Safari yangu ndani ya Habarileo kama mhariri msanifu

Nilijiunga na  gazeti hili wiki kadhaa kabla ya kuanza uchapishaji wake. Nilipokewa kwa namna ya ajabu na mchanyato wa waandishi walioku...


Nilijiunga na  gazeti hili wiki kadhaa kabla ya kuanza uchapishaji wake. Nilipokewa kwa namna ya ajabu na mchanyato wa waandishi waliokuwa wameajiriwa kuanza libeneke hili la serikali.
Mchanyato huu waandishi  mikiri kuwa niliona kuwa bora katika muda huo, na hata nilipokutana na moto wa Gwiji la habari, niliafiki kwa kuwa lilikuwa kundi la vijana wanaojiamini sana
Walipelekwa katika semina ya kuwaweka sawa ili wajue wajibu wao, walifika chumba cha habari baadaya semina hiyo wakiwa wameiva barabara kwa namna inavyofaa, na kwa namna walivyoona inafaa.
Wakati naingia nilikuwa natokea Jumba kubwa la magazeti  kitaani, yaani the Guardian Limited. Na hata Guardian Limited haikuwa mahali pangu pa kwanza kama msanifu, la hasha nilitokea televisheni ya CTN  baadaya kumaliza mkataba wangu wa mwaka mmoja.
Awali nilikuwa Media Holdings wachapishaji wa Mwananchi na The Express ambako niliajiriwa kama Naibu Mhariri Msanifu Mkuu wa Media Holdings kabla sijawa Mhariri wa Mwananchi, nikichukua nafasi ya mzee  Barnabas Maro.
Nikiwa mwananchi, CTN na  Nipashe  nilijifunza mengi sana kuhusu uendeshaji wa vyombo vya habari binafsi, kwani historuia yangu ilianzia katika vyombo vya serikali na baadaye ya chama tawala.
Nikiwa na uzoefu wa kutosha wa magazeti binafsi nilijikuta naingia katika chombo cha serikali chenye mchanganyiko mkubwa wa falsafa ya vyombo binafsi, ambayo mimi nilikuwa nimeibatiza jina la kanyaga twende ili mradi una ushahidi.
Kila mwajiri ana vitu vyake anavyotaka na hili ndilo muhimu sana kwa mhariri msanifu kujua kwani lile ambalo unaambiwa mara kwa mara katika mafunzo ya kujua dunia ipasavyo na hasa sheria za vyombo vya habari ni kitu kinachoeleweka  lakini hiki cha pili ni busara inayokuongoza.
Nakumbuka wakati tunaanza, vijana walilalamika kwamba kuna wazee wamewekwa pale  kurudisha nyuma  libeneke na wao wanataka kutoka kushindana na magazeti mengine kuonesha kwamba wao si mchezo hata kidogo na hasa ukizingatia kwamba wao ndio walikuwa mastaa walikotoka.
Naam, kwa mimi ambaye nilikuwa nimeshakaa katika vyombo vya serikali na vya  chama (nilikuwa Radio Tanzania na  Uhuru na Mzalendo) kwa takaribani miaka nane nilijua watajifunza kwamba utumishi wa umma katika staili wanayokwenda nayo ina ukakasi.
Na ndio maana  nilipompelekea toleo la kwanza baba yangu (naye ilitokea ni mtu wa habari) aliponiuliza kama tutaweza kuendelea na ubora wa gazeti  anaouona pale nilimjibu sijui kwa kuwa ni gazeti la kila siku na hili limeandaliwa kwa muda mrefu ili tutoke na Kishindo!
Alifurahishwa sana  na uchaguzi wa stori lakini alivutiwa sana na makala zilizokuwa zimeshiba kisawasawa.
Hata mimi niliona kuwa nguvu ya gazeti ni katika siku za usoni ni makala na habari za vijijini kama zityafanyiwa kazi kwa kuwa ushindani wa kawaida wa kisiasa na udaku ni kinyume na utamaduni wa chombo cha serikali.
Hii inatokana na ukweli kuwa nguvu ya maandishi katika gazeti hili ni kubwa hasa kutokana na kuwa gazeti la rejea.
Kazi ya usanifu
Nina kawaida ya kuwaambia watu wengi wanaoandika usimpe nafasi mhariri msanifu kuharibu stori yako na kuondoa fleva ambayo unataka iwepo.
Katika kazi hii ya uandishi wa habari ambapo robo tatu ya miaka yangu(nilianza rasmi kazi hii 1985) nimeifanya kama Mhariri msanifu kuna mambo ya msingi ambayo natakiwa kuyazingatia hivyo nikiona dalili ya kutaka kupelekwa chaka, nitajitahidi  kuvaa kiatu chako na hii kama nisipokuwa mwangalifu nitaondoa fleva yako na ikifikia hapa natakiwa kitaratibu kuondoa jina katika stori yako na kuiweka kama mchangiaji chini.
Kiukweli moja ya raha ya kuw amhariri msanifu ni kule kujikuta umekwama kuendelea na kusanifu maandishi kutokana na sentensi zisizoeleweka au kutupiwa maneneo yasiyoeleweka au yalipangwa kama matofali  yenye uzito tofauti.
Lipo tatizo la wazi kabisa la watu kupanga maneno tu lakini habari yenyewe (facts) ikatupiwa mgongo au kupakwa mafuta tu ya kuteleza , ikiwa haijashiba kisha unatandikwa na maneno magumu kutoka kwa mwandishi anayetaka kuonesha kwamba anajua anachoandika kumbe chenyewe kilistahili kuwa paragrafu mbili tu kujazia mapengo ya gazeti.
Nilipokumbana na  hayo kitu change cha kwanza nilichokuwa nafikiri wakati nasoma  maandiko ni kutoa misamiati isiyoeleweka, kisha setensi zisizoeleweka halafu huna stori , unarejea tena kujaribu kuitengeneza.
Tulianza na mjengo wa ukurasa hivyo maneno yakipungua inabidi urejee tena au uitupe stori utafute nyingine, mjengo ulilazimisha vitu vingi sana vibadilike.
Mnakubaliana na mhariri wa habari kwamba mtatumia mjengo namba Fulani lakini unakuja kuletewa maandiko ambayo  yana maneno yamejaa tu yasyokuwa na maana unatengeneza maandiko yawe na maana unajikuta umeondoka katika mjengo. Uzoefu wangu  ulinifanya baadae niseme mjengo utumike kutoondoka katika ramani lakini usiwe msaafu.
Lakini kazi ya kusanifu maandiko ya Habarileo mpaka leo ni ngumu si kwa sabau ya sentensi tu bali kukosekana kwa muongozo wa nini ndio nini katika uandishi wa Kiswahili kilichobora katika gazeti la serikali. Muongozo unaotumika ni ule wa gazeti la Kiingereza, ambao kwa vyovyote vile hauna mahusiano mazri na lugha ya Kiswahili ambayo wasemaji wake ni wa Manzese na  Mgeta
Ni dhahiri kwamba unapohariri maandiko, msanifu anakuwa na  nafasi kubwa ya kuona kwamba facts (takwimu) ni kitu ambacho si cha kuchezea lakini maoni unaweza kuyafanya inavyotakiwa.
Katika kipindi cha mwanzo chini ya uangalizi mkali wa Cassian Malima, hali ilikuwa shwari akitoa nafasi ya kuboireshwa kwa gazeti kwa namna inavyofaa kwa jinsi siku zinavyozidi kusonga, huku akitoa maelekezo kwa mujibu wa uzoefu wake.
Lakini leo hii tunapozungumza kuhusu usanifu katika gazeti hili, tunazungumzia zaidi Kiswahili  katika mashindano ya kuuza gazeti.
Katika medani ya siasa ndio kuna matatizo zaidi huku maandiko ya jamii ya kawaida yakionekana kama ni daraja la chini kuliko gazeti. Huenda hili linatokana na mabadiliko makubwa ya aina ya uandishi na kitambo kirefu kukaa bila kupata  retreat kama ile ya bagamoyo.
Wapo waandishi wageni wengi ambao hawajui nini maana ya kufanyiakazi gazeti la serikali na kwanini stori zinatakiwa kuwa na vyanzo vingi vya habari na lazima kuwe na seal yaani habari yenye uthibityisho wa ukweli usiokanushika.
Wahariri wasanifu kimsingi ni watu wa mwisho wanaohakikisha usahihi wa habari na utamu wa habari kabla haujamfikia mlaji. Wapo watu wanaosema wahariri wasanifu  hawana  sababu ya kuwapo.
Wanaona kwamba kazi ya mhariri msanifu ni kuharibu kopi aliyoandika kuifanya ama ipooze au iwe na msisimko usiotakiwa au kuadika kichwa cha habari ambacho si cha kweli.
Mimi naamini kwamba katika mfumo wa ulinzi wa kazi zinazoandikwa kwa kasi mhariri msanifu ndio geti kuu la mwisho  na kama yeye  akiwa makini anaweza kuokoa gazeti lisionekane ni kichwa cha mwendawazimu na kiwa mwangalifu gazeti litapata sifa sana kwa kufanyakazi yake kitaaluma.
Kimsingi hakuna mwandishi anayempenda msanifu anayefanyakazi yake kitaaluma kwani mara zote humfanya mwandishi asimamie vidole ili kazi iwe na maana iliyokusudiwa.
Katika gazeti la HabariLeo usanifu ni kazi ngumu kutokana na uasili wa kazi na pia kutokana na aina ya uandishi uliopo kwa sasa katika jamii na pia katika vyombo vya habari; huku vyombo vya habari vya kijamii vikiharibu kabisa mueonkano wa dhamira njema ya uandishi wa habari, uzushi na udaku
Ninaamini  kuna mabadiliko makubwa katika uandishi na utoaji wa habari kwa HabariLeo. Tunapozungumza miaka kumi tunazungumza mtoto aliye darasa la tatu akiwa ameanza shule akiwa na  umri wa miaka mitatu akaenda msingi akiwa na miaka 7  na mtoto huyu sasa hivi anajua nini anachotakiwa kwenda sekondari na pia chuo kikuu.
Nimefanyakazi na wahariri watatu mpaka sasa huku nikiwa chini ya wasanifu kurasa wakuu wawili, tofauti za filosofia ya  usahihi na spidi zinapishana sana.
Katika chumba cha habari cha HabariLeo , sasa hivi ugomvi sio wazee wananyima njia ya kufanyakazi , wameshabaini namna bora ya kuwa mtumishi wa umma,bali ni vichwa vya habari wanavyoona vinakera sokoni.
Ukitaka kutengeneza wahariri wasanifu wa baadae, unatoa nafasi ya uhuru wa watu kufikiria nini wanadhani kinauza, kisha unapeleka, hawa walio wadogo wanafikiri ni rahisi sana kutengeneza kichwa cha habari cha kuvutia katika mazingira ya spidi ya sasa, lakini wanapotoa hoja ujkawasikiliza kesho wanakuja na kitu kizuri zaidi.
Lakini nimejifunza kitu katika safari yangu, kazi hii haihitaji unafiki, inahitaji ushirikiano na ukweli na kila dhama ina dhama zake lakini la maana ni kutambua filosofi  nyuma ya kila habari unayohariri na kuna mufda maamuzi  yetu hayawezi kabisa kufanana na mahitaji ya soko bali mahitaji ya taaluma.
Na hii inanyima nafasi ya kuwa na simulizi na vichwa vya kusisimua kwa kuwa wanazuoni hubishana katika hilo wakati walaji hudharau hilo na kuvutiwa na kile kilichowatandika haraka usoni.
Wasanifu kazi kubwa ni kusahihisha na kuna wakati  unapiga mzinga kutokana na mwandishi kushindwa kwenda moja kwa moja au wakati wmingine unapiga mzinga kwa triki na unawakasirisha wakubwa.
Hakuna anayependa kufanya uhariri wa aina hii, na waandishi vijana wasingelipenda kuwa na mhariri wa aina hii lakini katika maisha yangu ya uandishi nimegundua unahitaji watu wa kufanya marekebisho na kuzuia ujinga kuwafikia walaji wa habari ambao pamoja na kutaka kuburudishwa wanahitaji kuelimishwa.
Wanahitaji habari ambayo imeandikwa vyema imenyooshwa na haina kigugumizi na wanaoweza kufanya hivyo kwa spidi ni wachache na ndio maana uhariri usanifu ni kazi ya mwalimu zaidi kuliko kuandika habari.kwani ni yeye ambaye anaangalia kazi  kabla ya kuchapishwa ni yeye anayenyoosha setensi na kuipa guvu inayotakiwa habari andikwa na kama ilivyokazi nyingine za uandishi wa habari mhariri msanifu anatakiwa kuwa makini na kasi katika kutekeleza kazi zake na has kuhakikishakwamba muda unazingatiwa.
Katika hili naweza kusema nimefanikiwakatika safari hii ambayo huenda bado muda kidogo tutapumzika.
Kila la Heri habariLeo
Description: https://ssl.gstatic.com/ui/v1/icons/mail/images/cleardot.gif


COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Safari yangu ndani ya Habarileo kama mhariri msanifu
Safari yangu ndani ya Habarileo kama mhariri msanifu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEikNnD82ziF4sZY0WDHHBhKhO6YpfxiX7vw8nKKFlIHy2CxJlJYQk1mcjmxBwYZv7mwhzpiE0b4d8LRKh9PP5k6ArUy6oVvles79MIfwUuZ58teTgYL58MFnFiIIBVpEbeRoKXip8RLA-6n/s320/PICHA+YA+BEDA+KATIKA+MASOMO.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEikNnD82ziF4sZY0WDHHBhKhO6YpfxiX7vw8nKKFlIHy2CxJlJYQk1mcjmxBwYZv7mwhzpiE0b4d8LRKh9PP5k6ArUy6oVvles79MIfwUuZ58teTgYL58MFnFiIIBVpEbeRoKXip8RLA-6n/s72-c/PICHA+YA+BEDA+KATIKA+MASOMO.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2018/03/safari-yangu-ndani-ya-habarileo-kama.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2018/03/safari-yangu-ndani-ya-habarileo-kama.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy