Kumbukumbu ya Samatta na Stars 2013: Je, Historia Itajirudia Leo Rabat?

TIMU ya Taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’,chini ya uongozi wa nahodha Mbwana Samatta na kiungo mchezeshaji mahiri, Faisal Salum 'Fei Toto...




TIMU ya Taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’,chini ya uongozi wa nahodha Mbwana Samatta na kiungo mchezeshaji mahiri, Faisal Salum 'Fei Toto',  leo kinaenda kuandika historia mpya katika michuano ya AFCON 2025 nchini Morocco kitakaposhuka dimbani kumenyana na miamba wa soka barani Afrika, Morocco, katika mchezo wa hatua ya 16 bora ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025). 

Mtanange huo wa kukata na shoka utapigwa kwenye Uwanja wa Prince Moulay Abdellah mjini Rabat.

Rekodi zinaonesha kuwa timu hizi mbili zimekutana mara nane katika michuano mbalimbali. Katika mikutano hiyo, Morocco imeibuka kidedea mara saba, huku Taifa Stars ikifanikiwa kuifunga Morocco mara moja pekee hapo Machi 24, 2013, siku ambayo Taifa Stars iliandika historia ya kipekee jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2014, Stars iliishangaza Afrika kwa kuichapa Morocco mabao 3-1.

Katika ushindi huo wa kishindo, Thomas Ulimwengu alifungua milango ya mabao kabla ya nahodha wa sasa, Mbwana Samatta, kupigilia msumari wa mwisho kwa mabao mawili (brace) yaliyoamsha hisia za kitaifa. Morocco walipata bao la kufuta machozi kupitia kwa Youssef El Arabi, huku mchezo wa marudiano mwezi Juni mwaka huo ukiisha kwa Morocco kushinda 2-1 mjini Marrakech.

Hata hivyo, jeraha la hivi karibuni zaidi liko kwenye michuano ya CHAN 2024 (iliyochezwa Agosti 22, 2025). Katika hatua ya robo fainali, Morocco waliiondoa Taifa Stars, waliokuwa wenyeji wenza, kwa ushindi mwembamba wa 1-0. Bao la Oussama Lamlioui katika dakika ya 65 lilitosha kuwapeleka Morocco nusu fainali na hatimaye kutwaa ubingwa huo.

Mchezo wa leo wa 16 bora katika AFCON 2025 siyo tu unatafuta nafasi ya robo fainali, bali ni fursa adhimu kwa vijana wa Miguel Gamondi kulipa kisasi cha kuondolewa nyumbani mwaka jana na kurudia maajabu ya mwaka 2013.

Katika hatua ya makundi ya michuano hii, Morocco walimaliza kileleni mwa Kundi A wakiwa na alama saba. Kwa upande wao, Taifa Stars walifuzu kama mmoja wa "washindi watatu bora" (best losers) baada ya kumaliza nafasi ya tatu katika Kundi C wakiwa na alama mbili.

Kuelekea mchezo huo, Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Miguel Gamondi, amebainisha kuwa mchezo huo utakuwa mgumu lakini wamejipanga vizuri kiufundi. Gamondi amesisitiza kuwa mbinu zitatofautiana kulingana na mahitaji ya mchezo.

"Tunajua nini cha kufanya kiufundi. Mliona namna tulivyocheza na Tunisia, itakuwa mechi ngumu ila mpira tunaenda kucheza wachezaji 11 dhidi ya 11. Haijalishi watakuwa na mashabiki wengi kiasi gani," alisema Gamondi.

Katika mchezo huu, Tanzania inatarajiwa kutumia mfumo wa 4-2-3-1 wakati Morocco wakitarajiwa kutumia 4-3-3. Morocco wanapewa nafasi kubwa kutokana na usahihi wao wa pasi, mashuti mengi langoni, na umiliki wa mpira.

Naye Kocha Mkuu wa Morocco, Walid Regragui, ametoa onyo kwa kikosi chake kutoibeza Tanzania. Regragui, ambaye anaifahamu Morocco vizuri kutokana na maisha yake hapo awali akiwa na klabu ya FUS Rabat, amesema Tanzania ina ligi nzuri na wachezaji mahiri wa kimataifa.

"Hakuna timu ndogo kwenye AFCON. Unapoteza mchezo mmoja na unatolewa; hii hatua haina chumba cha makosa kabisa," alisisitiza Regragui.

Historia Mpya kwa Stars

Hii ni mara ya nne kwa Taifa Stars kushiriki michuano ya AFCON tangu kuanzishwa kwake (ikishiriki miaka ya 1980, 2019, 2023, na sasa 2025). Hata hivyo, safari hii imeweka rekodi ya kipekee kwani ni mara ya kwanza kwa Tanzania kufanikiwa kuvuka hatua ya makundi na kuingia hatua ya mtoano yaani kutinga hatua ya 16 bora—mafanikio ambayo ni makubwa zaidi ikizingatiwa kuwa Kocha Ángel Miguel Gamondi alikabidhiwa timu wiki chache tu kabla ya mashindano kuanza.

Licha ya muda mfupi, Gamondi ameweza kupandikiza mbegu ya kujiamini, nidhamu, na mfumo thabiti kikosini.

"Kufuzu huku ni somo kubwa kwa Tanzania. Taifa lazima lijivunie," alisema Gamondi. "Nilitaka kubadilisha ile dhana ya kuonekana timu dhaifu (underdogs)... hatushiriki tena kwa ajili ya kutafuta 'heshima' pekee; tunaamini katika uwezo wetu wa kufika mbali."

Ligi ya Ndani Inavyobeba Timu ya Taifa

Tanzania imeingia AFCON ikiwa na hali ya kujiamini iliyojengwa kwa miaka mingi kupitia ukuaji wa ligi ya ndani. Klabu kama Simba SC, Young Africans (Yanga SC), na Azam FC zimewajengea wachezaji uzoefu wa michuano ya kimataifa ya CAF, jambo lililowapa ujasiri wa kuhimili presha katika mechi kubwa.

Matokeo uwanjani yanajieleza: Tanzania imefunga bao katika kila mechi ya hatua ya makundi. Faisal Salum alitikisa nyavu, huku Novatus Dismas—mchezaji anayekipiga nchini Uturuki na zao la Azam FC—akitoa pasi mbili za mabao (assists), akionyesha akili kubwa ya kushambulia akitokea safu ya ulinzi.

Katika hatua ya makundi, Tanzania iliihenyesha Nigeria (bingwa mara tatu) kabla ya kufungwa 2-1, wakaibana Tunisia (bingwa wa 2004) na kutoka sare, kisha wakagawana alama na Uganda. Matokeo haya ni dhihirisho kuwa Tanzania sasa inaweza kupambana na mataifa makubwa ya soka barani Afrika.

Umoja na Nguvu ya Kisaikolojia

Taifa Stars inadhihirisha alama ya "Pamoja" ya AFCON, ikionyesha umoja mkubwa ndani na nje ya uwanja. Miaka ya Gamondi aliyoishi Morocco imemsaidia kujua namna ya kukabiliana na presha ya wenyeji:

"Niliishi hapa kwa miaka mingi na najua presha inayotengenezwa na mashabiki wao, lakini wakati mwingine presha hiyo inaweza kuwaathiri wao wenyewe (Morocco)."

Chini ya uongozi wake, timu imeunganisha nidhamu ya mbinu na ari ya kutoogopa mpinzani—hali ambayo imeibadilisha Tanzania kutoka kuwa washiriki wa kawaida hadi kuwa washindani wa kweli.

Wachezaji Nguzo Wanaoongoza Mapambano

Nahodha Ally Samatta amekuwa muhimili wa timu, akiongoza kwa mfano na utulivu katika nyakati ngumu. Faisal Salum anatoa ubunifu na uwezo wa kumalizia mashambulizi, huku Novatus Dismas akiongeza nguvu kwenye mashambulizi kutokea nyuma. Kwa ujumla, timu imeonyesha uwiano mzuri na uwezo wa kutengeneza nafasi katika kila mchezo.

Mtihani wa Kihistoria Mbele

Sasa, Tanzania inajiandaa kuvaana na wenyeji Morocco katika hatua ya 16 bora—mpinzani mgumu mwenye msaada wa mashabiki wa nyumbani. Hata hivyo, Taifa Stars wanaingia uwanjani bila hofu, wakiwa wameimarishwa na matokeo yao ya hivi karibuni na imani ya pamoja.

Kuinuka kwa soka la Tanzania ni uthibitisho kuwa uwekezaji kwenye ligi ya ndani, uongozi madhubuti, na mentality ya kutoogopa vinaweza kuifikisha timu kwenye mafanikio ya kihistoria. Hawatafuti tena kuheshimiwa—wanajipatia heshima hiyo wenyewe, kwa pamoja.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,379,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,271,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,2,Habari,6022,habari dodoma,38,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,23,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,6,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,636,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,370,muziki na fasheni,18,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,5,SAYANSI ANGA,7,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,16,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Kumbukumbu ya Samatta na Stars 2013: Je, Historia Itajirudia Leo Rabat?
Kumbukumbu ya Samatta na Stars 2013: Je, Historia Itajirudia Leo Rabat?
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjbdTLm3big7BDZn7V-H_tVxJdHJPF0EqALF79Wezr4KvIjf9-Gc97DW5N1N_5lFXdPkSFASZaBCExrXNByQJZZAuwdBh9cQESM65FltBZG_avK8dehFpMV7mfQCcCP3ozre7RuR9FBCXKDRNB8XwaOfdD4Bdut0P-jlnA2yuCcnjdwG4P34dzMjYPnpZdy/s320/tanzania%20mbili.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjbdTLm3big7BDZn7V-H_tVxJdHJPF0EqALF79Wezr4KvIjf9-Gc97DW5N1N_5lFXdPkSFASZaBCExrXNByQJZZAuwdBh9cQESM65FltBZG_avK8dehFpMV7mfQCcCP3ozre7RuR9FBCXKDRNB8XwaOfdD4Bdut0P-jlnA2yuCcnjdwG4P34dzMjYPnpZdy/s72-c/tanzania%20mbili.jpg
Lukwangule Entertainment
https://lukwangule.blogspot.com/2026/01/kumbukumbu-ya-samatta-na-stars-2013-je.html
https://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2026/01/kumbukumbu-ya-samatta-na-stars-2013-je.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy