TFF mmekumbushwa simba ...fungeni mlango, au bado mpo mpo kwanza? Kauli ya Mheshimiwa Rais Juzi kwamba takrima ya Serikali kumlipia kocha wa...
TFF mmekumbushwa simba ...fungeni mlango, au bado mpo mpo kwanza?
Kauli ya Mheshimiwa Rais Juzi kwamba takrima ya Serikali kumlipia kocha wa timu ya taifa sio ya milele imeeleweka na ujumbe wake kwa TFF uko wazi na wala hauhitaji kushereheshwa.
Kauli hiyo ni ya muhimu kwa sababu TFF imehadharishwa mapema na wala huduma hazikusitishwa ghafla. Nionavyo, TFF inahitaji msaada wa mawazo na ushauri sasa hivi pengine kuliko wakati wowote uliopita, lakini TFF na yenyewe pia ione haja ya ninachokisema vinginevyo hesabu itakuja kujulikana wakati huo tutakuwa tayari tumeshachelewa.
Ningekuwa na uhakika wa Rais ajae katika awamu ya tano, walau nisingekuna kichwa kuifiria hoja hii ya leo ya TFF
kumuajiri kocha wa timu ya taifa kwa upana huu, lakini inaniwia ugumu kwa sababu mimi si mtabiri na hatima ya jambo hili naona iko mlangoni linakuja hata kama kesho hiyo ni 2015.
Kwa sasa pengine si muhimu sana kuyakariri mambo ambayo tumekuwa tukiyasema katika safu hii kuhusu haja na umuhimu wa shirikisho hili na vilabu hasa vya Simba na Yanga kijijengea uwezo. Tumezungumza sana na kilichotufanya tufanye vile na hata sasa ni kuwa viongozi hawa ni wa kupita hivyo wakivurunda tutabaki kuwalaumu tu kwa kutoweka misingi imara lakini ndio tutakuwa tumeumia kama taifa na wakati tutakapokuwa tunalaumu tutakuwa tayari tumeshachelewa. zitabaki stori.!
Kinachonipa wasiwasi ni utayari wa viongozi hawa kubadilika. hofu yangu si ya leo. Kuna wakati mmoja wa viongozi wake aliwahi kuulizwa wanawatumiaje wachezaji wa zamani kuwashauri wachezaji wa sasa katika timu ya Taifa? Alichojibu ndicho kilichinichosha. Alisema mchezaji wa zamani anayetaka kutoa ushauri aende TFF na wao watampangia kuzungumza. Ni sawa lakini hii kauli ya anayetaka? Mimi nilifikiri utartibu mzuri ungekuwa kuwaomba na hata kuwaalika badala ya kusema "anayetaka". anayevukwa nguo ndio huchutama. Kwa hili la TFF kuajiri kocha sia ajabu wakasema mwenye ushauri aje badala ya kuwaomba watu wachangie au kuwaalika kwenye mijadala. wote tunakumbuka jinsi King Kibadeni alivyotahadharisha kuhusu suala la kufix mechi na mambo ya rushwa. badala ya kumuuliza taratibu awape nondo wakaibuka na kauli. THIBITISHA. Jamani! hata huyo IGP mwenyewe na watu wake huwa hawaendi hivyo. matokeo yake wale wote wenye fununu na mambo ya rushwa katika michezo wamefunga midomo.
Bahati hii tuliyonayo ya kuwa na viongozi wanaopenda michezo na utamaduni ni muhimu tuitumie sasa. Juzi wakati mheshimiwa Rais analipotembelea Jengo la wamachinga na kusitisha kwa muda jukumu lile ili aone mazoezi ya timu ya Taifa walau kiduchu kwa wanaomfahamu Mheshimiwa Rais ni kitendo kile walikitegemea na wala hawakushangaa.
Yupo rafiki yangu mmoja aliniambia kuwa angeshangaa sana kama Rais asingeangalia angalau kwa sekunde mazoezi yale. Huyu ni Rais mwanamichezo aliyecheza na anayependa michezo. Waliokuwepo hapa jijini wakati Yanga inatoka kampala mwaka 1993 wanakumbuka. Ule uwanja wa ndani na basketball na kadhalika na kadhalika. Lakini ni lazima tukiri kuwa huyu ni Rais mpenda michezo yote na ndio maana imefika wakati sasa aangalie kusaidia michezo mingine. Wale wa riadha na wenyewe wajiandae wasiwe kama TFF ambao mbali ya kupewa ofa ya kumtafuta Kocha iliwachukua miezi kupeleka mapendekezo.
Wakati TFF inaangalia suala hili ni vyema pia itatumia fursa ilizonazo. Kwa kipindi kirefu ambacho Maximo anakuwa hayuko timu ya Taifa sijui wanamtumiaje. Kama hana cha kufanya au hajaambiwa kitu cha kufanya sia ajabu akatumia muda huo kuogelea kule ufukwe wa kigamboni. Mimi nilikuwa nafikiri kwa kuwa tumeletewa kocha kwa kweli tungemtumia kwelikweli. Atufundishie hata makocha wetu. Atoe mihadhara. Yawepo makongamano ya watu kujadili soka. Vyombo vya habari vikiombwa na kwa jinsi walivyo wanamichezo watakubali. Mbona watu walisaidia kampeni za Serengeti Boys inagwa baaadaye ikawa ndio zetu....! TFF ianze kujenga uwezo wa makocha wetu wa ndani kwa kutumia hawa kina Tonoko waliopo. Huyu Bushiri peke yake hawezi kuchukua ujuzi wote unahitajika mpango mkakati.
Lipo suala la viiingilio. Hili linasemwa kila kukicha. Vile viti vya kijani huwa havijai lakini watu wanashindwa kwenda kule kwa sababu ya bei. Lakini ni watu wanaokaa kwenye viti vile ndio wanaoshangilia timu muda wote. Waliokuwepo siku ya mechi na Black Stars ya Ghana waliona jinsi wale Waghana wachache waliokuwa pale viti vya bluu- VIP C walivyonyamazisha umati wa mashabiki. Kidoogo mzee Magoma moto ndio alikuwa anaenda nao sanjari. Sasa kama upangaji wa viingilio utakuwa haungalii siku ya mechi, muda wala tarehe katika mwezi ipo hatari kila siku shirikisho hili litasema linakula hasara.
Wakati huu TFF ni vyema waanze kujipanga pamoja na vyama vyao vya mikoa ili kuona ni jinsi gani watakuwa na udhamini wa maana au kuwa na mradi wa kudumu ambao utakuwa endelevu. Hii habari ya kutegemea makusanyo ya fedha za milangoni na malumbano haya mnayoendelea nayo na baadhi ya vilabu si ajabu wenye timu zao wakasusa kuja uwanjani hata kama uamuzi wao hautakuwa sahihi lakini watakuwa wamejeruhi mapato.
Wapo wanaonufaika na uuzwaji wa bidhaa za nembo ya Taifa na timu ya Taifa. Suala hili inaonekana kama halina mwenyewe au inaonekana kama ni biashara ya uchuuzi isiyo na tijara. Si kweli wati wananunua fulana na kofia kwa elfu kumi mpaka ishirini. Sisi tunasema TFF itoe zabuni za watu kutengeneza iuze hapa na mikoani. Pengine huu ni mradi usio na malipo lakini nenda pale jiji la Torino au tembelea Venice uona jinsi jezi za timu za Taifa zilivyo na bei ghali. Sisi hapa hiyo hatuna pengine tunaona huo ni umachinga.
Tulishawahi kusema kuhusu uwanja wa Karume lakini wapi. Kwa sasa wafadhili wa maana wameanza kujitokeza na pengine huu ndio wakati muafaka. Waambieni wawafundishe kuvua samaki badala ya kuwapa changu au vibua mnaposikia njaa. Jengeni basi uwanja wa maana mkubwa ambao mtakuwa na kitega uchumi chenu cha muda mrefu. Pengine hili nalo ni la muda mrefu sio dili kwa sababu uongozi wenyewe wa chama ni wa muda mfupi.
Basi alikeni timu za nje ziwe zinakuja hapa. Mbona kaka yangu Kadata alikuwa anazileta hapa timu za Zambia. Hili na lenyewe pengine lina usumbufu na kuogopa kula hasara.
Kama TFF inataka kuwa imara kimapato na kama alivyosema Mheshimiwa Rais mkiwa na uwezo mnaziepusha kuingiliwa katika maamuzi. TFF inapaswa kufikiria mara mbilmbui kuhusu mustakibara wake. TFF inahitaji viongozi watakaokuwa wanfikiria hatima ya nchi na sio hatima yao. Kina marehemu mzee Mangara wanakumbukwa leo kwa sababu waliifirikia zaidi Yanga kuliko walivyojifikiria wenyewe. Leo hii tunawakumbuka kwa hayo.
Kuna wakati niliwahi kuongea na kiongozi mmoja wa mpira nikamuambia mbona Dar inabaki kavu wikiendi zote hamna mechi mpaka au mpaka ligi ianze akaniambia aah maganga kama umeingia vichwani mwetu. Kuanzia mwezi ujao mechi itakuwa kila wiki. Leo hii nikimuona nitamshika masikio yake ni mwaka sasa. Wakati mwingine wala haihitaji kuapia ili ujue kama yapo mabadiliko ya dhati au changa la macho. Ni kwa matendo. Sijui kama TFF ipo tayari kwa hili. Huu ndio mtazamo wangu finyu. Siku njema.
Kauli ya Mheshimiwa Rais Juzi kwamba takrima ya Serikali kumlipia kocha wa timu ya taifa sio ya milele imeeleweka na ujumbe wake kwa TFF uko wazi na wala hauhitaji kushereheshwa.
Kauli hiyo ni ya muhimu kwa sababu TFF imehadharishwa mapema na wala huduma hazikusitishwa ghafla. Nionavyo, TFF inahitaji msaada wa mawazo na ushauri sasa hivi pengine kuliko wakati wowote uliopita, lakini TFF na yenyewe pia ione haja ya ninachokisema vinginevyo hesabu itakuja kujulikana wakati huo tutakuwa tayari tumeshachelewa.
Ningekuwa na uhakika wa Rais ajae katika awamu ya tano, walau nisingekuna kichwa kuifiria hoja hii ya leo ya TFF
kumuajiri kocha wa timu ya taifa kwa upana huu, lakini inaniwia ugumu kwa sababu mimi si mtabiri na hatima ya jambo hili naona iko mlangoni linakuja hata kama kesho hiyo ni 2015.
Kwa sasa pengine si muhimu sana kuyakariri mambo ambayo tumekuwa tukiyasema katika safu hii kuhusu haja na umuhimu wa shirikisho hili na vilabu hasa vya Simba na Yanga kijijengea uwezo. Tumezungumza sana na kilichotufanya tufanye vile na hata sasa ni kuwa viongozi hawa ni wa kupita hivyo wakivurunda tutabaki kuwalaumu tu kwa kutoweka misingi imara lakini ndio tutakuwa tumeumia kama taifa na wakati tutakapokuwa tunalaumu tutakuwa tayari tumeshachelewa. zitabaki stori.!
Kinachonipa wasiwasi ni utayari wa viongozi hawa kubadilika. hofu yangu si ya leo. Kuna wakati mmoja wa viongozi wake aliwahi kuulizwa wanawatumiaje wachezaji wa zamani kuwashauri wachezaji wa sasa katika timu ya Taifa? Alichojibu ndicho kilichinichosha. Alisema mchezaji wa zamani anayetaka kutoa ushauri aende TFF na wao watampangia kuzungumza. Ni sawa lakini hii kauli ya anayetaka? Mimi nilifikiri utartibu mzuri ungekuwa kuwaomba na hata kuwaalika badala ya kusema "anayetaka". anayevukwa nguo ndio huchutama. Kwa hili la TFF kuajiri kocha sia ajabu wakasema mwenye ushauri aje badala ya kuwaomba watu wachangie au kuwaalika kwenye mijadala. wote tunakumbuka jinsi King Kibadeni alivyotahadharisha kuhusu suala la kufix mechi na mambo ya rushwa. badala ya kumuuliza taratibu awape nondo wakaibuka na kauli. THIBITISHA. Jamani! hata huyo IGP mwenyewe na watu wake huwa hawaendi hivyo. matokeo yake wale wote wenye fununu na mambo ya rushwa katika michezo wamefunga midomo.
Bahati hii tuliyonayo ya kuwa na viongozi wanaopenda michezo na utamaduni ni muhimu tuitumie sasa. Juzi wakati mheshimiwa Rais analipotembelea Jengo la wamachinga na kusitisha kwa muda jukumu lile ili aone mazoezi ya timu ya Taifa walau kiduchu kwa wanaomfahamu Mheshimiwa Rais ni kitendo kile walikitegemea na wala hawakushangaa.
Yupo rafiki yangu mmoja aliniambia kuwa angeshangaa sana kama Rais asingeangalia angalau kwa sekunde mazoezi yale. Huyu ni Rais mwanamichezo aliyecheza na anayependa michezo. Waliokuwepo hapa jijini wakati Yanga inatoka kampala mwaka 1993 wanakumbuka. Ule uwanja wa ndani na basketball na kadhalika na kadhalika. Lakini ni lazima tukiri kuwa huyu ni Rais mpenda michezo yote na ndio maana imefika wakati sasa aangalie kusaidia michezo mingine. Wale wa riadha na wenyewe wajiandae wasiwe kama TFF ambao mbali ya kupewa ofa ya kumtafuta Kocha iliwachukua miezi kupeleka mapendekezo.
Wakati TFF inaangalia suala hili ni vyema pia itatumia fursa ilizonazo. Kwa kipindi kirefu ambacho Maximo anakuwa hayuko timu ya Taifa sijui wanamtumiaje. Kama hana cha kufanya au hajaambiwa kitu cha kufanya sia ajabu akatumia muda huo kuogelea kule ufukwe wa kigamboni. Mimi nilikuwa nafikiri kwa kuwa tumeletewa kocha kwa kweli tungemtumia kwelikweli. Atufundishie hata makocha wetu. Atoe mihadhara. Yawepo makongamano ya watu kujadili soka. Vyombo vya habari vikiombwa na kwa jinsi walivyo wanamichezo watakubali. Mbona watu walisaidia kampeni za Serengeti Boys inagwa baaadaye ikawa ndio zetu....! TFF ianze kujenga uwezo wa makocha wetu wa ndani kwa kutumia hawa kina Tonoko waliopo. Huyu Bushiri peke yake hawezi kuchukua ujuzi wote unahitajika mpango mkakati.
Lipo suala la viiingilio. Hili linasemwa kila kukicha. Vile viti vya kijani huwa havijai lakini watu wanashindwa kwenda kule kwa sababu ya bei. Lakini ni watu wanaokaa kwenye viti vile ndio wanaoshangilia timu muda wote. Waliokuwepo siku ya mechi na Black Stars ya Ghana waliona jinsi wale Waghana wachache waliokuwa pale viti vya bluu- VIP C walivyonyamazisha umati wa mashabiki. Kidoogo mzee Magoma moto ndio alikuwa anaenda nao sanjari. Sasa kama upangaji wa viingilio utakuwa haungalii siku ya mechi, muda wala tarehe katika mwezi ipo hatari kila siku shirikisho hili litasema linakula hasara.
Wakati huu TFF ni vyema waanze kujipanga pamoja na vyama vyao vya mikoa ili kuona ni jinsi gani watakuwa na udhamini wa maana au kuwa na mradi wa kudumu ambao utakuwa endelevu. Hii habari ya kutegemea makusanyo ya fedha za milangoni na malumbano haya mnayoendelea nayo na baadhi ya vilabu si ajabu wenye timu zao wakasusa kuja uwanjani hata kama uamuzi wao hautakuwa sahihi lakini watakuwa wamejeruhi mapato.
Wapo wanaonufaika na uuzwaji wa bidhaa za nembo ya Taifa na timu ya Taifa. Suala hili inaonekana kama halina mwenyewe au inaonekana kama ni biashara ya uchuuzi isiyo na tijara. Si kweli wati wananunua fulana na kofia kwa elfu kumi mpaka ishirini. Sisi tunasema TFF itoe zabuni za watu kutengeneza iuze hapa na mikoani. Pengine huu ni mradi usio na malipo lakini nenda pale jiji la Torino au tembelea Venice uona jinsi jezi za timu za Taifa zilivyo na bei ghali. Sisi hapa hiyo hatuna pengine tunaona huo ni umachinga.
Tulishawahi kusema kuhusu uwanja wa Karume lakini wapi. Kwa sasa wafadhili wa maana wameanza kujitokeza na pengine huu ndio wakati muafaka. Waambieni wawafundishe kuvua samaki badala ya kuwapa changu au vibua mnaposikia njaa. Jengeni basi uwanja wa maana mkubwa ambao mtakuwa na kitega uchumi chenu cha muda mrefu. Pengine hili nalo ni la muda mrefu sio dili kwa sababu uongozi wenyewe wa chama ni wa muda mfupi.
Basi alikeni timu za nje ziwe zinakuja hapa. Mbona kaka yangu Kadata alikuwa anazileta hapa timu za Zambia. Hili na lenyewe pengine lina usumbufu na kuogopa kula hasara.
Kama TFF inataka kuwa imara kimapato na kama alivyosema Mheshimiwa Rais mkiwa na uwezo mnaziepusha kuingiliwa katika maamuzi. TFF inapaswa kufikiria mara mbilmbui kuhusu mustakibara wake. TFF inahitaji viongozi watakaokuwa wanfikiria hatima ya nchi na sio hatima yao. Kina marehemu mzee Mangara wanakumbukwa leo kwa sababu waliifirikia zaidi Yanga kuliko walivyojifikiria wenyewe. Leo hii tunawakumbuka kwa hayo.
Kuna wakati niliwahi kuongea na kiongozi mmoja wa mpira nikamuambia mbona Dar inabaki kavu wikiendi zote hamna mechi mpaka au mpaka ligi ianze akaniambia aah maganga kama umeingia vichwani mwetu. Kuanzia mwezi ujao mechi itakuwa kila wiki. Leo hii nikimuona nitamshika masikio yake ni mwaka sasa. Wakati mwingine wala haihitaji kuapia ili ujue kama yapo mabadiliko ya dhati au changa la macho. Ni kwa matendo. Sijui kama TFF ipo tayari kwa hili. Huu ndio mtazamo wangu finyu. Siku njema.
COMMENTS