ZIFF mwaka wa 11 Watanzania mchecheto

TAMASHA la Nchi za Jahazi ambalo linahusisha nchi za Afrika, mataifa yaliyo katika bahari ya Hindi, India, pakistan na Iran ni moja ya matam...






TAMASHA la Nchi za Jahazi ambalo linahusisha nchi za Afrika, mataifa yaliyo katika bahari ya Hindi, India, pakistan na Iran ni moja ya matamasha yanayokua kwa kasi na mwaka huu, likiwa linatimiza miaka 11 linataka kuujadili utamaduni ambao upo njia ya panda.
Tamasha hili ambalo kwa sasa linaitisha kazi za fasihi na sanaa kutoka maeneo mbalimbali ya dunia; ni tamasha ambalo kama watanzania watalitumia vyema, si tu watauza kazi zao bali pia watawezesha watalii kumiminika kwa wingi kwa kuwa watajua nini kinatokea hapa nchini .
Ingawa kipindi hicho huwa ni muda wa kutamalaki kazi za sanaa na kuikumbatia fasihi ni kipindi ambacho wanautamaduni wanapata nafasi ya kuangalia kazi za wengine na pia kupata nafasi ya kufanya mauzo au mazungumzo na watuw engine kuhusiana na programu mbalimbali za kisanii.
Katika matamasha karibu kumi yote yaliyopita nimekuwa nikihimiza kipindi kama hiki kwa wananchi wa Tanzania kulienzi tamasha hili kw akupeleka kazi zao kwa wingi na si kuwaachia watu wa kigeni kutumia tamasha hili kujipandia ngazi.
Wapo wasanii wengi ambao wametumia jukwaa la tamasha la nchi za jahazi(ZIFF) kutengeneza mustakabali wa kazi zao ambazo zimekuwa zikihusudika hasa baada ya kuzinduliwa rasmi katika tamasha hilo ambalo hufanyika visiwa vya Unguja.
Watanzania wanaposhindwa kutumia Tamasha hilo ambalo kazi yake kubwa ni kuwakutanisha wasanii na kujadili masuala mbalimbali kupitia makongamano yake,unaanza kuona woga na kuthubutu unaowakabilki wasanii wengi wa Tanzania, wawe wa muziki, filamu au sanaa ya kuchonga na hata fasihi. Tamasha hilo kubwa ambalo linaweza kuelezwa kuwa bomba kuliko yote Afrika Mashariki na ya Kati, manake lipo la Amakula la Uganda na hili la karibuni la kenya ni jukwaa la kuuza na kukutana na soko au hata uhakiki wenye lengo la kuboresha zaidi kazi za msanii.
Mara zote katika tamasha hili kunakuwepo na vyombo mbalimbali vya habari vya nchini Tanzania na nchi za nje, vyombo ambavyo hutumika kupeleka ujumbe mbalimbali kwa watu wengine wa ughaibuni ambao hupenda kujua utamaduni katika eneo hili la afrika unaenziwa vipi.
Mkurugenzi wa tamasha hili, Dk Martin Mhando, amesema katika mazungumzo na mwandishi wa makala haya kwamba mwaka huu wamepania kufanya vitu vingi vizuri na ndio maana maandalizi ya tamasha yalianza Novemba mwaka jana na sasa wanaitisha kazi za watu mbalimbali kwa uhakiki.
Pamoja na filamu tamasha hilo pia hukutanisha wanazuoni wakijadili mada mbalimbali zenye upeo mkubwa na safari hii mabishano makubwa yatakuwa juu ya utamaduni njia ya panda.
Dk Martin mbaye kitaalamu ni mtengeneza sinema na hufundisha sinema katika chuo kikuu cha Australia,akizungumza kutoka katika ofisi za tamasha hilo zilizopo Forodhani katika Ngomekongwe mtaalamu huyo amesema ni kipindi muafaka kwa wasanii wa Tanzania wakatumia tamasha hilo ambalo mwaka jana serikali ya Zanzibar ilisema wazi kwamba italipiga jeki na kulitumia katika kufanikisha sekta ya utalii.
Katika eneo la ofisi ndipo pia lipo eneo kuu linalotumika kwa ajili ya kuonyesha filamu na pia muziki.Ukumbi huu wa zamani kabisa ambao ulikuwa unatumika kwa ajili ya shughuli mbalimbali ingawa kwanza ilikuwa ngome ya Wareno na baadaye kuwa kituo cha reli ingawa harufu yake kwa sasa haipo.
Harufu hiyo imesahaulika lakini ukifika pamoja na kuona sanaa pia unakutana na maelezo Ngome Kongwe hiyo ilikuwa na nini. Hapa watalii hujionea taarifa mbalimbali zilizorekodiwa za Sultan kutengeneza Reli kwenda Bububu na eneo lile lilikuwa ndilo karakarana na kituo cha reli. Mwaka jana kulikuwa na kila tarajio kwamba sinema ya Kitanzania itafungua dimba, pamoja na kwamba haikufungua dimba filamu nyingi zilioonyeshwa siku ya kwanza zilikuwa za Kitanzania na wakenya walitawala kwa nchi za Afrika mashariki.
Mwaka huu Filamu inayogusa Namibia ndiyo ityakayofungua dimba.Watanzania naambiwa wanasuasua kurekebisha mambo.
Kwa miaka 10 filamu za kitanzania zimekuwa hazitumiki kuanzisha tamasha hilo, si kwamba waandazi hawataki bali ushiriki wenye uhakika kutoka kwa watanzania ni mdogo sana.
kwa kuwa majaji wanatoka katika makundi matatu makubwa duniani na wanaozungumza Kiingereza na Kifaransa ni vyema kwa watengeneza sinema wa Tanzania ambao wanataka kuona soko la Ulaya kutumbukiza maelezo katika sinema zao kwa lugha ya Kiingereza ili wanaoamua (majaji) kuwa na nafasi ya kuangalia si ubora wa sinema pekee bali skrini yake na hadithi yenyewe.
Sinema kama ya Hammie Rajab ya Mama ambayo iliingizwa katika tamasha la tisa haikuweza kufua dafu kwa kuwa haikuwa na maelezo (subtitles): Ndio kusema kama watanzania wangelipenda waangaliwe kimataifa sinema zao zinastahili kuwa na maelezo ya Kiingereza.
Watanzania wanaotakiwa kupeleka kazi zao ni pamoja na wale wa filamu , fasihi watunzi wa vitabu na waghani mbalimbali, wachongaji na waumbaji wa mambo mbalimbali na pia wanamuziki na watu wa sanaa za jukwaani zikiwemo ngoma.
Inafaa kukumbuka kuwa Tamasha la nchi za majahazi si tu linaonyesha filamu lakini lina vitu vingi mno kiasi kama nilivyosema awali na kwamba wakati mwingine usipokuwa makini mengine yatakupita bila ya wewe kuwa na habari.
Vitu kama makongamano kwa watoto, wanawake, watengeneza sinema, wanamuziki, wahakiki wa filamu, wasanii wa jukwaa, michezo ya kuigiza, wachoraji na pia wasanifu maumbo ni vitu vinaweza kukupita kama nunavyoweza kupitwa na maonyesho ya sinema na maonyesho ya Forodhani kama huna uhakika unataka nini hasa.
Pamoja na uwingi wa masuala hayo,Mtendaji mkuu wa ZIFF Dk Martin Mhando alisema katika mazungumzo kuwa ushiriki wa Watanzania ni mdogo na hii inadumaza uwezo wa fikra kwa wasanii wa Tanzania kuweza kushiriki katika soko la kimataifa la sanaa. Wakati washiriki wa nje hupapatikia kutuma maombi na kutafuta maelekezo watanzania wenyewe pamoja na kupelekwa ushawishi bado wanaona kwamba si lazima kushiriki katika tamasha hili na mbaya zaidi hata vyombo vikuu vya habari vimekuwa havioni nafasi ya ZIFF katika kuboresha maisha ya wasanii na pia sanaa yenyewe.
Mwaka jana Vyombo vya nje kama BBC, Deutch Velle,VOA,Reuters AP, na AFP walituma watu wao kufanya kazi ya kurekodi matukio kwa shughuli mbalimbali na hata wengine wanafanya dokumentari ambazo baadaye wanaenda ama kuziuza kwao au kuwaonyesha watu kwa bei mbaya kabisa. Lakini vyombo vya habari vya tanzania vya elektroniki hata uhusiano wa kawaida hawataki au watataka kukutoza bei mbaya kwa huduma ya kuhabarisha.
"Makongamano mengi ambayo kwa kawaida huendeshwa na hata mwaka huu yapo yamelenga kuinua vipaji vya watanzania, lakini watanzania wenyewe huwa wanakosekana kwa wingi na badala yake watu kutoka Uganda, kenya, Rwanda, Zambia, Malawi wanajishughulisha hakika ni upotezaji wa nafasi ya pekee ya kuinuka kwa wasanii na sanaa yetu kujulikana kimataifa" anasema Dk Martin.
Ipo faida kuwa ya ushiriki katika tamasha hili. Kuna faida kubwa ambayo huenda haionwi vyema na serikali au watu kwa kawaida. Kimsingi mshiriki si tu anatangaza jina lake bali biashara yake na kupata mwelekeo mpya wa mafanikio ya wenzake.
Kimsingi tamasha la nchi za majahazi si tu linastahili kupangwa kuwa bora zaidi kwa ajili ya wasanii na kutangaza utamaduni wetu lakini pia lina nafasi kubwa ya kujadili utamaduni katika hali ya sasa ambapo utandawazi ni mwalimu mkorofi anayevuruga hata vinywa na matendo ya watu kwa sasa.
Ni wakati wa wasanii mbalimbali wakiwemo watengeneza sinema kupeleka kazi zao kwa Tamasha ili kupata nafasi ya kufanya mazungumzo na wenzao wa nje na hata wa ndani na kuwashawishi kushirikiana kutengeneza sinema hapa nchini kwa gharama nafuu zaidi.
Kama wasanii watajumuika kwakutuma kazi zao, tamasha hili litaendelea kubwa zaidi na kuwa na upeo mkubwa zaidi kuwaandaa watu wa kwenda kushiriki katika maonyesho ya nje ambayo ni muhimu zaidi katika kujitangaza. mwisho

COMMENTS

BLOGGER: 32
Loading...
Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,317,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,250,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,Habari,5087,habari dodoma,29,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,519,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,353,muziki na fasheni,6,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,3,SAYANSI ANGA,3,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,3,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: ZIFF mwaka wa 11 Watanzania mchecheto
ZIFF mwaka wa 11 Watanzania mchecheto
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj52iL78V0FylcGo6ltjoSYgquQEoYwQjpjwAMS-vgBKPFdWdfIUCaIUBS2JDPFFsip3SlDjJBrEHDUO6xZZt9Br7IVct9bCUukMbguBNmNhXgXPthnSpWe5LyMSTrlIzSZsckN891hLPkK/s320/CEO+Dr.+Martin+Mhando+(kushoto)akiwa+na+Imruh+bakari+mmoja+wa+viongozi+waliopita+wa+taasisi+hiyo+ya+ZIFF.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj52iL78V0FylcGo6ltjoSYgquQEoYwQjpjwAMS-vgBKPFdWdfIUCaIUBS2JDPFFsip3SlDjJBrEHDUO6xZZt9Br7IVct9bCUukMbguBNmNhXgXPthnSpWe5LyMSTrlIzSZsckN891hLPkK/s72-c/CEO+Dr.+Martin+Mhando+(kushoto)akiwa+na+Imruh+bakari+mmoja+wa+viongozi+waliopita+wa+taasisi+hiyo+ya+ZIFF.JPG
Lukwangule Entertainment
https://lukwangule.blogspot.com/2008/03/ziff-mwaka-wa-11-watanzania-mchecheto.html
https://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2008/03/ziff-mwaka-wa-11-watanzania-mchecheto.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy