BEDA MSIMBE REFLECTIONS:HUENDA TUMECHELEWA KUWA MAKINI ZAIDI KWENYE HIFADHI YA MAZINGIRA

  HEBU leo tufanye mjadala wa namna gani majibu hayo ya serikali bungeni yanaweza kuashiria kuwa Tanzania huenda imechelewa kuwa makini zaid...

 



HEBU leo tufanye mjadala wa namna gani majibu hayo ya serikali bungeni yanaweza kuashiria kuwa Tanzania huenda imechelewa kuwa makini zaidi kwenye hifadhi ya mazingira. tutazungumza huku tukizingatia pia hatua zinazochukuliwa sasa.

Majibu ya serikali kupitia Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Khamis Hamza Khamis, bungeni kuhusu Mamlaka ya Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) yanaibua maswali kadhaa ambayo yanaweza kutumika kujadili kama nchi imekuwa makini vya kutosha, au imechelewa, katika eneo hili muhimu.

Hoja Zinazoweza Kuashiria Kuchelewa/Kutokuwa Makini Mapema vya Kutosha ni pamoja na NEMC Kutokuwa Mamlaka Kamili Hadi Sasa.

Taarifa kwamba mchakato wa kulipa NEMC hadhi ya "Mamlaka" (NEMA) bado upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji na ndio umekwishaanza licha ya kuwa ndio utakaoipa nguvu ya kisheria na uwezo wa kimapato wa kusimamia majukumu yake ipasavyo, inaweza kuashiria kuwa nchi imechukua muda mrefu kufikia uamuzi na utekelezaji wa kuimarisha chombo chake kikuu cha usimamizi wa mazingira.

Kama NEMC imekuwa ikikosa nguvu za kisheria na uwezo wa kimapato uliotosha, huenda ndio sababu za majanga mengi yanayoambatana na udhaifu katika utekelezaji wa sera na sheria za mazingira kwa muda sasa.

Naibu Waziri alikiri kuwa NEMC imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali, hususani za kibajeti, zinazoathiri utekelezaji wa majukumu yake kwa ufanisi. Hii inaonyesha kwamba kwa muda mrefu, NEMC ilikuwa haijatengewa au haikuwa na uwezo wa kutosha kifedha kuendesha shughuli zake kikamilifu, jambo ambalo lisababisha udhaifu katika kufanya ukaguzi, kutoa elimu, na kuchukua hatua stahiki dhidi ya wachafuzi.

Hatua za sasa za kufanya mapitio ya kanuni za ada na tozo na kuongeza vyanzo vya mapato zinaashiria kuwa mfumo wa zamani haukuwa mzuri vya kutosha.

Ukiangalia kukwama au kuchelewa kwa utoaji wa vyeti vya Tathmini ya Athari kwa Mazingira (EIA) kutokana na changamoto za mifumo na miradi kukosa vigezo vya kulinda mazingira na afya nako kunaibua swali.

Kama miradi inafikia hatua ya kutaka vyeti vya EIA lakini haina vigezo vya msingi vya kimazingira, inaweza kuashiria kuwa usimamizi au umakini katika hatua za awali za upangaji miradi haukuwa imara, au kwamba kulikuwa na uzembe katika kuhakikisha waendelezaji wanakidhi masharti kabla ya kuendelea. 

Nisingependa kutoa mifano hapa lakini unaweza kuona athari za uchimbaji holela wa dhahabu unavyosababisha kusambaa kwa zebaki katika vyanzo vya maji: Na hata  harufu za kutisha kutoka katika machinjio na makazi ya watu.

Hapa pia unaweza kujua kwanini nafikiri sisi ni dampo la vifaa vya kielektroniki vinavyokaribia kufikia mwisho wake.

Pamoja na hayo changamoto za mifumo zilizoelezwa bungenipia zinaweza kuashiria uwekezaji au uboreshaji mdogo katika miundombinu ya kidijitali ya NEMC hapo awali.

Pamoja na hayo hatua za sasa za kuongeza idadi ya watumishi na kuanzisha Ofisi za Kanda ili kurahisisha huduma na kufikia wadau wengi, inaashiria kuwa kwa kipindi cha nyuma, NEMC ilikuwa na upungufu wa rasilimali watu na kuenea kijiografia, jambo lililofanya iwe vigumu kufanya usimamizi na ukaguzi wa kutosha nchi nzima.

Ukitazama maelezo yote hayo unaona kwamba ukitafiti utaona makubwa zaidi kuhusu uhifadhi wa mazingira hasa katika kipindi hiki ambacho kuna ufungaji wa mitambo ya aina mbalimbali kwa kazi mbalimbali kuanzia uchimbaji wa madini hadi utoaji wa huduma za mafuta.

Serikali ikikiri mapungufu hayo imesema  inachukua hatua kuweka hali sawa.

Ndio kusema licha ya changamoto za hapo awali, majibu ya serikali yanaonyesha kuwa sasa inatambua matatizo na inachukua hatua madhubuti kuyatatua. 

Hakika mchakato wa kuifanya NEMC kuwa Mamlaka, mapitio ya kanuni za fedha, uboreshaji wa mifumo ya ukusanyaji mapato, kuongeza watumishi, na kuanzisha ofisi za kanda ni ishara za umakini mpya na dhamira ya kuimarisha usimamizi wa mazingira.

Pia hatua ya kusimamia kikamilifu utekelezaji wa kanuni mpya za Ada na Tozo za 2024, zinazolenga kuongeza mapato kutoka kwa miradi yenye athari kubwa, inaonyesha hatua ya kimakusudi ya kuhakikisha shughuli zinazochafua zinalipia gharama za usimamizi na uhifadhi.

Kwangu mimi kutokana na majibu haya ya serikali bungeni, nahisi toka matatizo makubwa ambayo huenda mikaa kadha ijayo yatajionesha kutokana na kuwa na Nemc iliyodhoofi ikishindwa kutekeleza wajibu wake.

Na sote tunajua bila kuwa na mamlaka ya kupambana na uchafuzi wa mazingira tutabaki kila mara tukianzisha miradi ya kurejeleza.

Naamini kabisa wakati Tanzania imekuwa ikikabiliwa na changamoto za kimfumo, kibajeti na kiutekelezaji katika usimamizi wa mazingira kwa kipindi cha nyuma, na hivyo kusubiri madhara,jambo ambalo naweza kulitafasiri,tumechelewa kuwa na mfumo kamili na madhubuti wa usimamizi kama unavyohitajika. 

Kukiri kuwapo kwa changamoto hizo na hatua zinazoendelea kuchukuliwa sasa (mfano: mchakato wa Mamlaka bado unaendelea, hatua za sasa za kukabiliana na changamoto za kibajeti, sasa wanaongeza watumishi na ofisi) vinaonyesha kuwa mfumo wa zamani haukuwa na uwezo au rasilimali za kutosha kuilinda tanzania hii dhidi ya walafi na wavuunjaji wa sheria za mazingira.

Hata hivyo, majibu hayo pia yanaonyesha kuwa serikali sasa inatambua mapungufu hayo na imedhamiria kuyafanyia kazi ili kuimarisha NEMC na usimamizi wa mazingira nchini.

Hivyo, badala ya kusema "imechelewa" kwa ukali, tunaweza kusema kuwa majibu haya yanaashiria kuwa kumekuwa na muda mrefu ambao chombo kikuu cha usimamizi wa mazingira hakikuwa na uwezo au muundo (kama Mamlaka kamili) unaotakiwa ili kufanya kazi kwa ufanisi kamili, na sasa ndio jitihada kubwa zinafanyika kuimarisha hali hiyo.


COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,372,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,270,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,2,Habari,5866,habari dodoma,38,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,23,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,6,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,619,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,369,muziki na fasheni,18,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,5,SAYANSI ANGA,7,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,15,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: BEDA MSIMBE REFLECTIONS:HUENDA TUMECHELEWA KUWA MAKINI ZAIDI KWENYE HIFADHI YA MAZINGIRA
BEDA MSIMBE REFLECTIONS:HUENDA TUMECHELEWA KUWA MAKINI ZAIDI KWENYE HIFADHI YA MAZINGIRA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiky-mss7UzGnJi7qY9PdOd-99RZFe2FYfLT2nRXPa0aahx2HerIbpFtUd4100ocYZmVGvaTYe1aXu-QIrB0X-WbIhNeEfhb1bAFR6LYglsv6Pon81_3qhGU96Nlgiaoh8Naa-MVzw-9zFy4xu-7zJiElmpm2CDNHBFhPsbWlIF7SUvC1lK0uosXtdaCA9E/s320/beda%20msimbe%20reflections.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiky-mss7UzGnJi7qY9PdOd-99RZFe2FYfLT2nRXPa0aahx2HerIbpFtUd4100ocYZmVGvaTYe1aXu-QIrB0X-WbIhNeEfhb1bAFR6LYglsv6Pon81_3qhGU96Nlgiaoh8Naa-MVzw-9zFy4xu-7zJiElmpm2CDNHBFhPsbWlIF7SUvC1lK0uosXtdaCA9E/s72-c/beda%20msimbe%20reflections.jpg
Lukwangule Entertainment
https://lukwangule.blogspot.com/2025/05/beda-msimbe-reflectionshuenda.html
https://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2025/05/beda-msimbe-reflectionshuenda.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy