Nimerejea Dar es salaam baada ya kufanya ziara ya kikazi vijijini katika wilaya zote za mkoa wa Iringa na Ruvuma. Ilikuwa safari ambayo imen...
Nimerejea Dar es salaam baada ya kufanya ziara ya kikazi vijijini katika wilaya zote za mkoa wa Iringa na Ruvuma. Ilikuwa safari ambayo imenifumbua macho sana kuhusu maisha ya watu wetu huko vijijini.
Nasema imenifumbua macho kwa kuwa hakuna sababu ya msingi ya watu wa nchi hii kuwa maskini kiasi cha kuomba ruzuku na kuishi katika mazingira magumu.
safari zangu za vijiji zilinipeleka mpaka katika makao makuu ya wilaya ambako nako nilikutana na watawala ambao wenginje nilikuwa najiuliza kama kweli walikuwa wanastahili kuendelea kubaki serikalini.
Wapo watu ambao nadhani wapo wapo tu hakuna kitu kabisa.
Nasema hakuna kitu kabisa kwa sababu inakuwaje waraka wa serikali ulitolewa mwezi wa pili wa kuainisha wakulima na mahitaji yao ili kutoa nafasi serikali kuangalia uwezo wa ruzuku haujatekelezwa kwa muda wote huo mpaka msimu wa kilimo unakaribia.
Inakuwaje watumishi wa serikali wanaojua ukweli wa uwezo wa serikali wanafanya masikhara kwa kuingiza siasa na kuonekana hata hawajui ilani inayowaongoza na kisha wanamuuliza mtu wa kilimo umeniletea tani ngapi za ruzuku na watu wangapi safari hii watanufaika na ruzuku, mbona hii ruzuku ni kidogo ... mbona haya masharti mapya siwezi kuyasimamia ...na wakulima wengi ... yaani maneno mengine bwana yanadhihirisha ufinyu wa fikira kwa viongozi.
naam viongozi wengi nawabondea na hata wataalamu ambao wanashindwa kuwashawishi wakulima kutumia vyema raslimali walizonazo nao nawabondea bure tupu.
Naam na wananchi nao Mungu wangu wamekalia utajiri lakini wabishi wanaotaka vya bure na ukisomeshwa unasema si serikali ifanye yenyewe. Yaani pori mpaka karibu na nyumba yako unataka serikali ije ipalilie miembe na mikorosho ambayo iko uani mwako?
Unapata fedha za tumbaku na kahawa halafu unaishia kununua mipombe kudhihirisha umaarufu wako lakini nyumba ya bati huna.
Udongo unafaa kupata matofali ya kuchoma unataka serikali ije ikuchomee? Yaani bure aghali.
Ukitoka Tunduru kwenda masasi Lindi dar es salaamn njia nzima unaona dhahiri kwamba siasa ni korosho. lakini hakuna palizi, watu wanachoma moto kama palizi, hii inakuwaje hasa. halafu maneno mengi hata hao viongozi wenyewe nao matatizo, wana maneno kuliko vitendo.ndipo unapogundua kwanini tunahitaji azimio la iringa,Azimio la Musoma na hata la Arusha.
haki ya nani kama ndivyo hivi basi maisha ya dauni tauni ni bonge la atifisho na itatuchukua miaka milioni moja kubadili maisha yetu.
Tunaanzia wapi kuwabadili watanzania hawa ambao hawataki kushiriki katika ujenzi wa taifa kisayansi, uchawi, woga wa kubanwa na ujanja wa watu waliosoma wanaoiba? Mafisadi wapo wa aina nyingine, mbolea ya ruzuku imebadilishiwa mbinu za kumfikia mkulima viongozi hawajaelewa somo, wengine wanasema ukweli viongozi ndio waliokuwa wanachikichia mbolea ya ruzuku... basi mambo mashala kwelikweli.
Angalia mambo ambayo yanaweza kuwa na utalii watu wamebana tu kama hawajui. Nasikia hawa wabunge wakifika hutawaona tena.
Ofisi za wabunge wa Mafinga zimefungwa siku zote anasema mfanyakazi mmoja wa hapo. Watu wa kilimo wametoa taarifa ya kwenda kuzungumzia masuala ya kilimo na wahimizaji wabunge, tazama nimekuwa na watu wa wizara njia nzima katika mikoa miwili, Madc tu labda walionekana, wabunge waliingia mitini lakini wa Mafinga tuliambiwa hawajawahi kujitokeza katika ofisi zao.
hayo mambo, halafu ikifika mwezi Novemba wanasema salfa haikuwafikia wakulima wetu, wakulima gani ambao hujafika hata kutoa salamu angalau ukahimiza wasipalilie kwa kutumia moto na waache ujinga wa pom,be na kuoa na kutaliki waangalie mambo yao ya kiuchumi kwa kuwa fedha wanazo?
Mimi nasema kama kweli tunataka mabadiliko basi huku kunahitajika mapinduzi ya fikira na waliona dhamana basi wajitahidi lakini wasiketi dar pekee.
lukwangule
Nasema imenifumbua macho kwa kuwa hakuna sababu ya msingi ya watu wa nchi hii kuwa maskini kiasi cha kuomba ruzuku na kuishi katika mazingira magumu.
safari zangu za vijiji zilinipeleka mpaka katika makao makuu ya wilaya ambako nako nilikutana na watawala ambao wenginje nilikuwa najiuliza kama kweli walikuwa wanastahili kuendelea kubaki serikalini.
Wapo watu ambao nadhani wapo wapo tu hakuna kitu kabisa.
Nasema hakuna kitu kabisa kwa sababu inakuwaje waraka wa serikali ulitolewa mwezi wa pili wa kuainisha wakulima na mahitaji yao ili kutoa nafasi serikali kuangalia uwezo wa ruzuku haujatekelezwa kwa muda wote huo mpaka msimu wa kilimo unakaribia.
Inakuwaje watumishi wa serikali wanaojua ukweli wa uwezo wa serikali wanafanya masikhara kwa kuingiza siasa na kuonekana hata hawajui ilani inayowaongoza na kisha wanamuuliza mtu wa kilimo umeniletea tani ngapi za ruzuku na watu wangapi safari hii watanufaika na ruzuku, mbona hii ruzuku ni kidogo ... mbona haya masharti mapya siwezi kuyasimamia ...na wakulima wengi ... yaani maneno mengine bwana yanadhihirisha ufinyu wa fikira kwa viongozi.
naam viongozi wengi nawabondea na hata wataalamu ambao wanashindwa kuwashawishi wakulima kutumia vyema raslimali walizonazo nao nawabondea bure tupu.
Naam na wananchi nao Mungu wangu wamekalia utajiri lakini wabishi wanaotaka vya bure na ukisomeshwa unasema si serikali ifanye yenyewe. Yaani pori mpaka karibu na nyumba yako unataka serikali ije ipalilie miembe na mikorosho ambayo iko uani mwako?
Unapata fedha za tumbaku na kahawa halafu unaishia kununua mipombe kudhihirisha umaarufu wako lakini nyumba ya bati huna.
Udongo unafaa kupata matofali ya kuchoma unataka serikali ije ikuchomee? Yaani bure aghali.
Ukitoka Tunduru kwenda masasi Lindi dar es salaamn njia nzima unaona dhahiri kwamba siasa ni korosho. lakini hakuna palizi, watu wanachoma moto kama palizi, hii inakuwaje hasa. halafu maneno mengi hata hao viongozi wenyewe nao matatizo, wana maneno kuliko vitendo.ndipo unapogundua kwanini tunahitaji azimio la iringa,Azimio la Musoma na hata la Arusha.
haki ya nani kama ndivyo hivi basi maisha ya dauni tauni ni bonge la atifisho na itatuchukua miaka milioni moja kubadili maisha yetu.
Tunaanzia wapi kuwabadili watanzania hawa ambao hawataki kushiriki katika ujenzi wa taifa kisayansi, uchawi, woga wa kubanwa na ujanja wa watu waliosoma wanaoiba? Mafisadi wapo wa aina nyingine, mbolea ya ruzuku imebadilishiwa mbinu za kumfikia mkulima viongozi hawajaelewa somo, wengine wanasema ukweli viongozi ndio waliokuwa wanachikichia mbolea ya ruzuku... basi mambo mashala kwelikweli.
Angalia mambo ambayo yanaweza kuwa na utalii watu wamebana tu kama hawajui. Nasikia hawa wabunge wakifika hutawaona tena.
Ofisi za wabunge wa Mafinga zimefungwa siku zote anasema mfanyakazi mmoja wa hapo. Watu wa kilimo wametoa taarifa ya kwenda kuzungumzia masuala ya kilimo na wahimizaji wabunge, tazama nimekuwa na watu wa wizara njia nzima katika mikoa miwili, Madc tu labda walionekana, wabunge waliingia mitini lakini wa Mafinga tuliambiwa hawajawahi kujitokeza katika ofisi zao.
hayo mambo, halafu ikifika mwezi Novemba wanasema salfa haikuwafikia wakulima wetu, wakulima gani ambao hujafika hata kutoa salamu angalau ukahimiza wasipalilie kwa kutumia moto na waache ujinga wa pom,be na kuoa na kutaliki waangalie mambo yao ya kiuchumi kwa kuwa fedha wanazo?
Mimi nasema kama kweli tunataka mabadiliko basi huku kunahitajika mapinduzi ya fikira na waliona dhamana basi wajitahidi lakini wasiketi dar pekee.
lukwangule
COMMENTS