TAARIFA KWA VYOMBO VY A HABARI 30/01/2014 Mzee malecela akizungumza leo mchana Ndugu zangu waandishi wa habari, awali ya y...
TAARIFA KWA VYOMBO
VY A HABARI 30/01/2014
Ndugu zangu
waandishi wa habari, awali ya yote naomba niwasalimie na niwapongeze kwa
kufika mwaka mpya 2014,pia naomba
niwapongeze kwa kazi kubwa ambayo mmekuwa mkiifanya hasa kuhakikisha watanzania
wanapata habari kwa kila jambo linaloendelea kila kona ya taifa letu la
Tanzania
Ndugu waandishi wa
habari nimewaita hapa ili kuzungumza nanyi na mnisaidie kufikisha ujumbe kwa
watanzania hasa kuhusu jambo hili ambalo limekuwa gumzo kwa watanzania wengi la
mbio za urais 2015 kwa baadhi ya watu ndani ya chama changu cha mapinduzi
(CCM),kilichonisukuma zaidi na kupata hamu ya kuongea nanyi ni baada ya
kumsikia na kumuona kijana wetu ndani ya
chama cha mapinduzi bwana paul makonda akiwa na ujasiri wa kukemea vitendo mambo
haya yanayofanywa na baadhi ya viongozi bila uwoga wowote naomba tuchukue
fursa hii kumpongeza sana kijana huyu.
Nadiriki kusema
nampongeza kijana huyu hasa kwa kauli zake nzito na za kijasiri kwa maslahi ya
chama changu cha CCM ili chama kiendelee kupendwa na kuchaguliwa na watanzania.
Pia itakuwa si
busara kama sitawapongeza vijana wangu katibu mkuu wa chama ndugu ABDULRAHMAN
KINANA na NAPE NNAUYE kwa juhudi zao za dhati za kujenga chama na kuendelea
kuwaeleza wananchi juu ya misingi bora ya chama cha mapinduzi (CCM)kwa
kuwakemea viongozi wasiofaa bila kujali cheo na umaarufu wao ndani ya chama na
serikali,nawaomba waendelee na juhudi
zao hizo nami naziunga mkono juhudi zao na kama kuna watru wanaowabeza naomba
wasijali kwani kukemea viongozi wasiofaa ndani ya chama na serikali ni msingi
wa chama chochote kilichounda serikali.
Aidha nawaomba
watanzania wenzangu wazalendo wasikubali kukatishwa tama na kikundi cha watu
wachache wasio na mapenzi mema na taifa letu ambalo limekuwa mfano wa kuigwa
kwa amani,upendo,utulivu na mshikamano urithi tulioachiwa na baba yetu wa taifa
mwalimu julias kambarage nyerere ndani na nje ya mipaka ya bara letu la afrika.
Ndugu zangu
waandishi wa habari naomba niwaambie kuwa msemaji wa UVCCM kijana wetu paul
makonda namuunga mkono kwa kitendo chake
cha ujasiri cha kumkemea ndugu EDWARD NGOYAI LOWASA bila uwoga kwa jinsi
anavyokivuruga chama chetu kwa lengo la kutaka urais 2015 huku secretariet ya
chama ikiwa imekaa kimya wakati inajua kuwa muda wa kuanza mbio hizi bado na
kufanya hivi kwa sasa ni kukiuka misingi na katiba ya chama.hapa najiuliza kuwa ile misingi
imara ya uongozi ndani ya chama chetu cha mapinduzi iko wapi?mpaka tumuachie
mototo ndio akemee haya?je!hapa chama kiko wapi?
Ukweli ni kwamba
wanachama wetu na vijana wamekuwa njia panda huku wakitamani kusikia tamko au
karipio la chama juu ya suala hili la harakati za urais 2015 bila mafanikio.
Naomba niseme kuwa
bila kuwa na karipio au tamko la chama, hawa wanaotumia pesa zao hadharani kwa
lengo la kutafuta umaarufu na ushawishi kwa vijana ili kupata madaraka
wanaharibu misingi yetu bora ya uongozi iliyowekwa na waasisi wetu ndani ya
chama.
Kinachonisikitisha
zaidi ni kuona juhudu za uongozi wa sasa wa chama ngazi ya juu ikiwa ni pamoja
na sekretarieti inayoongozwa na katibu mkuu ABDULRAHMANI KINANA na katibu
mwenezi NAPE NNAUYE za kutetea chama hiki zinatiwa mchanga.
Ninaomba juhudi
hizi zisibezwe na watu wenye nia njema na chama.,ukweli ni kwamba vijana hawa
wamekuwa na juhudi kubwa sana ya kujenga na kuimarisha chama chetu kwa wananchi kila pembe ya taifa letu kwa
kukemea na kueleza misingi ya uongozi bora. swali:je! Chama hakioni haya mpaka
vijana ndio waone?
Kwa hili ni lazima
tubadilike ili kujenga chama chetu na naishauri
secretariet ya chama lazima ichukue hatua mara moja,kijana huyu paul
makonda asingesema haya yote kama hana uhakika wa ushahidi wa wa haya
aliyoyasema na nampongeza sana.
Vijana na
wanachama wengi wa CCM wamekuwa na hamu kwa muda mrefu ya kutaka kujua msimamo
wa chama chao bila mafanikio na ndio sababu ya baadhi ya
wengine kupoteza mwelekeo.
Sisi tulikijenga
chama hiki kwa taabu sana hapakuwa hata mtu mmoja aliyediriki kutumia fedha
zake kutaka madaraka.nidhamu,busara na uchungu wa rasilimali za taifa hili kwa
maslahi ya wananchi ndio vilituongoza kufuata misingi na maadili ya uongozi
ndani ya chama na serikali,ndio maana tunaumia sana kuona chama sasa kinataka
kutekwa na wenye fedha kwa uchu wa madaraka,mpaka tunashangaa na kujiuliza hizi
pesa wanatoa wapi?na haya madaraka wanayotaka kwa kununua ni kwa maslahi ya
nani?huku watanzania wakiendelea kuwa maskini.
Mfano hivi
karibuni baadhi ya viongozi wa chama ngazi ya juu wamejibishana kwenye vyombo
vya habari,vitendo hivi havina tija kwa chama na wala havileti umoja na
mshikamano ambao umedumu ndani chama kwa muda mrefu.
Mwisho Ninaomba
sekretarieti ichukue hatua haraka kama alivyoomba kijana wetu makonda na kweli
kuchelewa kuchukua hatua jambo hili kumejionyesha wazi kwamba utaleta
kutokuelewana ndani ya chama kusiko kuwa na lazima.
MWISHO
JOHN SAMWELI
MALECELA
KIDUMU CHAMA CHA
MAPINDUZI
COMMENTS