UNCUT: Kile ambacho Makala ya BBC haikukisema kuhusu Tundu Lissu

Na Norah Msemwa Nilitazama makala ya BBC Africa Eye kuhusu Tundu Lissu nikiwa na hisia zilizochanganyika. Kama Mtanzania, niliguswa kuona mt...



Na Norah Msemwa

Nilitazama makala ya BBC Africa Eye kuhusu Tundu Lissu nikiwa na hisia zilizochanganyika.

Kama Mtanzania, niliguswa kuona mtu aliyenusurika jaribio la kutisha la kuuawa, akaishi uhamishoni, na sasa ametumia zaidi ya mwaka mmoja mahabusu akisubiri kusikilizwa kwa kesi ya uhaini. 

Hakuna anayepaswa kubeza mateso ya kibinadamu yaliyoonyeshwa kwenye makala hayo, na kila Mtanzania anapaswa kutaka haki ipatikane kuhusu shambulio la mwaka 2017 ambalo bado halijapatiwa majibu, pamoja na kuhakikisha kuwa kesi ya sasa inaendeshwa kwa uwazi.

Lakini makala ilipoisha, nilijikuta nikiuliza swali tofauti: Ni nini kimeachwa nje? Na kwa nini kimeachwa nje?

Uandishi wa habari hauhusu tu kile kinachojumuishwa. Pia unahusu kile kinachoachwa. Kwa mtazamo wangu, BBC Africa Eye imeandaa makala yenye nguvu ya kihisia, lakini haijatoa taswira kamili ya mmoja wa wanasiasa wenye utata mkubwa nchini Tanzania.

Makala hayo yanatuonyesha kadhia aliyopitia Tundu Lissu, lakini haizungumzi kwa kina namna alivyoendesha siasa zake na maamuzi yaliyomfikisha katika migogoro hiyo ya mara kwa mara.

Tofauti hiyo ni muhimu.

Katika maisha yake ya kisiasa, Lissu amejijengea sifa ya kuwa mmoja wa viongozi wa upinzani wasiopenda maridhiano. Wafuasi wake humwona kama jasiri asiyeogopa. Wakosoaji wake humwona kama mwanasiasa anayependelea migongano ya kisiasa. Vyovyote mtu anavyoweza kumwelezea, wengi wanakubaliana kwamba mara nyingi amechagua siasa za makabiliano badala ya maridhiano.

Hata ndani ya makala hiyo, mke wake mwenyewe anaeleza athari ambazo familia imezipata kutokana na maisha yaliyojaa kesi mahakamani na vipindi vya kuwekwa mahabusu. Hilo limewasilishwa zaidi kama ushahidi wa kadhia aliyopitia. Lakini pia linaweza kuwafanya watazamaji waulize: Kwa nini mwanasiasa huyu amejikuta mara kwa mara katika migogoro ya kisheria kwa miongo kadhaa, ilhali viongozi wengine wa upinzani hawajapitia hali kama hiyo? Swali hilo linastahili kujadiliwa. Badala yake, makala inaonekana kutoa jibu kabla hata ya kuuliza swali.

Moja ya mambo makubwa yaliyoachwa ni muktadha mpana wa uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan. Makala inaonyesha kwa sekunde chache picha ya aliyekuwa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akimtembelea Lissu hospitalini mwaka 2017 alipokuwa akipona baada ya kushambuliwa. Ilikuwa ni ishara ya ubinadamu licha ya tofauti za kisiasa. Hata hivyo, Makala haichambui kwa kina maana ya tukio hilo wala mazingira ya kisiasa yaliyojitokeza baadaye chini ya uongozi wake.

Watanzania wanakumbuka kuwa muda mfupi baada ya kuingia madarakani, katika safari yake ya kwanza Brussels, Rais Samia alikutana hadharani na Lissu, akamkaribisha kurejea nchini na kuendelea na shughuli za kisiasa. Tangu wakati huo, serikali ililegeza baadhi ya vikwazo vya kisiasa na kuwezesha kurejea kwake kutoka uhamishoni.

Mambo hayo hayathibitishi kuwa kesi ya sasa ya uhaini haina masuala ya kisiasa. Lakini pia hayaungi mkono simulizi kwamba kadhia zilizomkuta Lissu zilikuwa endelevu bila mabadiliko yoyote. Ukweli unaonekana kuwa mgumu zaidi kuliko simulizi rahisi.

Makala pia inapita haraka katika sura muhimu ya hivi karibuni. Baada ya kurejea nchini, Lissu alikijenga upya CHADEMA, akafanya mikutano nchi nzima, akagombea na kushinda uenyekiti wa chama Januari 2025 kwa kumshinda Freeman Mbowe. Kabla ya uchaguzi huo, katika mahojiano na BBC kwa Kiswahili na Sammy Awami, alisema wazi kuwa "hakuna tena kuambiana mambo ya maridhiano yasiyokuwepo." Alisisitiza kuwa uongozi wake ungejikita katika mapambano makali na kudai mabadiliko.

Makala haijatoa uzito wa kutosha kuhusu kampeni ya "No Reforms, No Election", uamuzi wa CHADEMA kutosaini kanuni za maadili ya uchaguzi, hatua iliyofuatiwa na kutoshiriki uchaguzi, pamoja na hoja ambazo waendesha mashtaka wanazitaja katika kesi ya uhaini.

Kilichonishangaza zaidi ni namna suala la maridhiano ya kisiasa lilivyoshughulikiwa. Mtindo wa Lissu umeonekana mara nyingi kupendelea makabiliano kuliko maelewano, si tu na serikali bali hata ndani ya chama chake. Mwanasiasa anayepinga maridhiano ya ndani kabla ya kuchukua uongozi wa chama anaibua swali muhimu: Je, makabiliano yasiyo na nafasi ya maelewano ndiyo njia bora ya kuimarisha demokrasia? Watu wanaweza kutofautiana katika majibu yao, lakini BBC haikuliuliza swali hilo kwa kina.

Mimi si mtetezi asiyeona mapungufu ya hali ilivyo. Kama Watanzania wengi, ninaona changamoto katika utendaji wa serikali, kasi ya baadhi ya mageuzi na matatizo yanayoathiri maisha ya kila siku. Hata hivyo, Tanzania ndiyo nchi yangu. Kutazama kutoka nje ya nchi kunanifanya nihisi maumivu makubwa kuhusu mwelekeo wa taifa letu, hasa baada ya migawanyiko iliyofuatia uchaguzi wa mwaka 2025.

Ninafurahia maendeleo ya uchumi, ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), bandari, miradi ya nishati, kuimarika kwa ushirikiano wa Afrika Mashariki na maono ya Dira 2050. Wakati huohuo, naamini tunapaswa kuendelea kuimarisha taasisi, kulinda haki za kiraia na kuhakikisha haki inatendeka kwa uwazi huku tukidumisha utulivu unaovutia uwekezaji.

Hili linanileta kwenye swali muhimu: Wanawake wa Tanzania wako wapi? Wako wapi akina mama wanaoheshimika, wasomi, wafanyabiashara, majaji, viongozi wa dini, waandishi, wataalamu na viongozi wa jamii? Kwa nini sauti za wanawake wachache sana zinasikika zikihimiza siasa za utulivu, mazungumzo ya kikatiba na uongozi wenye kuwajibika kutoka pande zote? Taifa limekaa kimya kwa kiwango kikubwa mno. Tunaweza kufanya vizuri zaidi.

Nikihusianisha swali hilo na makala ya BBC, tofauti na lengo lililoonekana la watayarishaji wake, shujaa wangu ni Alicia Lissu. Simulizi yake ya utulivu ilizungumza zaidi kuliko picha zilizoonyeshwa. Kama mwanamke, nilielewa zaidi hali anayopitia yeye kuliko simulizi la kisiasa la Tundu Lissu. Kumuona akiwa kando ya kitanda cha mume wake huku akishuhudia akifarijiwa na aliyekuwa Makamu wa Rais ilikuwa ni ishara ya matumaini kwake. Anawakilisha wanawake wengi wa Kitanzania waliochoshwa na migogoro ya kisiasa isiyoisha na wanaotamani ukurasa huu ufungwe.

Wakati huu ni mkubwa kuliko mwanasiasa mmoja, waraka mmoja au serikali moja. Tanzania inahitaji viongozi wa upinzani wanaoweza kuikosoa serikali kwa uwajibikaji. Inahitaji serikali zinazojibu ukosoaji kupitia taasisi badala ya kujihami. Pia inahitaji uandishi wa habari wa kimataifa unaoeleza jamii kwa ukamilifu badala ya kuzigawanya katika simulizi rahisi za mashujaa na waovu.

BBC Africa Eye imefanikiwa kuwafanya watazamaji wamhurumie Tundu Lissu. Lakini haikufanikiwa kwa kiwango kilekile kuwasaidia kuielewa Tanzania.

Maswali kuhusu jaribio la kumuua Lissu mwaka 2017 yanahitaji majibu. Kesi ya sasa ya uhaini inahitaji kusikilizwa kwa haraka na kwa uwazi. Lakini umma pia unastahili kupata picha kamili ya mtu aliyeko katikati ya simulizi hili—si kadhia yake pekee, bali pia siasa zake, mbinu zake na maamuzi yake.

Ni hapo tu ndipo watazamaji wataweza kuamua wenyewe kama wanamtazama mwanamageuzi wa kidemokrasia, mwanasiasa anayependelea makabiliano, au kiongozi mwenye sifa za pande zote mbili.

Hiyo ndiyo simulizi ambayo nilitarajia BBC Africa Eye ingeisimulia.

COMMENTS

Name

Anga,12,Arusha,27,batiki,1,Burudani,455,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,313,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,3,Habari,7236,habari dodoma,40,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,23,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,7,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,746,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,376,muziki na fasheni,20,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,10,SAYANSI ANGA,14,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,17,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: UNCUT: Kile ambacho Makala ya BBC haikukisema kuhusu Tundu Lissu
UNCUT: Kile ambacho Makala ya BBC haikukisema kuhusu Tundu Lissu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg4j__QQio20qtbVK19xqs5jzDeUkB3BYcC05ocYbMtse0lHWGkVC00HK0mb2gNIaFbTaeanOT94JzGwn6xPwkO64U3pnHrRMMCZlXySw_JWf_oHCRjQA8KoPRIK2abPuyDER-N1OdVbQgwib0Ha0tWi-CpWCEBu2UOCgUwT3keg13gSh2dA_W7l5CaIUmE/s320/TUNDULISU.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg4j__QQio20qtbVK19xqs5jzDeUkB3BYcC05ocYbMtse0lHWGkVC00HK0mb2gNIaFbTaeanOT94JzGwn6xPwkO64U3pnHrRMMCZlXySw_JWf_oHCRjQA8KoPRIK2abPuyDER-N1OdVbQgwib0Ha0tWi-CpWCEBu2UOCgUwT3keg13gSh2dA_W7l5CaIUmE/s72-c/TUNDULISU.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2026/07/uncut-kile-ambacho-waraka-wa-bbc.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2026/07/uncut-kile-ambacho-waraka-wa-bbc.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy