HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUAHIRISHA MKUTANO WA SAB...
HOTUBA YA MHESHIMIWA
MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU
WA JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKATI WA KUAHIRISHA
MKUTANO WA SABA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA – DODOMA, TAREHE 23
APRILI 2012*
UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika,
1. Nitumie nafasi hii kumshukuru
Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema
kwa kutuwezesha
kutekeleza majukumu yote yaliyopangwa kwa ufanisi mkubwa
katika Mkutano huu wa
Saba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
ulioanza tarehe
10 Aprili 2012. Tumefanikiwa kufanya hivyo
kutokana na
maandalizi mazuri ya
Mkutano, ushirikiano miongoni Mwetu na Waheshimiwa
Wabunge wote kujiandaa
vizuri katika kuchangia hoja mbalimbali zilizopangwa.
Mheshimiwa Spika,
2. Katika Mkutano huu, tumepata
Waheshimiwa Wabunge Wapya Wawili
wote kutoka Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Napenda kutumia
nafasi hii kumpongeza
Mheshimiwa *Joshua Samwel Nassari* kwa
kuchaguliwa
kuwa Mbunge Mpya wa Jimbo
la Arumeru Mashariki. Vilevile, nampongeza
Mheshimiwa *Cecilia Daniel Paresso* kwa kuteuliwa kuwa Mbunge
kupitia Viti
Maalum (CHADEMA). Kipekee
kabisa nawapongeza Wananchi wa Arumeru Mashariki
kwa kutumia haki yao ya
Kidemokrasia vizuri. Lakini kwa dhati kabisa,
nakipongeza
Chama Cha Mapinduzi kwa kukubali Matokeo ya Uchaguzi Mdogo wa
Arumeru
Mashariki.
Kitendo hicho kinaonesha uungwana na ukomavu wa Kisiasa
na Demokrasia katika Nchi
yetu. Huu ni mfano mzuri wa kuigwa na Vyama
vingine vyote vya Siasa
Nchini.
3. Kwa Waheshimiwa Wabunge wapya
tunawatakia mafanikio na
tunawaahidi ushirikiano wetu ndani ya Bunge na katika
Kujenga Taifa letu.
Vilevile, napenda kutumia
nafasi hii pia kuwapongeza Waheshimiwa Madiwani
wote waliopata Ushindi
katika Chaguzi zilizofanyika katika Kata za
Vijibweni (Temeke),
Kiwangwa (Bagamoyo), Kirumba (Mwanza), Logangabilili
(Bariadi), Chang’ombe
(Dodoma), Kiwira (Rungwe),
Lizaboni (Songea) na Msambweni (Tanga). Tunawatakia wote waliochaguliwa
afya njema na
maisha mazuri ili muweze
kuwatumikia Wananchi waliowachagua na Taifa kwa
ujumla.
Mheshimiwa Spika,
4. Katika Mkutano huu wa Saba wa Bunge
tulifanya Uchaguzi wa
Wawakilishi wa Nchi yetu
katika Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Napenda nitumie nafasi
hii kuwapongeza wafuatao kwa kuchaguliwa kuwa
Wabunge wa Bunge hilo,
Mheshimiwa Makongoro Nyerere; Mheshimiwa Abdullah
Hassan Mwinyi; Mheshimiwa
Nderakindo Kessy; Mheshimiwa Angela Kizigha;
Mheshimiwa Adam Kimbisa;
Mheshimiwa Twaha Issa Taslima; Mheshimiwa Bernard
Murunya; Mheshimiwa
Shy-Rose Bhanji; na Mheshimiwa Mariam Ussi Yahya.
Tunawapongeza
Wote! Tuna imani kubwa
kwamba watatuwakilisha vyema katika Bunge la
Jumuiya ya Afrika ya
Mashariki kwa maslahi ya Tanzania Kiuchumi na Kijamii
na Nchi zote kwa ujumla.
Mheshimiwa Spika,
5. Tangu kuhitimishwa kwa Mkutano wa
Sita wa Bunge lako Tukufu,
kumekuwepo na matukio
mbalimbali ya kusikitisha, kusononesha, kuhuzunisha
na yenye Majonzi makubwa
yaliyosababishwa na Misiba na Ajali ambazo
zimesababisha Vifo na
kujeruhi Watanzania wenzetu wakiwemo Waheshimiwa
Wabunge.
6. Napenda kupitia Bunge lako Tukufu,
kutoa Salaam za Rambirambi
kwa Familia, Ndugu, Jamaa
na Marafiki wa Watanzania wote waliopoteza
Maisha. Tuwaombee
Marehemu wote ili Mwenyezi Mungu azilaze Roho zao Mahali
Pema Peponi. Amina!
7. Vilevile, nawapa pole Majeruhi wote
walionusurika na kupata
Majeraha kutokana na
Ajali mbalimbali zikiwemo ajali za Magari, Pikipiki,
Baiskeli na vifaa vingine
vya barabarani na ile ya Shirika la Ndege Nchini
(ATCL) iliyotokea kule
Kigoma.
Mheshimiwa Spika,
8. Wote tunafahamu kwamba katika
kipindi hiki tumekuwa na
Waheshimiwa Wabunge
wenzetu ambao wamekuwa wakisumbuliwa na Maradhi
mbalimbali. Tunamshukuru
Mwenyezi Mungu kwa kusikia Maombi yetu. Wote
tumefarijika kutokana na
kurejea kwa Mheshimiwa Dkt. Harrison George
Mwakyembe ndani
ya Bunge lako Tukufu akiwa
na Afya
Njema. Tunaamini Afya
yake itazidi kuimarika
katika siku zijazo. Vilevile, ni matumaini yetu
makubwa kwamba,
wenzetu wengine akiwemo Mheshimiwa Profesa Mark James
Mwandosya,
Mbunge wa Jimbo la Rungwe Mashariki
na Waziri wa Maji;
Mheshimiwa
Dkt.John Pombe Magufuli, Mbunge
wa Chato na
Waziri wa
Ujenzi; pamoja
na Mheshimiwa Highness Samson Kiwia, Mbunge wa Ilemela
ambao bado wako
katika Matibabu watapata nafuu haraka itakayowawezesha
kuungana na
sisi tena ndani ya Bunge letu Tukufu.
Mheshimiwa Spika,
9. Mwisho, naungana na Watanzania wote
kuipongeza Timu ya Simba
kwa kufikia Mzunguko wa
Tatu wa Mashindano ya Kombe la Mabingwa Barani
Afrika. Sote tunawatakia
Maandalizi mema ili wazidi kufanya vizuri katika
Mechi zijazo kwa kuwa
ushindi wao ni ushindi wa Nchi yetu. Kwa Wachezaji na
Viongozi, wao nawaasa
msibweteke na ushindi mlioupata, ila mnatakiwa
kuelewa kuwa safari bado
ni ngumu na ndefu.
