UNIDO TAYARI KUSAIDIA TANZANIA YA VIWANDA

UNIDO tayari kusaidia Tanzania ya viwanda UNIDO tayari kusaidia Tanzania ya viwanda Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Viwanda...

UNIDO tayari kusaidia Tanzania ya viwanda

UNIDO tayari kusaidia Tanzania ya viwanda

Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Viwanda (UNIDO) limesema litasaidia Watanzania kutimiza ndoto za kuwa taifa lenye uchumi wa kati linalotegemea viwanda kwa kuunga mkono utendaji wa pamoja wa sekta ya umma na binafsi.

Kauli hiyo imetolewa katika hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Sekta Binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO Li Yong ambaye alikuwa katika ziara ya kwanza nchini Tanzania na pia ya kwanza nje ya makao makuu ya Shirika hilo baada ya kuchaguliwa kwake kwa mara ya pili mwaka jana.

Alisema katika hotuba yake kwamba moja ya majukumu makubwa ya shirika hilo ni kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) hasa lengo namba tisa la maendeleo na teknolojia kwa ajili ya ustawi wa nchi hizo.

Aidha alisema ili kufanikisha hilo kumesisitizwa ushirikiano ambao ni lengo namba 17 la SDGs.

Alisema sekta binafsi ikishirikiana vyema na serikali ndiyo inayoendesha uchumi hasa katika kutoa fursa za kazi kwani asilimia 80 ya kazi kila mwaka hutolewa na sekta binafsi.

Alisema katika hotuba yake hiyo kwamba amefurahishwa na malengo ya Tanzania na nia ya Shirika hilo kuona kwamba malengo hayo kuelekea uchumi wa kati wa viwanda yanatekelezwa kwa kuangalia vionjo muhimu.

Aidha alisema kwamba wataendelea kushirikiana na sekta binafsi kupitia TSPF kuhakikisha kwamba wananchi wanashirikishwa katika malengo ya maendeleo ili kuwa na malengo endelevu na yanayozingatia mazingira.

Naye Mwenyekiti wa Sekta Binafsi nchini- TPSF Dr. Reginald Mengi akizungumza katika hafla hiyo aliitaka UNIDO kusaidia kutengeneza utajiri nchini Tanzania.

Dr. Mengi alisema kwamba ziara ya kiongozi huyo imekuja wakati muafaka, wakati ambapo Tanzania inaelekeza macho yake katika uchumi wa kati na hivyo kuwa na nafasi ya kusaidia ndoto hiyo kufanikiwa.

Alisema wakati nchi nyingi zimekuwa zikipiga maendeleo, zimekuwa na msingi dhaifu wa uchumi wa viwanda kutokana na kusafirisha zaidi bidhaa ambazo hazijasindikwa au zinazotokana na uziduaji.

Alisema hali hiyo pamoja na kuipa utajiri nchi imekuwa haitawanyi utajiri uliopo.

Alisema kutokana na hali hiyo, UNIDO ina kazi kubwa ya kusaidia Tanzania kufikia lengo lake la viwanda hata kusaidia kuanzishwa kwa maeneo ya viwanda (Industrial Park).

Aidha aliishukuru UNIDO kwa kuwezesha sekta binafsi na serikali kukaa pamoja kupitia Baraza la Taifa la Biashara ambako kunakuwa na mazungumzo yenye tija kuhusiana na maendeleo ya biashara na uchumi nchini Tanzania.

Alifafanua kwamba UNIDO ina nafasi kubwa ya kuisaidia Tanzania hasa katika mipango mikakati yake kwa kuunganisha sekta binafsi na umma ili kuiharakisha Tanzania kuelekea uchumi wa kati wenye kutegemea viwanda.

Wakati huo huo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda pamoja na Kimataifa Dr Augustine Mahiga, ambaye wizara yake ndiye ilimwalika Mkurugenzi mkuu huyo, pamoja na kumshukuru kwa kuitikia wito huo aliitakabkusaidia kuchagiza maendeleo ya viwanda.

Alisema kwamba viwanda vya Tanzania bado vichanga na vinahitaji kusaidiwa na kupewa nguvu ya kuendelea mbele kwani pamoja na uchanga wake mchango wake katika kuelekea uchumi wa kati ni mkubwa.

Awali kabla ya hafla ya chakula cha mchana UNIDO ilitiliana saini na serikali ya Tanzania waraka wa kusaidia kuitoa Tanzania katika mipango ya kitaifa kwenda kwenye mipango ya nchi na washirika ili kufikia uchumi wa kati.

Makubaliano hayo yalisainiwa jijini Dar es Salaam kati ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO, Li Yong huku yakishuhudiwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.

Mwenyekiti wa Sekta Binafsi nchini- TPSF Dr Reginald Mengi (wa tatu kulia) akifurahi jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuendeleza Viwanda – UNIDO Bw. Li Yong (kushoto), Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage (wa pili kushoto) pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Kikanda na Kimataifa Dr Augustine Mahiga (kulia) katika chumba maalum mara baada ya kuwasili kwenye hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na sekta binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu huyo wa UNIDO iliyofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Godfrey Simbeye akitoa utambulisho wakati wa hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Sekta Binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO Li Yong (hayupo pichani) ambaye alikuwa katika ziara ya kwanza nchini Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Sekta Binafsi nchini- TPSF Dr Reginald Mengi akisalimia wadau wa sekta binafsi na wageni waalikwa wakati wa hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Sekta Binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO Li Yong (wa pili kulia) ambaye alikuwa katika ziara ya kwanza nchini Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Wengine ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage (kulia), Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuendeleza Viwanda nchini (UNIDO), Stephen Kargbo (wa pili kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) Leodegar Tenga (kushoto) wakiwa meza kuu.

Mwenyekiti wa Sekta Binafsi nchini- TPSF Dr Reginald Mengi akitoa neno la ukaribisho kwa Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO Li Yong (hayupo pichani) na wadau walioshiriki hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Sekta Binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu huyo wa UNIDO ambaye alikuwa katika ziara ya kwanza nchini Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akizungumza ambapo alisema Tanzania inategemea kunufaika na ujio wa mgeni huyo, katika uendelezaji wa viwanda nchini wakati wa hafla hiyo ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Sekta Binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO Li Yong (hayupo pichani) ambaye alikuwa katika ziara ya kwanza nchini Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Kikanda na Kimataifa Dr Augustine Mahiga akizungumza katika hafla hiyo ambapo alisema ujio huo unatokana na mwaliko wa wizara yake uliofanywa kimkakati wakati huu ambapo serikali imedhamiria kuigeuza Tanzania kuwa ya viwanda iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuendeleza Viwanda – UNIDO Bw. Li Yong akitoa salamu za UNIDO wakati wa hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Sekta Binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu huyo ambaye alikuwa katika ziara ya kwanza nchini Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Sekta Binafsi nchini- TPSF Dr Reginald Mengi (kulia) akiteta jambo na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuendeleza Viwanda nchini (UNIDO), Stephen Kargbo wakati wa hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Sekta Binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO Li Yong (hayupo pichani) ambaye alikuwa katika ziara ya kwanza nchini Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Viongozi wa meza kuu wakifanya ‘Cheers’ ishara ya kutakiana afya njema na ushirikiano mwema katika maendeleo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuendeleza Viwanda – UNIDO Bw. Li Yong wakati wa hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Sekta Binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu huyo ambaye alikuwa katika ziara ya kwanza nchini Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Pichani juu na chini ni sehemu ya wadau wa sekta binafsi na serikali walioshiriki kwenye hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Sekta Binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO Li Yong (hayupo pichani) ambaye alikuwa katika ziara ya kwanza nchini Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuendeleza Viwanda – UNIDO Bw. Li Yong katika picha ya pamoja na wadau wa sekta binafsi na viongozi wa serikali mara baada ya hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Sekta Binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu huyo ambaye alikuwa katika ziara ya kwanza nchini Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Sekta Binafsi nchini- TPSF Dr Reginald Mengi na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuendeleza Viwanda – UNIDO Bw. Li Yong wakiagana kwa furaha mara baada ya zoezi la picha ya pamoja wakati wa hafla ya chakula cha mchana iliyoandaliwa na Sekta Binafsi kwa Mkurugenzi Mkuu huyo ambaye alikuwa katika ziara ya kwanza nchini Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,301,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,23,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: UNIDO TAYARI KUSAIDIA TANZANIA YA VIWANDA
UNIDO TAYARI KUSAIDIA TANZANIA YA VIWANDA
http://dewjiblog.co.tz/wp-content/uploads/2018/03/MENGI-AGANA.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2018/03/unido-tayari-kusaidia-tanzania-ya.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2018/03/unido-tayari-kusaidia-tanzania-ya.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy