Temporary Shelter

CHATROOM

Sunday, June 16, 2013

KIDUKU KINAPOKOLEA HEBU FIKIRIA NI WAPI



APIYO AZIKWA KIJIJINI KWAKE



Jeneza la Apiyo likifikishwa eneo la maziko

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda leo aliongoza mamia ya waombolezaji kumzika aliyekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Timoth Apiyo, nyumbani kwake kijiji cha Marasibora, kilometa 56 kutoka Musoma mjini, mkoani Mara.
Pinda  alitoa pole kwa familia na wakazi wa Kijiji cha Mara Sibora,Wilaya ya Rorya na Mkoa wa Mara kwa kumpoteza kiongozi na mzalendo aliyeitumikia nchi yake kwa uadilifu.
Wengine waliohudhuria maziko ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu); Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue; Makatibu Mkuu Viongozi wastaafu, Balozi Paul Rupia, Balozi Marten Lumbanga na Philemon Luhanjo pamoja na mke wa hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere pia walishiriki.
Waziri Mkuu Pinda akitoa salamu za mwisho

Pinda akizungumza na mjane wa Nyerere, Maria Nyerere mazikoni

jeneza lenye mwili wa Apiyo likishushwa kaburini

Apiyo (82) alifariki hospitalini, Millpark Johannesburg Afrika Kusini usiku wa Juni 10, alikokwenda kutibiwa na mwili wake kurejeshwa nchini wiki hii.
Alistaafu kuwa Katibu Mkuu wa Rais, Ikulu, sasa Katibu Mkuu Kiongozi, mwaka 1986. Ameacha mjane
na watoto saba.
Wasifu uliotolewa kabla ya mwili wake kushushwa kaburini, ulielezea utumishi wake uliotukuka.  Alianza utumishi wa Serikali katika ngazi ya chini akiwa Bwanashamba, baada ya kuhitimu Shahada ya Kilimo kutoka Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda.
Afya yake ilianza kutetereka mwaka 1996 baada ya kupata ugonjwa wa kiharusi. Aliwahi kutibiwa India na Afrika Kusini, kabla ya hali yake kuzorota zaidi mapema mwezi huu na hatimaye kukutwa na mauti.
Alipolazwa ni kwenye kaburi lililo ndani ya uwanja wa nyumba yake, kando ya kaburi la marehemu mke wake, Rhoda Apiyo, aliyefariki mwaka 2006.
Wakazi wa Kijiji cha Mara Sibora  na familia ya marehemu Apiyo wameipongeza Serikali
kwa mchango wao mkubwa tangu kifo cha ndugu yao nje ya nchi na na kuletwa nchini kisha kufanikisha maziko kwa heshima kijijini hapo.
Mkuu wa Mkoa wa Mara,  John Tuppa amewapongeza wakazi wa kijiji hicho na viongozi  wa  vyama vya siasa na Serikali kwa kujitokeza kwa wingi katika maziko hayo.

steps yawatambua washirika wake wa karibu yawapa tuzo

Bosi wa steps akishangiliwa

Shilole alikuwapo

JB naye akiepwa tuzo na mkurugenzi wa Steps

wasanii waliopewa tuzo.Steps husambaza sinema za watu hawa

Mzee majuto pia

MSHINDI WA REDD’S MORO 2013 APATIKANA

Mshindi  wa taji la Redd's Miss  Morogoro 2013 ,mrembo , Diana Laizer
(21)  akiwapungia
mkono wananchi  waliofika ukumbini kushuhudia kinyang’anyiro cha kuwania
taji hilo   ( kulia ) ni mshindi wa pili , Sabra Islam (18) wakati ( kulia)
ni mshindi wa tatu, Muzne Abduly ( 19) ni mara baada ya majaji kuwatangaza
kushinda nafasi hizo, shindano hilo lilifanyika usiku wa jana ( Juni 15)
katika  Ukumbi wa Hoteli ya Nashera ya Mjini Morogoro.

( Picha hii mali ya John Nditi wa habarileo).

Marieta ndiye Redd’s Miss Chang’ombe

MREMBO Marieta Boniface juzi usiku alifanikiwa kutwaa taji la Redd’s Miss Chang’ombe, katika kinyang’anyiro kilichokuwa kikali kilichofanyika kwenye viwanja vya TCC Club, vilivyopo Chang’ombe, Dar es Salaam.

Marieta alifanikiwa kuwashinda warembo wengine 12 walioshiriki katika kinyang’anyiro hicho ambacho kilikuwa na upinzani mkali.

Kutokana na ushindi huo, Marieta alizawadiwa pikipiki yenye thamani ya Sh milioni 1.5 ambayo ilitolewa na wadhamini wenza Kampuni ya Kishen Enterprises Ltd.

Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu aliyekuwa mgeni rasmi ndiye aliyemkabidhi zawadi hiyo na kusema amefurahishwa kwa kiasi kikubwa na shindano hilo na yupo tayari kulisaidia zaidi.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa taji, Marieta alisema anaamini kwa dhati atafanikiwa kufika mbali zaidi kwani amedhamiria kuhakikisha anaibeba Chang’ombe katika shindano la Redd’s Miss Tanzania.

Shindano la Redd’s Miss Tanzania kwa sasa linadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia kinywaji chake cha Redd’s Original.

KAULI YA MHE JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KUHUSU SHAMBULIO LA MLIPUKAO ARUSHA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
amepokea kwa mfadhaiko, mshituko na huzuni kubwa taarifa za shambulio la
mlipuko lililotokea katika mkutano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA) mjini Arusha jioni ya leo, Jumamosi, Juni 15, 2013, tukio ambalo
limesababisha vifo vya watu wawili na majeruhi ya Watanzania kadhaa.

Aidha, Rais Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa jamaa na ndugu wa
wafiwa wote na pia ametuma pole nyingi kwa majeruhi ambao wameumizwa na
kujeruhiwa katika tukio hilo ovu na katili.

Vile vile, Rais Kikwete amewatumia salamu za pole viongozi wa CHADEMA
kufuatia tukio hilo la woga mkubwa na pia kuviagiza vyombo vya ulinzi na
usalama kuchukua hatua stahiki za kuchunguza kwa haraka, kubaini,
kuwakamata na kuwafikisha mbele ya sheria wote waliohusika na tukio hilo,
wawe watu wa ndani ya nchi ama nje ya nchi.

Katika salamu zake za rambirambi na za pole kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha,
Mheshimiwa Magesa Mulongo, Rais Kikwete amesema: “Nimepokea kwa mfadhaiko,
mshituko na huzuni kubwa shambulio la mlipuko lililotokea katika mkutano wa
CHADEMA mjini Arusha jioni ya leo, tukio ambalo limesababisha vifo na
majeruhi ya Watanzania wenzetu.”

Amesema Rais Kikwete: “Nakutumia wewe Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa
Magesa Mulongo salamu zangu za rambirambi kufuatia vifo na pole nyingi
kutokana na majeruhi katika tukio hilo na naomba kupitia kwako unifikishie
salamu zangu za rambirambi kwa jamaa na ndugu wa wafiwa na pole nyingi sana
kwa majeruhi.”

“Kadhalika naomba unifikishie salamu zangu za pole kwa viongozi na
wanachama wa CHADEMA kutokana na tukio hilo. Naomba uwajulishe kuwa uchungu
wao ni uchungu wetu sote na msiba wao  ni msiba wetu pia. Nataka wajue kuwa
tupo pamoja nao katika kipindi hiki kigumu na cha majonzi na huzuni
mkubwa,” amesema Mheshimiwa Rais Kikwete.

Rais Kikwete amemwambia Mkuu wa Mkoa wa Arusha: “Kadhalika, nimeviagiza
vyombo vya ulinzi na usalama kuchukua hatua za haraka kuwasaka wahusika,
kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria. Aidha, nawataka
viongozi wa Serikali ngazi ya kitaifa, Mkoa wa Arusha na Wilaya ya Arusha
mjini kuhakikisha kuwa majeruhi wote wanapata matibabu ya haraka na huduma
za tibabu stahiki.”

Aidha, Rais Kikwete ametoa wito maalum kwa wananchi akisema: “Kwa wananchi
wenzangu, Watanzania wenzangu, napenda kutoa wito wa kuviachia vyombo vya
ulinzi na usalama kufanya kazi yao vizuri ili tuweze kuwabaini waovu
waliofanya kitendo hiki.”

“ Natambua kuwa yatakuwepo maneno mengi na hisia mbali mbali zitakazojaribu
kulielezea tukio hilio ovu na katili kwa njia mbali mbali. Nawasihi
tujiepushe na kuchukua dhana na hisia zetu au maneno ya watu wengine kuwa
ni ukweli wa tukio hili. Tujipe nafasi ya kutafakari vizuri na kufanya
uamuzi ulio bora.”

Ameongeza Rais Kikwete: “Mimi siamini kuwa Watanzania au wafuasi wa vyama
vya siasa wanachukiana kiasi cha kufanyiana matendo ya unyama wa aina hii.
Naamini kuwa hiki ni kitendo cha mtu ama watu wasioitakia mema nchi yetu,
watu ambao wanatafuta kila sababu ya kupandikiza chuki miongoni mwa raia
ama makundi ya raia, ili nchi yetu iingie kwenye machafuko makubwa.”

“Ndugu zangu, Watanzania wenzangu, naomba tuzinduke,  ili tusiwape nafasi
watu hawa waovu ya kuweza kutimiza malengo yao ya kuvuruga amani na utulivu
wa nchi yetu kwa kuleta mifarakano baina yetu. Mungu Ibariki Tanzania,
Mungu Ibariki Afrika.”
TANGAZA NASI LEO

xx