WAZEE
280 wa kituo cha Sakila Hope for Elderly wamepatiwa zawadi ya
Christmasi na Wafanyakazi wa Kampuni ya Tanzania Cigarate Company (TCC) yenye
thamani ya Sh, milioni 10.
Wafanyakazi
hao wametumia fedha hizo kuwanunulia Wazee hao, vyakula ,nguo na
kuwakabidhi zawadi hizo, katika hicho, kilichopo Kata ya
Kikatiti , Wilaya ya Arumeru.
Mratibu
wa Kituo cha Sakila Hope for Elderly, Humphery Mafie akitoa shukurani kwa
niaba ya wazee hao ,alisema hayo jana na kusisitiza kuwa ,wafanyakazi hao ni
mfano wa kuigwa na kutaka watu wengine kujitokeza kusaidia wazee hao ,kwa kuwa
ni baraka kuwasaidia makundi hayo.
Mafie
alisema kuwa wanakazi kubwa ya kuwatunza na kuwapatia mahitaji wazee
hao na kudai kuwa ipo haja ya jamii nzima kushiriki kuwapatia msaada ili waweze
kuendelea kuishi kuwa siyo kazi rahisi kutunza kundi hilo kwa
kuwa wana mahitaji mengi ikiwa ni pamoja na kuwajengea nyumba za
kuishi katika makazi yao .
Aidha
anasema wanao wazee zaidi ya 10 wanaoishi kambini na kuomba jamii kujitokeza
kuwasaidia ili waaendelea kuishi na kusaidia jamii zao kwa kuwashauri kwa
kuzingatia ukweli kuwa wazee ni hazina
Mchungaji
Joseph Urio wa kanisa la Evangalism International ,Ngyeku,akielezea
huduma hiyo alisema kuwa watu wengi wamekuwa wabinafsi na familia zao
na kusahau wazee na kushindwa hata
kuwapatia chakula na kudai kuwa kitendo hicho ni kibaya.
Mchungaji
Urio alifafanua kuwa baadhi ya wazee wana watoto wao wenye uwezo wa kuwatunza
lakini wamekuwa wabinafsi na hawataki kusikia kuhusu jambo la kuwatunza wazazi
wao.
Wazee
wanaotunzwa katika kituo hicho wanatoa simulizi na kudai kuwa wana matumaini ya
kuishi maisha marefu kwa msaada wa vyakula na mavazi wanayopata
kutoka kutoka kwa watu wenye mapenzi mema na Kitu hicho.
Source:HabariLeo
Post a Comment
Post a Comment