Muziki unavyomuita nyoka akutambae

Msanii  Helen John akicheza na nyoka HAKUNA simulizi linalogusa nyoka katika jamii lilililojema. Na kawaida nyoka akionekana hutafu...


Msanii  Helen John akicheza na nyoka
HAKUNA simulizi linalogusa nyoka katika jamii lilililojema. Na kawaida nyoka akionekana hutafutiwa fimbo na kuuawa papo hapo.Katika simulizi zote nyoka ni adui mkubwa wa binadamu na panapokuwapo na urafiki wa binadamu na nyoka, hofu na hisi mbaya hutawala.
Kulingana na hofu iliyotawala ndani ya simulizi za kitamaduni za makabila mbalimbali  hapa nchini, watu wanapokutana na nyoka wanaona wamekutana na mkosi na balaa kubwa na wakati mwingine hudhani kuwa ni uchuro.
Kwa wanasayansi nyoka ni kiumbe mwenye damu baridi atambaaye na hupatikana  sehemu mbalimbali duniani ambapo katika bara la Afrika kuna aina 450 za nyoka na wengi ni wale wenye sumu ya wastani na wengine kali zenye uwezo wa kuua sawia.
Pamoja na nyoka kutambulika kuwa ni viumbe hatari kutokana na sumu walizonazo ingawa wapo ambao hawana sumu, nyoka ni sehemu ya utunzaji wa ikolojia na adui mkubwa wa panya.
Ingawa simulizi katika jamii nyingi kuhusu nyoka ni zile za kutisha zipo jamii mbalimbali duniani ambazo hutumia nyoka kama chakula na wengine huwatumia kama sehemu ya ngoma za asili.
Ndio kusema kwa watu wengine nyoka wamekuwa ni sehemu ya maisha.
Nje kidogo ya Manispaa ya Dodoma kwenye njia ya kuelekea Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kuna Kata ya Dodoma inayojulikana kama Makulu.
Eneo hili ndilo ambalo linalobeba historia nzito ya Mji wa Dodoma kutokana na kuwa makazi ya Machifu kwa miaka ya nyuma japo wajukuu wa machifu hao wengine wapo mpaka leo.
Eneo hili ndipo anapoishio Mzee Lazaro Masuma Chihoma (63), Miongoni mwa wazee wanaojua vyema nyoka, maisha yake,shida zake na hata umuhimu wake kwa jamii.
Pamoja na kuwa mtu anayefahamu nyoka vizuri yeye pia ni mganga wa tiba za asili mwenye tabia ya kula nyoka tena bila hata ya kupika.
Pia mzee huyu ambaye hujihusisha na masuala ya uganga wa tiba za asili na kufanya matambiko toka mwaka 1969 baada ya kuoteshwa na mizimu ingawa alianza rasmi kazi za uganga 1974,anawafahamu nyoka kwa kiasi cha kusisimua.
Kulingana na maelezo yake, alianza kuongozana na mizimu kwenda kuonyeshwa dawa tangu akisoma shule ya msingi Ihumwa . Ingawa anatibu magonjwa yote ya binadamu , mwaka 1976 alianza kupewa elimu na mizimu ya kukamata nyoka na kukaa nao na dawa za sumu zote za nyoka.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Chihoma amekuwa akiishi na baadhi ya nyoka kwenye ofisi yake iliyopo eneo la Dodoma Makulu na pindi anapowahitaji kwa shughuli zake huwaita.
Miongoni mwa nyoka ambao anakaa nao na wengine wako kwenye Mlima wa Bwibwi na wengine huwafahamu kwa majina  ya kabila la Kigogo ni swila, koboko, swaga, moma, nyamhando, nzokalu, gwagu, sansavumea (chatu), hato na Fira (kobra).
“Wakati wowote ukitaka kuwaona nakuletea kwani nina uwezo wa kwenda kuwaita na kuwabeba na kuja nao nyumbani.Hapa nyumbani ninaishi na aina saba za nyoka akiwemo kobra, swaga koboko, nyamhando, mlalu, moma ambao  nimewachimbia mashimo na wale nyoka wakubwa wanakaa kwenye mapango ya milima ya Bwibwi na huwezi kuwaleta hapa
nyumbani itakuwa ni fujo” anasema.
Moja ya vitu ambavyo vinaonesha utaalamu wa mzee huyu katika kuwa rafiki na nyoka ni namna anavyowaita nyoka hao.
Anasema nyoka wana muziki ambayo hupenda kuisikiliza na wanapopigiwa muziki hiyo hata awe kwenye shimo la urefu kiasi gani hutoka na kwenda kwa anayepiga muziki huo na kama akigundua kuwa mtu huo ni rafiki basi huanza kumtambaa mwilini taratibu.Raha hiyo ya muziki anayoisikia nyoka hupelekea kuwa rafiki wa binadamu kwa kufurahi na kwa kucheza pamoja.
Pamoja na kutumia muziki kuwaita pia huwa anatumia mizizi ambayo hufanya nyoka wamzoee na hata anapowaita huja bila kuwa na wasiwasi.
“Mimi napiga vifaa vya utamaduni kama malimba, zeze, ndonondo, sinjila na ipango hivi ni vifaa vinasababisha hadi nyoka  akusogelee ili muwe pamoja hata unapoenda porini unatafuta kichaka kizuri unaanza kupiga na nyoka wengine wanaanza  kuja pembezoni mwako na wakikuona una wasiwasi wanaanza kutambaa na wakikuta hushtuki wanajua kuwa ni rafiki yao” anasema.
Pia anasema kuna nyimbo ambazo unatakiwa kuimba wakati wa kupiga vifaa hivyo nyimbo ambazo zinaendana na mizimu ili nyoka  wakikusogelea na hata akija mgonjwa kagongwa na nyoka lazima uzitumie nyimbo hizo wakati unamtibu.
 “Nyoka ni muhimu sana kaika kazi zangu na pia hunipatia nyama kama unavyoona ninaikausha na ninakuwa nakula taratibu mpaka itakapoisha” anasema.
Pamoja na kuelezea mlo wake wa nyoka, mzee huyu ana mashaka makubwa na maendeleo yanayofanyika kwamba yatafuta kizazi cha nyoka na kuleta mkosi.
Katika moja ya utafiti uliowahi kufanyika mkoani Dodoma, eneo la Chuo Kikuu cha Dodoma(UDOM)  imeelezwa kuwa kuna aina 16 za nyoka walio katika familia saba.
Tanzania ambayo inajulikana kimataifa kama sehemu ya hifadhi ya bayoanui katika bara la Afrika kwa Dodoma suala la ujenzi bila kuzingatia masuala ya asili na umuhimu wake kunatishia kuondoa nyoka katika sehemu pia.
Ipoa haja ya kuhakikisha kwamba nyoka wanahifadhiwa kwa kuwa ndio wanaotunza mfumo wa ekolojia na kukosekana kwao kutaleta shida kama mzee huyu anavyosema.
Kuna mradi wa ujenzi unaotarajiwa kufanyika eneo la Ndejengwa ambalo ndilo hukaliwa na nyoka hao ambao wengi ni wa matambiko.Pamoja na hofu yake anaamini kwamba  nyoka hawatakimbia bali wataishi katika nyumba hizo kwa maana wameingiliwa kwenye mji wao.
“Wameingia kwa fujo kuanza ujenzi eneo hili walitakiwa kuonana na wenyeji wa milima hii tunaishi kwa kimila pale kuna matambiko” alisema
Alisema kuwa nyoka hao wamekuwa wakitumika kwa kazi za matambiko na nyoka wa namna hiyo hawaondoki kirahisi.
Anasema nyoka ingawa anatumika kama dawa  kuna wakati hutumika kama chakula kama anavyofanya yeye na huliwa akiwa mbichi bila hata ya kupikwa huku wengine wakichomwa na unga wake kulambwa na kuwa tiba ya sumu mbalimbali zinazoingia mwilini.
Chakula cha nyoka kinatajwa kuwa ni unga na panya na kama unga ukikosekana hata majivu hutumika.
Chihoma anasema nyoka mdogo anapomeza panya wawili huweza kukaa hata miezi miwili hadi mitatu na hapo huwa anakwenda haja ndogo tu hadi panya aliyemmeza aoze na hatimaye kupata haja kubwa.
Pia nyoka ni moja ya wanyama wanaotajwa kuwa hawasumbuki katika suala la njaa kwani anapomeza panya unyevunyevu wa kuoza kwa panya ule humfanya hata asisikie kiu ya maji kwani akila mara moja tu anapumzika kwani atakaa muda mrefu bila kutafuta chakula.
Kitendo cha kuwaua nyoka kila wanapokutana nao kwa sababu mbalimbali  wananchi wanaondoa ekolojia katika hali yake huku nyoka wakiendelea kupungua.
Nyoka wanasaidia sana kudhibiti panya ambao ni wadudu waharibifu wa mahindi na kama wakiendelea kuwapo ni dhahiri panya hawawezi kuwapo.
Akizungumzia dawa ya nyoka alisema:“Nyoka wadogo ukishawachoma na kugeuka majivu unachangana na dawa ya mti unaoitwa mpande na mti wa mwaliganza na ngwenyangale hizo dawa ukizichanganya na nyoka na tayari unaondoa simu ya nyoka katika mwili wa binadamu, unachanja,
unachua na nyingine unampa kwenye maji anakunywa.”
Pia anasema kuwa, mtu anapogongwa na nyoka anapocheleweshwa na sumu kuanza kusambaa lazima umchanje na kuvuta sumu kwa kutumia pembe kubwa ya mbuzi au pembe ya ng’ombe iliyochongwa na kuwa ndogo ambayo huwa maalum kwa ajili ya kunyonya sumu ya nyoka.
“Ukishanyonya sumu na kutoka unampa mgonjwa dawa na hapo anakuwa amepona,” anasema Chihoma.

Source: Sifa Lubasi,Habarileo





COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,372,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,270,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,2,Habari,5866,habari dodoma,38,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,23,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,6,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,619,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,369,muziki na fasheni,18,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,5,SAYANSI ANGA,7,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,15,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Muziki unavyomuita nyoka akutambae
Muziki unavyomuita nyoka akutambae
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiO1jluTzJ0FASINQx0unRIWNwN2am6pLcllCjNV7ZfR82CmeQpProIHXAPNlHZg6ObA6h5sn8H-x5AJcVhcd4yEpHVKoIiM6i8ydEN3lVWQaChsyvbk91ncC5VCRm8LF5kYe46wYL1R2Q/s320/nyoka.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiO1jluTzJ0FASINQx0unRIWNwN2am6pLcllCjNV7ZfR82CmeQpProIHXAPNlHZg6ObA6h5sn8H-x5AJcVhcd4yEpHVKoIiM6i8ydEN3lVWQaChsyvbk91ncC5VCRm8LF5kYe46wYL1R2Q/s72-c/nyoka.jpg
Lukwangule Entertainment
https://lukwangule.blogspot.com/2015/12/muziki-unavyomuita-nyoka-akutambae.html
https://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2015/12/muziki-unavyomuita-nyoka-akutambae.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy