Simulizi la Jumatatu..Mimi! Mi mtamu wewe...!

JUA lilikuwa linakuchwa taratibu katika maeneo haya ya milima ya Uluguru pande za Mgeta. Maeneo ya Lukwangule tayari yalishapoteza nuru yake...

JUA lilikuwa linakuchwa taratibu katika maeneo haya ya milima ya Uluguru pande za Mgeta. Maeneo ya Lukwangule tayari yalishapoteza nuru yake ya mchana na kiza kilikuwa kimejivuta kama bibi kizee.
Wakati maeneo hayo kiza kinajivuta maeneo ya kijiji cha lusungi yalikuwa bado yanachechemea na mwanga kidogo uliokuwa unavuka.
kuku wote walishaingia katika mabanda yao, wakiwa wametulia tayari kupitisha usiku mwingine tulivu. wanyama wa usiku taratibu walianza kutoka katika maficho yao, bundi mmoja akaanza kulia.
Katika nyumba moja mama kuku alikuwa anahesabu watoto wake huku analia,mbuzi katika mabanda walikuwa wanacheua na kondoo nao pia, walikuwa wameshafunguliwa makopo midomoni mwao na wametulia huku beberu mmoja mgomvi akiwa ametiwa kamba sawia.
Msichana mmoja mweusi wa wastani, mrefu na ambaye alikuwa na umbile la nane, akiwa na mfuko wake mgongoni alikuwa anatembea taratibu katika barabara inayoelekea Bumu. Njiani alikuwa peke yake, lakini alikuwa anashika kasi ya mtu ambaye hakuwa na mazoea ya milima au ambaye ni mgonjwa.
Mwenda binti pekee kwa baba na mama Mwenda alikuwa ameondoka nchini miaka saba iliyopita kwenda kusomea udaktari nchini Russia. Baada ya kupata vyeti vyake alikuwa na kila sababu ya kurejea nyumbani na kuungana na watu wake. Alikuwa amewamisi wazazi wake ambao alikuwa na mazoea ya kuwaandikia barua lakini wenyewe walikuwa na mazoea ya kutomjibu.
Alijua kwanini hawataki kumjibu. Walimweleza mapema kwamba wanaomba awatumie salamu kila mara lakini wao hawataweza kujibu kwa sababu za kiusalama.Walimwambia kwamba baba yake mdogo alikufa kwa namna ya ajabu nchini Canada baada ya kusoma barua iliyotoka nyumbani akidhani inatoka kwa ndugu zake.
Mzee mmoja mchawi alimuua ndugu yao na akatamba kijiji kizima kwamba amewapatia na hilo hawatakaa walisahau maisha yao yote.
Aliingia Dar es salaam saa nne akitokea Nairobi, Kenya ambako aliunga ndege yake. Aliunga mara nyingi sana usafiri wake kwani alipotoka Moscow, alifika Addis Ababa, Ethiopia ambako alikaa kwa siku nzima kabla ya kusafirishwa na Ethiopia Airline na kushushwa Nairobi kenya ambako alichukua Kenya Airways na kutua uwanja wa ndege wa Dar es salaam saa nne asubuhi.
Mpaka saa saba alikuwa amefika kwa ndugu yake Magomeni Mikumi katika nyumba ya Uyeka. Aliketi kwa muda kabla ya kuondoka kwenda kutafuta usafiri wa Morogoro . Pale kwa shangazi yake Magomeni nusura asiondoke baada ya kukutana na wadogo zake ambao walishakua wakubwa wakimshangaashangaa.Lakini alipiga moyo konde hasa baada ya kuelezwa kuwa wazazi wake hawakuwa katika hali nzuri sana inafaa kwenda kuwaona.
Saba nusu, pale Magomeni mapipa alikuwa abiria wa mwisho katika Double Coaster moja ambayo haikubeba abiria tena mpaka inaingia morogoro saa kumi na nusu. Alifikiria sana kwenda gesti kulala lakini aliamua kufanya kitu kimoja cha maana cha kwenda katika soko la Morogoro kuona kama hakuna lori linalopandisha kwenda kwao Mgeta.
Binti huyu bahati ilikuwa kwake, kwani anatia mguu tu akaliona lori ambalo lilikwishapakia pumba na mabati likiwa tayari kuondoka.
"Vipi mnapanda mlimani?"
"Ndio bibiye unataka usafiri?"
"Ndio kama inawezekana"
"Utakuwa mwanamke peke yako huko nyuma manake mbele kumejaa."
"Wala usijali, mpaka Lolo bei gani?"
"Mpaka Lolo? Lolo ndio wapi Hading'oka"
"Ndio Madukani kwani wewe hupajui?"
"Nimechemsha kila mara inakuwa taabu kukumbuka.mama wewe ingia tu tutaelewana sisi binadamu."
"Ninaweza kuwa sina hela hiyo?"
"Huonekani kama huna hiyo hela nitakayoihitaji. nataka shilingi 1,500 tu"alisema dereva na kisha akamhimiza apande kwani anataka kuingia bado kweupe.
Alifika Lolo lakini hakushuka, kwa kuwa lori lilikuwa alinaelekea Tchenzema, akashukia visomoro ndipo alipoanza taratibu hatua za kurejea kwao, huku fikira zikimuumiza.
Atawakuta namna gani watu wake na watakuwa vipi. Alikumbuka wadogo zake kutoka kwa mama mdogo wake hakujua atawakuta vipi.
Lakini kule nyumbani Baba yake alikuwa amelala akiwa mgonjwa na mama yake alikuwa anahangaika kufanya hiki na kile ili kusawazisha mambo kabla ya kuanza kumhudumia mgonjwa wake.
kama vile mtu aliyekwisha choka mawazo ya mtoto wake wa pekee yalikuwa yakimjia. Alifikiria mtoto wake kwa miaka saba hajawahi kumtia machoni, watu walikuwa wanamdhihaki na ndugu wa mume walikuwa wameacha kumsaidia ndugu yao zamani kabisa na juhudi kubwa ilibaki kwake yeye ambaye ndiye mke.
Kazi za shamba, kazi za kilimo, kazi za kutunza mifugo hazikuwa na msaidizi kwani hata wale walio wadogo wanaonekana kama wameambiwa wasifike pale, alikuwa anaonekana mchawi anamloga mume wake.
Mama Mwenda hakuwa na muda wa kumsaida mume wake kwa kipindi kile cha jioni ilikuwa lazima akimbizane na kutwanga kwanza kabla hajampatia chakula mgonjwa wake ambaye hakuonyesha hata dalili za kupona katika ugonjwa wake.

Siku ile alimaliza kutwanga mapema akampikia mumewe na baada ya kumkanda kwa maji ya uvuguvugu alimnyanyua na kumsaidia kumlisha. Alipoona mgonjwa wake yupo safi naye akala na kisha kuanza kujiandaa kwa usiku.
Wakati anafunga mlango kwa kuweka michi na kinu alisikia hodi ambayo alidhani kwamba ni kichaa chake.
Hodi ilirejewa tena na tena na mwisho wake akaamua kuchungulia hakuamini aliyemuona pale ndani na badala ya kumfungulia mlango akakimbilia kwa mume wake.
"Baba Mwenda, mwenda amerudi" alisema huku akiwa anashangilia.
"Yupo wapi?" aliuliza mzee kwa sauti ya taabu.
"Yupo nje"
"Sasa si kiza kimeingia unawezaje kumwacha nje"
"Ohh Mungu ashukuriwe" alikimbilia nje na kuanza kutoa vifaa alivyoweka mlangoni, akafungua mlango na kumkumbatia mwanawe kwa muda mrefu sana kabla ya kumsalimia na kumtazmaa kila mahali katika mwili wake.
"Mhh mama hujaacha tu kunikagua kote huko?"
"Mwanangu sijakuona muda gani?"
"Si hivi nipo mama." alisema akitabasamu alikuwa anamjua mama yake huwa anamkagua hata akitoka shule.Alikuwa na kawaida hiyo kiasi ya kwamba alikuwa wakati mwingine anamuona mama yake kuwa kero.
" Wooh umekuwa na rangi gani sasa manake bluu si bluu , weusi si weusi rangi gani hii" alisema huku akimpokea begi kubwa mgongoni na kwenda kuiweka katika chanja ambayo ilitengenezwa vyema kwa ajili ya kuwekea
mizigo.
Aliitazama nyumba yao, nyumba iliyomlea. Alitaka kuibadili kama watu wengine walivyobadili nyumba za wazazi wao. Alikuwa ameona nyumba nyingi zikiwa zimejengwa pau na wala si misonge kama ya kwao ingawa ilijengwa vyema.
Ilikuwa nyumba ambayo ina chumba tatu, chumba cha ndani ambacho ni jiko ambako kila mara alikuwa akihimizwa kulala humo kutokana na joto lake, chumba cha wazazi wake ambacho kilikuwa karibu na zizi la kuku na mbuzi na kondooo na kingine ambacho kilikuwa na mwanga na safi kwa ajili ya wageni.

Alikumbuka kitanda chake cha teremka tukaze ambacho baba yake alikuwa amemnunulia godoro la sufu baada ya kupata nafasi ya kwenda shule ya sekondari ya Kilakala kutoka Bumu.Ilikuwa taabu kidogo kukumbuka kama mto wake ulikuwa upo au la.
"Mhh nambie hali ya baba mama" alisema huku akiwa amekaa katika kiti cha fito kilichokuwa katika sebule ya nyumba yao hiyo ya msonge.Alikuwa ni miongoni mwa watoto ambao hawakuwa wanadeka, alikuwa amechangamka na mama yake lakini kitendo cha kutomuona baba yake pale akitoka kumuona kilimpa shida kidogo, alitarajia habari mbaya manake miaka saba si sawasawa.
"Baba yako yupo ndani hali yetu si sawasawa mwanangu" alisema kwa huzuni kisha akaanza kumweleza taabu ilianza kukohoa na ilipofika kukohoa damu wote waliwakimbia.
"Unaponiona hapa sina la kufanya, hatuna hela, hatuna dawa nimekuwa nikihangaika na mibaazi mpaka sasa tupo tu. baba zako wamenikimbia mimi sasa ndiye muuguzaji." alisema huku anadondosha machozi.
Mwenda aliamka na kwenda kumkumbatia mama yake na kisha akaongoza mahali ambapo alijua lazima baba yake yupo, chumba cha kati ambacho huwashwa moto.Kweli alimkuta baba yake.
Hali ya baba yake ilimtisha.
Alimsalimia na kumuitikia kwa taabu kubwa.
Haikuwa rahisi kuelewa kama anamsikia vyema baba yake au la. Akakimbilia kumbariki kisha akatulia sana.
"Mama ilianza lini?"
"Tunamwaka mmoja" alitulia.
Alimwangalia akatazama mapigo yake kisha akatoka na kukimbilia begi lake.
Ilikuwa taabu kubwa katika moyo wake, alijua baba yake ana kifua kikuu na huenda naye mama yake ana kifua kikuu pia.
Alienda kuchukua vidonge vya kutuliza maumivu na saplimenti za vitamini.
"Mama baba anakula?" alimuuliza mama yake wakati anaingia tena katika chumba kile.
"Bado anaweza kula japo kwa taabu."
"Basi mpe dawa hizi na kikopo hiki akikohoa tia mate yake." alisema.
"Yanini mama?" aliisikia sauti yake dhaifu.
"Kesho asubuhi asubuhi nataka kwenda kituo cha Afya Mgeta nijue nini."
"Mtaalamu amesema wamemroga kwa sababu wewe upo Ulaya" alisema mama mtu
"Inawezekana mama lakini pia inawezekana baba ana kifua kikuu ndio maana ukimpa mibaazi inatulia"
"Haya mama" alisema mama yake na kisha akachukua vidonge vile na kuhangaika kumpa mgonjwa na baada ya kumaliza kumpa alikohoa lakini hakutoa damu badaaye alipokohoa alitwaa makohozi na kuona yanadamu na kohosi la kawaida.
Bila hata kujiuliza swali mwenda alitambua kwamba nafasi ya baba yake kupona ni hamsini hamsini, kifua kikuu kilikuwa kimetafuna sana....

Kwa leo kwaheri tutaonana Jumatatu ijayo kwa mwendelezo

COMMENTS

BLOGGER: 2
Loading...
Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,301,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,23,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Simulizi la Jumatatu..Mimi! Mi mtamu wewe...!
Simulizi la Jumatatu..Mimi! Mi mtamu wewe...!
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2011/03/simulizi-la-jumatatumimi-mi-mtamu-wewe.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2011/03/simulizi-la-jumatatumimi-mi-mtamu-wewe.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy