TANGAZA NASI LEO

Wednesday, March 7, 2012

Bandari wapiga jeki mchezo wa bao


Makamu wa Rais wa Shirikisho la Mchezo wa Bao Tanzania(SHIMBATA)
Anna Senkoro (katikati) akiongea na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam
wakati wa kupokea msaada shilingi milioni 3 na kapeti kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa
Bandari Tanzania(TPA) kwa ajili ya kuendeleza mchezo wa bao nchini. Wengine ni Rais
wa Shirikisho la Mchezo wa Bao Tanzania(SHIMBATA) Monday Likwepa(kushoto) na Afisa
Mawasiliano wa TPA Cecilia Korassa(kulia)

Picha na Tiganya Vincent-MAELEZO-Dar es salaam

Local miners reported Missing following Geita rockslide

NHIF YAWEKA KAMBI YA UPIMAJI AFYA STENDI KUU MKOANI SINGIDA NA KUTOA MSAADA KTK HOSPITALI ZA MKOA HUO


MGANGA MKUU MFAWIDHI WA HOPSITALI YA MKOA WA SINGIDA DKT. SULEMANI MTTANI AKIMWELEZA MJUMBE WA BODI YA NHIF BWN ALEX MAGESE MAANDALIZI YA AWALI YA UKARABATI WA JENGO(ALIPO PICHANI) LITAKALOTUMIKA KUWAHUDUMIA WANACHAMA WA NHIF NA CHF HIVI KARIBUNI.

MJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI WA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA BWN. ALEX P. MAGESA AKITOA ZAWADI YA MASHUKA 700 KWA NIABA YA HOSPITALI,ZAHANATI NA VITUO VYA AFYA MKOANI SINGIDA KWA MUUGUZI MKUU WA MKOA HUO BI.ELLETRUDE MAKOWI

DR. KUBONYA WA NHIF AKIMPA USHAURI WA NAMANA YA KULINDA AFYA YAKE KUTOKANA NA UZITO ULIOONGEZEKA BWN ALLY JUMANNE AKIWA NI MMOJA WA WAKAAZI WALIOJITOKEZA KUPIMA NA KUJUA HALI ZA AFYA ZAO LEO MKOANI SINGIDA,NHIF IMEWEKA KAMBI HIYO MAHUSUSI IKIWA NI KUWAHAMASISHA WANANCHI KUWA NA UTAMADUNI WA KUPIMA AFYA MARA KWA MARA.

Taarifa za uwepo wa chuo FEKI NCHINI

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania imepokea taarifa kupitia matangazo yanayotolewa na chuo kinachojiita “Japan Bible Institute Graduate School of Theology” kikijitangaza kwamba kinatoa shahada mbalimbali za uzamivu (PhD) kwenye nyanja za dini na jamii. Chuo hiki kinajitangaza kwamba kinawakilisha tawi la taasisi iliyopo nchini Marekani na kwamba makao yake makuu kwa bara la Afrika yapo Dar es Salaam, pamoja na kwamba eneo halisi ofisi zao zilipo haijaelezwa kwenye matangazo yao.

Tume inachukua fursa hii kuuarifu umma kwamba chuo hiki hakitambuliki kwa mujibu wa sheria na kwamba wamiliki wa Japan Bible Institute Graduate School of Theology hawana kibali cha kutoa elimu ya chuo kikuu ambayo inatambuliwa hapa nchini. Tume inatoa tahadhari kwa umma kuepuka ulaghai ambao unafanywa na watu katika eneo hili la elimu ya juu na hivyo umma unashauriwa kuchukua tahadhari kwani vyeti watakavyotolewa havitambuliwi na Tume na hivyo haviwezi kutumika hapa nchini.

Pia, wamiliki wa chuo hiki na wawakilishi wake waliopo Tanzania wanapewa onyo kuacha mara moja kutoa matangazo ya shahada za aina hiyo hapa nchini bila kufuata taratibu. Hatua za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakaye kwenda kinyume na tangazo hili.

Aidha, Tume inapenda kuwaarifu watu wote wenye lengo la kuanzisha vyuo vikuu nchini au kutoa programu za vyuo vikuu wawasiliane na Tume ili kupata maelekezo juu ya taratibu zinazotakiwa kufuatwa. Pia umma unasahauriwa kutoa taarifa kwa Tume ama vyombo vingine vya dola pale ambapo wana wasiwasi na uhali wa programu ama tuzo inayotangazwa au kutolewa na taasisi yoyote bila kufuata taratibu.

Imetolewa na:
Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania
S.L.P. 6562
DAR ES SALAAM

Nyimbo 10 bora za Whitney Houston

Gwiji wa muziki wa pop mwanadada Whitney Houston ambaye alikutwa amekufa katika bafu Jumamosi Februari 11 katika hoteli ya Beverly Hills saa chache kabla ya kuingia katika hafla ya mentor wake Clive Davis kwenye hafla ya kabla ya Tuzo za Grammy na kuzikwa nyumbani kwao ameacha nyimbo kumi ambazo zinatisha. Wakati dunia inamlilia mwanadada huyu hebu tuangalie nyimbo zake 10 bora zilizotikisa dunia na ambazo nyingi bado zinatikisa.


"I Will Always Love You" -- 1992
Houston's bigest hit was actually a cover of a 1970s Dolly Parton single, but when the pop diva sang it for her film The Bodyguard, she managed the rare feat of not only making the song her own but creating the definitive version of the unforgettable track. It's one of the longest-running singles of all time, staying No. 1 for a then-record of 14 weeks.
"Greatest Love of All" -- 1986
Anyone who grew up in the '80s can probably sing this entire song verbatim. The inspiration anthem spent three weeks topping Billboard's pop charts, and is one of Houston's signature tracks, considered the pinnacle of her self-titled debut album.

"How Will I Know" -- 1986
One of Houston's three biggest hits from her first album, this single showed off Houston's crossover appeal as a pop, R&B and dance artist. The upbeat single with the catchy hook stayed No. 1 for two weeks.

"I Wanna Dance With Somebody (Who Loves Me)" -- 1987
The first single released from Houston's sophomore album, Whitney, "I Wanna Dance With Somebody" immediately topped the charts, just as the pop star earned the honor of being the first female artist to debut an album at No. 1. The song went on the win a Grammy for best female pop vocal performance.

"So Emotional" -- 1987
Another of Houston's dance hits, "So Emotional" (from her second album, Whitney) had a strong guitar riff that gave it a rock feel. Penned by hitmakers Billy Steinberg and Tom Kelly, who were best known for Madonna's "Like a Virgin" and Cyndi Lauper's "True Colors," the single was the singer's sixth consecutive No. 1 hit, tying Houston with The Beatles and The Bee Gees.

"Saving All My Love For You" -- 1985
Originally recorded by R&B couple Marilyn McCoo and Billy Davis Jr. in the late '70s, Houston's cover from her debut album became the first of her many No. 1 hits. Unlike many of her other songs, which bolstered Houston's then clean-cut image, "Saving All My Love" is from the perspective of a mistress discussing her affair with a married man.


"Didn't We Almost Have It All" -- 1987
Nominated for best song at the 1988 Grammys Awards, "Didn't We Almost Have It All" was Houston's second single and No. 1 hit from her album Whitney. It's speculated that the song is about Houston's failed relationship with football player Randall Cunningham.


"I'm Your Baby Tonight' -- 1990
Written by R&B hitmakers L.A. Reid and Babyface, "I'm Your Baby Tonight" was the title track from Houston's third studio album. It went on to reach the top of the Billboard charts, making the dance hit her eighth No. 1 single.


"Where Do Broken Hearts Go" -- 1988
Houston was reportedly reluctant to include the single in her second studio effort, but Clive Davis persuaded her to record the song. It became her record-breaking seventh consecutive No. 1 hit, making her (to this day!) the only recording artist ever to accomplish that feat.

"The Star Spangled Banner" -- 1991
So many artists are famous for flubbing the national anthem, but not Houston. We're not sure any pop star has performed "The Star Spangled Banner" as beautifully as the pitch-perfect Houston at Super Bowl XXV, a particularly poignant year, because our troops were serving in the Persian Gulf.

Tuesday, March 6, 2012

Mbeya masoko yaendelea kuteketea ,sasa Tunduma



Maduka yapatayo kumi katika eneo la jirani na mpakani mwa
Tanzania na Zambia mjini Tunduma wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya yameteketea
kwa moto usiku wa kuamkia leo na kusababisha hasara kubwa.
Mashuhuhuda wa tukio hilo wanasema moto huo ulizuka saa 8 usiku na ulianza
katika chumba kimoja wapo katika soko hilo lililo upande wa pili wa lile
lililoteketea kwa moto mwishoni mwa mwaka jana lakini likajengwa upya na
hivi karibuni makamu wa rais Mohamed Gharib Bilal akalifungua alipokuwa
ziarani mkoani hapa.
mashuhuda wanasema huenda chanzo cha moto huo ni mshumaa uliokuwa umewashwa na
kusahaulika katika chumba hicho kwakuwa umeme ulikuwa umekatika usiku huo,
lakini pia huenda ni hitilafu ya umeme ambao wanadhani ulirejea ukiwa na
nguvu kubwa.
Kwa mujibu wa mkuu huyo wa wilaya chanzo cha moto huo hakijajulikana lakini
thamani ya mali zilizoteketea inakadiriwa kufikia milioni 300.
Hii si mara ya kwanza kwa mkoa wa Mbeya kukumbwa na tukio kama hili,kwani
kwa miezi mfululizo matukio ya kuungua masoko yamekuwa yakitokea mkoani
hapa ambapo lilianza soko la Mwanjelwa,likafuatiwa na la Uhindini,baadaye
Sido,yakafuata soko la Forest na Tunduma upande mmoja kabla ya hili la
upande wa pili kukumbwa na mkasa huo.

Mohammed Dewji akwaa tuzo ya Kiongozi Kijana Duniani


TAASISI ya World Economic Forum (WEF) imemtangaza mjasiriamali kijana nchini, Mohammed Dewji (pichani) kuwa mshindi wa Tuzo ya Kiongozi Kijana wa Duniani (YGL) wa mwaka huu.
Dewji, ambaye anajulikana zaidi kwa jina la MO, ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL) na Mbunge wa Singida Mjini, na kwamba ni mjasiriamali pekee Afrika Mashariki aliyepewa heshima hiyo mwaka huu.
Heshima hiyo hutolewa kila mwaka na WEF ambayo hutambua zaidi ya vijana viongozi 200 duniani kote kutokana na mafanikio yao, ushiriki wao katika jamii na mchango wao katika kutengeneza dunia ya baadaye.
Kamati ya uteuzi huo iliyoongozwa na mwenyekiti wake, Malkia Rania Al Abdullah wa Ufalme wa Jordan, ilimchagua Dewji baada ya kupitia taarifa za vijana wengi kutoka maeneo mbalimbali duniani.
Vigezo vya kuteuliwa kwake kushika heshima hiyo ni rekodi yake ya kitaaluma katika mafanikio yake, uwajibikaji wake katika jamii na kutumia nafasi ya uongozi na kuwa mfano duniani.
Washindi wa Tuzo ya YGL 2012 wataungana na jumuiya kubwa ya Mkutano wa Viongozi Vijana wa Dunia ambao unawajumuisha watu 668. Mkutano huo wa YGL unafanyika kila mwaka, ambao mwaka huu utafanyika Mexico kuanzia Aprili 14 hadi 18.
Viongozi Vijana wa Dunia hujikita katika shughuli za kijamii, kujumuika katika matukio yanayoandaliwa na WEF na kuandaa matukio yao wenyewe na kufanya ubunifu wao pamoja na vikosikazi.
“Ninaishukuru sana WEF kwa kunipatia heshima hii kama kiongozi kijana, ninaweza kuwasaidia vijana wa Tanzania kutimiza ndoto za maisha yao ili kuweza kupata maisha mazuri,” alisema Dewji leo.
MO anakuwa Mtanzania wa tatu kushinda katika tuzo hiyo akitanguliwa na mmiliki wa kampuni inayoshughulikia ndege binafsi, Executive Jets, Suzan Mashibe na aliyekuwa Mshauri wa Uchumi wa Rais Jakaya Kikwete, Elsie Kanza.
Mfanyabiashara huyo alizaliwa mwaka 1975 mkoani Singida, na alipata elimu yake ya awali katika Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST) na mwaka 1992 alienda Marekani na kupata elimu ya juu ya sekondari.
Katika Shule ya Sekondari ya Florida ndipo alipoanza kuonesha dalili za uongozi baada ya shuleni hapo kuchaguliwa kuwa Rais wa wanafunzi na ndipo jina la MO liliposhika.
MO baadaye alihamia katika Chuo Kikuu cha Georgetown jijini Washington DC, ambako alisomea masuala ya biashara ya kimataifa na fedha, na masomo machache ya Theolojia. Chuo hicho huwajenga wanafunzi wake kufanya kazi zao kwa mafanikio. Kutokana na hilo, kuanzia mwaka 1998, alianza kujikita katika biashara za familia yake ambako alipanda hadi kufikia katika uongozi wa juu katika muda wa miaka miwili.
Chini ya uongozi wake, MeTL Group ilijibadilisha na kuwa kundi la makampuni lililokuwa na kampuni tanzu 12 katika muda usiozidi muongo mmoja. Hilo limeiwezesha kampuni hiyo kuchangia asilimia tatu katika Pato ya Taifa na kuajiri watu 24,000. Dewji ni mpenzi na mfadhili wa soka ya Tanzania na amekuwa akichangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya timu ya Taifa (Taifa Stars).
Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, MO aliwania na kushinda kiti cha ubunge cha Singida Mjini kwa tiketi ya CCM kwa zaidi ya asilimia 90 ya kura zote. Mwaka 2007, alichaguliwa kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa na alishinda tena ubunge 2010.