Filamu

Kazi ya Mussa Banzi yenye simulizi za asili

Na Beda Msimbe
TUPO kwenye wakati ambapo simulizi nyingi za mapenzi lakini kila simulizi unaweza kuliona raha yake kubwa ni kuonesha mitikisiko ya kupenda na kufumaniana au kuachana.
Simulizi hizi siku zote zimelenga kuywapata vijana ambao ndio waangalizi wa sinema.
Mussa Banzi naye hayuko nyuma katika hilo, lakini kwa mara nyingine tena mapenzi ameyaunga katika simulizi la zamani, simulizi ambalo chanzo chake ni kitu kidogo,kisasili cha ndege Gawa.
Kwa wakazi wa Mkuyuni ndege Gawa wamempachika jina la mpasua sanda kutokana na ukweli kuwa anapolia au unapomuona usiku ujuwe hapo kwenye nyumba yako kuna mushkeri utakuandamana, kifo.
Lakini unapofika mwishoni mwa hadithi hii unagundua kwamba ndege huyu anapoonekana mchana hasa jioni huwa anatoa taarifa nzuri ya mabadiliko ya maisha yako kutoka kule unakotoka.
Gawa ndiye anayejenga simulizi ambalo upande mkubwa lina chuki na husuda na migogoro ya kifamilia ambayo ilikuwa inatishia ustawi wa maeneo  na mapenzi.
Naam madairekta wawili Mussa Banzi na Mgeni khamisi walifanya kazi ya kutosha  kutafuta watu wanaofanana na mazingira na mazingira yanayofanana na hadithi hii, hadithi ambayo ina aina ya raha yake kwa kuzingatia kwamba imetwaliwa kutoka katika imani za kiasili.
Simulizi lake ,limejijenga katika imani za wananchi kwamba ndege huyo gawa anapokutokea unajawa na mikosi au misiba. Lakini jinsi banzi alivyotwisti simulizi ndege huyo anakuja na taswira nyingine, ya bahati na mabadiliko ya maisha ya watu.
Binti ambaye alikuwa anangoja kukutana na mchumba wake mtoni anakuta akimshangilia ndege gawa kwa rangi zake, lakini mwenzake anamuona kwamba, ndege huyo ni mikosi.
Baada ya kupewa maelezo hayo  Avana , nafasi iliyochezwa Husna Chobis, anaondoka mtoni pale na kuelekea kwa mganga Nyambi nafasi iliyochezwa na Nyambi kuitaka tafsiri ya kuonwa na ndege huyo jioni ile.
Maelezo ya fundi (mganga) yanamchanganya Avana ambaye alisema kwamba ana mchumba wake Diko, mtu ambaye alikuwa anajua kusoma.
Fundi anasema kwamba Avanna hataolewa na mchumba wake wa sasa lakini ataolewa na mchumba ambaye hajui kusoma na anaishi maisha ya kawaida kijiji kwao.
Utabiri huu wa Nyambi ndio unakuja kutokea lakini si kwa namna ambayo wewe unaweza kuing’amua kwa haraka.
Anaporejea kutoka kwa Fundi, Avana anampasulia wazi mpenzi wake Diko kwamba ndiyo imetoka hawawezi kufunga ndoa.
Ukiangalia simulizi hili lipo wakatik wakoloni wanaingia na wananchi wanapewa maarifa ya dini ya wazungu lakini wakati huo huo watu waliopata nafasi ya kusoma wakila njama kuwapora wengine mali zao.
Pili majeshi aliyecheza nafasi ya mama yake Avanna alionekana kuwa kweli mama mchimvi ambaye  alikuwa anakula njama za kumpora Chega eneo lake la mto mbezi , eneo alilorithi kutoka kwa baba yake.
Chega ambaye kitaalamu ni fundi (mganga) bado kijana lakini akiishi na dada yake Otesa nafasi iliyochezwa na Sada Ubeo.
Katika mazingira yaliyolelewa na simulizi hili uadui unaibuliwa tangu mapema, uadui ambao unafanya familia ya  Chega na akina Avanna kutolewana.
Familia hizi zenye uadui wa muda mwingi na njama za wazi za kutaka kumiliki mali za wengine zinasababisha vifo vya watu wasiokuwa na hatia, lakini mwishoni  sumu iliyooenea inakuja kutanzuliwa na haja ya matibabu kwa Avanna kitu kilichotokea bila hata kutarajiwa.
Baada ya njama za kutwaa ardhi kirahisi kutofanikiwa zinaandaliwa njama za kumuua Chega lakini kwa bahati mbaya anauawa mtu mwingine na Chega analipuka kwa hasira.
Anafika kwa akina Avanna na kuanzisha varangati kubwa ambalo kesho Avanna mwenyewe anashiriki lakini kwa namna  ya pekee ugomvi unamalizika na mama Avanna anaendeleza njama zake kwa kumfikisha Chega kwa mamlaka.
Chega anashinda shauri lile na kuwashutumu sana familia ile kama muuaji.
Lakini siku moja Avanna akiw amtoni anaanguka na mtu aliyemuohjna alimkimbiza kw amatibabu nyumbani wka fundi Chega ambaye awali anakataa lakini baada ya kuraiwa na dada yake anamtibia na anapoamka anagombana naye kwanini anamshikashika.
Naam, ni simulizi la aina yake ambalo baadaye linaokoa na kubadili kabisa tabia ya Avanna,anatokea kumpenda Chega na kukubali kuolewa naye, mtihani mkubwa ukiwa inakuaje watoto wa maadui wanapokutana na kuanzisha mapenzi.
Kuonesha kwamba kweli anampenda Chega, Avanna aliiba hati halisi ya eneo la mto mbezi aliyoibiwa Chega na rafiki yake Funga na kumrejeshea mwenyewe.
Lakini katika kumpoteza Chega mama wa Avanna aliagiza wabaya wake kufanyakazi ya kumuua Chega ambaye alipondeka vibaya lakinbi alipona na baadaye yeye na Avanna kufanya mazungumzo na mama yake Avanna.
Simulizi hili linamalizika wka amani zaidi na kuonekana kwamba kumbe mapenzi yanaweza kuondoa chuki.
Gawa yule ambaye  mtabiri Nyambi alisema kuonekana kwake kutabaduili mfumo wa Avanna, kweli alipeleka salamu sahihi kwani kutoka mtoto wa kike jeuri asiyejali, mpaka mpenzi mwenye kujali na hata kuwa fimbo ya kujishikiza Chega.
Moja ya vitu vya kifolosophia ambavyo unaweza kuona katika picha ni maji yakiwa yanatiririka na katika simulizi za watu wa Morogoro, maji ni uhai na unaondoa fitina zote na kusafisha dhambi.
Maji huunganisha  na maji hutumika kutambika. Kwa wanaojua maana ya maji ,banzi alifanya vyema kuanza na kumalizia katika maji ambako ndiko kwenye uhai.
Hadithi nimeipenda kwa kuwa ilikuwa imejaa nakshi zinazotakiwa, simulizi za kienyeji katika mazingira ya kienyeji, majira ya kati ambayo hayaumizi sana.
Kiukweli simulizi la gawa ambalo pengine ni simulizi la nne lenye mwelekeo wa asili kutoka kw a Mussa Banzi kunaonesha bado haja kubwa ya watuj kuendelea kutumia masimulizi ya zamani ambayo yapo tele kutengeneza vitu vyenye asili ya kikweli kweli.
Banzi ndiye aliyemwezesha Jennifer Kyaka kutokelezea katika dunia ya uigizaji katika filamu ya Odama,  moja ya filamu zenye kusaka mazingira ya zamani buila kutumia kompyuta.Filamu nyingine ni Beyonce na Adima.
Simulizi zote hizo huwa zimelenga kusema kwamba mapenzi ndio hasa mwisho wa migogoro na matatizo ya mali na maisha ya binadamu.
Aidha namna ya watu wanavyozungumza katika filamu hizi  inakupa mazingira bora zaidi za namna nyingine ya kuigiza huku ukiwa hupati vionjo kinyume na vile ambavyo vinaharibu na kuchafua hali ya hewa.
Simulizi hili bado unaweza kuliona na watu wengine wakubwa kwa kuwa mapenzi si ya kuchusha na wala mauaji hayatishi kihivyo. Usiku wake umechukuliwa katika hali bora zaidi, bila kutegemea kompyuta.
mwisho


DOA LA NDOA
Sijamwelewa Mtitu

KUSEMA ukweli, haki ya nani vile sikuweza kumwelewa dairekta wangu  William Mtitu katika sinema yake ya Doa la Ndoa. Kwenye sinema hii kinyume na fikira na  huwa inanoga ikiwa hivyo, watu wawili wanauawa. Dairekta anamuua mtu kwa risasi na mwingine anamuua kwa zidisho la dawa katika mwili wake.
Niliona si sawasawa, lakini nikasema huyu dairekta anayependa kuua watu katika simulizi zake za kuomba msamaha ana akili gani hasa? Sitaki hata kujibu kwani nilikuwa nadhani simulizi kama Doa la ndoa, filamu ambayo inafanana kijina na filamu fulani ya marehemu Kanumba,  inayohusu wanandoa ilistahili kuonesha matunda ya kuomba msamaha na kupatikana.
Kwa sinema ya Kanumba tatizo lilikuwa hilohilo kunyimwa nafasi ya kufanya mapenzi, hali iliyomfanya atafute kwingine, ila katika sinema ya mtitu pamoja na kunyimwa nafasi hiyo jamaa aligangamala, akatulia kumsubiri wake ajirudi.
Mimi nafikiri hatujafikia ubazazi wa Hollywood wa kuua bila sababu na katika simulizi hili la mapenzi mauaji yaliyofanyika yana walakini hasa kutokana na staili ya masimulizi na mantiki ambayo mimi naweza kusema yanastahili kuwa na uhai, hasa ukizingatia kwamba mauaji hayo hayakutatua tatizo bali kisirani.
Nasema kisirani kutokana na ukweli kuwa  mwandishi wa skripti alijitahidi sana kuonesha mapenzi ni sehemu ya maisha kukoseana na kusameheana na kuwa mkweli katika roho. Hapa wawili walikuwa si wa kweli katika roho, lakini akamwacha mmoja akiwa huru kama vile yeye si chanjo cha upuuzi ulikokuwa unafanyika miongoni mwa wanandoa wawili Mussa Kompaund kama Alex na  Irene Uwoya kama Winnie.
Mariam Ismail kama Irene ndiye hasa mpuuzi, kwani alikuwa kwa namna fulani anajua anachokifanya Winnie na jamaa yake Irene, Nashon nafasi iliyochezwa na Ibrahim Mputa.
Ndani ya sinema hii aliye na moyo wa mapenzi ya kwelikweli ni  Alex ambaye pamoja na kushughulikiwa na mkewe mara mbili na kumfumania mara moja bado alidiriki kumrejesha nyumbani na kumwandalia Hepibesidei bila kujua kwamba mkewe amelamba kiasi kikubwa cha dawa zilizomuua na pale hakuwa amepumzika bali amekwenda moja kwa moja.
Kilikuwa kilio kwa Alex kilio ambacho mimi nasema si cha lazima sana kufanyika kwani bado filamu ingelipenda kwa kumuua mtu mmoja au kutomuua kabisa, lakini jamaa wakaendelea kuishi. Doa la Ndoa ya Mtitu iliweka twisti ndogo sana ambayo haikupi muonjo wa moja kwa moja, lakini mastaa ni wale waliokuwa na bifu la leo na kesho na jana Wolper kwa Kanumba na Uwoya kwa Mtyitu.
5 effects wanaweza kuwa na sababu za kutafuta fedha za chapuchapu, lakini wanaua ukuaji wa filamu kwa kuwa na mawazo ya skripti yanayofana na mno ila mwisho tofauti.
Masuala ya mapenzi humu ndani na hasa mazungumzo yake pamoja na Uwoya kutumia sana lugha ya kujishaua (ndio fikira zangu) na Kompaund kuonekana kutulia, mtu anayejua anachokifanya, sinema hii huwezi kuwa karibu na jamaa unayemheshimu kidogo lugha imekuwa kama tundu la maji mabovu, asali inaonekana kutiririka muda wote na hata maleba hasa ya bibie Uwoya yalikuwa yanatoa motisha mwingine.
Usibishe ukadhani nadanganya kuna maneno hapa yanaweza kukutia wazimu... mapenzi alisema Irene, si gari si nini bali namna unavyojisikia ukiwa pembeni mwa mtu ... ah hapo anamwambia mchuchu wake na si mume wake katika hoteli ya kifahari waliokokuwa wakifanya vurugu zao.
Simulizi la Mtitu kama Dairekta linaanza pale ambapo watu hawaelewani kisha tu naingia katika sababu na sababu yenyewe ni ujauzito uliotoka. Lakini ukiangalia utaona shida hasa pale ambapo Nashon rafiki mkubwa wa Alex anamtwaa mke wa jamaa huku akimwambia jamaa yake anachotaka mkewe ampe kwani ipo siku mambo yatakuwa poa kumbe yeye alikuwa akuimla kisogo jamaa.
Unaweza kusema kwamba ni urafiki wa mashaka na lazima mtu uwe na mashaka lakini katika simulizi hili, unaweza kusema wazi kwamba kuna kuchapia kwingi katika maisha, lakini wapiga picha walienda vyema huku mhariri akitumia zaidi mtindo wa kufyuzi badala ya kukata huku akifunga na kufungua matukio dalili ya kukua kwa utaalamu wa kuhariri filamu.

Mimi nimekuwa na hamu ya kumuuliza Mtitu hivi inakuwaje anaua kama ametumia maneno matatu kama yale ya mapenzi, ya kuombana msamaha na angalau Alex na Winnie walikuwa wameanza gari lao upya.
Niliyemuona kuwa staa hasa wa sinema hii Kompaund wengine waliuza sura na maumbile yao ingawa mdada Mariam akipata picha bora zaidi hasa ya aksheni anaonekana kutulia vyema katika skrini.
Je, niseme nini hasa kuhusu filamu hii ya kuona majumbani?Kama vile hujui maneno ya kuliwazana baada ya ukakasi mkubwa unaokumbana nao huku ukiambiwa baada ya kazi..'baby your are the best' , ukiangalia bila kutumia akili unaweza kumshushia kipondo cha wazimu dairekta wa sinema hii kwani amekuletea gogoro ambalo linafunua mtima wako.
Katika maana halisi ya doa, filamu hii haina doa ina  mtafaruku, kwani doa hufutwa na nguo kuvaliwa huyu Mtitu hakutaka kuvaa aliwaua wahusika wake kama mshahara wa dhambi ni mauti, hii si sawasawa.

 


FUNGATE
Kwanini Dairekta Claud 112 amuua Niza bila sababu?



WIKI hii nilipata nafasi ya kuangalia sinema ya Fungate ambayo imetengenezwa na Issa Mussa maarufu kama Claud 112.

Katika sinema hii pamoja na kuridhika na staili ya uhariri nilisikitishwa na kitendo cha dairekta kumuua Niza (nafasi iliyochezwa na mdada Yobnesh Yussuph) bila sababu yoyote ile ya msingi. Nilikasirika kwa sababu nyingi sana na moja ya sababu hizo Niza alipata shida ambazo si zake na kumpelekea kujiua si sawa sawa.

Wakati naandika makala haya mafupi nilimtwangia Claud 112 kwa ufafanuzi kama Dairekta kwanini alimuua binti yule akacheka sana kisha akasema:" kiongozi hadithi ile imelenga kutufunza wanaume tusisababishe umauti kwa wanawake kwa kuwaahidi tusichowapa"

Alisema katika mazungumzo yetu kwamba mara zote wanaume tumekuwa tukijidai kwamba ndio wenye maamuzi , hali ambayo baadae inawaathiri wenzetu hasa wale wenye maamuzi ya haraka na mara zote tunasababisha kifo kama Niza alivyofanya baada ya kufikiri hawezi kupata penzi la Tobi (nafasi iliyochezwa na Issa Mussa).

 Simulizi la kadhia hii ni jema sana hasa staili iliyotumika ambayo ilikuw ainafanya twisti ndani ya simulizi na kuona mwishoni kabisa mkasa na kisa ni kitu gani.

Ndani ya filamu hii  makosa yamepachiwa sehemu mbili yaani kila upande unaonekana kufanya vurugu fulani. Wakati Tobi (Issa Mussa-Cloud 112) anamvuruga Niza na kumuahidi kumuoa kisha anaenda kumuoa Luwi (nafasi iliyochezwa na Manka Maina), Luwi yeye alikuwa ametelekeza penzi la Kila (nafasi iliyochezwa na  Liberty Msuya).

Kimsingi filamu hii ina rangi ya kupendeza kwa maana ya kwamba matukio mengi yapo kikubwa zaidi na japokuwa inakubalika kwa daraja la 16 kipo kipande kidogo kinaleta kiza (katika mapenzi ya kubakana) kisha katika mauaji. Cut katika sehemu zote mbili zilikuwa za kiungwana, uhakika na bila kupoteza ladha unakuja kujua nini kimetokea.

Naam,  ni Fungate na Tobi anaondoka na Luwi kwenda kukamilisha ndoa yake, nje kidogo na kwao mahali bomba ambako walitarajia kutulia, lakini njiani wanafuatwa na mdada mmoja ambapo tangu unaanza simulizi mpaka eneo fulani huweiz kujua kulikoni.

Huku kulikoni ndio kunafanya simulizi hili uendelee kuwa nalo mpaka mwisho huku vipande fulani, vikiashiria imani ya Dairekta kwamba akili ya binadmau huiona matukio kabla ya kutokea labda uinachoshindwa ni kutafsiri tu. Tobi anafuatwa na mwanamke ambaye alikuwa amemuahidi kumuoa na  mbaya zaidi hakuwa amemwambia mwenzake ambaye naye huko alikotoka alikuwa amemtelekeza mwenzake kwa kukosa fedha na kazi.

Wakiwa ndani ya gari safi la kispoti Tobi na mkewe wanafika katika hoteli ambayo  Niza naye anafika. Unaweza kusema ni bahati tu lakini baadaye unalazimika kuunga kwamba  simulizi la hadithi hii linaenda mbele na nyuma na unapoanzia ni katikati.

Niza alipata taarifa ya wapi anapoenda Tobi na akamfuatilia na alikuwa na nia njema kwani kulikuwa na ahadi na pia kulikuwa na penzi na hata wafanyakazi wa ofisini kwake Tobi walikuwa wanalitambua hilo wakashangazwa na bosi wao kumuoa Luwi badala ya Niza.

Seleka la hotelini mpaka kifo ndilo ambalo unatakiwa kuliangalia.

Kimsingi Issa anapanda katika kutengeneza sinema zake na unaweza kuliona hilo hasa katika lugha, watu wanaofanya kasti,wanaotengeneza sinema na hata katika ufuatiliaji wa mambo.

Anayefurahisha sana katika sinema hii si Cloud 112  ni Yobnesh Yussuph, mwanamke aliyecheza kama Niza,aliyependa kisha akaona penzi lake linavyoyeyuka mithili ya barafu, tena kwa muda mfupi tu akashangaa amemkosea nini Tobi.

Unaiona hisia ile kwenye macho, kwenye mwili na kwenye kila kiungo chake na watu kama hawa ndio wanaoipa chati sinema, plani zake, lakini pasi shaka dairekta akiwa pia muigizaji nayo imeipa ladha fulani kwani mwenyewe alijinyima sana  laini za kuzungumza akawapa akina manka na Yobnesh.

Mimi ningelisema kwamba watunzi wanakomaa, wpaiga picha wanakomaa na wahariri wanaanza kuelewa kwamba hawatengenezi michezo ya kuigiza bali wanatengeneza filamu.

Ukiangalia sana picha hii si mikasa ya ndoa, ni maamuzi mabovu yasiyozingatia hisia za watu, uzushi wa wanaume na mapenzi yanavyopofusha maisha na kutufanya tuwe na kauli zinazosababisha karaha kwa wengine.

Kutapata na ukweli anaoujua baada ya kukumbushwa kunaleta hisia kali kwamba wanaume wanatakiw akuwa waangalifu sana katika maisha  na hasa kwenye ahadi zao.

laini ambayo nitaikumbuka ni ile ya kwenye ndoto, wewe sizungumzi na mbwa nazungumza na mwenye mbwa.. alisema Niza katika ndoto ya Tobi.. ishara mbaya kabisa.

Mwisho




Megan Denise Fox :Mwanamwali aliyefanya vyema ndani ya
Transformers: Revenge of the Fallen

NI mwanamitindo muigizaji ambaye kila anapoigiza anakuacha hoi. Ni mwigizaji aliyezaliwa Mei 16, 1986 wa Marekani aliyeanza shughuli zake za kuigiza 2001.

Alipata nafasi ya kujulikana kw aupana mwaka 2004, alipoigiza Confessions of a Teenage Drama Queen. Mwaka 2007, aliigiza Mikaela Banes, kama mapenzi wa Shia LaBeouf kwenye filamu ya Transformers. Fox alicheza tena katika mititiriko wa filamu hiyo wa mwaka 2009: Transformers: Revenge of the Fallen. ndio filamu niliyoipenda nitakusimulia kama nitapata muda na mwaka 2009 aliigiza filamu nyingine ya Jennifer's Body.

Fox pamoja na kuwa muigizaji mzuri ni mrembo wa haja ambaye alitokea katika majalida kadhaa ya urembo.

Mwanamwali huyu aliyezaliwa Oak Ridge, Tennessee, Marekani aliolewa mwaka 2010 na Brian Austin Green na wana mtoto mmoja ni  binti wa Gloria Darlene (née Cisson) na Franklin Thomas Fox. Wazazi wa Fox waliachana wakati yeye akiwa na miaka 12.

Akiwa na miaka 16 aliigiza filamu ya Holiday in the Sun, (2001)  baadaye aliigiza  What I Like About You na  Two and a Half Men,  Bad Boys II  (2003). Mwaka 2004, aliigiza Confessions of a Teenage Drama Queen akiwa na Lindsay Lohan,akicheza kama Carla Santini, mpinzani wa Lola (Lohan).

Fox pia aliigiza katika televisheni ya ABC ya Hope & Faith, akicheza kama Sydney Shanowski na Jennifer's Body mwaka 2009.

Fox in October, 2007 with two of her tattoos visible

Fox ambaye amekuwa akilinganishwa mara kwa mara na  Angelina Jolie na vyombo vya habari vya Ulaya Magharibi kutokana na michoro katika mwili, na nywele na urembo wao kwa sasa anafabnyakazi ya ziada kuondoa michoro hiyo.

Pamoja na urembo wake Transformers  ndiyo iliyomfanya ajulikane zaidi katika dunia ya sinema , alimudu nafasi hiyo.

Fox alijuana na muigizaji Brian Austin Green kuanzia mwaka 2004, walipokutana katika usukaji wa Hope & Faith akiwa na miaka 18 na jamaa akiwa na miaka 30. Mwaka 2006, walichumbiana lakini wakiachana 2009 na kutangaza kurudiana tena  Juni 2010 na Juni 24, 2010, wawili hao walioana kwa faragha katika hoteli ya Four Seasons Resort katika kisiwa cha Hawaii.
Fox na Green wana mtoto mmoja kwa jina la Noah Shannon Green, ambaye alizaliwa Septemba 27, 2012.
Fox ni mama mdogo kwa mtoto wa Green anayejulikana kwa jina na Kassius (Aliyezaliwa 30, 2002), ambaye alitokana na uhusiano wake na  muigizaji Vanessa Marcil Giovinazzo.

Filamu ya Transformers: Revenge of the Fallen  2009  aliyocheza kama Mikaela Banes akiwa na akina Shia LaBeouf, Megan Fox, Josh Duhamel, Tyrese Gibson, na John Turturro, huku Rainn Wilson akiwa kama profesa anayejua kuchekeshainaanzia pale ambapo filamu ya kwanza imeishia.

Huku adui katika sinema hiyo Megatron akiwa amezikwa chini kabisa ya bahari, Optimus Prime na rafiki yake Autobot wakiwa pamoja na askari wanadamu wanaangalia mabaki yaliyotawanyika duniani  kote ya  Decepticons .

Wakati mambo hayo yote yafanyika Sam Witwicky, ambaye ndiye shujaa wa filamu ya kwanza ya mwaka 2007, yuko bize akijiandaa kwa mwaka wake wa kwanza chuoni, rafiki yake wa kike, Mikaela Barnes, alikuwa katika gereji ya baba yake akiendelea na kazi bila kung'amua kwamba Cybertron ambaye ni miongoni mwa wazee wa Decepticon akijulikana kama  “The Fallen”  anatengeneza mpango wa kuivamia dunia.

Alikuwa anahitaji kufika katika chanzo cha energon,  damu inayowaendeshaTransformers wote. Na kama akifanikiwa maana yake ni balaa kubwa na maangamizi kwa binadamu. Huku dunia ikikabiliwa na majanga makubwa Sam na Mikaela lazima waungane kwa mara nyingine  tena na  Optimus na Autobots kumkabili adui mpya mwovu na mwenye nguvu kubwa.


The Angel
FILAMU iliyotengenezwa nchini Norway imepelekwa kwa ajili ya tuzo za Oscar lakini  uhakiki wa filamu hiyo uliofanywa na baadhi ya wahakiki inafanya ionekane kushindwa hata kabla ya wakati wenyewe.
Katika uhakiki wao wafuatiliaji wamesema kwamba unahitaji kuwa na moyo wa chuma ili kuweza kuipenda sinema hiyo ya uteja ambayo inaonekana taratibu inaimeza dunia.
Filamu hiyo "The Angel," imetengenezwa katika mazingira ya kudhani kwamba hakuna filamu nyingine ya aina hiyo iliyokwisha tengenezwa.
Hali hiyo inatokana na kujirudia kwa maeneo kadha yale yale yaliyozoeleka na hata katika sinema yenyewe maeneo hayo yanaendele akujitokeza hapa na pale.
Mwandishi na mtengeneza sinema  hiyo Margreth Olin anadai kuwa filamu hiyo inamwakilisha rafiki yake , yaani simulizi ni la rafiki yake na ama hakika unaweza kuona jinsi jamaa anavyoteseka naye katika njia nzma.
Mateja katika filamu hii ni wengi  wa umri tofauti lakini wanaishia kwa  Maria Bonnevie ambaye  kw anamna Fulani analeta uhai kwa kuwa yeye angalau anafanya vitu ambavyo ni sawasawa.
Hilo hasa ni kutokana na kumwangalia motto wake katika masuala ya usafi vinginevyo filamu hiyo ni  mbaya  huku ikiwa inaunyanyasaji wa kijinsia, pombe, ukahaba, na hakuna kitu chochote kile kinachofanyika kuhakikisha kwamba hali hiyo inakemewa na kurekebishwa. Inaonekana kama kitu kinachofaa.
Ukiiangalia kwa makini unaona kwamba labda fuilamu hii haizungumzii uteja inazungumzia matatizo ya kifamilia kizazi kwa kizazi. Kinachofurahisha ni kuwa amewatumia vyema wanawake kuelezea tatizo  lakini swali linalokuja ni kwa namna gani anatengeneza filamu kama vile hakuna kilichowahi kuzunguzmwa kuhusu uteja hasa ikizingatiwa kwamba kunasinema nyingi zimezungumzia shauri hilo.
Ni shauri la familia kujikuta katika matatizo kutokana na uteja na hata wazazi wanapokuwa wateja na watoto wanashindwa kule ainakuwaje hasa. hilo nis hauri la pekee lakini mwendesheji Olin alipaswa kufahamu kwamba ameishiwa na sinema nyingi za aina hii zimeshatengenezwa.



COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
static_page
Lukwangule Entertainment: Filamu
Filamu
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/p/filamu.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/p/filamu.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy