Na Mwandishi wetu Mpango mkakati wa AGRA wenye kaulimbiu ya kuchochea masoko jumuishi na yenye ushindani katika kilimo ili kuleta mabadili...
Na Mwandishi wetu
Mpango mkakati wa AGRA wenye kaulimbiu ya kuchochea masoko jumuishi na
yenye ushindani katika kilimo ili kuleta mabadiliko kwenye mifumo ya chakula
nchini Tanzania umezinduliwa mjini Dodoma leo Jumatano.
Uzinduzi huo umefanywa Waziri wa
Mifugo na Uvuvi Abdallah Hamis Ulega ambaye alkipongeza AGRA kwa kuja na mkakati huo wenye kugusa maeneo man
manne muhimu.
Katika uzinduzi huo alikuwepo pia Waziri Mkuu Mstaafu na Mwenyekiti wa
Baraza la Rais la chakula na kilimo, Mizengo Pinda.
Katika salmu zake kwenye uzinduzi huo Waziri wa Kilimo, Hussein Mohamed
Bashe, akiwakilishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Geofrey Mweli
alisema serikali imeweka kipaumbele katika sekta ya kilimo ili kutengeneza
maisha zaidi huku ikihakikisha kuwa vijana na wanawake wanajumuishwa.
“Tanzania inalenga kuwa ghala la chakula kwa Afrika na dunia nzima.
Tumejitolea kufungua uwezo wa sekta ya kilimo, ambayo kwa sasa inachangia
asilimia 25 ya Pato la Taifa na ni chanzo kikuu cha fedha za kigeni na chanzo
cha ajira na utajiri.”
Alisema pamoja na mabadiliko ya teknolojia pia rais sanmia suluhu Hassan
ametoa kibali cha kuajiri maofsia ugani wa kutosha na vifaa kusaidia kuleta
mapinduzi
Pinda akizungumza alisema pamoja na kutambua mafanikio makubwa ambayo
Tanzania imefikia bado kuna kazi kubwa ya kukabili umaskini mkubwa uliopo
vijijini.
Ametaka sekta zote na wizara husika kuendeleza juhudi za kupambana na
umaskini wa kipato na kuipa mifumo ya chakula
"Tuna ardhi, tuna kila kitu
kinachohitajika. Tunachohitaji kufanya ni kuweka kipaumbele katika maendeleo na
uboreshaji wa mifumo ya chakula ili kujenga maisha endelevu na kuinua jamii za
vijijini."
Pinda :.. Tumefanya vizuri katika maeneo mengi na kubwa ni utulivu wa
nchi yetu...mfumo wetu wa chakula haujapewa nafasi ya kutosha..kufungua uelewa
zaidi juu ya hali ya nchi na umuhimu wa kuongeza kasi ya kutumia ardhi yetu
ipasavyo na ndani ya rdhi yetu ipasavyo na ndani ya kipindi kifupi."
alisema Pinda.
Alisema kuna umuhimu wa Nidhamu ya kazi na kujikita katika teknolojia za
kileo kama walivyo Israel ambao hawana mito lakini wana kilimo cha umwagiliaji
chenye tija.
Mkakati huo umelenga kuwajengea uwezo vijana na wanawake wa Kitanzania katika mnyororo wa thamani wa kilimo na hivyo kukuza ajira ukuaji wa ustawi wa jamii na uchumi.
Mkakati huo unajumuisha uboreshaji wa upatikanaji wa fedha na masoko, na
kukuza utumiaji wa teknolojia mahiri za hali ya hewa na matumizi ya pembejeo,
kama vile mbegu na mbolea.
Mkakati huo umelenga kuwa na jukwaa thabiti la kushirikisha maarifa na
ubunifu na kukuza mijadala yenye maarifa kuhusu changamoto katika kilimo na
biashara na kuboresha ufikiaji wa afua muhimu za kifedha kwa lengo la kuwezesha
matumizi makubwa ya teknolojia na sayansi katika kilimo.
Mkakati huo unatarajiwa kunufaisha wakulima milioni
tatu nchini kwa kuwapatia masoko ya mazao yao.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana katikauzinduzi
huo Mkakati huo umeganyiwanyika katika maeneo tofauti Kijiografia ikiwamo
Nyanda za Juu Magharibi, Kanda ya Kati, Nyanda za Juu Kusini, Nyanda za Juu
Kaskazini na Zanzibar.
Aidha imeelezwa kuwa mazao yaliyopewa kipaumbele ni
pamoja na mahindi, mtama, maharagwe, mihogo, alizeti, soya, ngano, viazi na
mazao ya bustani.
Akizungumza wakati wa hafla ya kuzindua mkakati huo,
Mkuu wa Kikanda wa AGRA, Afrika Mashariki, Profesa Jean Jacques M. Muhinda alisema taasisi yake katika miaka hiyo
mitano imelenga kuunga mkono juhudi za serikali ya Tanzania kuwa na uzalishaji
mkubwa wa chakula.
“Tanzania imeonyesha umahiri katika kubadilisha
mifumo yake ya kilimo cha chakula. Katika kipindi cha miaka mitano ijayo,
tunanuia kusaidia kufungua fursa zaidi za kilimo na masoko wakati nchi
inapoendelea kufanya mabadiliko chanya kwenye kilimo. Tumejitolea kuunga mkono
vipaumbele vya serikali kwa sekta ya kilimo
ambayo imekuwa ikijijenga kwa miaka mingi.”
AGRA ambayo iliingia Tanzania mwaka 2006 imekuwa
ikifanya kazi na serikali na mashirika binafsi na yale ambayo si ya kiserikali
katika kuvutia uwekezaji, kusaidia mageuzi ya sera na kutoa zana za kilimo,
maarifa na msaada kwa wakulima.
Aidha AGRA imeshirikiana na sekta binafsi kupitia
Tanzania Agro-Industrialization Development Flagship,TAIDF, katika kuhakikisha
kilimo kinakua na kinachangia katika pato la Taifa.
TAIDF ni mradi mkubwa wa kuwezesha maendeleo ya
viwanda vya kilimo kwa kuhamasisha na kuratibu ubia kati ya sekta ya umma na
sekta binafsi; katika mradi huu ufadhili wa Dola za Marekani milioni 300 zilipatikana na kunufaisha wakulima zaidi ya
milioni moja.
Serikali pia ilitoa vivutio mbalimbali vya kodi ili
kuvutia uwekezaji kutoka sekta binafsi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Geofrey
Mweli alisema Tanzania imelenga kuwa ghala la chakula kwa nchi za Afrika na
duniani kote na hivyo haina budi kufungua uwezo wa sekta ya kilimo.
“Tanzania inalenga kuwa ghala la chakula kwa Afrika
na dunia nzima. Tumejitolea kufungua uwezo wa sekta ya kilimo, ambayo kwa sasa
inachangia asilimia 25 ya Pato la Taifa na ni chanzo kikubwa cha fedha za
kigeni na chanzo cha ajira na utajiri." alisema Mweli.
Mwei alisema kwamba serikali ya awamu ya sita
imeweka kipaumbele sekta ya kilimo ili kukiwezesha kupaa huku ikisaidia kupata
ajira wanawake na vijana.
Uzinduzi wa mkakati huo mpya wa AGRA unafanyika
wakati Tanzania ikijiandaa kuwa mwenyeji wa Kongamano la Mifumo ya Chakula
Afrika 2023 (AGRF) litakaloanza Septemba 4
na kumalizika Septemba 8 mkoani Dar es salaam.
AGRF ni jukwaa kuu la Afrika lenye lengo la
kuendeleza ajenda ya kilimo na mifumo ya chakula.
Mkutano huo utaleta pamoja makundi mbalimbali
ikiwamo viongozi, watunga sera, wanasayansi, wakuu wa serikali, taasisi za
kibinafsi, wakulima na vijana: ambao watakubaliana juu ya hatua za kivitendo
ili kupata suluhisho kwa mifumo ya chakula barani Afrika.
"Jukwaa la mwaka huu lina umuhimu wa kipekee
katika safari ya bara la Afrika kuelekea usalama wa chakula na ustawi wa
pamoja." alisema
Mada ya mkutano wa 2023,itakuwa Regenerate, Recover, Act: Africa’s solutions
to Food Systems Transformation, inalenga kuhakikisha bara la Afrika linaonesha
umadhubuti wake katika kubadilisha mifumo ya chakula ili kuzalisha chakula cha
kutosha na chenye lishe ndani yake na kuboresha jinsi kinavyozalishwa hasa
ukizingatia mabadiliko ya hali ya hewa.
Afrika kwa sasa ni muagizaji mkuu wa chakula kutoka
nje, na inaonekana uagizaji wa chakula utaendelea kupanda kutoka dola bilioni
43 mwaka 2019 hadi dola bilioni 110 mwaka 2025 kama hatua za makusudi
zisipochukuliwa kukabili hali hiyo.
Kwa mujibu wa tovuti ya AGRA, shirika hilo linafanya
kazi zake kuwiana na Mpango wa Kuendeleza Sekta ya Kilimo nchini (ASDP II),
unaolenga kubadilisha mifumo ya kilimo nchini Tanzania sambamba na kuongeza
tija na kipato kwa wakulima wadogo.
AGRA pia inachochea ushirikishwaji wa sekta binafsi
na uwekezaji katika kilimo kwa kushirikiana na serikali na washirika wa
kimkakati.
Baada ya kujenga msingi thabiti wa teknolojia, ubia
na miundo, AGRA iko tayari kuongeza kilimo chenye jumuishi na chenye ushindani
nchini Tanzania.
Mkakati wake wa 2017-2021 uliunganisha ulilenga
kuchochea na kudumisha Mabadiliko ya Kilimo Jumuishi. Mabadiliko hayo yalilenga
kuongeza mapato na kuboresha usalama wa chakula kwa kaya za wakulima wadogo
milioni 1.5 kwa kuwekeza dola za Marekani milioni 28.
kiasi hicho cha
fedha kimewekezwa ambapo dola
milioni 11.3 zilisambazwa kupitia ruzuku 31 tofauti ambapo wakulima 742,865
walinufaika.
Aidha, Mpango wa Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya
Pili umenufaika na ruzuku kubwa ya dola milioni 1.672. Zaidi ya wakulima 42,000
wamefaidika moja kwa moja na mpango huo, wakiongezewa na wakulima 34,000
walioathiriwa kupitia mipango mingine mbalimbali.
Kutokana na juhudi hizo Mauzo ya mazao chini ya
mipango ya AGRA yalivutia $1.6 milioni.
Wakati AGRA ikizindua mpango mkakati wake mpya,
shirika limedhamiria kuendelea kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuleta
mabadiliko na ukuaji wa sekta ya kilimo nchini Tanzania.
COMMENTS