Maganga Feruzi wa The Football anasemaje?

TFF mmekumbushwa simba ...fungeni mlango, au bado mpo mpo kwanza? Kauli ya Mheshimiwa Rais Juzi kwamba takrima ya Serikali kumlipia kocha wa...

TFF mmekumbushwa simba ...fungeni mlango, au bado mpo mpo kwanza?

Kauli ya Mheshimiwa Rais Juzi kwamba takrima ya Serikali kumlipia kocha wa timu ya taifa sio ya milele imeeleweka na ujumbe wake kwa TFF uko wazi na wala hauhitaji kushereheshwa.

Kauli hiyo ni ya muhimu kwa sababu TFF imehadharishwa mapema na wala huduma hazikusitishwa ghafla. Nionavyo, TFF inahitaji msaada wa mawazo na ushauri sasa hivi pengine kuliko wakati wowote uliopita, lakini TFF na yenyewe pia ione haja ya ninachokisema vinginevyo hesabu itakuja kujulikana wakati huo tutakuwa tayari tumeshachelewa.

Ningekuwa na uhakika wa Rais ajae katika awamu ya tano, walau nisingekuna kichwa kuifiria hoja hii ya leo ya TFF
kumuajiri kocha wa timu ya taifa kwa upana huu, lakini inaniwia ugumu kwa sababu mimi si mtabiri na hatima ya jambo hili naona iko mlangoni linakuja hata kama kesho hiyo ni 2015.

Kwa sasa pengine si muhimu sana kuyakariri mambo ambayo tumekuwa tukiyasema katika safu hii kuhusu haja na umuhimu wa shirikisho hili na vilabu hasa vya Simba na Yanga kijijengea uwezo. Tumezungumza sana na kilichotufanya tufanye vile na hata sasa ni kuwa viongozi hawa ni wa kupita hivyo wakivurunda tutabaki kuwalaumu tu kwa kutoweka misingi imara lakini ndio tutakuwa tumeumia kama taifa na wakati tutakapokuwa tunalaumu tutakuwa tayari tumeshachelewa. zitabaki stori.!

Kinachonipa wasiwasi ni utayari wa viongozi hawa kubadilika. hofu yangu si ya leo. Kuna wakati mmoja wa viongozi wake aliwahi kuulizwa wanawatumiaje wachezaji wa zamani kuwashauri wachezaji wa sasa katika timu ya Taifa? Alichojibu ndicho kilichinichosha. Alisema mchezaji wa zamani anayetaka kutoa ushauri aende TFF na wao watampangia kuzungumza. Ni sawa lakini hii kauli ya anayetaka? Mimi nilifikiri utartibu mzuri ungekuwa kuwaomba na hata kuwaalika badala ya kusema "anayetaka". anayevukwa nguo ndio huchutama. Kwa hili la TFF kuajiri kocha sia ajabu wakasema mwenye ushauri aje badala ya kuwaomba watu wachangie au kuwaalika kwenye mijadala. wote tunakumbuka jinsi King Kibadeni alivyotahadharisha kuhusu suala la kufix mechi na mambo ya rushwa. badala ya kumuuliza taratibu awape nondo wakaibuka na kauli. THIBITISHA. Jamani! hata huyo IGP mwenyewe na watu wake huwa hawaendi hivyo. matokeo yake wale wote wenye fununu na mambo ya rushwa katika michezo wamefunga midomo.


Bahati hii tuliyonayo ya kuwa na viongozi wanaopenda michezo na utamaduni ni muhimu tuitumie sasa. Juzi wakati mheshimiwa Rais analipotembelea Jengo la wamachinga na kusitisha kwa muda jukumu lile ili aone mazoezi ya timu ya Taifa walau kiduchu kwa wanaomfahamu Mheshimiwa Rais ni kitendo kile walikitegemea na wala hawakushangaa.

Yupo rafiki yangu mmoja aliniambia kuwa angeshangaa sana kama Rais asingeangalia angalau kwa sekunde mazoezi yale. Huyu ni Rais mwanamichezo aliyecheza na anayependa michezo. Waliokuwepo hapa jijini wakati Yanga inatoka kampala mwaka 1993 wanakumbuka. Ule uwanja wa ndani na basketball na kadhalika na kadhalika. Lakini ni lazima tukiri kuwa huyu ni Rais mpenda michezo yote na ndio maana imefika wakati sasa aangalie kusaidia michezo mingine. Wale wa riadha na wenyewe wajiandae wasiwe kama TFF ambao mbali ya kupewa ofa ya kumtafuta Kocha iliwachukua miezi kupeleka mapendekezo.

