TAARIFA KWA UMMA MSAMAHA WA RAIS KWA WAFUNGWA KATIKA KUADHIMISHA MIAKA 54 YA MUUNGANO WA TANZANIA TAREHE 26 APRILI, 2018 Katika ...
TAARIFA KWA UMMA
MSAMAHA WA
RAIS KWA WAFUNGWA KATIKA KUADHIMISHA MIAKA 54
YA MUUNGANO
WA TANZANIA TAREHE 26 APRILI, 2018
Katika kuadhimisha Miaka 54 ya Muungano wa
Tanzania tarehe 26 Aprili, 2018
Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutumia madaraka
aliyopewa chini ya Ibara ya 45(1)(d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania ametoa msamaha kwa wafungwa wafuatao:-
(i)
Wafungwa wote wapunguziwe robo (1/4)
ya adhabu zao baada ya punguzo la kawaida la moja ya tatu (1/3) linalotolewa chini ya Kifungu 49(1)
cha Sheria ya Magereza Sura ya 58, wafungwa hao
sharti wawe wametumikia robo (1/4) ya adhabu zao
gerezani isipokuwa wafungwa walioorodheshwa katika Ibara ya 2(i – xxi).
(ii)
Wafungwa wagonjwa wenye magonjwa kama UKIMWI,
Kifua kikuu (TB) na Saratani (Cancer) ambao wako kwenye “terminal stage”. Wafungwa hawa wathibitishwe na Jopo la Waganga
chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa
Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya.
(iii)
Wafungwa wazee wenye umri wa miaka sabini (70) au
zaidi. Umri huo uthibitishwe na Jopo la
Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga
Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya.
(iv)
Wafungwa wa kike walioingia na mimba gerezani,
pamoja na wale walioingia na watoto wanaonyonya na wasionyonya.
(v)
Wafungwa wenye ulemavu wa mwili na akili (Physical disability and mental disability).
Ulemavu huo uthibitishwe na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya.
2. Aidha, Msamaha wa Mheshimiwa Rais
hautawahusu wafungwa wafuatao:-
(i)
Wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa au kwa
makosa ya kujaribu kuua (attempt to
murder).
(ii)
Wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa na
adhabu hiyo kubadilishwa kuwa kifungo cha maisha au kifungo gerezani.
(iii)
Wafungwa waliohukumiwa kifungo cha maisha
gerezani.
(iv)
Wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa ya
kujihusisha na usafirishaji na matumizi ya madawa ya kulevya kama vile cocaine, heroin, bhangi n.k.
(v)
Wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa ya
kujihusisha na uombaji na upokeaji au utoaji rushwa.
(vi)
Wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa ya
unyang’anyi na unyang’anyi wa kutumia silaha au kujaribu kutenda makosa hayo (robbery with violence, armed robbery and
attempted robbery).
(vii)
Wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa ya
kupatikana na silaha, risasi au milipuko isivyo halali (fire arms, ammunitions and explosives).
(viii)
Wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa ya
shambulio la aibu, kunajisi, kubaka na kulawiti, ukatili dhidi ya watoto au
kujaribu kutenda makosa hayo.
(ix)
Wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa
kifungo kwa kosa la kuwapa mimba wanafunzi wa Shule za Msingi na Shule za
Sekondari na ambao walitenda kosa hilo wakiwa na umri wa miaka kumi na nane
(18) na kuendelea.
(x)
Wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa ya wizi
wa magari na pikipiki, uharibifu wa miundombinu au kujaribu kutenda makosa
hayo.
(xi)
Wafungwa wanaotumikia kifungo chini ya Sheria ya
Bodi ya Parole (Act. No. 25/1994), Sheria ya Huduma kwa Jamii (Act. No. 6/2002)
na Kifungo cha Nje {The Prisons (Extra Mural Penal Employment) Regulation}.
(xii)
Wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa
kifungo kwa makosa ya kutumia vibaya madaraka yao na kuhujumu uchumi.
(xiii)
Wafungwa waliowahi kupunguziwa kifungo na Msamaha
wa Mhe. Rais na bado wangali wanaendelea kutumikia sehemu ya kifungo kilichobaki.
(xiv)
Wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kwa
kosa la kuzuia watoto kupata masomo.
(xv)
Wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kwa
kosa la utekaji wa watoto, kupoka na kufanya biashara ya binadamu (Human
Trafficking).
(xvi)
Wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kwa
kosa la kukutwa na viungo vya binadamu.
(xvii)
Wafungwa wanaotumikia vifungo kwa makosa ya
kujihusisha kwa namna yoyote ile na nyara za Serikali na ujangili (poachers).
(xviii)
Wafungwa wanaotumikia vifungo kwa makosa ya
wizi/ubadhirifu wa fedha za Serikali.
(xix)
Wafungwa
wanaotumikia vifungo kwa makosa ya kutoroka au kujaribu kutoroka chini ya
ulinzi halali au kusaidia kutendeka kwa makosa hayo na bado wangali wanatumika
adhabu hizo.
(xx)
Wafungwa
walioingia gerezani baada ya tarehe 7 Aprili, 2018.
(xxi)
Wafungwa
waliowahi kufungwa gerezani (warudiaji) na wale wenye makosa ya kinidhamu
gerezani.
3. Wafungwa 3,319 watafaidika na Msamaha huu ambapo 585 wataachiliwa huru tarehe 26 Aprili, 2018 na 2,734 watabaki gerezani kumalizia
sehemu ya kifungo kilichobaki baada ya kupewa msamaha huu. Ni mategemeo ya
Serikali kwamba watarejea tena katika jamii kushirikiana na wenzao katika
ujenzi wa Taifa na kwamba watajiepusha kutenda makosa ili wasirejee tena
gerezani.
Imetolewa
na:
Meja Jenerali (Mstaafu) Projest Rwegasira
KATIBU MKUU
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
COMMENTS