute.
WHY
Why
ni Bongo movies pamoja na viashiria vya mwanzo kuwa katika sinema kubwa
za Ulaya kwa kuonesha ndege nyingi angani, kuonesha nini kimo ndani ya sinema,
simulizi hili ndani unafungua na ndege na kumalizia na pingu.
Kiasi
fulani simulizi la mapenzi lililoenda kombo kwa uwongo, uzandiki,ukahaba na
subira dhaifu ya kudonoa ukweli na kasha bahati mbaya ya kupitiliza wakati wa
urekebishaji wa mambo. Kama ilivyo sinema yenyewe Kwanini (WHY) unaweza kubaini
maswali mengi mno. Kuna swali katika mapenzi, kuna swali katika maisha, kuna
swali katika undugu, kuna swali katikia kuokoa maisha na kuna swali katika haki
za binadamu. Mbaya zaidi suala kwanini kuwapo kwa kichefuchefu cha roho mbaya,
uwongo na usaliti.
Tunu
(Jennifer) aliwakilisha vyema nafasi yake ya maumivu ya upenzi na upendo kiasi
ya kwamba unaiona wazi katika sura yake na miondoko yake japo ana mistari
michache zaidi katika sinema hii.
Shamsa
Ford yumo katika sinema hii kwani yeye ndiye aliyesababisha Jamal kupata wazimu
baada ya kufa mikononi mwake wakati akitaka
kumzuia.
Kuna
baadhi ya sehemu zinasisimua lakini namna walivyomtaka Jamal awe kichaa nadhani
kunakosa la maandiko twisti za stori
haionekani wazi.
Nabii
Mswahili
Katika
sinema hizi nne nilizoangalia mwishoni
mwa mwaka hii ndiyo my favourite. Imetoka
kabisa katika sinema tulizozoea naiona kama Feature lakini wahusika wake katika
visa vidogo vidogo wamejenga hisia katika maisha ya kawaida yenye kujali
wastani na kiasi.
Kichaa
ambaye kwangu mimi kama mjulimlisha hoja na mtoa hoja kuu,anawakilisha taifa
lenye makunyanzi mengi katika maleba iliyojivika, ikiwa na busara lakini
haiaminiki. Simulizi lake japo liko na vipande hadithi imeungwa kutazama
uhalisia wa maisha katika jamii, mitafaruku katika rushwa kubwa na ndogo na
wajibu wa kila mwanakaya kutunza mazingira yake kuwa safi kuanzia
kichwani(akili) nyumbani anavyoongoza kaya na jinsi anavyoopokea shauri
mbalimbali.,
Hayo
ni machache niliyoyaona ambayo nilitaka
kushea nawe wakati tunamalizia mwaka, mwakani tutakuwa sana na review na
critique mbalimbali za sinema za hapa nyumbani.
Katika
sinema nimesema nimeipenda Nabii Mswahili na humu ndani kuna maeneo mawili ya
suspense ambayo yanakufanya usisimke
bila kuona. Moja ni wakati baba anamchapoa mwanawe anavyotoka
kumtandika,fmbo ilivyochakaa na alivyofura kwa hasira na mauaji ya ustaadhi
ambapo mtu anatoka amejaa damu na
kutimka, haitoshi kusimulia jinsi darekta alivyoskoa hapa.
Pia
kwenye close up za Why, Tunu ameshaini sana, ameshika nafasi yake ya
maumivu vyema kabisa. Unayeangalia unayaona yale maumivu,maumivu ya kupenda na
kuona unachopenda kinaharibika.
Tchao
Naitwa
Beda Msimbe nikiwa hapa kwetu Goba
Post a Comment
Post a Comment