Sunday, June 16, 2013
APIYO AZIKWA KIJIJINI KWAKE
7:53 PM
No comments
| Jeneza la Apiyo likifikishwa eneo la maziko |
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda leo aliongoza mamia ya waombolezaji
kumzika aliyekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Timoth Apiyo, nyumbani kwake
kijiji cha Marasibora, kilometa 56 kutoka Musoma mjini, mkoani Mara.
Pinda alitoa pole kwa
familia na wakazi wa Kijiji cha Mara Sibora,Wilaya ya Rorya na Mkoa wa Mara kwa
kumpoteza kiongozi na mzalendo aliyeitumikia nchi yake kwa uadilifu.
Wengine waliohudhuria maziko ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais
(Mahusiano na Uratibu); Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue; Makatibu
Mkuu Viongozi wastaafu, Balozi Paul Rupia, Balozi Marten Lumbanga na Philemon
Luhanjo pamoja na mke wa hayati Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere pia
walishiriki.
| Waziri Mkuu Pinda akitoa salamu za mwisho |
| Pinda akizungumza na mjane wa Nyerere, Maria Nyerere mazikoni |
| jeneza lenye mwili wa Apiyo likishushwa kaburini |
Apiyo (82) alifariki hospitalini, Millpark Johannesburg Afrika
Kusini usiku wa Juni 10, alikokwenda kutibiwa na mwili wake kurejeshwa nchini
wiki hii.
Alistaafu kuwa Katibu Mkuu wa Rais, Ikulu, sasa Katibu Mkuu
Kiongozi, mwaka 1986. Ameacha mjane
na watoto saba.
Wasifu uliotolewa kabla ya mwili wake kushushwa kaburini,
ulielezea utumishi wake uliotukuka.
Alianza utumishi wa Serikali katika ngazi ya chini akiwa Bwanashamba,
baada ya kuhitimu Shahada ya Kilimo kutoka Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda.
Afya yake ilianza kutetereka mwaka 1996 baada ya kupata
ugonjwa wa kiharusi. Aliwahi kutibiwa India na Afrika Kusini, kabla ya hali
yake kuzorota zaidi mapema mwezi huu na hatimaye kukutwa na mauti.
Alipolazwa ni kwenye kaburi lililo ndani ya uwanja wa nyumba
yake, kando ya kaburi la marehemu mke wake, Rhoda Apiyo, aliyefariki mwaka
2006.
Wakazi wa Kijiji cha Mara Sibora na familia ya marehemu Apiyo wameipongeza
Serikali
kwa mchango wao mkubwa tangu kifo cha ndugu yao nje ya nchi na
na kuletwa nchini kisha kufanikisha maziko kwa heshima kijijini hapo.
Mkuu wa Mkoa wa Mara,
John Tuppa amewapongeza wakazi wa kijiji hicho na viongozi wa
vyama vya siasa na Serikali kwa kujitokeza kwa wingi katika maziko hayo.
steps yawatambua washirika wake wa karibu yawapa tuzo
4:45 PM
No comments
MSHINDI WA REDD’S MORO 2013 APATIKANA
12:41 PM
No comments
Marieta ndiye Redd’s Miss Chang’ombe
12:07 PM
No comments
MREMBO Marieta Boniface juzi usiku alifanikiwa kutwaa taji la Redd’s Miss Chang’ombe, katika kinyang’anyiro kilichokuwa kikali kilichofanyika kwenye viwanja vya TCC Club, vilivyopo Chang’ombe, Dar es Salaam.
Marieta alifanikiwa kuwashinda warembo wengine 12 walioshiriki katika kinyang’anyiro hicho ambacho kilikuwa na upinzani mkali.
Kutokana na ushindi huo, Marieta alizawadiwa pikipiki yenye thamani ya Sh milioni 1.5 ambayo ilitolewa na wadhamini wenza Kampuni ya Kishen Enterprises Ltd.
Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu aliyekuwa mgeni rasmi ndiye aliyemkabidhi zawadi hiyo na kusema amefurahishwa kwa kiasi kikubwa na shindano hilo na yupo tayari kulisaidia zaidi.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa taji, Marieta alisema anaamini kwa dhati atafanikiwa kufika mbali zaidi kwani amedhamiria kuhakikisha anaibeba Chang’ombe katika shindano la Redd’s Miss Tanzania.
Shindano la Redd’s Miss Tanzania kwa sasa linadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia kinywaji chake cha Redd’s Original.
Marieta alifanikiwa kuwashinda warembo wengine 12 walioshiriki katika kinyang’anyiro hicho ambacho kilikuwa na upinzani mkali.
Kutokana na ushindi huo, Marieta alizawadiwa pikipiki yenye thamani ya Sh milioni 1.5 ambayo ilitolewa na wadhamini wenza Kampuni ya Kishen Enterprises Ltd.
Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu aliyekuwa mgeni rasmi ndiye aliyemkabidhi zawadi hiyo na kusema amefurahishwa kwa kiasi kikubwa na shindano hilo na yupo tayari kulisaidia zaidi.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa taji, Marieta alisema anaamini kwa dhati atafanikiwa kufika mbali zaidi kwani amedhamiria kuhakikisha anaibeba Chang’ombe katika shindano la Redd’s Miss Tanzania.
Shindano la Redd’s Miss Tanzania kwa sasa linadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia kinywaji chake cha Redd’s Original.
KAULI YA MHE JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KUHUSU SHAMBULIO LA MLIPUKAO ARUSHA
11:56 AM
No comments
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amepokea kwa mfadhaiko, mshituko na huzuni kubwa taarifa za shambulio la mlipuko lililotokea katika mkutano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mjini Arusha jioni ya leo, Jumamosi, Juni 15, 2013, tukio ambalo limesababisha vifo vya watu wawili na majeruhi ya Watanzania kadhaa. Aidha, Rais Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa jamaa na ndugu wa wafiwa wote na pia ametuma pole nyingi kwa majeruhi ambao wameumizwa na kujeruhiwa katika tukio hilo ovu na katili. Vile vile, Rais Kikwete amewatumia salamu za pole viongozi wa CHADEMA kufuatia tukio hilo la woga mkubwa na pia kuviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuchukua hatua stahiki za kuchunguza kwa haraka, kubaini, kuwakamata na kuwafikisha mbele ya sheria wote waliohusika na tukio hilo, wawe watu wa ndani ya nchi ama nje ya nchi. Katika salamu zake za rambirambi na za pole kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Magesa Mulongo, Rais Kikwete amesema: “Nimepokea kwa mfadhaiko, mshituko na huzuni kubwa shambulio la mlipuko lililotokea katika mkutano wa CHADEMA mjini Arusha jioni ya leo, tukio ambalo limesababisha vifo na majeruhi ya Watanzania wenzetu.” Amesema Rais Kikwete: “Nakutumia wewe Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Magesa Mulongo salamu zangu za rambirambi kufuatia vifo na pole nyingi kutokana na majeruhi katika tukio hilo na naomba kupitia kwako unifikishie salamu zangu za rambirambi kwa jamaa na ndugu wa wafiwa na pole nyingi sana kwa majeruhi.” “Kadhalika naomba unifikishie salamu zangu za pole kwa viongozi na wanachama wa CHADEMA kutokana na tukio hilo. Naomba uwajulishe kuwa uchungu wao ni uchungu wetu sote na msiba wao ni msiba wetu pia. Nataka wajue kuwa tupo pamoja nao katika kipindi hiki kigumu na cha majonzi na huzuni mkubwa,” amesema Mheshimiwa Rais Kikwete. Rais Kikwete amemwambia Mkuu wa Mkoa wa Arusha: “Kadhalika, nimeviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuchukua hatua za haraka kuwasaka wahusika, kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria. Aidha, nawataka viongozi wa Serikali ngazi ya kitaifa, Mkoa wa Arusha na Wilaya ya Arusha mjini kuhakikisha kuwa majeruhi wote wanapata matibabu ya haraka na huduma za tibabu stahiki.” Aidha, Rais Kikwete ametoa wito maalum kwa wananchi akisema: “Kwa wananchi wenzangu, Watanzania wenzangu, napenda kutoa wito wa kuviachia vyombo vya ulinzi na usalama kufanya kazi yao vizuri ili tuweze kuwabaini waovu waliofanya kitendo hiki.” “ Natambua kuwa yatakuwepo maneno mengi na hisia mbali mbali zitakazojaribu kulielezea tukio hilio ovu na katili kwa njia mbali mbali. Nawasihi tujiepushe na kuchukua dhana na hisia zetu au maneno ya watu wengine kuwa ni ukweli wa tukio hili. Tujipe nafasi ya kutafakari vizuri na kufanya uamuzi ulio bora.” Ameongeza Rais Kikwete: “Mimi siamini kuwa Watanzania au wafuasi wa vyama vya siasa wanachukiana kiasi cha kufanyiana matendo ya unyama wa aina hii. Naamini kuwa hiki ni kitendo cha mtu ama watu wasioitakia mema nchi yetu, watu ambao wanatafuta kila sababu ya kupandikiza chuki miongoni mwa raia ama makundi ya raia, ili nchi yetu iingie kwenye machafuko makubwa.” “Ndugu zangu, Watanzania wenzangu, naomba tuzinduke, ili tusiwape nafasi watu hawa waovu ya kuweza kutimiza malengo yao ya kuvuruga amani na utulivu wa nchi yetu kwa kuleta mifarakano baina yetu. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika.”
Subscribe to:
Posts (Atom)