SHUGHULI ZA SERIKALI
(a) Maswali
Mheshimiwa Spika,
10. Katika Mkutano huu wa Saba
tunaouhitimisha leo, Jumla ya Maswali *
131* ya Msingi na mengine
*315* ya Nyongeza kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge
yalipata majibu ya Serikali. Vilevile, jumla ya Maswali *16* ya Msingi na
*
9* ya Nyongeza kupitia
utaratibu wa Maswali ya Papo kwa Papo kwa Mheshimiwa
Waziri Mkuu yalijibiwa.
(b) Miswada
Mheshimiwa Spika,
11. Katika Mkutano huu Miswada ifuatayo
ilisomwa na kujadiliwa:
(i) Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya
Sheria Mbalimbali za
Biashara wa Mwaka 2011
[*The Business Laws (Miscellaneous Amendments) Bill,
2011*];
(ii) Muswada wa Sheria ya Taasisi ya
Utafiti wa Mifugo Tanzania wa
Mwaka 2011 (*The Tanzania
Livestock Research Institute Bill, 2011*);
(iii) Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya
Sheria za Mifuko ya
Hifadhi ya Jamii wa Mwaka
2012 [*The Social Security Laws (Amendments) Act,
2012*]; na
(iv) Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya
Sheria Mbalimbali wa Mwaka
2011 [*The Written Laws
(Miscellaneous Amendments) (No.2) Act, 2011*].
Vilevile, Muswada wa
Sheria ya Haki za Wagunduzi wa Mbegu za Mimea wa Mwaka
2012 [*The Plant
Breeder’s Rights Bill, 2012*] ulisomwa kwa mara ya kwanza.
(c) Taarifa Mbalimbali
* *
*Mheshimiwa Spika,*
12. Bunge lako Tukufu lilipata fursa ya
kupokea na kujadili Taarifa
mbalimbali kama
ifuatavyo:
(i) Taarifa za Kamati za Bunge
zinazosimamia Fedha za Umma; na
(ii) Taarifa za Kamati za Bunge za Kisekta
na zisizo za Kisekta.
Mheshimiwa Spika,
13. Napenda nitumie nafasi hii kuwashukuru
kwa dhati Waheshimiwa
Wabunge wote kwa kazi
nzuri ambayo wameifanya katika siku zote za Mkutano
huu zikiwemo kujadili na
kupitisha Miswada niliyotaja hapo juu. Nawashukuru
pia kwa michango yenu
wakati wa kujadili Taarifa mbalimbali
zilizowasilishwa hapa
Bungeni.
Mheshimiwa Spika,
14. Kipekee kabisa nitumie nafasi hii
kuwapongeza Wenyeviti
na Wajumbe
wa
Kamati za Bunge zilizowasilisha Taarifa mbalimbali mbele ya
Bunge
lako Tukufu. Ni dhahiri
kuwa utaratibu huu unatoa fursa kwa Waheshimiwa
Wabunge kupitia kwa kina
masuala mbalimbali ya Kisekta na kutoa
ushauri
kwa Serikali. Aidha, utaratibu
huu unatusaidia kuwepo kwa ‘*Checks and
Balances*’ ndani ya Nchi
yetu. Niwashukuru pia Wabunge wote kwa jinsi
walivyochangia kwenye
mjadala wa kujadili
Taarifa hizo.
Waheshimiwa Wabunge
wameonesha hisia zao katika kujadili masuala yote haya
muhimu na mengineyo na
hasa katika Mwenendo wa Matumizi ya Fedha za
Serikali kwenye Wizara,
Taasisi za Umma, Mikoa na Mamlaka za Serikali za
Mitaa. Nawashukuru sana
kwa kujadili Taarifa zote kwa uwazi na hatimaye
kutoa mapendekezo kwa
Serikali namna ya kushughulikia matatizo
yaliyojitokeza kwenye
maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Spika,
15. Mapendekezo ya Waheshimiwa Wabunge yako
katika makundi muhimu
yafuatayo:
Kwanza:
Ni uimarishaji wa Uongozi na Utendaji katika Wizara, Taasisi za
Serikali,
Mashirika ya Umma, Mikoa na Serikali za Mitaa;
Pili:
Ni usimamizi wa Sheria, Kanuni na Taratibu zinazohusu
masuala ya
Mapato na Matumizi ya Fedha;
Tatu:
Ni uimarishaji wa hatua za Kupambana na Rushwa, Ubadhirifu
na Wizi wa Mali
za Umma;
Nne: Ni uendelezaji wa hatua za kubana
matumizi yasiyo ya
lazima ndani ya
Serikali na Vyombo vyake; na
Tano: Ni ulinzi wa Rasilimali za Nchi kwa
maslahi ya Taifa letu.
*Mheshimiwa Spika,*
16. Siku
zote Serikali imekuwa tayari
kupokea ushauri wa Bunge lako
Tukufu na baada ya
kusikiliza mjadala na mapendekezo ya Waheshimiwa
Wabunge, Serikali
inaahidi kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa Ushauri na
Mapendekezo yaliyomo
katika Taarifa hizo. Niwahakikishie Waheshimiwa
Wabunge kwamba Serikali
itachukua hatua stahiki kuimarisha usimamizi na
utendaji ndani ya Wizara
na Serikali za Mitaa na Vyombo vyake na
kuhakikisha Viongozi na
Watendaji wake wanafanya kazi kwa umakini na
uadilifu zaidi.
Mheshimiwa Spika
17. Katika
Hotuba yangu hii
ningependa kuzungumzia kwa kifupi
mambo machache
yanayohusu: Hatua zilizofikiwa katika Mchakato wa Kutekeleza
Sheria ya Mabadiliko ya
Katiba; Dhana ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii;
Matokeo ya Shule za
Msingi na Kidato cha Nne Mwaka 2011; Maendeleo ya
Viwanda; Sensa ya Watu na
Makazi; na mwisho Mpango wa Kutoa Kifuta Machozi
cha Mifugo.
HATUA
ZILIZOFIKIWA KATIKA MCHAKATO
WA KUTEKELEZA SHERIA YA
MABADILIKO YA KATIBA
Mheshimiwa Spika,
18. Kama Waheshimiwa Wabunge watakavyokumbuka,
katika Mkutano wa Sita
mwezi Februari 2012,
Bunge lako Tukufu lilijadili na kupitisha Marekebisho
ya Sheria ya Mabadiliko
ya Katiba (Sura ya 83). Napenda kuliarifu Bunge
lako Tukufu kuwa, mara
baada ya Marekebisho hayo kupitishwa, Mheshimiwa
Rais Dkt. Jakaya Mrisho
Kikwete kupitia Tangazo la Serikali
Namba 66
la tarehe
24 Februari 2012;
alialika Vyama vya Siasa
vyenye Usajili wa Kudumu,
Jumuiya za Dini, Asasi za
Kiraia, Taasisi na Makundi ya Watu wenye malengo
yanayofanana kuwasilisha
kwake majina ya watu wanaoweza kuteuliwa kuwa
Wajumbe wa Tume
itakayoratibu na kukusanya maoni ya Wananchi kuhusu
Mabadiliko ya Katiba.
* *
19. Kwa mujibu wa Tangazo hilo, siku ya
mwisho ya kuwasilisha
mapendekezo
ya majina
ilikuwa tarehe 16 Machi 2012. Hata
hivyo, kutokana na umuhimu
wa
zoezi hilo na ili
kutoa fursa zaidi
kwa Wananchi na
Taasisi
au Makundi yaliyopo Mikoani, Mheshimiwa Rais kupitia Tangazo la
Serikali
Namba 101 la tarehe 16
Machi 2012 aliongeza muda huo hadi
tarehe 23
Machi 2012. Mapendekezo
ya majina yaliyopokelewa yalikuwa mengi na hivyo
kumpa Mheshimiwa Rais
uwanja mpana zaidi wa kufanya uteuzi.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
20. Tarehe 6 Aprili 2012, Mheshimiwa Rais
baada ya kushauriana na
Mheshimiwa Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, aliteua
Wajumbe 32 wa Tume
itakayoratibu na Kukusanya Maoni ya Wananchi kuhusu
Mabadiliko ya Katiba.
Pamoja na Wajumbe hao, Mheshimiwa Rais aliteua Katibu
na Naibu Katibu wa Tume
hiyo. Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Wajumbe,
Katibu na Naibu Katibu wa
Tume waliapishwa na Mheshimiwa Rais tarehe 13
Aprili 2012. Kutokana na
*umuhimu wa Tume hii katika historia ya Nchi yetu*,
naomba niwataje Wajumbe
wote wa Tume walioteuliwa:
1. Mheshimiwa
Jaji Joseph Sinde
WARIOBA – Mwenyekiti;
2. Mheshimiwa Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino
RAMADHANI - Makamu Mwenyekiti;
3. Mheshimiwa Dkt. Salim Ahmed SALIM – Mjumbe;
4. Ndugu Abubakar Mohammed ALI – Mjumbe;
5. Ndugu Ally Abdullah Ally SALEH – Mjumbe;
6. Mheshimiwa Al-Shaymaa J. KWEGYIR (Mb.) –
Mjumbe;
7. Ndugu Awadh Ali SAID – Mjumbe;
8. Dkt. Edmund Adrian Sengondo MVUNGI – Mjumbe;
9. Ndugu Esther P. MKWIZU – Mjumbe;
10. Ndugu Fatma Said ALI – Mjumbe;
11. Ndugu Humphrey POLEPOLE – Mjumbe;
12. Ndugu Jesca Sydney MKUCHU – Mjumbe;
13. Ndugu John J. NKOLO – Mjumbe;
14. Ndugu Joseph BUTIKU – Mjumbe;
15. Ndugu Kibibi Mwinyi HASSAN – Mjumbe;
16. Ndugu Maria Malingumu KASHONDA – Mjumbe;
17. Ndugu Muhammed Yussuf MSHAMBA – Mjumbe;
18. Ndugu Mwantumu Jasmine MALALE – Mjumbe;
19. Prof. Mwesiga L. BAREGU – Mjumbe;
20. Ndugu Nassor Khamis MOHAMMED – Mjumbe;
21. Ndugu Omar Sheha MUSSA – Mjumbe;
22. Prof. Palamagamba J. KABUDI – Mjumbe;
23. Mheshimiwa Raya Suleiman HAMAD – Mjumbe;
24. Ndugu Richard Shadrack LYIMO – Mjumbe;
25. Ndugu Riziki Shahari MNGWALI – Mjumbe;
26. Alhaj Said EL- MAAMRY – Mjumbe;
27. Ndugu Salama Kombo AHMED – Mjumbe;
28. Ndugu Salma MAOULIDI – Mjumbe;
29. Ndugu Simai Mohamed SAID – Mjumbe;
30. Ndugu Suleiman Omar ALI – Mjumbe;
31. Ndugu Ussi Khamis HAJI – Mjumbe;
32. Ndugu Yahya MSULWA – Mjumbe;
33. Ndugu Assaa Ahmad RASHID – Katibu; na
34. Ndugu Casmir Sumba KYUKI – Naibu Katibu.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
21. Kwa namna ya pekee, nampongeza Mheshimiwa Jaji Joseph Sinde
Warioba, Waziri Mkuu na
Makamu wa Kwanza wa Rais Mstaafu kwa kuteuliwa kuwa
Mwenyekiti wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba na Mheshimiwa Augustino
Ramadhani, Jaji Mkuu
Mstaafu wa Tanzania kwa kuteuliwa kuwa Makamu
Mwenyekiti. Vilevile,
napenda kuwapongeza Wajumbe wote, wakiwemo Katibu na
Naibu Katibu kwa
kuteuliwa kuunda Tume hii. Ni matumaini yangu na ya
Watanzania wote kwa
ujumla kuwa, Wajumbe wa Tume watatumia ujuzi, maarifa
na uzoefu wao katika
kuhakikisha wanatekeleza majukumu waliyopewa kwa
mujibu wa Sheria na kwa
ufanisi mkubwa.
*Serikali ilivyojipanga
(Maandalizi ya Tume)*
* *
*Mheshimiwa Spika,*
22. Wakati wa hafla ya kuwaapisha
Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti,
Wajumbe, Katibu na Naibu
Katibu wa Tume, Mheshimiwa Rais aliihakikishia
Tume kuwa Serikali itaipa
kila aina ya ushirikiano
ili itekeleze
majukumu yake kwa
ufanisi. Kwa niaba ya Serikali kupitia Bunge lako Tukufu,
naomba kwa mara nyingine
tena nikuhakikishie kuwa Serikali imejipanga kwa
kuweka mazingira
yatakayoiwezesha Tume kutekeleza majukumu yake kama Sheria
ya Mabadiliko ya Katiba
(Sura ya 83) inavyoelekeza. Hivi sasa, Serikali
inakamilisha maandalizi
muhimu kuiwezesha Tume kuanza kazi tarehe 1 Mei
2012 kama ilivyopangwa.
*Mheshimiwa Spika,*
23. Naomba
kutumia fursa hii kuwaomba Wananchi wote kuipa Tume
ushirikiano wa kutosha
ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.
Vilevile, napenda
kuwasihi Wananchi wajitokeze kwa wingi
katika Mikutano
itakayoitishwa na Tume na watoe maoni yao kwa uhuru na utulivu
bila
vikwazo vyovyote. Lengo
la Serikali ni kuhakikisha kuwa Watanzania wote
wanashiriki kikamilifu
bila ubaguzi wowote katika mchakato huo wa kuandika
Katiba Mpya ili Nchi yetu
iweze kupata Katiba itakayokidhi mahitaji ya
Karne hii na miaka mingi
ijayo.
*Mheshimiwa Spika,*
24. Napenda kusisitiza maagizo ya Mheshimiwa
Rais aliyoyatoa siku ya
kuwaapisha Wajumbe wa
Tume kwamba Mchakato huu wa Mabadiliko ya Katiba siyo
mchakato wa kuwepo au
kutokuwepo kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Huu
ni mchakato unaolenga
kukubaliana namna bora ya kuendesha Nchi kwa
kuzingatia uwepo wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, uwepo wa Haki za
Binadamu na Misingi ya
Utawala Bora, uwepo wa Mihimili Mitatu ya Dola yaani
Bunge, Mahakama na
Serikali na namna nzuri ya kuboresha utendaji kazi wa
Mihimili hiyo. Ninawaomba
Waheshimiwa Wabunge kuwaelimisha Wananchi juu ya
kuzingatia mambo haya ya
msingi wakati wa kutoa maoni yao.
*MIFUKO YA HIFADHI YA
JAMII*
* *
*Mheshimiwa Spika, *
25. Waheshimiwa Wabunge watakumbuka kuwa
Bunge lako Tukufu
lilipitisha Sheria Namba
8 ya Mwaka 2008 ya kuanzisha Mamlaka ya Usimamizi
na Udhibiti wa Sekta ya
Hifadhi ya Jamii.* *Umuhimu wa Hifadhi ya Jamii
Nchini unatambuliwa ndani
ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
katika Ibara ya *11(1)*
inayosomeka, nanukuu:
* *
*“Mamlaka ya Nchi itaweka
utaratibu unaofaa kwa ajili ya kufanikisha
utekelezaji wa Haki ya
Mtu Kufanya Kazi, Haki ya kujipatia Elimu na Haki ya
kupata Msaada kutoka kwa
Jamii wakati wa Uzee, Maradhi au hali ya Ulemavu,
na katika hali nyinginezo
za mtu kuwa hajiwezi.”* Mwisho wa kunukuu.
* *
Hivyo, Hifadhi ya Jamii
ni nguzo muhimu katika kutekeleza dhana ya Utawala
Bora katika Jamii na
kuchochea ukuaji wa Uchumi.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
26. Lengo Kuu la kuwa na Mipango ya Hifadhi
ya Jamii ni kuondoa
Umaskini wakati wa Uzee
na kutoa kinga ya Kiuchumi na Kijamii
pale
panapotokea matukio na
majanga mbalimbali yanayosababisha kupungua kwa
kipato. Hivi sasa kuna
Mifuko Sita ya Hifadhi ya Jamii ambayo inatoa Mafao
ya muda mfupi na muda
mrefu kulingana na taratibu zilizopo katika Sheria za
Mifuko husika. Mifuko
hiyo ni Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF);
Mfuko wa Pensheni kwa
Mashirika ya Umma (PPF); Mfuko wa Pensheni kwa
Watumishi wa Umma (PSPF);
Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Serikali za
Mitaa (LAPF); Mfuko wa
Akiba kwa Watumishi wa Serikali (EGPF); na Mfuko wa
Taifa wa Bima ya Afya
(NHIF).* *
*Mheshimiwa Spika,*
27. Kwa mujibu wa takwimu zilizopo, ni
Asilimia *5.9* tu ya nguvu
kazi ya Watanzania
waliopo katika Sekta rasmi ndiyo wanaopata huduma ya
Mifuko ya Hifadhi ya
Jamii. Takwimu hizi ni kielelezo tosha kuonesha
changamoto inayoikabili
Sekta ya Hifadhi ya Jamii katika kuhakikisha
Watanzania wengi
wanajiunga na kunufaika na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.
Aidha, changamoto hii si
kwa Wananchi wanaojishughulisha katika Sekta isiyo
rasmi tu bali hata kwa
wale waliopo katika Sekta rasmi ambao kwa namna moja
au nyingine
hawajajiandikisha katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
28. Changamoto nyingine zinazokabili Mifuko
hii ya Hifadhi ya Jamii
ni pamoja na kupishana
sana kwa Mafao kati ya Mfuko mmoja na mwingine japo
kiwango cha kuchangia
kinalingana yaani Asilimia 20 ya Mshahara wa
Mtumishi. Lipo pia tatizo
la Pensheni isiyoendana na gharama za maisha,
gharama kubwa za
uendeshaji wa Mifuko, huduma hafifu kwa Wanachama wa
Mifuko, Kukosekana kwa
Kanuni za Uwekezaji zinazolingana pamoja na Idadi
kubwa ya Wananchi
kutoelewa umuhimu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
29. Katika kukabiliana na baadhi ya
changamoto zilizoko kwenye Sekta
hii ya Hifadhi ya Jamii,
Serikali imechukua hatua mbalimbali. Moja ya hatua
hizo ni kuanzisha na
kutekeleza Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka
2003 ambayo ni Dira ya
shughuli zote za Hifadhi ya Jamii hapa Nchini.
Vilevile, mwaka 2008
Serikali ilianzisha Mamlaka ya Hifadhi ya Jamii.
Jukumu kubwa la Mamlaka
hii ni kusimamia Sekta ya Hifadhi ya Jamii ikiwamo
Mifuko yote ya Hifadhi ya
Jamii Nchini. Ni matumaini yangu kuwa Mamlaka ya
Hifadhi ya Jamii
itatusaidia kuzifanyia kazi Changamoto nilizozitaja hapo
juu na nyingine ili
kuhakikisha kuwa Watanzania wengi wanajiunga na kupata
Hifadhi ya Jamii.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
30. Ili kuhakikisha kuwa Mamlaka ya
Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya
Hifadhi ya Jamii,
Serikali ilileta katika Kikao hiki cha Bunge Muswada wa
Marekebisho ya Sheria za
Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Nichukue fursa hii
kulipongeza Bunge lako
Tukufu kwa kupitisha Muswada huu. Muswada huo
uliopitishwa na Bunge
unalenga kuwianisha Sheria za Mifuko na Sheria ya
Mamlaka ya Hifadhi ya
Jamii. Lengo ni kuipa Mamlaka uwezo zaidi wa
kutekeleza majukumu yake;
na kuiwezesha Mifuko kutoa huduma bora kwa
Wanachama wake. Muswada
huu unaiwezesha pia Mifuko kutambua uwezo wa
Mamlaka kuleta mageuzi
kwenye Sekta kwa kutoa Miongozo mbalimbali.
*Mheshimiwa Spika,*
33. Nachukua fursa hii kuwakumbusha Waajiri
wanaokiuka Sheria kwa
kuwachagulia Wafanyakazi
wao wapya, Mifuko ya kujiunga nayo kinyume na
matakwa ya Wafanyakazi
hao waache kufanya hivyo. Kila Mwajiri anatakiwa
kuweka mazingira
yatakayomwezesha Mfanyakazi kuchagua Mfuko anaoupenda.
Mazingira hayo ni pamoja
na kuialika Mifuko yote kutoa maelezo kuhusu Mafao
na huduma zao na kuwapa
fursa Wafanyakazi kufanya maamuzi ya kujiunga na
Mfuko waupendao. Ni
matumaini yangu kuwa Mamlaka itaweka Kanuni
zitakazowezesha Mifuko
kuandikisha Wanachama kwa utaratibu unaokubalika na
unaomlinda Mwanachama.
34. Kwa upande wa Uwekezaji, Mamlaka
imekamilisha tathmini ambayo
itawezesha kutengeneza
Miongozo kwa Mifuko kuwekeza katika Vitega Uchumi
mbalimbali. Vilevile,
*Mamlaka itaweka mkakati kabambe wa kuelimisha Umma
ili Wananchi wengi zaidi
waweze kujiunga na Mifuko hii kwa kuwa sasa
wanaruhusiwa kujiunga na
Mifuko hiyo bila kujali kama wako Sekta Rasmi au
isiyo Rasmi*. Napenda pia
kutumia fursa hii kutoa wito kwa Waheshimiwa
Wabunge na Wananchi wote
kutoa ushirikiano stahiki kwa Mamlaka ili
kwa
kushirikiana na Wadau
mbalimbali tuboreshe, tuimarishe na kuwa na Sekta ya
Hifadhi ya Jamii iliyo
endelevu.
* *
*MATOKEO YA MTIHANI WA
KUMALIZA ELIMU YA MSINGI MWAKA 2011*
* *
*Mheshimiwa Spika,*
35. Mwaka 2011 Wanafunzi *983,545* wa Darasa
la Saba walifanya
mtihani wa Taifa. Kati
yao Wanafunzi *567,567,* *sawa na Asilimia 58.28 *ya
waliofanya mtihani
walifaulu. Kiwango cha Ufaulu cha mwaka 2011,
ikilinganishwa na kile
cha mwaka 2010 unaonesha kupanda kwa Asilimia
*4.76*kutoka
*Asilimia 53.52 ya mwaka
2010 hadi 58.28 mwaka 2011*.
* *
*Mheshimiwa Spika, *
36. Tathmini inaonesha Ufaulu kimasomo
umeongezeka kwa *masomo ya
Hisabati, Kiingereza na
Sayansi*.
i) *Kiwango cha Ufaulu kwa Somo la
Hisabati* kilikuwa *Asilimia
39.4 mwaka 2011*
ikilinganishwa na Asilimia *24.7 mwaka 2010*;
ii) *Kiwango cha Ufaulu kwa Somo la
Kiingereza* kilikuwa
Asilimia *46.7 mwaka
2011* ikilinganishwa na Asilimia *36.5 mwaka 2010*; na
iii) *Kiwango cha Ufaulu kwa Somo la
Sayansi* kilikuwa Asilimia
61.3 mwaka 2011
ikilinganishwa na Asilimia 56.1 mwaka 2010.
37. Taarifa zinaonesha kuwa kiwango cha
ufaulu kwa masomo ya
Kiswahili na Maarifa ya
Jamii kilishuka kwa mwaka 2011 ikilinganishwa na
mwaka 2010. Kwa mfano,
Ufaulu kwa Somo la Kiswahili ulikuwa Asilimia 68.6
mwaka 2011 ikilinganishwa
na Asilimia 71.0 mwaka 2010; na kiwango cha
ufaulu kwa Somo la
Maarifa ya Jamii kilikuwa Asilimia 54.8 mwaka 2011
ikilingnishwa na Asilimia
68.0 mwaka 2010.
* *
*Mheshimiwa Spika, *
38. Ni kweli kwamba, kwa muda mrefu
tumekuwa na matatizo ya ufaulu
katika masomo ya Sayansi
Nchini, lakini matokeo ya mwaka 2011 yanaonesha
kuwa juhudi zinazochukuliwa
na Serikali katika kukuza masomo hayo zimeanza
kuzaa matunda. Napenda
kuwapongeza Wanafunzi, Wazazi, Walezi, Walimu na
Watendaji wote
walioshiriki katika kuleta mafanikio hayo.
*Uchaguzi wa Wanafunzi
kuingia Kidato cha Kwanza mwaka 2012*
* *
*Mheshimiwa Spika,*
39. Katika Uchaguzi wa kuingia Kidato cha
Kwanza mwaka 2012, jumla ya
Wanafunzi *515,187,* sawa
na Asilimia 90.1 ya Wanafunzi waliofaulu
walichaguliwa kuingia
Kidato cha Kwanza katika Shule za Sekondari za
Serikali. Idadi hii iliongezeka
kwa Asilimia 12.49 kutoka Wanafunzi *456,350
* mwaka 2010. *Taarifa
nilizopokea kutoka Mikoa 12 ya Arusha, Dar es
Salaam, Dodoma, Iringa,
Mara, Morogoro, Mwanza, Lindi, Kilimanjaro,
Pwani,
Ruvuma
na Tanga, ***
*zinaonesha kuwa
Wanafunzi wote waliofaulu wamejiunga na Kidato cha Kwanza.
Nitumie nafasi hii
kuipongeza Mikoa hii kwa kuhakikisha kuwa hakuna
Wanafuzi waliofaulu na
kushindwa kujiunga na Sekondari. ***
40. Hata hivyo, sehemu kubwa ya Mikoa
niliyoitaja inaonesha kuwepo
kwa uhaba mkubwa wa
Vyumba vya Madarasa na Madawati. Naiagiza Mikoa yote
kuhakikisha mapungufu
haya yanashughulikiwa katika Bajeti ya mwaka
2012/2013. Aidha, Mikoa
iwe na Mipango endelevu ya kujenga Vyumba vya
Madarasa na kutengeneza
Madawati badala ya kusubiri matokeo ya Mtihani na
kuchaguliwa kwa Wanafunzi
ndipo ianze kuweka mikakati.
* *
*Matokeo ya Kidato cha
Nne mwaka 2011*
* *
*Mheshimiwa Spika,*
41. Matokeo ya Kidato cha Nne ya mwaka 2011
yanaonesha kuwa Wanafunzi
*181,880,* sawa na
Asilimia *53.6 *ya Wanafunzi *339,330* waliofanya
Mtihani walifaulu.
Kiwango hicho kimeongezeka kutoka Wanafunzi
*177,011*waliofaulu mwaka
2010 ikiwa ni sawa na Asilimia
*50.4* ya Wanafunzi
*351,214* waliofanya Mtihani.
* *
*Mheshimiwa Spika, *
42. Tangu mwaka 2008, Asilimia ya Wanafunzi
wanaofeli Mitihani ya
Kidato cha Nne imekuwa
ikiongezeka na kufikia Asilimia *16.3,* mwaka 2009
Asilimia *27.5,* mwaka
2010 Asilimia *49.6 *na kushuka tena hadi Asilimia *
43.3,* mwaka 2011. Sababu
za kushuka kwa ufaulu huo ni pamoja na upungufu
wa Walimu, Vifaa vya
Kufundishia na kujifunzia na kuimarika kwa udhibiti wa
uvujaji wa mitihani ya
Kidato cha Nne. Vilevile, inaelezwa na Wanataaluma
na Watafiti kwamba
kuondolewa kwa Mtihani wa Kidato cha Pili kumechangia
sana matokeo mabaya ya
Kidato cha Nne.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
43. Kutokana na hali ya kuongezeka kwa idadi
ya Wanafunzi
wanaofeli Mtihani
wa Kidato cha Nne,
Serikali imechukua hatua kadhaa zikiwemo za kuongeza na
kuimarisha usimamizi wa
matumizi ya *‘capitation grant’* ili kupunguza
tatizo la upungufu wa
Vifaa vya Kufundishia
na Kujifunzia Shuleni;
Kutekeleza mikakati ya
kuongeza idadi na ubora wa Walimu; na kujenga uwezo
wa Wakuu wa Shule
kusimamia ufundishaji na ujifunzaji wa kila siku.
44. Ni matarajio yangu kwamba tukiyafanya
haya, tutaweza kufikia Azma
yetu ya kuwa na matokeo
mazuri katika siku zijazo. Niwaombe Wadau wote wa
Elimu wakiwemo
Waheshimiwa Wabunge, Viongozi, Walimu, Wazazi, Walezi na
Wanafunzi kila mmoja
atimize wajibu wake katika utoaji wa Elimu kuanzia,
Nyumbani, Shuleni na
Vyuoni ili tuweze kuinua Kiwango cha Ubora wa Elimu
Nchini.
* *
*MAENDELEO YA
VIWANDA *
* *
*Mheshimiwa Spika,*
45. Tarehe 16 hadi 23 Septemba 2011
nilifanya ziara Mkoa wa Mara na
kutembelea Kiwanda cha
Nguo cha Musoma Textile (MUTEX). Tarehe 2 hadi 4
Desemba 2011 nilifanya
ziara nyingine fupi Mkoa wa Mwanza na kutembelea
Kiwanda cha kutengeneza
Nguo cha Mwanza Textile (MWATEX). Kwa kweli
nilikuta Viwanda hivyo
vinakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo za
kukosekana kwa umeme wa
uhakika, Wataalam na teknolojia ya kisasa.
Nilielezwa kuwa
changamoto hizo zinavikabili Viwanda vingi vya Nguo Nchini.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
46. Sote hapa tunafahamu kuwa maendeleo
makubwa na ya kasi kwenye
Nchi mbalimbali
Ulimwenguni yalichangiwa kwa kiasi kikubwa na maendeleo ya
Viwanda vya Nguo na
Mavazi. Viwanda hivi hutoa Soko la uhakika kwa zao la
Pamba linalolimwa hapa
Nchini; huajiri kiasi kikubwa cha Wafanyakazi na
hivyo kuwa na mchango
mkubwa katika kupunguza tatizo la ajira na umaskini
hasa miongoni mwa Vijana.
Pia, huchangia Mapato kwa Serikali na Mifuko ya
Hifadhi ya Jamii.
Kutofanya vizuri kwa Viwanda hivi kunaikosesha Serikali
na Wananchi Mapato na
kuongeza tatizo la ajira Nchini. Niliona kuna umuhimu
wa kutafuta ufumbuzi wa
changamoto zilizo ndani ya uwezo wa Serikali.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
47. Tarehe 23 Machi 2012, niliitisha
Mkutano wa Wadau wa Sekta Ndogo
ya Viwanda vya Mavazi na
Nguo ili kwa pamoja tuweze kuainisha changamoto
zinazoikabili Sekta hiyo
na kupata mapendekezo ya namna ya kukabiliana na
changamoto hizo. Kufuatia
Mkutano huo, iliundwa Timu ya Wataalam ili iweze
kuangalia changamoto hizo
kwa kina na kutoa mapendekezo ya hatua za
kuchukuliwa na Serikali
pamoja na Wadau wote ili kukabiliana na changamoto
hizo. Timu hiyo ilipewa
mwezi mmoja na wakati wowote kuanzia sasa
itawasilisha taarifa yake
Serikalini.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
48. Tarehe 15 Aprili 2012, nilipata fursa ya
kutembelea viwanda
vya *Sunflag
(Tanzania) Ltd, *Kiwanda
cha *A to Z na Minjingu Mines and Fertilizer
Limited* vyote vya Mkoani
Arusha. Katika Viwanda vya Nguo vya *Sunflag* na *A
to Z* nilifarijika kuona
idadi kubwa ya Watumishi walioajiriwa na kwamba
zaidi ya Asilimia 80
walikuwa ni akina Mama. Nawapongeza Viongozi wa
Viwanda hivi kwa jitihada
ambazo wanazifanya kuendeleza uzalishaji na hivyo
kuchangia Mapato kwa
Serikali na Ajira kwa Wananchi.
* *
*Mheshimiwa Spika, *
49. Kiwanda cha *Sunflag* ni Kiwanda pekee
Nchini kinachozalisha nguo
kuanzia
hatua ya Pamba
kutoka kwa Mkulima hadi nguo
za kuvaa. *
Sunflag* wamekuwa ni Soko
zuri na la uhakika la Pamba ya
Wakulima.
Nawapongeza
kwa uamuzi wao huo ambao
una faida kubwa kwa Wakulima wa Pamba. Viongozi wa
Viwanda hivyo walinieleza
changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo.
Serikali itafanya kila
lililo ndani ya uwezo wake kuimarisha Viwanda
vinavyotumia pamba ya
Tanzania na kuweka mazingira yatakayoendelea kuvutia
uwekezaji katika Sekta
hii ya Nguo na Mavazi. Baada ya kupata taarifa ya
Timu niliyoitaja hapo
awali, Serikali itachukua hatua zitakazoondoa
changamoto zinazovikabili
Viwanda vya Nguo na Mavazi Nchini.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
50. Katika Kiwanda cha *Minjingu Mines and
Fertilizer
Limited*nilielezwa kuwa
wamefanikiwa kuzalisha mbolea ya
*Minjingu Mazao *ambayo
ni bora kuliko Mbolea aina ya DAP kwa kuwa ina
virutubisho vya Nitrogen,
Phosphorous, Sulphur, Calcium na rutuba kama
Magnesium, Zinc na
Boroni. Aidha, Minjingu Mazao ina bei ndogo kuliko DAP.
Kiwanda kwa sasa kina
akiba (*stock*) ya Tani 5,600 ya Phosphate na Tani
7,100 ya *Minjingu
Mazao*. Nilielezwa kuwa matumizi ya Mbolea ya Minjingu
Nchini yamekuwa
yakipungua mwaka hadi mwaka kutokana na matatizo mbalimbali
ikiwemo hujuma
inayofanywa kwenye Mfumo
wa Ruzuku za
Pembejeo.
Napenda kuhimiza Wizara
ya Kilimo, Chakula na Ushirika ione namna ya
kukikwamua Kiwanda cha
Minjingu kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu –
TAMISEMI ili kuongeza
matumizi ya mbolea za Minjingu.
*SENSA YA WATU NA MAKAZI
YA MWAKA 2012*
*Mheshimiwa Spika, *
51. Itakumbukwa kuwa Mheshimiwa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania wakati akitoa
hotuba yake ya kumaliza mwaka 2011 alitangaza rasmi
dhamira
ya Serikali kufanya Sensa ya Watu na Makazi ambayo imepangwa
kufanyika
Nchini
kote tarehe 26
Agosti 2012. Mheshimiwa Rais
alisisitiza kuwa
Sensa ya Watu na Makazi
pamoja na Vitambulisho vya Taifa ni mojawapo ya
vipaumbele vya Taifa kwa
mwaka huu wa 2012. Tarehe 12 Aprili 2012,
Waheshimiwa Wabunge
walipata fursa ya kuhudhuria Semina kuhusu Sensa ya
Watu na Makazi ya mwaka
2012. Katika Semina hiyo yalitolewa maelezo ya kina
kuhusu hatua iliyofikiwa
katika maandalizi ya Sensa ya Watu na Makazi. Nina
imani kuwa baada ya
Semina hiyo ya tarehe 12 Aprili 2012, hivi sasa
Waheshimiwa Wabunge wana
uelewa mpana kuhusu umuhimu wa taarifa zitokanazo
na Sensa na kwamba
watatumia uelewa huo kuwaelimisha Wananchi umuhimu wa
kujiandikisha.
*Mheshimiwa Spika, *
52. Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012
madhumuni yake makubwa ni
kupata takwimu kuhusiana
na idadi ya Watu na kukusanya Taarifa za kina za
Kiuchumi, Kijamii na
Maelezo ya Makazi. Taarifa hizi hutumiwa na Serikali
na Taasisi nyingine kwa
shughuli mbalimbali za Mipango na maendeleo.
Serikali pia hutumia
Takwimu zitokanazo na Sensa katika kutunga Sera,
kufanya maamuzi juu ya
Utawala wa Umma kwa kuzingatia mahitaji halisi na
vigezo vingine kama vile
umri, jinsia na vinginevyo.
*Mheshiwiwa Spika*,
53. Sensa
ya mwaka 2012
ina umuhimu wa
kipekee kwa kuwa
taarifa zitakazokusanywa
zitatumika kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa
Dira ya Taifa ya
Maendeleo ya Mwaka 2025 kwa Tanzania Bara na mwaka 2020
kwa Tanzania Zanzibar.
Vilevile, taarifa hizo zitatumika kutathmini Mkakati
wa Kukuza na Kupunguza
Umaskini Tanzania Bara (MKUKUTA) na Mkakati wa
Kupunguza Umaskini
Tanzania Zanzibar (MKUZA). Takwimu hizo zitatumika pia
kutathmini utekelezaji wa
Malengo ya Milenia ifikapo mwaka 2015; Mpango wa
Maendeleo wa Miaka Mitano
wa 2011/2012 – 2015/2016 pamoja na kubuni
mikakati ya utekelezaji
wa Mpango Elekezi wa Miaka 15 wa Utekelezaji wa
Dira ya Taifa ya
Maendeleo hadi mwaka 2025.
*Mheshimiwa Spika, *
54. Pamoja na maandalizi yanayoendelea hivi
sasa, mafanikio ya Sensa
yatategemea sana ushiriki
wa Umma na Wadau wengine. Sisi Waheshimiwa
Wabunge ni Wajumbe wa
Kamati za Sensa za Wilaya na Halmashauri zetu na moja
ya majukumu ya Kamati
hizo ni kuhamasisha na kuelimisha Umma kuhusu umuhimu
wa Sensa ya Watu na
Makazi ili kuhakikisha kuwa kila mtu atakayelala Nchini
*Usiku wa Kuamkia* siku
ya Sensa, yaani tarehe 25 Agosti 2012 *kuamkia
tarehe 26 Agosti 2012*,
anahesabiwa, na kwamba anahesabiwa mara moja tu.
*Mheshimiwa Spika, *
55. Zoezi* *hili ni la Kitaifa hivyo
linahitaji uhamasishaji na
ushirikishwaji wa
Wananchi wote. Natoa wito kwa Wananchi wote
kushiriki
kikamilifu katika zoezi
la Sensa ya Watu na Makazi na
kutoa ushirikiano
mkubwa kwa Makarani wa
Sensa watakaofanya kazi ya Kuhesabu Watu siku ya
tarehe 26 Agosti 2012.
Vilevile, naomba nitumie fursa hii kuwaomba
Waheshimiwa Wabunge
washirikiane na Viongozi wengine kusimamia
utekelezaji
wa shughuli zote za Sensa
katika Wilaya na Halmashauri kwa kuhakikisha kuwa
elimu kwa Wananchi
inatolewa. Nawaomba pia Waheshimiwa Wabunge kutumia
nafasi zao kama
Wawakilishi wa Wananchi kuhamasisha na
kuelimisha Umma
kuhusu umuhimu wa
kushirikiana na Makarani wa Sensa wakati wa kipindi cha
kuhesabu Watu kwa kutoa
Takwimu sahihi na hivyo kupata taarifa sahihi kwa
ajili ya Mipango endelevu
ya maendeleo. Kaulimbiu yetu kila wakati iwe
ni *Sensa
kwa Maendeleo ya Taifa:
Jiandae Kuhesabiwa. *Napenda kuwatakia mafanikio
mema katika kazi hii
muhimu kwa Taifa letu.
*MPANGO WA KUTOA KIFUTA
MACHOZI CHA MIFUGO *
* *
*Mheshimiwa Spika, *
56. Mwaka 2008/2009, Mikoa ya Kaskazini
hasa Mikoa ya Arusha na
Manyara ilikumbwa na
ukame mkubwa ambao ulisababisha Vifo kwa Mifugo.
Kutokana na ukubwa wa
tatizo hilo, Mheshimiwa Rais
aliahidi kutoa
Kifuta Machozi
kwa
kuwapatia Mifugo ya Mbegu
Wafugaji waliopoteza Mifugo yao yote katika
Wilaya za Longido,
Monduli na Ngorongoro. Katika kutekeleza Ahadi ya Rais,
Serikali iliunda Kikosi
Kazi ambacho kilibaini kuwepo kwa Vifo vya Ng’ombe *
403,839;* Mbuzi *211,201*
na Kondoo *121,118 *katika Wilaya hizo. Vilevile,
Kikosi Kazi kilibaini
kwamba jumla ya Kaya *6,127* katika Wilaya hizo
zilipoteza Mifugo
kutokana na ukame. Wilaya ya Longido ilikuwa na jumla ya
Kaya *2,852;* Monduli
Kaya *1,484* na Ngorongoro Kaya
*1,791*zilizoathirika na
ukame ulioambatana na Vifo na Mifugo.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
57. Katika mwaka 2011/2012, Serikali ilitoa
Tamko Bungeni kuhusu
kutekeleza ahadi ya kutoa
Kifuta Machozi kama mbegu (*seed stock*) kwa Kaya
zilizopoteza Mifugo yote
ili ziweze kurudi katika hali yao ya awali kama
Wafugaji. Aidha, Mradi
maalum ulianzishwa kwa ajili ya kununua Mifugo
(Ng’ombe na Mbuzi) kwa
ajili ya Wilaya husika. Ununuzi wa Mifugo hiyo
utafanyika katika ngazi
ya Halmashauri za Wilaya kwa kuzingatia Sheria ya
Manunuzi Na. 21 ya mwaka
2004.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
58. Kufuatia kuundwa kwa Kamati mbalimbali
(Mkoa, Halmashauri, Kata
na Vijiji za kusimamia
utekelezaji wa Mpango wa Kusambaza Mifugo ya Kifuta
Machozi, Halmashauri za
Wilaya zilielekezwa kutangaza zabuni za kuwapata
wanunuzi wa Mifugo ndani
ya maeneo ya Wilaya husika katika kipindi cha Siku
Tisini (90). Utekelezaji
wa Zoezi hili utafanyika kwa Awamu kulingana na
upatikanaji wa fedha.
