DK MPANGO AUNGANA NA UMATI WA VATICAN KUMUAGA PAPA FRANCIS
HomeHabari

DK MPANGO AUNGANA NA UMATI WA VATICAN KUMUAGA PAPA FRANCIS

VATICAN CITY, Vatican  MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Dk Phillip Mpango ni miongoni mwa viongozi wa dunia na wananchi we...



VATICAN CITY, Vatican 

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Dk Phillip Mpango ni miongoni mwa viongozi wa dunia na wananchi wengine wapatao 250,000 walijitokeza kwenye Misa ya mazishi na maziko ya Papa Francis mjini Vatican.

Aidha kulingana na makadirio ya Vatican, takriban watu wengine 150,000 walijipanga katika barabara za katikati mwa Roma kushuhudia msafara wa kwanza wa mazishi ya Papa nje ya Vatican katika kipindi cha karne moja. 






Katika homilia Viongozi wa dunia na waumini wa Kikatoliki na wananchi wengine walipata nafasi ya kumfahamu vyema Papa Francis aliyesisitiza kujali kwake watu "waliotengwa zaidi ya waliotengwa" na kuonyesha matakwa yake ya kukumbukwa kama mchungaji mnyenyekevu. 

Ingawa marais na wakuu wa kifalme walihudhuria Misa katika Uwanja wa Mtakatifu Petro, wafungwa na wahamiaji walipokea jeneza la Francis katika makazi yake ya mwisho katika kanisa kuu lililokuwa ng'ambo ya mji Basilika la Maria Maggiore.





Dk. Mpango ambaye alimwakilisha Raais Samia suluhu Hassan katika maziko hayo alisema namna bora ya kumuenzi aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani ni kudumisha amani pamoja na kujali masikini.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa Misa ya Mazishi katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, Vatican alisema Papa Francis alikuwa mnyenyekevu na mtu aliyefanya jitihada kubwa za utafutaji amani maeneo mbalimbali duniani na kuacha alama ikiwemo tukio la kuwabusu miguu viongozi wa Sudan ili waweze kuachana mapigano. 



Makamu wa Rais amesema kati ya nyaraka za mwisho alizosaini hayati Papa Francis ni pamoja na barua aliyomwandikia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kumtakia heri ya siku njema ya Miaka 61 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Katika Misa hiyo ya Mazishi, Makamu wa Rais ameongozana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, Balozi wa Tanzania Vatican Mhe. Balozi Hassan Mwameta pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi. Swahiba Mndeme.


Katika safari yake kutoka Vatican umati uliokuwa umejipanga barabarani ulikuwa na sura tofauti huku wengine wakipiga makofi na kushangilia "Papa Fransisko" wakati gari lililobeba jeneza lake, lisilo la kifahari likipita kuelekea Kanisa Kuu la Mtakatifu Maria Mkuu, umbali wa kilomita 6, toka Vatican.

Wakati kengele zilipolia, wabebaji wa jeneza walipita mbele ya makumi kadhaa ya wahamiaji, wafungwa, na watu wasio na makazi waliokuwa wameshika waridi nyeupe nje ya kanisa kuu. Mara baada ya kuingia ndani, wabebaji wa jeneza walisimama mbele ya picha ya Bikira Maria ambayo Papa Francis aliheshimu sana. Watoto wanne waliweka waridi miguuni mwa madhabahu kabla ya sherehe ya maziko kuanza. Makadinali baadaye walifanya ibada ya maziko.   


"Ninasikitika sana kwamba tumempoteza," alisema Mohammed Abdallah, mhamiaji mwenye umri wa miaka 35 kutoka Sudan, ambaye alikuwa mmoja wa watu waliompokea Papa Francis katika makazi yake ya mwisho. "Papa Francis aliwasaidia watu wengi, wakimbizi kama sisi, na watu wengine wengi duniani."


Hapo awali, Kadinali Giovanni Battista Re alimsifu Papa Francis wakati wa Misa ya Vatican kama Papa wa watu, mchungaji aliyefahamu jinsi ya kuwasiliana na "wadogo kati yetu" kwa mtindo usio rasmi na wa hiari.   

Licha ya msisitizo wa Papa Fransis kwa wasio na nguvu, wenye nguvu walikuwa wengi katika mazishi yake wakiwemo Rais wa Marekani, Donald Trump na Rais wa zamani Joe Biden; Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres na Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer na Prince William na wakuu wa kifalme wa bara la Ulaya wakiongoza zaidi ya ujumbe rasmi 160. 



Rais wa Argentina Javier Milei alikuwa na nafasi ya heshima kutokana na uraia wa Papa Francis, hata kama hao wawili hawakuelewana sana.

Aidha Trump na Zelenskyy walitumia nafasi hiyo kukutana faragha. Picha zilionesha wawili hao wakiwa wamekaa peke yao, wakitazamana na kuinama kwenye viti katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, ambako Papa Francis mara nyingi alihubiri haja ya amani na mwisho wa vita vya Urusi na Ukraine.


Imeelezwa kuwa Makumi ya maelfu ya watu walijitokeza kabla ya alfajiri Vatican na wakati ukuta mweupe wa Mtakatifu Petro ukiangaza rangi ya waridi jua lilipochomoza Jumamosi na umati huo ulikimbilia uwanjani kupata nafasi ya kusikiliza Misa kwa kujinafasi. Skrini kubwa za televisheni ziliwekwa kwenye barabara zinazozunguka kwa wale ambao hawakuweza kukaribia waliweza kuangalia televisheni hizo.

Vyombo vya habari vya Italia viliripoti kuwapo kwa doria kubwa huku helikopta za polisi zikizunguka juu, ikiwa ni sehemu ya operesheni kubwa ya kiusalama ambayo mamlaka za Italia ziliweka. Katika doria hizo za kuchunga usalama pia kuwa na zaidi ya polisi 2,500, wanajeshi 1,500, na melivita ikiwa pwani ya Roma.


"Alikuwa Papa mwenye haiba sana, mwenye utu sana, mwenye fadhili, zaidi ya yote mwenye utu sana," alisema Miguel Vaca, kutoka Peru ambaye alisema alikuwa amelala nje usiku kucha karibu na uwanja kumuaga Papa Francis. "Inasisimua sana kumuaga."   






Uhusiano Maalum na Kanisa Kuu

Francis, Papa wa kwanza wa Amerika ya Kusini na Papa wa kwanza wa Mjezuit, alifariki Jumatatu ya Pasaka akiwa na umri wa miaka 88 baada ya kupata kiharusi wakati akipona nimonia.

Uchaguzi wa kanisa kuu pia ulikuwa na umuhimu wa ishara kutokana na uhusiano wake na shirika la kidini la Jesuit la Fransisko. Mtakatifu Ignatius Loyola, ambaye alianzisha Wajezuiti, alisherehekea Misa yake ya kwanza katika kanisa hili siku ya Krismasi mwaka 1538.




Kanisa kuu hili ni makazi ya Mapapa wengine saba, lakini haya ni mazishi ya kwanza ya Papa nje ya Vatican tangu Papa Leo XIII, ambaye alifariki mwaka 1903 na kuzikwa katika kanisa kuu lingine la Roma mwaka 1924.


Umati Ulisubiri Masaa Kumuaga Papa Francis


Kwa siku tatu wiki hii, zaidi ya watu 250,000 walisimama kwa saa kadhaa kwenye mstari kutoa heshima zao za mwisho wakati mwili wa Papa Francis ulipolazwa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro. Vatican iliweka kanisa kuu wazi usiku kucha ili kuwawezesha kutoa heshima zao za mwishoa, lakini  wakati milango ilipofungwa kwa umma saa 7 jioni siku ya Ijumaa, waombolezaji wengi walikuwa bado.


Alfajiri Jumamosi, walikuwa wamerudi, wengine wakikumbuka maneno aliyosema usiku wa kwanza wa kuchaguliwa kwake na katika upapa wake wote.


"Tuko hapa kumheshimu kwa sababu alisema kila wakati 'msisahau kuniombea,'" alisema Dada Christiana Neenwata kutoka Nigeria. "Kwa hivyo tuko hapa pia kumpa upendo huu aliotupa."



mwisho

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,313,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,248,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,Habari,5055,habari dodoma,27,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,518,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,353,muziki na fasheni,6,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,2,SAYANSI ANGA,2,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,3,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: DK MPANGO AUNGANA NA UMATI WA VATICAN KUMUAGA PAPA FRANCIS
DK MPANGO AUNGANA NA UMATI WA VATICAN KUMUAGA PAPA FRANCIS
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjub9dZ2s6u6SJe7jM53A_dwu114WLIvhF0JntEeouYLre29cU2GYuc-UoWPiJmFqKPtQb3_x7QitdRxfng7FLQKdR1rbEP33hjJlfaqUCPgtzDD3emWhcBdQt7Zu7tM5FNl4KkOapdBYkuRPxZ2mvq-04zCdMYOApJATADMI_YfWvL1vgjekA6L0jBHBq2/s320/3.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjub9dZ2s6u6SJe7jM53A_dwu114WLIvhF0JntEeouYLre29cU2GYuc-UoWPiJmFqKPtQb3_x7QitdRxfng7FLQKdR1rbEP33hjJlfaqUCPgtzDD3emWhcBdQt7Zu7tM5FNl4KkOapdBYkuRPxZ2mvq-04zCdMYOApJATADMI_YfWvL1vgjekA6L0jBHBq2/s72-c/3.jpg
Lukwangule Entertainment
https://lukwangule.blogspot.com/2025/04/dk-mpango-aungana-na-umati-wa-vatican.html
https://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2025/04/dk-mpango-aungana-na-umati-wa-vatican.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy