Ijumaa iliyopita kwenye ukumbi wa New World Cinema kulikuwa na tafrija ya uzinduzi wa tuzo za filamu Tanzania – Vinara Film Award zitakazofa...
Ijumaa iliyopita kwenye ukumbi wa New World Cinema kulikuwa
na tafrija ya uzinduzi wa tuzo za filamu Tanzania – Vinara
Film Award zitakazofanyika Mei mwaka huu.
Tuzo za Vinara wa Filamu linaratibiwa na One Game
Promotions.Tuzo hizi zimesajiliwa kisheria na kutolewa
kibali na Baraza la Sanaa la Taifa Tanzania.
Mzinduaji wa tuzo hizo alikuwa mbunge wa Kinondoni Idd
Azzan ambaye aliwapasha vipande vyao watengeneza na wacheza
sinema wa bongo.
Tuzo hizo zinadhaminiwa na kampuni ya bia ya Breweries bidhaa yake ya Ndovu.
Utoaji tuzo za Vinara wa Filamu Tanzania, unalenga katika
kuifanya sanaa ya Tanzania kupata nguvu mpya na kuwafanya
watengenezaji na wadau sanaa kufanya bidii katika ushindani
wa soko la sanaa .
Tuzo za Vinara wa Filamu Tanzania pia zinalenga kuwafanya
wananchi kuendelea kuwa na mwamko wa kupenda kazi
zinazotengenezwa na Watanzania .
Pia zimelenga makundi mbalimbali ya wadau wa sekta ya
filamu katika nyanja mbalimbali wanaojitahidi kuinua sanaa
ya filamu nchini.
One Game Promotions imesema filamu zinazowajibika kwenye
tuzo hizi ni filamu ndefu (feature films) tu na
zilizokakuguliwa na Bodi ya Ukaguzi wa Filamu Tanzania. Na
ni zile tu ambazo zimetengenezwa katika Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania na Watanzania wenyewe au nje ya mipaka lakini
watengenezaji wakiwa ni Watanzania.
Fomu zitatolewa bure na zitapatikana katika ofisi za
waandaaji wa tuzo.Katika fomu hizo, kutaainishwa mambo
muhimu ambayo mtengenezaji wa filamu atapaswa kujaza.
Kama vile; Jina kamili la kampuni iliyotengeneza filamu au
video na anwani kamili, Jina la Mtayarishaji Mkuu wa filamu
(Executive Producer), Jina la Mtayarishaji wa filamu.
(Producer), Jina la Mtunzi wa hadithi (Story Writer), Jina
la Mwandishi wa skripti (Scriptwriter), Jina la Muongozaji
(Director), Jina la Mhariri (Editor), Majina kamili ya
wasanii wote waliyoigizia katika filamu husika
(Characters), Jina la Muongozaji wa Taa (Lightsman), Jina
la Mrekebishaji Sauti (Soundman), Jina la Mpiga Picha
(Cameraman), Jina la Meneja wa Mandhari (Location Manager),
Jina la Mpangiliaji wa Picha (Cinematographer), Jina la
Mtunzi wa Muziki (Music Composer), Jina la Studio
iliyofanya/zilizofanya kazi kwa filamu husika.Fomu itakuwa
na maswali mengine kama vile; filamu imetengenezwa lini ,
mahali ilikotengenezwa, maudhui ya filamu na lugha
iliyotumika.
Baada ya fomu hizo kujazwa kwa usahihi, zitatumwa kwenye
ofisi za waandaji, kwa mkono au njia ya posta kwa anuani
kamili ya waandaji. Watengenezaji wa filamu husika
watapaswa kuambatanisha na mkanda wa filamu (VHS/DVD/VCD).
Zoezi la utumaji fomu na kuzikusanya litaanza siku ya
tangazo la kwanza na kufungwa mwezi mmoja baadae.Shughuli
za utoaji tuzo, zitataambatana na burudani toka kwa wasanii
mbalimbali wa nchini watakaochaguliwa kutumbuiza na kupamba
shamrashamra hizo.
Kutakuwa na jopo la majaji wanane (8) watakaochaguliwa na
waandaji kwa kushirikiana na Baraza la sanaa la Taifa
nchini watakaokuwa na jukumu la kupitia filamu zote na
kuzitolea uamuzi.Filamu zitakazoingizwa kuwania tuzo ni
zile zilizotengenezwa na Watanzania kuanzia Januari 2007
hadi mwisho wa siku ya kualikwa watengenezaji kuingiza
filamu zao ambayo itakuwa Machi 31.
Tuzo zitatolewa katika vipengeke vifuatavyo:-Filamu Bora ya Mwaka, Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kiume,
Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kike, Muigizaji Bora Chipukizi
wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa
Kike, Mwongozaji Sinema Bora wa Mwaka, Mchekeshaji Bora wa
Mwaka, Mwandishi Bora wa Filamu, Mtunzi Bora wa Filamu,
Filamu Bora ya kutisha, Muigizaji Mwandamizii Bora wa kike
(supporting actor), Muigizaji Bora Mwandamizi wa Kike; Adui
Bora kwenye Filamu, imbo Bora wa Mwaka (Sound Track),
Mhariri Bora wa Filamu.
Pia itatolewa tuzo ya heshima kwa wale waliotoa machango
wao kukuza sanaa nchini.Zawadi zitahusisha vyeti na fedha
taslimu na mshindi atakuwa mmoja katika kila kipengele.
na tafrija ya uzinduzi wa tuzo za filamu Tanzania – Vinara
Film Award zitakazofanyika Mei mwaka huu.
Tuzo za Vinara wa Filamu linaratibiwa na One Game
Promotions.Tuzo hizi zimesajiliwa kisheria na kutolewa
kibali na Baraza la Sanaa la Taifa Tanzania.
Mzinduaji wa tuzo hizo alikuwa mbunge wa Kinondoni Idd
Azzan ambaye aliwapasha vipande vyao watengeneza na wacheza
sinema wa bongo.
Tuzo hizo zinadhaminiwa na kampuni ya bia ya Breweries bidhaa yake ya Ndovu.
Utoaji tuzo za Vinara wa Filamu Tanzania, unalenga katika
kuifanya sanaa ya Tanzania kupata nguvu mpya na kuwafanya
watengenezaji na wadau sanaa kufanya bidii katika ushindani
wa soko la sanaa .
Tuzo za Vinara wa Filamu Tanzania pia zinalenga kuwafanya
wananchi kuendelea kuwa na mwamko wa kupenda kazi
zinazotengenezwa na Watanzania .
Pia zimelenga makundi mbalimbali ya wadau wa sekta ya
filamu katika nyanja mbalimbali wanaojitahidi kuinua sanaa
ya filamu nchini.
One Game Promotions imesema filamu zinazowajibika kwenye
tuzo hizi ni filamu ndefu (feature films) tu na
zilizokakuguliwa na Bodi ya Ukaguzi wa Filamu Tanzania. Na
ni zile tu ambazo zimetengenezwa katika Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania na Watanzania wenyewe au nje ya mipaka lakini
watengenezaji wakiwa ni Watanzania.
Fomu zitatolewa bure na zitapatikana katika ofisi za
waandaaji wa tuzo.Katika fomu hizo, kutaainishwa mambo
muhimu ambayo mtengenezaji wa filamu atapaswa kujaza.
Kama vile; Jina kamili la kampuni iliyotengeneza filamu au
video na anwani kamili, Jina la Mtayarishaji Mkuu wa filamu
(Executive Producer), Jina la Mtayarishaji wa filamu.
(Producer), Jina la Mtunzi wa hadithi (Story Writer), Jina
la Mwandishi wa skripti (Scriptwriter), Jina la Muongozaji
(Director), Jina la Mhariri (Editor), Majina kamili ya
wasanii wote waliyoigizia katika filamu husika
(Characters), Jina la Muongozaji wa Taa (Lightsman), Jina
la Mrekebishaji Sauti (Soundman), Jina la Mpiga Picha
(Cameraman), Jina la Meneja wa Mandhari (Location Manager),
Jina la Mpangiliaji wa Picha (Cinematographer), Jina la
Mtunzi wa Muziki (Music Composer), Jina la Studio
iliyofanya/zilizofanya kazi kwa filamu husika.Fomu itakuwa
na maswali mengine kama vile; filamu imetengenezwa lini ,
mahali ilikotengenezwa, maudhui ya filamu na lugha
iliyotumika.
Baada ya fomu hizo kujazwa kwa usahihi, zitatumwa kwenye
ofisi za waandaji, kwa mkono au njia ya posta kwa anuani
kamili ya waandaji. Watengenezaji wa filamu husika
watapaswa kuambatanisha na mkanda wa filamu (VHS/DVD/VCD).
Zoezi la utumaji fomu na kuzikusanya litaanza siku ya
tangazo la kwanza na kufungwa mwezi mmoja baadae.Shughuli
za utoaji tuzo, zitataambatana na burudani toka kwa wasanii
mbalimbali wa nchini watakaochaguliwa kutumbuiza na kupamba
shamrashamra hizo.
Kutakuwa na jopo la majaji wanane (8) watakaochaguliwa na
waandaji kwa kushirikiana na Baraza la sanaa la Taifa
nchini watakaokuwa na jukumu la kupitia filamu zote na
kuzitolea uamuzi.Filamu zitakazoingizwa kuwania tuzo ni
zile zilizotengenezwa na Watanzania kuanzia Januari 2007
hadi mwisho wa siku ya kualikwa watengenezaji kuingiza
filamu zao ambayo itakuwa Machi 31.
Tuzo zitatolewa katika vipengeke vifuatavyo:-Filamu Bora ya Mwaka, Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kiume,
Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kike, Muigizaji Bora Chipukizi
wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa
Kike, Mwongozaji Sinema Bora wa Mwaka, Mchekeshaji Bora wa
Mwaka, Mwandishi Bora wa Filamu, Mtunzi Bora wa Filamu,
Filamu Bora ya kutisha, Muigizaji Mwandamizii Bora wa kike
(supporting actor), Muigizaji Bora Mwandamizi wa Kike; Adui
Bora kwenye Filamu, imbo Bora wa Mwaka (Sound Track),
Mhariri Bora wa Filamu.
Pia itatolewa tuzo ya heshima kwa wale waliotoa machango
wao kukuza sanaa nchini.Zawadi zitahusisha vyeti na fedha
taslimu na mshindi atakuwa mmoja katika kila kipengele.
COMMENTS