Zuma alisema anajiuzulu mara moja japokuwa hakubaliani na uamuzi wa chama cha ANC cha kumtaka ajiuzulu.Chama cha ANC kilikuwa kimemuambia...
Zuma alisema anajiuzulu mara moja japokuwa hakubaliani na uamuzi
wa chama cha ANC cha kumtaka ajiuzulu.Chama cha ANC kilikuwa kimemuambia
aondoke madarakani au akabiliwe na kura ya kutokuwa na imani naye bungeni.
Zuma mwenye umri wa miaka 75 ambaye
amekuwa madarakani tangu mwaka 2009, amekuwa akituhumiwa matumizi mabaya ya
madaraka, ufisadi na rushwa.
Zuma katika hotuba yake ya kujiuzulu
alianza hotuba kwa kucheka na kufanya mzaha na waandishi wa hahari.
Baada ya kuwashukuru wale ambao amefanya
kazi nao kwa miaka kadhaa, Zuma alisema ameamua kujiuzulu kuepusha nyufa zaidi
katika chama chake cha ANC.
Alisema hataki kuona ANC inapotea au
kumeguka kwa sababu yake na hivyo anaamua kujiuzulu.
"Licha ya kutokubaliana na uamuzi
wa chama changu, siku zote nimekuwa mwanachama mwenye nidhamu wa ANC.
"Ninapoondoka, nitaendelea
kuwatumikia watu wa Afrika Kusini sawa na ANC, chama ambacho nimekitumikia
maisha yangu yote."
Lakini Zuma aliyezaliwa katika familia masikini na baadae kuishi
uhamishoni sababu ya kupinga ubaguzi wa rangi kabla ya kupanda ngazi na kushika
hatamu kama rais wa watu, hawezi kunusurika kashfa hizi kila mara.
Licha ya kukana mara zote tuhuma za rushwa dhidi yake tuhuma hizo
zimekuwa zikijirudia kila mara.
Zuma
mwaka 2009 kuelekea uchaguzi mkuu tayari alikuwa akikabiliwa na tuhuma za
rushwa na ubakaji.
Alituhumiwa kumbaka rafiki wa familia
yake ambaye anaishi na virusi vya ukimwi mwaka 2006, na wakati wa shauri
mahakamani Zuma alisema mahakamani kuwa alioga ili kujikinga na virusi vya
ukimwi.
Alikumbwa pia na tuhuma za utakatishaji
wa fedha na kupanga mpango katika mkataba tata wa silaha wa mwaka 1999. Mwaka
2017 iliamua tuhuma 18 za rushwa dhidi yake ziangaliwe upya.
Mara zote Zuma amekanusha tuhuma hizo na
kuapa kuachia ngazi ikithibitika kama ni kweli amehusika.
'Raisi wa Watu'
Ulikuwa ni utu wake ndio ulimpeleka Zuma madarakani mwaka 2009 wafuasi
wake waliona namna alivyokuwa akikubalika na wengi na kushika hisia zao na kuwa
mbadala wa Rais Thabo Mbeki ambaye alionekana kuwa mbali na watu.
Ukaribu wa bwana Zuma katika usimamizi na utetezi wa mila na desturi
katika familia ni miongoni mwa sababu zilizosababisha kujizolea wafuasi hasa
kwa raia masikini wa nchi hiyo wengi wao wakiwa ni wakazi wa vijijini.
Zuma
mwenye miaka 75 anajivunia ndoa za mitala kama ilivyo ilivyo desturi ya wazulu.
Zuma kwa sasa ana wake wa nne ameoa mara sita ana watoto 21 na mmoja wa wake
zake raia wa Msumbiji ,Kate Mantsho alijiua mwaka 2000.
Kadhalika anasifa ya kutokuwa mwaminifu katika ndoa zake na analea
mtoto wa nje ya ndoa na mwanamke mwingine.
Imani hii ya raia kwa Zuma kama rais wa watu haikudumu kwa muda mrefu
,mapema mwaka 2013 moshi ulianza kufuka baada ya Zuma kuboresha makazi yake ya
kijijini kwao Nkandla kaskazini mwa KwaZulu-Natal akitumia hela za serikali.
Wakati wa ibada ya mazishi ya Rais wa kwanza mweusi wa Taifa hilo
Nelson Mandela wafuasi wa ANC walikuwa wakimkosoa wazi wazi mbele ya wageni
mbali mbali wa kimataifa akiwemo aliyekuwa Rais wa Marekani wakati huo Barrack
Obama.
''Anakula wakati tuna njaa'' mmoja wa waandamanaji alisema na kuamsha
hasira kwa waandamanaji juu wa maboresho Zuma aliyofanya kwenye makazi yake
huko Nkandla ikiwa na eneo la kufugia ng'ombe, ukumbi wa Sanaa , bwawa la
kuogelea ,sehemu ya wageni na banda la kuku.
Bw Zuma alifanikiwa kulipa hela za ziada alizotumia.
Visa vya kisheria vinavyomuandama Zuma
§ 2005: Alituhumiwa kwa rushwa ya mabilioni ya dola kwenye mkataba wa silaha wa mwaka 1999 madai
ambayo yalitupiliwa mbali kabla hajawa rais mwaka 2009
§ 2016: Mahakama iliamuru ashitakiwe kwa makosa 18 ya rushwa dhiya yam kata wa silaha ambao
alikatia rufaa
§ 2005: Aishitakiwa kwa kumb'aka rafiki wa familia na
kufutiwa mashitaka2006
§ 2016: Mahakama iliamuru kuwa amekiuka kiapo chake kama
raisi na kutumia fedha za serikali kuboresha makazi yake binafsi fedha
ambazo alizilipa baadae
§ 2017: Wakili wa serikali alisema ateu jaji kiongozio wa
kamati ya kuchunguza iwapo ana uhusiano na familia tajiri ya Gupta madai ambayo
ameyakanusha
§ 2018: Zuma alikubali maombi hayo
Miaka mitatu Mahakama kuu nchi Afika
kusini iliamua kwamba amekiuka katiba kwa kushindwa kulipa pesa za serikali
alizo tumia kuboresha makazi yake binafsi
Rasi Zuma aliwaomba radhi raia wa nchi
hiyo kwa tuhuma hizo na kulipa fedha hizo.
Lakini tuhuma hizi za makazi
zilitarajiwa kufunikwa na tuhuma kubwa zaidi za namna alivyoingia madarakani.
Baada ya muda kidogo mahusiano ya Zuma
na familia tajiri ya India Gupta yakaanza kumulikwa tuhuma zikiwa ni kwamba
walishinikiza uteuzi wa baraza la mawaziri ili waweze kupata mikataba yenye
fedha nyingi ya serikali.
Tuhuma hizi zimepingwa vikali na Zuma
mwenyewe na hata familia ya Gupta.
Akiwa na miaka 17 Zuma alijiunga na ANC
na kuwa mwanacha hodari katika tawi lake la Jeshini Umkhonto We Sizwe,
mwaka1962.
Wake zake Zuma
§ Gertrude
Sizakele Khumalo alimuoa mwaka 1973
§ Nompumelelo
Ntuli (2008)
§ Thobeka
Madiba (2010)
§ Gloria
Bongi Ngema (2012)
Wake aliotalikiana nao
§ Nkosazana
Dlamini-Zuma (alimuoa mwaka 1972; na kuachana naye 1998)
§ Kate
Mantsho (alimuoa 1976; alifariki 2000)
Alihukumiwa kwa kula njama za kutaka
kupindua serikali ya kibaguzi ya makaburu na kufungwa miaka 10 katika gereza la
kisiwa cha Robben pamoja na Nelson Mandela.
Inaelezwa Zuma alikuwa akichochea morali
ya wapigania uhuru hawa kwa nyimbo na tungo za kizalendo na wengi wana amini
hiki ndo kilimfanya kuwa maarufu miongoni mwa Raia hata wale wa vijini kabla ya
kuupata uraisi
COMMENTS