Serikali imesema itaendelea kufanya tathmini wakati wa utekelezaji wa Sera ya Wazee iliyoboreshwa ambayo ina tamko la kuwataka Watoto kuwaji...
Serikali imesema itaendelea kufanya tathmini wakati wa utekelezaji wa Sera ya Wazee iliyoboreshwa ambayo ina tamko la kuwataka Watoto kuwajibika kuwatunza Wazazi na endapo kutakuwa na umuhimu wa kuwepo na sheria maalum kwa Wazee wakati wa utekelezaji basi Wizara itaanzisha mchakato huo.
Kauli hiyo ya serikali imetolewa bungeni na Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wanawake na Makundi maalumu.
Serikali ilikuwa inajibu swali la mbunge wa Moshi Vijijini Profesa Patrick Ndakidemi akliyetaka kujua lini serikali itatunga sheria itakayojumuisha mtoto wa kuwatunza wazazi wake wakizeeka.
Aidha serikali katika majibu yake imesema pia itaendelea kuwalea na kuwapatia matunzo Wazee wasiojiweza ambao hawana familia na ndugu wa kuwatunza kupitia Makazi ya Wazee na Wasiojiweza 13 yanayomilikiwa na Serikali.
Matokeo ya Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 inaonyesha kuwa idadi ya watu wenye umri wa miaka 60 na zaidi ni 2,689,178 ambapo wanawake ni 1,446,808 na wanaume ni 1,242,370.
Wakati jumla ya idadi ya Watanzania kwa mujibu wa Sensa ya 2022 ni 61,741,120 ni asilimia 4.35
Mwaka 2015 tamko la wazee
Mwaka 2015 Chama cha Wastaafu na Wazee (CHAWAMU) mkoani Mtwara kiliitaka serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, kutatua changamoto zinazowakabili wazee ikiwa ni pamoja na kupitisha sera ya Taifa ya Wazee na kuwa na sheria.
Akizungumza mkoani humo, katibu wa chama hicho, Wilberd Nandonde, alisema sera hiyo ambayo ilitungwa toka mwaka 2003 bado haijawa sheria na ni muda mrefu umepita jambo ambalo linasababisha changamoto nyingi zinazowakabili kutofanyiwa kazi.
Kwanini swali limeulizwa?
Mbunge aliyeuliza swali hii ni msomi na majibu ya serikali yamekuwa yakisiasa mno kutokana na mazingira ya Tanzania yalivyo kwa sasa na takwimu za ukatili kwa wazee.
Ukijiuliza kwanini mbunge huyu kauliza swali kuhusu sheria ya kushurutisha matunzo Serikali na serikalikk nayo kusema itaendelea kufanya tathmini wakati wa utekelezaji wa Sera ya Wazee iliyoboreshwa ambayo ina tamko la kuwataka Watoto kuwajibika kuwatunza Wazazi na endapo kutakuwa na umuhimu wa kuwepo na sheria maalum kwa Wazee wakati wa utekelezaji basi Wizara itaanzisha mchakato huo, unaona upande wa pilik wa pazia lipo tatizo.
Kauli hiyo ya serikali ambayo imetolewa bungeni na Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wanawake na Makundi maalumu ikijibu swali la mbunge wa Moshi Vijijini Profesa Patrick Ndakidemi aliyetaka kujua lini serikali itatunga sheria itakayojumuisha mtoto wa kuwatunza wazazi wake wakizeeka, inatengeneza fikira kubwa hasa unapotembea mitaanik na kukuta kundi la ombaomba lenye umri mkubwa na wajukuu wao.
Ingawa serikali katika majibu yake imesema pia itaendelea kuwalea na kuwapatia matunzo Wazee wasiojiweza ambao hawana familia na ndugu wa kuwatunza kupitia Makazi ya Wazee na Wasiojiweza 13 yanayomilikiwa na Serikali, shida zilizopo sasa za mtu mmoja mmoja zinadai hatua za haraka za malezi ya jamii au serikali kuiongeza idadi ya nyumba za wazee.
Tukifanya uchambuzi kuna uwezekano mkubwa kwamba mbunge alikusudia kupata tamko la serikali kutokana na kudnelea kuzorota kwa mahusiano katika ngazi ya familia.
Ingawa asilimia ya wazee ni ndogo kwa sasa (4.35% kulingana na sensa ya 2022), idadi kamili ya wazee (2.6M+) ni kubwa, na kuna kundi la wazee wasiojiweza ambao hawana ndugu au familia ya kuwatunza, na wanategemea makazi ya serikali 13 tu. Hii inaweza kuwa haitoshi.
Aidha kuna kulegea kwa Mila na Desturi za Utunzaji ambapo Hapo zamani, utunzaji wa wazee ulikuwa jukumu la kiasili la familia na jamii. Lakini kutokana na mabadiliko ya kijamii, kama vile uhamiaji kutoka vijijini kwenda mijini, mabadiliko ya muundo wa familia, na changamoto za kiuchumi, baadhi ya familia huenda zinashindwa au hazitekelezi kikamilifu jukumu hili.
Kwangu mimi pia naona kama Mbunge anaweza kuwa anaona uhitaji wa kuimarisha ulinzi wa kisheria kwa wazee ili kuhakikisha wanapata matunzo stahiki, hasa wale wanaopuuzwa na watoto wao licha ya watoto kuwa na uwezo.
Lakini jambo jingine ambalo ni la kweli ikiwa wazee wengi wataishia kutegemea makazi ya serikali pekee, mzigo wa kifedha na kimatunzo kwa serikali utaongezeka. Sheria inaweza kusaidia kusambaza jukumu hilo kwa familia.
Wakati mwingine, watoto hupuuza wazazi wao wakiwa hai lakini huibuka kudai mali au urithi wanapofariki. Sheria ya matunzo inaweza kutoa msingi wa kisheria wa kushughulikia masuala hayo.
Pia swali hili la m bunge linaweza pia kuwa filimbi ya kutaka kama nchi kuanza Kujipanga kwa Kuzeeka kwa Jamii: Ikumbukwe kuwa Tanzania itaanza kushuhudia ongezeko la wazee katika miaka ijayo. Mbunge anaweza kuwa anaona mbele na kutaka sheria ziwe tayari kabla ya suala hilo kuanza kuwa changamoto kubwa zaidi.
Swali la mbunge linaweza pia kuwa ni njia ya kuunga mkono au kuimarisha tamko la Sera ya Wazee iliyoboreshwa, ambayo tayari inawataka watoto kuwajibika. Kuweka sheria kunaweza kutoa meno kwa tamko hilo.
Kwa kifupi, naamini mbunge anaweza kuwa anaangalia jinsi ya kuimarisha usalama wa kijamii na kiuchumi wa wazee nchini Tanzania, akizingatia mabadiliko ya kijamii na changamoto zinazowakabili.
mwisho
COMMENTS