Aidha, Awamu ya Kwanza itaanza kwa kununua Ng’ombe
500 kwa kila Wilaya.
Lengo ni kukamilisha zoezi hili kabla ya Kiangazi
kuanza.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
59. Napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu
kuwa Uzinduzi wa Mpango wa
kutoa Kifuta Machozi
ulifanywa na Mheshimiwa Rais, Dkt. Jakaya Mrisho
Kikwete tarehe 19
Februari 2012 katika Wilaya ya Longido ambapo Serikali
ilitumia Shilingi Milioni
*213* kwa kununua na kusambaza Ng’ombe 500.
60. Aidha, ununuzi wa Mifugo kwa ajili ya
Wilaya za Monduli na
Ngorongoro utakamilika
mara Serikali itakapokamilisha taratibu za kutuma
fedha kwa Halmashauri za
Wilaya hizo. Kiasi cha Shilingi Milioni *206
*zimetengwa
kwa ajili ya Wilaya ya
Monduli na Shilingi Milioni *218* kwa ajili ya
Wilaya ya Ngorongoro ili
kuwezesha ununuzi wa Ng’ombe 500 kwa kila Wilaya.
61. Matumaini yangu ni kuwa zoezi la kutoa
Kifuta Machozi kwa
Wananchi wa Wilaya za
Monduli na Ngorongoro litakamilika katika muda mfupi
ujao kwa kuwa Mifugo hiyo
ipo tayari kwa Wazabuni. Kinachosubiriwa ni
malipo ya fedha. Natoa
wito kwa Wafugaji na Wananchi walioathirika na ukame
ambao wanasubiri Awamu ya
Pili kuwa na subira wakati Serikali inatafuta
fedha za kutekeleza
Mpango huu.
*HITIMISHO*
* *
*Mheshimiwa Spika, *
62. Kabla ya kuhitimisha hotuba yangu,
napenda kusisitiza maeneo
muhimu yafuatayo:
*Kwanza*: Tumeanza
Mchakato wa Utekelezaji wa Sheria ya
Mabadiliko ya
Katiba. Mchakato ambao ni
Msingi wa Utawala Bora. Natoa wito kwamba,
Tuwaelimishe Wananchi
kuhusu Mambo ya Msingi wakati wa kuchangia Maoni, na
kwamba Mabadiliko ya
Katiba siyo Mchakato wa kuwepo au kutokuwepo kwa
Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
*Pili: *Tunayo Mifuko ya Hifadhi ya Jamii
ambayo tukiitumia vizuri,
ni kinga na kichocheo
muhimu cha Kuondoa Umaskini na Kukuza Uchumi.
Tushirikiane na Mamlaka
ya Hifadhi ya Jamii kuwaelimisha Wananchi kuhusu
umuhimu wa kujiunga na
Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa faida yao, kwani hivi
sasa haijalishi kama uko
kwenye Sekta Rasmi au Isiyo Rasmi.
*Tatu: *Bado tunazo changamoto nyingi katika
Sekta ya Elimu, hasa
katika Miundombinu na
Ubora wa Elimu kwa ujumla. Tushirikiane katika
kutekeleza Mikakati ya
kutuwezesha kuwa na Elimu Bora kwa Watoto wetu.
Tuwajengee utamaduni wa
kujiamini na kushiriki kikamilifu katika kuboresha
Miundombinu muhimu
kuanzia Shule za Msingi, Sekondari hadi Vyuo.
*Nne: *Kuwepo kwa Viwanda Nchini ni muhimu kwa
maendeleo yetu na
Uchumi wa Nchi. Pamoja na
changamoto zilizopo ni vizuri kuweka umuhimu wa
kutumia bidhaa
zinazozalishwa na Viwanda vyetu.
*Tano: *Tarehe 26 Agosti 2012 itakuwa ni Siku ya
Sensa ya Watu na Makazi
Nchini. Tuwahamasishe
Wananchi waelewe umuhimu wa kuhesabiwa siku hiyo na
utaratibu utakaotumika
ikiwa ni pamoja na kila Mtu kuhakikisha anahesabiwa
na kwamba anahesabiwa
mara moja tu.
*Mheshimiwa Spika,*
63. Tunapohitimisha Mkutano huu wa Saba,
pamoja na kumshukuru
Mwenyezi Mungu tunao
wajibu wa kiungwana kuwashukuru pia wote walioshiriki
katika kutoa huduma
muhimu katika kufanikisha Mkutano huu. Nitumie fursa
hii kutoa shukrani
za dhati kwako wewe Mheshimiwa
Spika kwa kutuongoza
vizuri na hatimaye kukamilisha
Vikao vyote kama ilivyopangwa. Vilevile,
namshukuru Naibu Spika
pamoja na Wenyeviti wa Bunge kwa kazi nzuri.
Niruhusu nimshukuru Dkt.
Thomas Kashilillah, Katibu wa Bunge na Wasaidizi
wake kwa kutuwezesha
kufanya kazi hii kwa ufanisi mkubwa. Niwashukuru pia
Wataalam wote ambao
mchango wao kwetu umekuwa ni muhimu sana. Niwashukuru
Askari, Madereva,
Wanahabari kwa kushiriki kikamilifu katika kufanikisha
Mkutano huu.* *
* *
*Mheshimiwa Spika,*
64. Leo tunapohitimisha Mkutano huu wa Saba,
tunapata fursa ya
kujiandaa kwa ajili ya
Mkutano wa Nane ambao ni Mahsusi kwa ajili ya Bajeti
ya Mwaka 2012/2013.
Napenda kuwatakia maandalizi mema kwa
ajili ya
Bajeti ya Serikali. Ni
dhahiri kwamba bado tuna changamoto nyingi. Nawasihi
kila mmoja wetu kujiwekea
malengo ya kutimiza wajibu wake katika kufikia
yale yote tunayoyatarajia
kuyafanya kwa ajili ya Maendeleo ya Nchi yetu.
Nimalizie kwa kuwatakia
nyote safari njema ya kurejea katika maeneo yenu ya
kazi.
* *
*Mheshimiwa Spika,*
65. Baada ya kusema haya, naomba kutoa hoja
kwamba Bunge lako Tukufu
liahirishwe hadi tarehe
*12 Juni 2012* Saa *3:00* *Asubuhi*, litakapokutana
kwenye Ukumbi huu hapa
Mjini Dodoma kujadili Bajeti ya Serikali.
66. *Mheshimiwa Spika, *naomba kutoa hoja.
*
COMMENTS