Wito wa Dkt. Biteko kwa Vyombo vya Habari na Usalama Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

  Dar es Salaam, Tanzania Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko,Julai 9,2025 ametoa wito mzito kwa vyombo vya habari ...

 



Dar es Salaam, Tanzania

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko,Julai 9,2025 ametoa wito mzito kwa vyombo vya habari na vyombo vya ulinzi na usalama nchini kuhakikisha wanatoa nafasi ya haki na usawa kwa wagombea wote kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Akisisitiza umuhimu wa kuheshimu maoni tofauti na kulinda mshikamano wa kitaifa, Dkt. Biteko alizungumza jijini Dar es Salaam katika mkutano uliowakutanisha wadau wa sekta ya habari.

Umuhimu wa Umoja katika Kipindi cha Uchaguzi

Dkt. Biteko alisisitiza kuwa uchaguzi ni kipindi nyeti kinachopaswa kuwa na umoja wa kitaifa, akieleza kuwa taarifa nyingi husambaa na kuwa msingi wa maamuzi ya wananchi kuhusu nani wa kumchagua.

"Katika kipindi hiki cha uchaguzi ni kawaida hata watu wa familia moja kutofautiana kimawazo. Mkutano huu ni sehemu ya kuwaleta pamoja wadau ili pamoja na tofauti zetu, tusalie wamoja. Sisi ni Watanzania wenye nia ya kuijenga nchi yetu na kuifanya istawi zaidi," alisema Dkt. Biteko.

Jukumu la Vyombo vya Habari katika Uchaguzi Huru na Haki



Naibu Waziri Mkuu alibainisha mchango mkubwa wa vyombo vya habari katika kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa uwazi, kwa kufuatilia na kuripoti matukio mbalimbali kabla, wakati na baada ya uchaguzi. Alivitaka vyombo hivyo kuwa waaminifu kwa jamii kwa kusambaza taarifa sahihi na za kuaminika.

"Katika zama hizi ambapo nguvu ya mhariri imepungua na taarifa huweza kusambazwa bila kupitia mchakato rasmi wa uhariri, ni muhimu sana kwa wanahabari kutumia weledi wao na kulinda tasnia hii kwa wivu mkubwa. Tukikosa uangalizi, tunaweza kugawanyika kama taifa," alionya Dkt. Biteko.

Alitaja ongezeko kubwa la vyombo vya habari nchini, likiwemo magazeti 375, vituo vya redio 247, vyombo vya habari mtandaoni 355, blogu 72, na vituo vya televisheni 68, akisema haya ni matokeo ya mazingira bora yaliyowekwa na serikali. Vyombo hivi vimeajiri idadi kubwa ya vijana na vinatoa mchango mkubwa katika uchumi wa nchi.

Serikali na Sekta ya Habari: Hatua na Dhamira

Dkt. Biteko alipongeza serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kipaumbele kikubwa kwa sekta ya habari, akitaja hatua za mwanzo alizochukua Rais ikiwemo kufungua baadhi ya vyombo vya habari vilivyokuwa vimefungiwa na kurejesha leseni vilivyonyang’anywa.

Aliongeza kuwa serikali imeanzisha Bodi ya Ithibati kwa Waandishi wa Habari ili kuhakikisha huduma za habari na utangazaji zinazingatia viwango vya weledi na maadili.

"Waandishi wa habari mnapaswa kuwa walinzi wa kweli, wajenzi wa amani na waoneeni wivu taaluma yenu. Katika mazingira haya ya teknolojia na taarifa potofu, mnapaswa kuwa waangalifu sana na kuhakikisha jamii inapata habari sahihi," alisisitiza.

Aidha, aliwataka wanahabari kutumia lugha ya staha, kuepuka uchochezi, na kuripoti kwa usawa bila upendeleo wakati wa kampeni, uchaguzi na hata baada ya uchaguzi.

Habari kama Nyenzo ya Uwazi na Uwajibikaji

Dkt. Biteko alisisitiza kuwa sekta ya habari ni nyenzo muhimu sana katika kukuza uwazi, uwajibikaji na ufuatiliaji wa mwenendo wa uchaguzi. Waandishi wa habari wana jukumu la kuhamasisha makundi yote ya jamii kushiriki katika uchaguzi, ikiwemo wanawake, vijana na watu wanaoishi katika mazingira magumu.

"Mnapaswa kuwa zaidi ya waandishi wa habari. Tambueni kuwa kupitia kazi yenu, taifa la Tanzania linaweza kubaki moja au kugawanyika. Kwa hiyo kuwa walinzi wa amani, wachunguzi wa ukweli, na chombo safi cha jamii kisichochafuliwa na uzushi au chuki," alisisitiza.

Usalama wa Waandishi wa Habari na Ushirikiano na NEC

Kwa upande wa vyombo vya ulinzi na usalama, Dkt. Biteko alieleza kuwa serikali imejipanga kuhakikisha waandishi wa habari wanafanya kazi zao katika mazingira salama, huru na rafiki. Alisisitiza kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kulinda usalama wa wanahabari na mali zao wakati wote wa uchaguzi.

"Tutahakikisha kuwa kila mwanahabari anarudi nyumbani kwake akiwa salama. Tutaendelea kulisimamia hili kwa nguvu zote kupitia vyombo vyetu vya dola," alisema.

Alimaliza kwa kutoa wito kwa waandishi wa habari kuendelea kushirikiana kwa karibu na Tume Huru ya Uchaguzi (NEC) ili kupata taarifa sahihi na kwa wakati, na kuzitaka taasisi za habari kujitathmini mara kwa mara.

Mchango wa Tasnia ya Habari na Uzinduzi wa Mfumo wa Kidigiti



Tasnia ya habari nchini inatajwa kuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi kabla na baada ya uhuru, ambapo uwepo wa baadhi ya vyombo vya habari vya awali kama vile gazeti la Sauti ya TANU na redio Sauti ya Dar es Salaam vilisaidia kutoa mchango mkubwa katika kujenga umoja, utaifa na kuhamasisha ushiriki wa harakati za kudai uhuru.

Kwa mujibu wa utafiti wa Taasisi ya REPOA (Research on Poverty Alleviation) wa mwaka 2022, vyombo vya habari ndiyo chanzo kikuu cha taarifa za kisiasa kwa wananchi, ambapo zaidi ya asilimia 76 hupata taarifa za kisiasa kupitia redio na televisheni. Kutokana na hilo, Dkt. Biteko ameviasa vyombo vya habari kutoa majukwaa ya mijadala ya kisera na kisiasa ambayo huwasaidia wapiga kura kufanya maamuzi sahihi.

Katika mkutano huo, Dkt. Biteko alizindua rasmi Mfumo wa Kidigiti wa TAI – Habari wa kusajili na kutoa ithibati kwa waandishi wa habari, unaosimamiwa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari. Hadi sasa, zaidi ya waandishi 2900 wamesajiliwa kupitia mfumo huu unaotoa Vitambulisho vya Kidigiti (Digital Press Card).

Mawazo ya Wadau Wengine



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi, alisema mkutano huo unalenga kuweka msingi madhubuti wa ushirikiano kati ya Serikali, vyombo vya habari, asasi za kiraia, taasisi za usalama na NEC, ili kulinda amani na kuhimiza usawa wa fursa kwa vyama vyote vya siasa.

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe. Albert Msando, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila, aliahidi kuendelea kushirikiana na vyombo vya habari kupata taarifa sahihi.



Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, alisisitiza umuhimu wa weledi katika sekta ya habari kuelekea uchaguzi mkuu.

 

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,341,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,252,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,1,Habari,5210,habari dodoma,29,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,534,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,353,muziki na fasheni,6,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,5,SAYANSI ANGA,3,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,13,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,3,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Wito wa Dkt. Biteko kwa Vyombo vya Habari na Usalama Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Wito wa Dkt. Biteko kwa Vyombo vya Habari na Usalama Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjWAoJ7PRqLE3MiQbhxIHpu8TWNF2pQRDBAIOUwjbXqrdvCQvreRsu2dZ3cXs9y-wx5fTq10dpEdkHrkWrig3aCXdJnqeFDIMpuHn2XjyfbqImFIP4qzikoiRZvDbarm9aIVgaZSJyztQ9QJZVhWmnRl6w7UjwrOaw3Io8I5nsZJmGYUeI0kFI74kw3Hqmb/s320/biteko.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjWAoJ7PRqLE3MiQbhxIHpu8TWNF2pQRDBAIOUwjbXqrdvCQvreRsu2dZ3cXs9y-wx5fTq10dpEdkHrkWrig3aCXdJnqeFDIMpuHn2XjyfbqImFIP4qzikoiRZvDbarm9aIVgaZSJyztQ9QJZVhWmnRl6w7UjwrOaw3Io8I5nsZJmGYUeI0kFI74kw3Hqmb/s72-c/biteko.jpg
Lukwangule Entertainment
https://lukwangule.blogspot.com/2025/07/wito-wa-dkt-biteko-kwa-vyombo-vya.html
https://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2025/07/wito-wa-dkt-biteko-kwa-vyombo-vya.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy