Nilijiunga na gazeti hili wiki kadhaa kabla ya kuanza uchapishaji wake. Nilipokewa kwa namna ya ajabu na mchanyato wa waandishi walioku...
Nilijiunga
na gazeti hili wiki kadhaa kabla ya kuanza uchapishaji wake. Nilipokewa
kwa namna ya ajabu na mchanyato wa waandishi waliokuwa wameajiriwa kuanza
libeneke hili la serikali.
Mchanyato
huu waandishi mikiri kuwa niliona kuwa bora katika muda huo, na hata
nilipokutana na moto wa Gwiji la habari, niliafiki kwa kuwa lilikuwa kundi la vijana
wanaojiamini sana
Walipelekwa
katika semina ya kuwaweka sawa ili wajue wajibu wao, walifika chumba cha habari
baadaya semina hiyo wakiwa wameiva barabara kwa namna inavyofaa, na kwa namna
walivyoona inafaa.
Wakati
naingia nilikuwa natokea Jumba kubwa la magazeti kitaani, yaani the
Guardian Limited. Na hata Guardian Limited haikuwa mahali pangu pa kwanza kama
msanifu, la hasha nilitokea televisheni ya CTN baadaya kumaliza mkataba
wangu wa mwaka mmoja.
Awali
nilikuwa Media Holdings wachapishaji wa Mwananchi na The Express ambako
niliajiriwa kama Naibu Mhariri Msanifu Mkuu wa Media Holdings kabla sijawa
Mhariri wa Mwananchi, nikichukua nafasi ya mzee Barnabas Maro.
Nikiwa
mwananchi, CTN na Nipashe nilijifunza mengi sana kuhusu uendeshaji
wa vyombo vya habari binafsi, kwani historuia yangu ilianzia katika vyombo vya
serikali na baadaye ya chama tawala.
Nikiwa
na uzoefu wa kutosha wa magazeti binafsi nilijikuta naingia katika chombo cha
serikali chenye mchanganyiko mkubwa wa falsafa ya vyombo binafsi, ambayo mimi
nilikuwa nimeibatiza jina la kanyaga twende ili mradi una ushahidi.
Kila
mwajiri ana vitu vyake anavyotaka na hili ndilo muhimu sana kwa mhariri msanifu
kujua kwani lile ambalo unaambiwa mara kwa mara katika mafunzo ya kujua dunia
ipasavyo na hasa sheria za vyombo vya habari ni kitu kinachoeleweka
lakini hiki cha pili ni busara inayokuongoza.
Nakumbuka
wakati tunaanza, vijana walilalamika kwamba kuna wazee wamewekwa pale
kurudisha nyuma libeneke na wao wanataka kutoka kushindana na magazeti mengine
kuonesha kwamba wao si mchezo hata kidogo na hasa ukizingatia kwamba wao ndio
walikuwa mastaa walikotoka.
Naam,
kwa mimi ambaye nilikuwa nimeshakaa katika vyombo vya serikali na vya
chama (nilikuwa Radio Tanzania na Uhuru na Mzalendo) kwa takaribani miaka
nane nilijua watajifunza kwamba utumishi wa umma katika staili wanayokwenda
nayo ina ukakasi.
Na ndio
maana nilipompelekea toleo la kwanza baba yangu (naye ilitokea ni mtu wa
habari) aliponiuliza kama tutaweza kuendelea na ubora wa gazeti anaouona
pale nilimjibu sijui kwa kuwa ni gazeti la kila siku na hili limeandaliwa kwa
muda mrefu ili tutoke na Kishindo!
Alifurahishwa
sana na uchaguzi wa stori lakini alivutiwa sana na makala zilizokuwa
zimeshiba kisawasawa.
Hata
mimi niliona kuwa nguvu ya gazeti ni katika siku za usoni ni makala na habari
za vijijini kama zityafanyiwa kazi kwa kuwa ushindani wa kawaida wa kisiasa na
udaku ni kinyume na utamaduni wa chombo cha serikali.
Hii
inatokana na ukweli kuwa nguvu ya maandishi katika gazeti hili ni kubwa hasa
kutokana na kuwa gazeti la rejea.
Kazi ya
usanifu
Nina
kawaida ya kuwaambia watu wengi wanaoandika usimpe nafasi mhariri msanifu
kuharibu stori yako na kuondoa fleva ambayo unataka iwepo.
