Sunday, November 22, 2009

MSAFARA WA WAZIRI MKUU WAZUIWA KWA MABANGO NEWALA

· Wananchi wakaa njiani, akubali kushuka na kuwasikiliza
· Wamzomea mbunge wao, wakataa kumsikiliza

MSAFARA wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda jana ulilazimika kusimama njiani baada ya wakazi wa kijiji cha Mkunya wilayani Newala, Mtwara kuziba njia wakiwa na mabango huku bango kubwa likimwomba asimame na kuwasikiliza japo kwa dakika 10.
Baadhi ya mabango hayo yalisomeka: “Waziri Mkuu tunakuomba usimame japo dk.10 usikilize kilio chetu”; “Maji ni mradi wa wakubwa”; “walinda chanzo cha maji hawana maji”; “Mfumo wa Stakabadhi Ghalani haufai”; “Korosho kwa mkopo ni ufisadi pia”; na “Malipo ya pili 2005 wakulima wa korosho bado hatujalipwa.”
Tukio hilo lilitokea jana mchana (Jumamosi, Novemba 21, 2009) wakati akielekea kwenye bonde la mto Ruvuma kukagua kituo cha maji cha Mkunya na kupokea taarifa ya kilimo cha umwagiliaji kwenye bonde la mto Ruvuma ambako pia alikabidhi powertillers mbili kwa vikundi vya Mpilipili na KIWOPA kutoka kata ya Kitangari wilayani humo.
Mara baada ya kukuta njia imefungwa, Waziri Mkuu aliteremka garini na wakazi hao walipoomba wamkabidhi risala yao, ili awasikilize kwa dadika chache, yeye aliwaruhusu waisome.
Katika risala yao, wakazi hao walisema wana kero za maji za kutopata maji safi na salama, kutolipwa malipo ya korosho na kutopatiwa pembejeo za ruzuku lakini uongozi wa wilaya umekuwa ukiwapuuza na kuficha taarifa badala ya kuwasaidia.
“Sisi tunaishi kwenye vijiji vya mwanzo kutoka katika chanzo cha maji lakini yanatupita na kwenda kuwafaidisha wengine... zamani tulikuwa tukipata lakini sasa umegeuzwa kuwa mradi mkubwa kwa mhandisi na vigogo wengine...” ilisema sehemu ya risala yao.
Walisema kwamba tatizo la uhaba wa maji katika eneo lao limedumu kwa zaidi ya miaka 15 jambo ambalo linawafanya watumie muda mwingi kusaka maji badala ya kuutumia muda huo kwenye kilimo.
Walisema kuna watu wachache wanaopelekewa maji na kujaziwa katika visima vyao ili wayauze kwa wananchi wengine kwa sh. 500/- kwa kila ndoo na baadhi ya watu wanajaziwa maboza na kupita mitaani wakiyauza maji hayo kwa sh. 500/- hadi 700/- kwa ndoo moja.
Wakizungumzia kuhusu mfumo wa stakabadhi za mazao ghalani, wakazi hao walisema hawautaki mfumo huo kwa sababu hawalipwi hela yote ya sh. 700/- kwa kila kilo kama walivyoahidiwa. “Tuliambiwa bei ya dira ni sh. 700/- kwa kilo kwa mikupuo ya sh. 490/- na sh. 210/- lakini hailipwi yote... tuliambiwa tutahusishwa wakati wa mauzo ya mnada, tunaomba bei ya dira itangazwe upya na wananchi washirikishwe kwenye minada ili wajue kinachoendelea.”
Pia waliiomba Serikali iwasaidie kuwapatia pembejeo na mbolea za ruzuku kwani bei ni kubwa na wengi wanashindwa kuzimudu.
Akijibu hoja zao, Waziri Mkuu alisema kupitia risala yao amebaini kuwa tatizo kubwa linalowakabili ni ukosefu wa maji katika vijiji 12 wakati bomba la maji kutoka chanzo cha maji hadi Newala mjini linapita hapo. Chanzo cha maji cha Mkunya kipo urefu wa mita 800 kwenda chini kutoka safu za milima ya (plateau) Makonde ambako wakazi hao wanaishi.
Aliwaahidi wakazi hao kwamba kabla hajaondoka tarehe 24 atakuwa amepata ufumbuzi wa tatizo hilo. “Hata kama maji hayatoshi itabidi kuwe na mgao walau mara mbili au tatu kwa wiki ili wa huku chini mpate na wa mjini nao wapate, ” alisema huku akishangiliwa na wakazi hao.
Alisema ili kukabiliana na tatizo la watu kuuza maji kwenye maboza au visima vyao binafsi, mhadisi mkazi atapaswa aweke ratiba ya kugawa maji na kuyasambaza kwenye viula vya maji (public water points) ili watu wote wapate.
Akizungumzia kuhusu mfumo wa stakabadhi za mazao ghalani, Waziri Mkuu alisema mfumo huo hauna tatizo ila una mapungufu ambayo itabidi yaangaliwe upya na kumtaka Mkuu wa Mkoa huo. Kanali (mst) Anatoli Tarimo kujipanga upya na kusambaza elimu ya mfumo huo kwa wakulima wa mkoa huo.
Kuhusu pembejeo za ruzuku, Waziri Mkuu ambaye jana alikuwa katika siku ya tatu ya ziara yake mkoani Mtwara, alisema atahakikisha anafuatilia suala hilo ili katika mwaka wa fedha ujao mikoa ya Lindi na Mtwara iingizwe katika programu hiyo. “Mikoa hii miwili haikuwemo kwenye orodha kwa sababu tulijua ninyi ni wakulima wa korosho tu... nimegundua mnalima mazao mengi tu yanayohitaji mbegu bora na mbolea kama vile ufuta, karanga, mpunga na mahindi.”
Katika hali isiyo ya kawaida, Waziri Mkuu alipomwita Mbunge wa jimbo hilo ambaye pia ni Waziri wa Habari na Utamaduni, Bw. George Mkuchika ili awasalimie, wakazi hao walimzomea na kusambaa huku wakisema hatumtaki! Mkutano huo ulilazimika kuisha na Waziri Mkuu kuendelea na safari hadi kwenye chanzo cha maji.
Leo Waziri Mkuu anaendelea na ziara yake ya siku sita katika mkoa wa Mtwara kwa kutembelea wilaya ya Tandahimba ambako ataweka jiwe la msingi kwenye ghala la mazao katika kijiji cha Mahuta na bwawa la malamba katika kijiji cha Malamba kabla ya kufungua jengo la OPD katika hospitali ya wilaya hiyo. Mchana atafungua tawi la benki ya NMB wilayani hapo na kuweka jiwe la msingi kwenye kiwanda cha kubangua korosho kabla ya kufanya mkutano wa hadhara kwenye kijiji cha Kitama.

SOURCE:OFISI YA WAZIRI MKUU

Kutoka wavuti ya subi na mambo matamu .. hebu iangalie hii kwa makini

Document Type: Grants Notice
Funding Opportunity Number: USAID-TANZANIA-10-002-RFA
Closing Date for Applications: Dec 16, 2009
Category of Funding Activity: Health
Expected Number of Awards: 1
Estimated Total Program Funding: $130,000,000
CFDA Number(s): 98.001 -- USAID Foreign Assistance for Programs Overseas
Cost Sharing or Matching Requirement: No

Eligible Applicants : Nonprofits having a 501(c)(3) status with the IRS, other than institutions of higher education

Additional Information on Eligibility: Non profit and for-profit organization as long as they do not include fee or profit element in their application.

Agency Name : Tanzania USAID-Dar es Salaam

Description
The purpose of this Request for Applications (RFA) is to enable USAID/Tanzania to support IRS and other related malaria control services for Mainland Tanzania and Zanzibar. The RFA is therefore soliciting for responsive and responsible firms willing to provide Indoor Residual Spraying (IRS) and related services, with the overall goal of reducing the burden of malaria in Tanzania.

Link to Full Announcement: http://bit.ly/5OG3uP
Link to Application Packet Download: http://bit.ly/7dSP1J

If you have difficulty accessing the full announcement electronically, please contact:
Samuel Kiranga
Grantor
Phone: 2668503
eMail: Acquisition Specialist (skiranga@usaid.gov)

Get this and other opportunities delivered into your inbox when you sign your email address at wavuti.com
Proud to be of service!
Subi: wavuti.com

BAN KI MOON ASISITIZA MAGEUZI YA VIWANDA AFRIKA



Ikiwa ni miaka 20 sasa tangu Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipopitisha Azimio la kuifanya Novemba 20 kuwa siku ya Kimataifa ya Viwanda Afrika, ukuaji wa sekta hiyo ni wa asilimia moja ikilinganishwa na mabara mengine.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, ameyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati alipokuwa akifungua mjadala kuhusu suala zima la umuhimu wa viwanda kwa maendeleo ya Bara la Afrika.
Mjadala huo ambao ulikuwa chini ya usimamizi ( moderator) wa Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Augustine Mhiga uliandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda ( UNIDO). Kama sehemu ya maadhimisho ya siku hiyo.
Akawaeleza wajumbe wa mjadala huo ambao mada yake ilikuwa, “ mikakati na sera za viwanda, ufumbuzi wa mabadiliko ya uchimi kwa afrika. Kwamba, mwaka uliopitia ( 2008) ulikuwa mwaka wa tano mfululizo ambapo Afrika ilishuhudia ukuaji mzuri wa uchumi wake kwa kiwango cha asilimia tano.
Hata hivyo anasema Katibu Mkuu. Licha ya ukuaji huu mzuri ambao umesukumwa zaidi na uzalishaji wa bidhaa, kilimo na utali, bado ukuaji wa sekta ya viwanda si mzuri na haukuleta matokeo yaliyotarajiwa.
“ Takwimu zinaonyesha mwenendo wa ukuaji wa viwanda katika Afrika ni wa asilimia moja ya ukuaji wa viwanda duniani kote, ni wazi kwamba kwa mwenendo huu, maendeleo ya viwanda Afrika bado ni wa kusuasua sana ikilinganishwa na nchi zinazoendelea”. Akasema Ban Ki Moon
Na kwa sababu hiyo, Ban Ki Moon anatoa changamoko kwa viongozi wa Afrika na wataalamu mbalimbali kutafuta mbinu zaidi pamoja na kuwa na majadiliano ya kina ya namna ya kusukuma mbele ukujai wa viwanda, ambao amesema ni muhimu sana kwa maendeleo ya bara hilo na watu wake.
Akabainisha kwamba utandawazi na ukuaji wa haraka wa teknolojia, kunatoa changamato kwa Afrika kujiangalia upya katika suala zima la maendeleo ya viwanda na matumizi ya teknolojia za kisasa.
“ Kuna makubaliano ya jumla kwamba tunahitaji mikakati na sera madhubuti ili kusukuma mbele maendeleo ya viwanda katika Afrika. Lakini kuna maoni na mitizamo tofauti kuhusu ni mikakati ipi na sera zipi ambazo ni sahihi katika kusukuma maendeleo ya viwanda Afrika “anasema
Na kuongeza “Tunahitaji majadiliano zaidi kuhusu namba bora ya kuleta mageuzi ya viwanda Afrika na kuamua nini tunachoweza kujifunza kutoka wa wenzetu wengine ambao wamefanikiwa kuleta mabadiliko hayo maendeleo ya na mfano ukiwa ni kule ninakotoka mimi, Bara la Asia. Akasisitiza Ban Ki Moon ambaye asili yake ni Korea ya Kusini.
Katibu Mkuu huo anasisitiza pia, haja ya a viongozi wa Afrika kujitazama na kujifunza kwa nini Afrika imeshindwa kuweka kipaumbele katika maendeleo ya viwanda.
“ Majadiliano haya ya leo ni uwanja mzuri wa kujadiliana na kubadilishana mawazo kuhusu ajenda hii muhimu sana kwa maendeleo ya Afrika. Nimatumaini yangu pia kwamba majadiliano haya yataanzisha mchakato wa uhakiki na uchambuzi wa kina ndani ya Umoja wa Mataifa na ndani ya nchi za Afrika kuhusu umuhimu wa maendeleo ya viwanda.
Naye msimamizi wa mjadala huo , Balozi Augustine Mahiga allisema mjadala huo licha ya kutathimini umuhimu wa viwanda kwa maendeleo ya afrika, lakini pia ulikuwa ukitoa fursa kwa washiriki kuelewa ni kwa nini Baraza Kuu la Umoja wa mataia miaka 20 iliyopita, iliamua kupitisha uamuzi wa busara wa kutenga siku maalum ya kutoa msukumo kwa maendeleo ya viwanda Afrika.
Akasema “ mjadala huo ulikuwa ukifanyika katika kipindi ambacho Dunia ilikuwa ikiibuka kutoka katika moja ya mtikisiko mkubwa wa kuyumba kwa uchumi. Huku Afrika ikikabiliwa na changamoto kadhaa.
Akawaeleza washiriki wa majadiliano hayo akiwamo Rais wa Baraza Kuu la 64 la Umoja wa Mataifa, Dkt. Ali Abdussalam Treki, mabalozi, wataalamu wa masuala ya uchumi na wataalamu kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda, (UNID). Kwaba Afrika inatakiwa kuzitumia changamoto hizo kuleta mageuzi ya viwanda pamoja na kutumia teknolojia za kisasa sahihi na zinazolinda mazingira.
Mwaka 1989 kupitia Azimio namba 44/237, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, katika mkutano wake wa 44 kwa kauli moja lilipitisha Azimo hilo la kuifanya Novemba 20 kuwa siku ya kimataifa kwa lengo la kuhamasisha Jumuia ya Kimataifa na Afrika kutilia mkazo mageuzi ya Viwanda kwa maendeleo ya Afrika.



Mwisho.

Picha:
KATIBU MKUU WA UMOJA WA MATAIFA, BAN KI MOON, AKITETA JAMBO NA BALOZI WA TANZANI AKATIKA UMOJA WA MATAIFA, DKT AUGUSTINE MAHIGA, MUDA MFUPI KABLA YA KUANZA KWA MJADALA KUHUSU UMUHIMU WA MAGEUZI YA VIWANDA KWA MAENDELEO YA AFRIKA. BAN KI MOON ALITOA HOTUBA YA UFUNGUZI WA MJADALA HUO AMBAO USIMAMIZI WAKE ( MODERATOR) ALIKUWA NI BALOZI WA TANZANIA.

BALOZI WA TANZANIA KATIKA UMOJA WAMATAIFA, AUGUSTINE MAHIGA, AKIONGOZA MADADILIANO KUHUSU UMUHIMU WA VIWANDA KWA MAENDELEO YA AFRIKA, MJADALA HUO ULIFANYIKA KAMA SEHEMU YA MAADHIMISYO YA SIKU YA KIMATAIFA YA VIWANDA KWA AFRIKA AMBAYO HUADHIMISHWA NOVEMBA 20. KUSHOTO KWAKE NI KATIBU MKUU WA UMOJA WA MATAIFA, BAN KI MOON NA KULIA NI RAIS WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA, DKT. ALI ABDUSSALAM TREKI

SOURCE: MAURA MWINGIRA UBALOZI WA TANZANIA NEW YORK

Zain yatesa katika Tuzo Bora

Kampuni ya Zain imenyakua tuzo tatu katika tamasha la kila mwaka la Dunia kwa Kampuni za Mawasiliano kwa nchi za Mashariki ya Kati lillofanyika Dubai mwishoni mwa wiki.
Taarifa iliyotolewa jijini jana na kampuni ya Zain Tanzania ilizitaja zawadi hizo kama Tuzo ya Kampuni Bora, Tuzo ya Mwonekano Bora wa Huduma na pia Tuzo ya Ubunifu Bora wa huduma.
“Zain ipo juu sana katika Nyanja nyingi za mawasikliano.kampuni iemweza kuangalia mambo muhimu kama vile ubora,upatikanani na huduma bora kwa ujumla”, taarifa hiyo ilisema, ikimkariri mmoja wa majaji wa tuzo hizo.
Taarifa hiyo ilisema kuwa tuzo hizo zina lengo la kutambua kazi bora katika maeneo kumi na moja kupitia katika sekta ya mawasiliano katika enelo la Mashariki ya Kati na pia wadau wengine ambao wamesaidia kukuza sekta hiyo ulimwenguni.
“Tunayo rekodi nzuri katika shughuli zetu ambao zinakwenda sambamba na mwonekano mzuri ambao umewevutia watumiaji wengi katika eneo lote la mashariki ya Kati”, alisema Mtendaji Mkuu wa kundi la makampuni ya Zain, Dr Saad Al Barrak.
Alisema kuwa Zain ambayo inaendesha shughuli zake katika nchi mbalimbali uliwenguni ikiwemo Tanzania inatoa huduma bora na pia kuboresha maisha ya watu katika nchi hizo.
“Kwa kupitia huduma yetu ya “Mtandao Mmoja”, tunayo zaidi ya miaka miwili tu ili kufikia lengo la kuwa kati ya kampuni kumi bora duniani na zawadi hizi zinatupa moyo wa kuweza kuyafikia malengo haya”, alisema.
Kwa kuweza kushinda zawadi ya kuwa kampuni bora baada ya kuyashinda makampuni mengine katika ukanda wa mashariki ya Kati,Zain imetambuliwa mchango wake kutokana na ubunifu wa huduma zake, uongozi imara na pia mtizamo wake kwa maendeleo ya baadae ya kampuni.
Taarifa hiyo ilisema kuwa kwa tuzo ya huduma bora,majaji walitambua mchango wa kampuni katika kipindi cha miaka miwili tangu izinduliwe nap ia jinzi kampuni hiyo ilivyoweza kuweza kujitangaza na pia kujijenga.
Pia kampuni hiyo imezawadiwa kutokana na mtandao wake ambao unawezesha mtumiaji kuweza kuendelea kuwasiliana kwa kulipia kiwango kile kile kwa nchi za Afrika na Mashariki ya Kati katika nchi zaidi ya 20 na hivyo kuwapunguzia mzigo wa kulipia zaidi.
“Kwa kutoa huduma ya punguzo kwa huduma ya wasafiri,Zain imeonyesha mfano kwa kuona kuwa huduma ya maasikliano ni muhimu na sio anasa”, ilisema taarifa hiyo.
Hafla hiyo ambayo inawatuza watu binafsi na makampuni ambayo yameonyesha uwezo wa kutoa huduma bora ilihudhuriwa na na watu mashuhuri duniani kutoka katika sekta hiyo ya mawasiliano.
SOURCE:Zain

kama hakuna shule watoto lazima wasome hata chini ya miti.. mlogolo bwana


Mwalimu, Msuya Shaabani ( kulia) ambaye ni mke wa mmoja wa wafugaji wa kabila la kisukuma akionyesha ishara eneo la makazi yasiyorasmi ya wafugaji wa kabila hilo ambao watoto wao wamelazimika kuwapatia elimu ya darasa la kwanza ndani ya msitu wa hifadhi ya asili wa Nanji, katika kijiji cha Igumbiro, Tarafa ya Lupiro, Wilayani Ulanga, Mkoa wa Morogoro, kama walivyokutwa juzi msituni humo.Picha na mdau John Nditi wa HabariLeo.

Saturday, November 21, 2009

Waliojeruhiwa ajali ya basi la Taqwa watajwa, pamoja na masahihisho ya facts


Kamanda wa polisi mkoani Dodoma Zelothe Stephen (pichani) amesema kuwa mpaka sasa ni vigumu kutambua idadi kamili ya watu waliokufa kutokana na ajali ya basi la Taqwa ambalo lilipinduka na kuungua leo asubuhi.
Stephen alisema kuwa wanashindwa kutambua idadi kamili ya watu waliokufa kutokana na gari hilo kutekeatea na kuwa upelelezi unaendelea ili kujua idadi ya watu waliokufa.
Licha ya basi hilo kuwa na uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 60 utingo wa basi hilo Mohamed Shaban alisema kuwa gari hilo lilikuwa na abiria 40 ambapo kati yao 35 walipandia Jijini Dar es Salaam na wengine watano walipandia Morogoro.
Gari la zima moto kutoka Dodoma lilifika katika eneo la ajali, basi hilo likiwa linaishia majira ya saa nane mchana na wakaishia kuzima cheche zilizobaki.
Kaimu Mganga mkuu wa Hospitali kuu ya Mkoa wa Dodoma Jacob Chembele alisema kuwa alipokea jumla ya majeruhi 18 mnamo majira ya saa 8mchana ambapo kati yao 15 walitibiwa na kuruhusiwa na wengine watatu bado wamelazwa kutokana na hali zao kutokuwa nzuri.
Dk Chembele aliwataja majeruhi waliolazwa wakiwemo raia wawili wa nchini Rwanda kuwa ni Fatuma Safari (30),Uwitonze Marie( 36)na mkazi wa Wilaya ya Manyoni Anna Francis (18)wote wamelazwa wodi namba 10 katika hospitali hiyo kuu ya Mkoa wa Dodoma.
Kaimu mganga mkuu huyo alisema kuwa majeruhi wengine watano wamepelekwa katika zahanati ya Wilaya ya Kongwa ambapo walitibiwa na kuruhusiwa ila wanatarajiwa kupelekwa katika hospitali hiyo ya Mkoa kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi zaidi.
BASI la Taqwa linalofanya safari zake kutoka Dar es Salaam kwenda nchini Rwanda limepinduka na kuwaka moto na katika eneo la Pandambili huku idadi ya watu waliokufa katika ajali hiyo kutofahamika na wengine 23 kujeruhiwa vibaya.
Licha ya idadi ya watu waliokufa mpaka sasa kutofahamika ni maiti mbili tu ndizo zilizopatikana ikiwemo maiti moja inayodhaniwa kuwa na dereva wa basi hilo Hasimu Abd (34), na maiti ya mtoto mdogo ambaye hajajulikana umri wake wala jina.
Basi hilo aina ya Scania lenye namba za usajili T 985 ARK lililokuwa lina toka Dar es saalam kwenda Kigali Rwanda (awali niliandika ni Bujumbura)limepinduka katika eneo la Pandambili wilayani Kongwa mjini hapa.
Tukio hilo limetokea leo saa 5 asubuhi baada ya basi hilo kuacha njia na kupinduka na baadaye kuwaka moto wakati likijaribu kulipita lori lililokuwa mbele ya barabara hiyo.

Mustafa Hassanali First Solo Art Exhibition to be Unveiled


Inspired by nature, the feel of the Morning Dew, The warmth of the Setting Sun, The chills of the Cool Weather,(a rarity in this Haven of Peace)…. It’s the Small things which bring Joy to Our Lives…
Mother Nature has given us in Abundance; it’s up to us how we use it as we go through this Journey called “Life”. Wastage is denying the Deprived of their Right by the Privileged Few…
“Hence Over the time since I Started My atelier we have been part of the Special Moments of So many People Lives and with each moment Came Left over Fabrics…. A pile which Kept on growing…”Hassanali Explained
The flamboyance and rich cocktail of Colour inspired this Collection of Art from Left over Fabrics and Haberdashery ranging from Khanga Kitenge, Bazein, and Satins. The Beauty of Mustafa Hassanali Signature mark to the world of Art shall bring a Different Voice that “WE CARE”
The Exhibition will run at Alliance Francaise From 23 to 28 November 2009 from 1000-1800HRS
Being Environment Conscious, Mustafa Hassanali has been selected as a Climate Change Icon by the British Council Tanzania for his role in creating an Initiative for a Better cleaner and Neater Future for Tanzanian through Art, Fashion, and Design.
Mustafa Hassanali’s commitment is to not only to promote the creative sector Industry especially Fashion in Tanzania , but also emphasise the Made in Tanzania Concept.
The Exhibition is part of Mustafa Hassanali Tenth Anniversary Celebration since His first Crowning Outfit Designed for Miss Tanzania 1999 Hoyce Temu