Sunday, November 15, 2009

Jamaa waua wala mwili wa waliyemuua na kuuza sehemu nyingine kwa vioski


Polisi nchini Urusi wamewakamata watu wanne wasiokuwa na makazi kwa tuhuma za kuua mtu mwenye umri wa miaka 25 kumla sehemu ya mwili wake kuuza baadhi kwa kebab and pie kiosk. Skip related
The alarm was raised when bits of a corpse were found near a bus stop on the outskirts of Perm, about 720 miles east of Moscow.
A statement on the Perm police website said the three alleged cannibals had previous criminal records.
The statement said they were detained on suspicion of stabbing a man to death and then chopping him up for food.
It went on: "After carrying out the crime, the corpse was divided up.
"Part was eaten and part was also sold to a kiosk selling kebabs and pies."
It was not clear from the statement if the kiosk had cooked any of the man's flesh and sold it to customers.

Mtu wa mwisho katika dhahama ya same azikwa ni mtoto kutoka ukoo ambao umepata maafa makubwa


Mkuu wa wilaya ya Same ibrahimu Marwa akiweka udongo huku mkuu wa mkoa Bi monica MBEGA akishuhudia wakati wa maziko ya mtoto NDIMANGWA ELINEMA (5)ambaye alikuwa miongoni mwa wanavijiji 24 waliofunikwa na maporomoko ya udongo kijiji cha Goha, Same na kufa. Nimeambiwa kwamba Anne Kilango mbunge wa Same aliangua kilio kisichotulizwa baada ya kushuhudia maafa yaliyozuka katika kijiji cha asili za babu yake. Mtoto huyu aliyezikwa anatoka katika ukoo uliopoteza watu wake 14 na kubakiza watatu.habari zaidi soma HabariLeo

Ukitaka kwenda kwetu Mgetalaizma upite Mlali na huu ndio usafiri and i am not jocking


Ukitaka kwenda kwetu milimani Nyandira Tchenzema huko Mgeta ilipo Lukwangule ni lazima upite hapa Mlali.Pichani ni watoto wawili wakiwa na kaka yao ambao majina yao hayakufahamika mara moja Kata ya Mlali, Wilaya ya Mvomero, wakiwa ndani ya mkokoteni unaovutwa na punda huku ukiwa na shehena ya mzigo ikiwemo saruji .Picha na Mdau John Nditi anayefanya shughuli zake na HabariLeo.

Juma Nyumayo ameshughulikiwa na matapeli wa mtandaoni jamaa zake kuweni macho

Hii ni barua ambayo nimeletewa katika e mail yangu.
Ni baruja yenye lugha ile ile ya jamaa wanaosaka vitu mtandaoni.
Naamini kipindi kama hiki Juma mwenyewe hawezi tena kufungua boksi lake.
Kutokana na hali hii naamini kabisa kwamba Juma Nyumayo yuko fiti nyumbani kwake Songea na anaendelea na libeneke lake la habari na ufundishaji kama kawaida.
Wakati fulani Da Subi wa nukta 77 sasa wavutui alitoa onyo dhidi ya wahuni wnaaoingia katika mtandao na kutaka uwapatie detail za pasi yako katika boksi. hakuna kitu kama upgrading inayotaka sijui utoe pasi, Ukibanwa ukatoa madhara yake ni makubwa.Marafiki wa Nyumayo lazima kuwa macho katika hili.
Hii ndiyo barua niliyoletewa na ambayo naamini imesambazwa kote.
Lukwangule

iHope this finds you well and i believe everything is okay with you.I had a trip to London for a workshop/seminar. Unfortunately the seminar committees bus that was conveying us to the invitees hotel had a brake failure and collided with a produce supply vehicle and burst into flames,i escaped with minor 1st degree burns and in the ensuing inferno,i lost my travel documents and certificates of immeasurable value.By a stroke of luck,passing paramedics on their way to the scene of a robbery happened to see us and called for a back up vehicle to convey the survivors to the hospital and the dead to the mortuary.I would have put a call through to you but unfortunately my phone got lost in the incident as well.

I'm gradually recuperating but as fast as my health is recuperating, so is my health bill accumulating. I even need to undergo a skin grafting operation but the funds are witholding me.I would need you to help me with about 1250 Pounds to help me in settling my hospital bills.I should expect to see you on my return and hope i resume fully hale and hearty.
My hope on you as i pray this message gets to you as i am using the matron in charges PDA.
Regards,
juma

Kilimo cha Mwani cha dorora Lindi


ZAO la mwani mkoani Lindi limeshuka kwa uzalishaji kutoka tani 363.5 kwa mwaka 2007/2008hadi kufikia kg 215.7 mwaka 2008/2009 kutokana ukosefu wa pembejeo kwa wakulima sambamba na kutopanda kwa bei.
Mkuu wa mkoa wa Lindi Saidi Mecky Sadiki aliyasema hayo juzi wakati alipokuwa akitoa taarifa za mkoa mbele ya mgeni rasmi waziri mkuu Mizengo pinda, wilayani Kilwa.
Alisema zao hillo hulimwa katika vijiji vya Songosongo, Masoko, Songomara Pnde na Namwendo, Mkoma katika halamshauri ya wilaya Kilwa.
Alisema katika wilaya ya Lindi vijijini mwani hulimwa katika vijiji sita vya Ruvu, Mchinga I Mchinga II, Shuka, Mongomongo na Mmumbu.
Alisema zao hilo linachukuwa nafasi kwa jamii waishioa katika ukanda wa Mwambo wa Pwani kuweza kuwaondolea lea umasikini kwenye wilaya za Kilwa na Lindi, mkoani humo.
Sadiki alisema katika halmashauri ya mji zao hilo linalimwa katika mtaa wa Kitumbwikwera katika eneo la Mwitingi na kasi yake ni ya kusuasua uzalishaji wake.
Alisema wilaya ya Kilwa ilizalisha kwa mwaka 2006/2007 tani zipatazo 83 waliuza shs 18,260,000 mwaka 2007/2008 walizalisha tani 37 na kuingiza shs 8,140,000 na mwaka 2008/2009 ilizalishwa tani 40.5 sawa na kuuza shs 8,910,000 na kwa kilo moja iliuzwa shs 220 kwa kipindi cha miaka hiyo.
Alifafanua katika wilaya ya Lindi katika mwaka 2006/2007 tani zilizozalishwa 118 na kuuzwa shs 25,960,000 2007/2008 tani 326.5 ziliingizwa shs 71,831,760 na katika mwaka 2008/2009 tani 162 zilizalishwa sawa na shs 35,640 na kwa kilo moja iliuzwa shs 220.
Alisema uzalishaji umepungua kiasi hicho hali inasababidsha wakulima kukata tamaa kutokana bei kuwa ya chini mno halingani na gharama za uzalishaji wake.

Jaydee sahani moja na Kidjo na Nd'our






WANAMUZIKI Angelique Kidjo wa Benin, Yossou Nd'our wa Senegal na Mtanzania Judith Wambura ‘Lady Jay Dee’, juzi walizikonga nyoyo za mashabiki katika sherehe iliyoandaliwa na mfanyabiashara maarufu Mo Ibrahim.
Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na maelfu ya watu akiwamo Rais Jakaya Kikwete, burudani hiyo iliwafanya wageni waalikwa kuimba na kucheza. Lady Jay Dee akiwa na bendi yake ya Machozi alikuwa wa kwanza kupanda jukwaani na kuimba wimbo wake wa ‘Siku hazigandi’.
Baada ya Lady Jay Dee kumaliza, ilifuata burudani kutoka kwa Yossou Nd'our ambaye alipanda jukwaani akiwa wamevalia nguo ya utamaduni wa Senegal na kuimba kwa dakika tatu kisha aliwaelekeza watu waliokuwepo ukumbini hapo namna ya kuimba ambapo kila mmoja aliungana naye kuimba kiitikio.
Baada ya hapo, Nd'our aliimba na Kidjo, ambapo safari hii Nd'our aliwaomba baadhi ya viongozi waliokuwepo ukumbini hapo kucheza naye. Wakiongozwa na Rais Kikwete, viongozi hao akiwamo Salim Ahmed Salim, Vuai Nahodha, Mo Ibrahim na viongozi wengine, walijumuika kwa pamoja.
Tukio hilo lilichukua takribani dakika 15 na baadaye aliimba Kidjo peke yake, safari hii aliimba wimbo wa Malaika kwa ufanisi mkubwa.
Nd'our alimalizia kwa kuimba wimbo unaohamasisha maendeleo ya Afrika ambapo aliimba kwa hisia kali na ndipo alifunga dimba la burudani kwa siku hiyo.
Wakati wa tafrija, Rais Kikwete alionekana akizungumza na msanii Nd'our na Lady Jay Dee, hali iliyozusha fikra vichwani mwa watu kuwa alikuwa akimpigia debe Lady Jay Dee kwa Nd'our kuwa amuendeleze kimuziki.
Wasanii hao Nd'our na Kidjo jana waliimba pamoja katika tamasha maalumu lililofanyika kwenye viwanja vya Karimjee.
source: Evance Ng’ingo wa HabariLeo
Picha: Issa Muhidin wa Daily News

Mwisho.

Rais akwea pipa kuelekea Roma, Italia


RAIS Jakaya Mrisho Kikwete ameondoka nchini leo, Jumapili, Novemba 15, 2009, kwenda Italia, kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi Kuhusu Usalama wa Chakula Duniani.
Rais Kikwete atakuwa miongoni mwa wakuu wengi wa Nchi na Serikali duniani kuhudhuria Mkutano huo wa siku mbili unaoanza kesho, Jumatatu, Novemba 16, 2009, kwenye Makao Makuu ya Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) mjini Rome, Italia.
Mkutano huo muhimu unalenga kujadili na kuafikiana kuhusu mikakati ya pamoja ya nchi zote duniani kuhusu jinsi ya kuendeleza kilimo ili kukabiliana na ukosefu wa chakula cha kutosha katika baadhi ya nchi katika zama za sasa za mabadiliko ya tabianchi.
Kwa mujibu wa ratiba ya Mkutano huo, Rais Kikwete amepangiwa kukutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mhe. Ban Ki Moon jioni ya leo, mara tu baada ya kuwa amewasili mjini Rome.
Rais Kikwete atahutubia Mkutano huo kesho, Jumatatu, Novemba 16 mchana, na pia atakutana na viongozi mbali mbali wa mashirika yanayohusiana na kilimo na chakula duniani.
Miongoni mwa viongozi ambao Rais Kikwete atakutana na kufanya mazungumzo nao ni pamoja na Rais wa IFAD, Dkt. Kanayo F Nwanze pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani la WFP, Josette Sheeran.

Pichani: Jana alitoka kuwatembelea wananchi wa Msoga ambao majengo yao yaliezuliwa na upepo mkali uliovuma hivi karibuni.