Katika
kazi hii ya uandishi wa habari ambapo robo tatu ya miaka yangu(nilianza rasmi
kazi hii 1985) nimeifanya kama Mhariri msanifu kuna mambo ya msingi ambayo
natakiwa kuyazingatia hivyo nikiona dalili ya kutaka kupelekwa chaka,
nitajitahidi kuvaa kiatu chako na hii kama nisipokuwa mwangalifu
nitaondoa fleva yako na ikifikia hapa natakiwa kitaratibu kuondoa jina katika
stori yako na kuiweka kama mchangiaji chini.
Kiukweli
moja ya raha ya kuw amhariri msanifu ni kule kujikuta umekwama kuendelea na
kusanifu maandishi kutokana na sentensi zisizoeleweka au kutupiwa maneneo
yasiyoeleweka au yalipangwa kama matofali yenye uzito tofauti.
Lipo
tatizo la wazi kabisa la watu kupanga maneno tu lakini habari yenyewe (facts)
ikatupiwa mgongo au kupakwa mafuta tu ya kuteleza , ikiwa haijashiba kisha
unatandikwa na maneno magumu kutoka kwa mwandishi anayetaka kuonesha kwamba
anajua anachoandika kumbe chenyewe kilistahili kuwa paragrafu mbili tu kujazia
mapengo ya gazeti.
Nilipokumbana
na hayo kitu change cha kwanza nilichokuwa nafikiri wakati nasoma
maandiko ni kutoa misamiati isiyoeleweka, kisha setensi zisizoeleweka halafu
huna stori , unarejea tena kujaribu kuitengeneza.
Tulianza
na mjengo wa ukurasa hivyo maneno yakipungua inabidi urejee tena au uitupe
stori utafute nyingine, mjengo ulilazimisha vitu vingi sana vibadilike.
Mnakubaliana
na mhariri wa habari kwamba mtatumia mjengo namba Fulani lakini
unakuja kuletewa maandiko ambayo yana maneno yamejaa tu yasyokuwa na
maana unatengeneza maandiko yawe na maana unajikuta umeondoka katika mjengo.
Uzoefu wangu ulinifanya baadae niseme mjengo utumike kutoondoka katika
ramani lakini usiwe msaafu.
Lakini
kazi ya kusanifu maandiko ya Habarileo mpaka leo ni ngumu si kwa sabau ya
sentensi tu bali kukosekana kwa muongozo wa nini ndio nini katika uandishi wa
Kiswahili kilichobora katika gazeti la serikali. Muongozo unaotumika ni ule wa
gazeti la Kiingereza, ambao kwa vyovyote vile hauna mahusiano mazri na lugha ya
Kiswahili ambayo wasemaji wake ni wa Manzese na Mgeta
Ni
dhahiri kwamba unapohariri maandiko, msanifu anakuwa na nafasi kubwa ya
kuona kwamba facts (takwimu) ni kitu ambacho si cha kuchezea lakini maoni
unaweza kuyafanya inavyotakiwa.
Katika
kipindi cha mwanzo chini ya uangalizi mkali wa Cassian Malima, hali ilikuwa
shwari akitoa nafasi ya kuboireshwa kwa gazeti kwa namna inavyofaa kwa jinsi
siku zinavyozidi kusonga, huku akitoa maelekezo kwa mujibu wa uzoefu wake.
Lakini
leo hii tunapozungumza kuhusu usanifu katika gazeti hili, tunazungumzia zaidi
Kiswahili katika mashindano ya kuuza gazeti.
Katika
medani ya siasa ndio kuna matatizo zaidi huku maandiko ya jamii ya kawaida
yakionekana kama ni daraja la chini kuliko gazeti. Huenda hili linatokana na
mabadiliko makubwa ya aina ya uandishi na kitambo kirefu kukaa bila
kupata retreat kama ile ya bagamoyo.
Wapo
waandishi wageni wengi ambao hawajui nini maana ya kufanyiakazi gazeti la
serikali na kwanini stori zinatakiwa kuwa na vyanzo vingi vya habari na lazima
kuwe na seal yaani habari yenye uthibityisho wa ukweli usiokanushika.
Wahariri
wasanifu kimsingi ni watu wa mwisho wanaohakikisha usahihi wa habari na utamu
wa habari kabla haujamfikia mlaji. Wapo watu wanaosema wahariri wasanifu
hawana sababu ya kuwapo.
Wanaona
kwamba kazi ya mhariri msanifu ni kuharibu kopi aliyoandika kuifanya ama ipooze
au iwe na msisimko usiotakiwa au kuadika kichwa cha habari ambacho si cha
kweli.
Mimi
naamini kwamba katika mfumo wa ulinzi wa kazi zinazoandikwa kwa kasi mhariri
msanifu ndio geti kuu la mwisho na kama yeye akiwa makini anaweza
kuokoa gazeti lisionekane ni kichwa cha mwendawazimu na kiwa mwangalifu gazeti
litapata sifa sana kwa kufanyakazi yake kitaaluma.
Kimsingi
hakuna mwandishi anayempenda msanifu anayefanyakazi yake kitaaluma kwani mara
zote humfanya mwandishi asimamie vidole ili kazi iwe na maana iliyokusudiwa.
Katika
gazeti la HabariLeo usanifu ni kazi ngumu kutokana na uasili wa kazi na pia
kutokana na aina ya uandishi uliopo kwa sasa katika jamii na pia katika vyombo
vya habari; huku vyombo vya habari vya kijamii vikiharibu kabisa mueonkano wa
dhamira njema ya uandishi wa habari, uzushi na udaku
Ninaamini
kuna mabadiliko makubwa katika uandishi na utoaji wa habari kwa HabariLeo.
Tunapozungumza miaka kumi tunazungumza mtoto aliye darasa la tatu akiwa ameanza
shule akiwa na umri wa miaka mitatu akaenda msingi akiwa na miaka 7
na mtoto huyu sasa hivi anajua nini anachotakiwa kwenda sekondari na pia chuo
kikuu.
Nimefanyakazi
na wahariri watatu mpaka sasa huku nikiwa chini ya wasanifu kurasa wakuu
wawili, tofauti za filosofia ya usahihi na spidi zinapishana sana.
Katika
chumba cha habari cha HabariLeo , sasa hivi ugomvi sio wazee wananyima njia ya
kufanyakazi , wameshabaini namna bora ya kuwa mtumishi wa umma,bali ni vichwa
vya habari wanavyoona vinakera sokoni.
Ukitaka
kutengeneza wahariri wasanifu wa baadae, unatoa nafasi ya uhuru wa watu
kufikiria nini wanadhani kinauza, kisha unapeleka, hawa walio wadogo wanafikiri
ni rahisi sana kutengeneza kichwa cha habari cha kuvutia katika mazingira ya
spidi ya sasa, lakini wanapotoa hoja ujkawasikiliza kesho wanakuja na kitu
kizuri zaidi.
Lakini
nimejifunza kitu katika safari yangu, kazi hii haihitaji unafiki, inahitaji
ushirikiano na ukweli na kila dhama ina dhama zake lakini la maana ni kutambua
filosofi nyuma ya kila habari unayohariri na kuna mufda maamuzi
yetu hayawezi kabisa kufanana na mahitaji ya soko bali mahitaji ya taaluma.
Na hii
inanyima nafasi ya kuwa na simulizi na vichwa vya kusisimua kwa kuwa wanazuoni
hubishana katika hilo wakati walaji hudharau hilo na kuvutiwa na kile
kilichowatandika haraka usoni.
Wasanifu
kazi kubwa ni kusahihisha na kuna wakati unapiga mzinga kutokana na
mwandishi kushindwa kwenda moja kwa moja au wakati wmingine unapiga mzinga kwa
triki na unawakasirisha wakubwa.
Hakuna
anayependa kufanya uhariri wa aina hii, na waandishi vijana wasingelipenda kuwa
na mhariri wa aina hii lakini katika maisha yangu ya uandishi nimegundua
unahitaji watu wa kufanya marekebisho na kuzuia ujinga kuwafikia walaji wa
habari ambao pamoja na kutaka kuburudishwa wanahitaji kuelimishwa.
Wanahitaji
habari ambayo imeandikwa vyema imenyooshwa na haina kigugumizi na wanaoweza
kufanya hivyo kwa spidi ni wachache na ndio maana uhariri usanifu ni kazi ya
mwalimu zaidi kuliko kuandika habari.kwani ni yeye ambaye anaangalia kazi
kabla ya kuchapishwa ni yeye anayenyoosha setensi na kuipa guvu inayotakiwa
habari andikwa na kama ilivyokazi nyingine za uandishi wa habari mhariri
msanifu anatakiwa kuwa makini na kasi katika kutekeleza kazi zake na has
kuhakikishakwamba muda unazingatiwa.
Katika
hili naweza kusema nimefanikiwakatika safari hii ambayo huenda bado muda kidogo
tutapumzika.
Kila la
Heri habariLeo
COMMENTS