Wakati TFF inaangalia suala hili ni vyema pia itatumia fursa ilizonazo. Kwa kipindi kirefu ambacho Maximo anakuwa hayuko timu ya Taifa sijui wanamtumiaje. Kama hana cha kufanya au hajaambiwa kitu cha kufanya sia ajabu akatumia muda huo kuogelea kule ufukwe wa kigamboni. Mimi nilikuwa nafikiri kwa kuwa tumeletewa kocha kwa kweli tungemtumia kwelikweli. Atufundishie hata makocha wetu. Atoe mihadhara. Yawepo makongamano ya watu kujadili soka. Vyombo vya habari vikiombwa na kwa jinsi walivyo wanamichezo watakubali. Mbona watu walisaidia kampeni za Serengeti Boys inagwa baaadaye ikawa ndio zetu....! TFF ianze kujenga uwezo wa makocha wetu wa ndani kwa kutumia hawa kina Tonoko waliopo. Huyu Bushiri peke yake hawezi kuchukua ujuzi wote unahitajika mpango mkakati.


Lipo suala la viiingilio. Hili linasemwa kila kukicha. Vile viti vya kijani huwa havijai lakini watu wanashindwa kwenda kule kwa sababu ya bei. Lakini ni watu wanaokaa kwenye viti vile ndio wanaoshangilia timu muda wote. Waliokuwepo siku ya mechi na Black Stars ya Ghana waliona jinsi wale Waghana wachache waliokuwa pale viti vya bluu- VIP C walivyonyamazisha umati wa mashabiki. Kidoogo mzee Magoma moto ndio alikuwa anaenda nao sanjari. Sasa kama upangaji wa viingilio utakuwa haungalii siku ya mechi, muda wala tarehe katika mwezi ipo hatari kila siku shirikisho hili litasema linakula hasara.

Wakati huu TFF ni vyema waanze kujipanga pamoja na vyama vyao vya mikoa ili kuona ni jinsi gani watakuwa na udhamini wa maana au kuwa na mradi wa kudumu ambao utakuwa endelevu. Hii habari ya kutegemea makusanyo ya fedha za milangoni na malumbano haya mnayoendelea nayo na baadhi ya vilabu si ajabu wenye timu zao wakasusa kuja uwanjani hata kama uamuzi wao hautakuwa sahihi lakini watakuwa wamejeruhi mapato.

Wapo wanaonufaika na uuzwaji wa bidhaa za nembo ya Taifa na timu ya Taifa. Suala hili inaonekana kama halina mwenyewe au inaonekana kama ni biashara ya uchuuzi isiyo na tijara. Si kweli wati wananunua fulana na kofia kwa elfu kumi mpaka ishirini. Sisi tunasema TFF itoe zabuni za watu kutengeneza iuze hapa na mikoani. Pengine huu ni mradi usio na malipo lakini nenda pale jiji la Torino au tembelea Venice uona jinsi jezi za timu za Taifa zilivyo na bei ghali. Sisi hapa hiyo hatuna pengine tunaona huo ni umachinga.


Tulishawahi kusema kuhusu uwanja wa Karume lakini wapi. Kwa sasa wafadhili wa maana wameanza kujitokeza na pengine huu ndio wakati muafaka. Waambieni wawafundishe kuvua samaki badala ya kuwapa changu au vibua mnaposikia njaa. Jengeni basi uwanja wa maana mkubwa ambao mtakuwa na kitega uchumi chenu cha muda mrefu. Pengine hili nalo ni la muda mrefu sio dili kwa sababu uongozi wenyewe wa chama ni wa muda mfupi.

Basi alikeni timu za nje ziwe zinakuja hapa. Mbona kaka yangu Kadata alikuwa anazileta hapa timu za Zambia. Hili na lenyewe pengine lina usumbufu na kuogopa kula hasara.

Kama TFF inataka kuwa imara kimapato na kama alivyosema Mheshimiwa Rais mkiwa na uwezo mnaziepusha kuingiliwa katika maamuzi. TFF inapaswa kufikiria mara mbilmbui kuhusu mustakibara wake. TFF inahitaji viongozi watakaokuwa wanfikiria hatima ya nchi na sio hatima yao. Kina marehemu mzee Mangara wanakumbukwa leo kwa sababu waliifirikia zaidi Yanga kuliko walivyojifikiria wenyewe. Leo hii tunawakumbuka kwa hayo.

Kuna wakati niliwahi kuongea na kiongozi mmoja wa mpira nikamuambia mbona Dar inabaki kavu wikiendi zote hamna mechi mpaka au mpaka ligi ianze akaniambia aah maganga kama umeingia vichwani mwetu. Kuanzia mwezi ujao mechi itakuwa kila wiki. Leo hii nikimuona nitamshika masikio yake ni mwaka sasa. Wakati mwingine wala haihitaji kuapia ili ujue kama yapo mabadiliko ya dhati au changa la macho. Ni kwa matendo. Sijui kama TFF ipo tayari kwa hili. Huu ndio mtazamo wangu finyu. Siku njema.

COMMENTS

Name

Anga,12,Arusha,27,batiki,1,Burudani,447,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,287,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,3,Habari,7054,habari dodoma,39,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,23,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,6,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,739,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,376,muziki na fasheni,20,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,9,SAYANSI ANGA,12,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,17,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Maganga Feruzi wa The Football anasemaje?
Maganga Feruzi wa The Football anasemaje?
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2008/08/maganga-feruzi-wa-football-anasemaje.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2008/08/maganga-feruzi-wa-football-anasemaje.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy