Ikulu yalalamikia coverage ya vyombo vya Habari Mbeya

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS UNITED REPUBLIC OF TANZANIA Telephone: 255-22-2114512, 2116898 E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.co...

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA


Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ziara ya Mheshimiwa Rais Mkoani Mbeya

Rais Jakaya Mrisho Kikwete alihitimisha ziara yake ya siku 10 yenye mafanikio makubwa katika Mkoa wa Mbeya jana mchana, Jumamosi, Oktoba 18, 2008.

Kwa bahati mbaya sana, baadhi ya vyombo vya habari nchini, na hasa magazeti, vimeandika baadhi ya matukio ya ziara hiyo, kwa namna ya wazi ya kuwapotosha wananchi kuhusu ziara hiyo ambako Rais alitembelea wilaya zote saba zenye halmashauri nane za Mkoa huo.

Taarifa hii inalenga kuweka bayana ukweli ulivyokuwa katika ziara hiyo ambako, kwa mara nyingine, Rais alipata nafasi nyingine nzuri kufanya kile ambacho hukifurahia sana kukifanya- yaani kukutana na wananchi, kusililiza kero zao, karaha zao, raha zao, mafanikio yao, na mahitaji yao ambayo wanaamini Rais wao anaweza kusaidia kuyatafutia majawabu.

(a) Rais akatisha ziara ya mkoa

Rais alipanga kukaa katika Mkoa wa Mbeya kwa siku 10. Amefanya hivyo. Hakukatisha ziara hiyo kama ilivyoandikwa katika baadhi ya magazeti. Aliingia Mbeya Oktoba 9, akaondoka Oktoba 13 jioni kwenda Tanga kuzima Mwenge, na akarejea jioni ya Oktoba 14 na kuondoka jana, Oktoba 18, jumla ya siku 10 kamili.

Ni vyema kujua kuwa kila Rais anapoweka mguu katika Mkoa wowote, iwe ni asubuhi, mchana ama jioni ni siku kamili ya kuwapo kwake katika Mkoa ama eneo hilo.

Kilichotokea ni kwamba kwa sababu ya ratiba kuwa na shughuli nyingi, ziko shughuli mbili ambazo hakuweza kuzifanya. Ameahidi atapata nafasi ya kwenda tena Mbeya kuzifanya shughuli hizo.


(b) Mkutano wa majumuisho ya ziara kwenye Uwanja wa Sokoine

Na wala Rais hakuahirisha kuhutubia wananchi wa Mbeya kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine wakati wa majumuisho yake ya Mkoa huo kama inavyodaiwa.

Rais hakupangiwa kuhutubia mkutano kwenye uwanja huo kwa sababu alikwishakuhutubia mkutano wa hadhara kwenye uwanja huo Februari 19, 2006, alipokwenda kuwashukuru wananchi wa Mkoa huo kwa kukichagua Chama cha Mapinduzi (CCM) kuendelea kuongoza nchi yetu.

Na wala Rais hafanyi majumuisho ya ziara za mikoa kwenye mikutano ya hadhara. Huifanya kazi hiyo kwa kukutana na viongozi wa kisiasa, kijamii, kiuchumi, kidini, na kiusalama wa mikoa katika mkutano wa viongozi. Ndivyo alivyofanya jana katika Ukumbi wa Mkapa mjini Mbeya.

(c) Kutotembelea Mbeya Vijiji

Kama nilivyoeleza hapo juu, Rais alitembelea wilaya zote saba za mkoa huo zenye halmashauri nane kwa sababu Mbeya yenyewe ni wilaya moja lakini ina halmashauri mbili, moja ya mjini na nyingine ya vijijini.

Wakati mwingine uelewa wa waandishi wetu unapumbazisha kabisa. Jana, kabla ya kuingia kwenye mkutano wa majumuisho, Rais alitemebelea kiwanda cha kutotoa vifaranga vya kuku katika eneo la Songwe, ujenzi wa uwanja wa kimataifa wa Songwe, pamoja na kuzindua hospitali teule ya wilaya ya Ifisi, vyote vikiwa katika eneo la Wilaya ya Mbeya lakini katika maeneo ya vijijini.



(d) JK akiri Mbeya ni pagumu

Huu pia ni upotoshaji mwingine. Kama kuna kitu Rais amekisema wakati wa majumuisho ya ziara yake jana ni kuumwagia sifa sana mkoa huo kwa jitihada za maendeleo ya wananchi – iwe katika elimu, iwe katika afya, iwe katika kilimo, iwe ni katika huduma za maji, iwe ni katika ufugaji, iwe katika umwagiliaji na maeneo mengine muhimu ya maendeleo.

Kile kinachoelezwa kuwa Mbeya ni pagumu, ni pale alipowasihi viongozi kujenga tabia na mwenendo wa uongozi wa pamoja akisizitiza kuwa viongozi hao wanajenga nyumba moja na hivyo hawana sababu ya kugombea fito kwa sababu ya tofauti zilizopo miongoni mwa baadhi ya viongozi wa Mkoa huo. Tofauti miongoni mwa viongozi wachache wa mkoa huo haziufanyi mkoa mzima wa Mbeya kuwa mgumu.

(e) Msafara wa Rais kupigwa mawe

Mwenendo mzima ambao uongozi wa Mkoa wa Mbeya unaweza kujivunia ni kujitokeza kwa wingi mno kwa mamia kwa mamia ya wananchi wa mkoa huo kila alipopita Rais ama kwenda kwa shughuli za maendeleo wakati wa ziara hiyo.

Kila sehemu, wananchi walimtaka asimame, wamwone, awasalimie. Na kama ilivyo ada, hakusita, hata sehemu moja, kufanya hivyo.

Hamu ya wananchi wa Mbeya kumwona na kumsikiliza Rais wao ndiyo ilimfanya Mhe. Rais kusema kuwa alikuwa ameondoka Mkoa wa Mbeya akiwa na kumbukumbu nzuri za wema, ukarimu na upendo wa wananchi wa Mbeya.

Ilikuwa ni hamu hiyo hiyo ambayo wananchi wa kijiji cha Kanga walikuwa nayo wakati Rais anafanya ziara ya Wilaya ya Chunya ambako alipitia na kuhutubia mikutano mikubwa ya wananchi katika maeneo ya Chunya Mjini, Makongolosi na Mkwajuni.

Kwa bahati mbaya wakati anawasili katika kijiji cha Kanga tayari ilikuwa usiku kati ya saa moja na saa mbili kwa sababu ratiba ya maeneo mengine ilikuwa imecheleshwa mno na hamu ya wananchi wa maeneo hayo kumsimamisha na kumwona Rais wao. Hivyo, msafara wake ukapita bila kusimama katika kijiji hicho.

Kile kitendo cha kiongozi wao kutosimama katika kijiji hicho ambako wananchi walikuwa wamejitokeza kwa mamia, wakasimama barabarani kwa saa nyingi wakiwa na hamu kumwona Rais wao, kikachochea na kusisimua tahayari (frustration) kwa vijana ambao wakaanza kurusha mawe kwenye baadhi ya magari yaliyokuwa kwenye msafara.

(d) Magari ya Rais

Magari ya Rais, kwa maana ya magari yote yanayotengeneza sehemu kuu ya msafara wa Rais, hayakutupiwa hata jiwe moja. Na wala Rais mwenyewe hakupata habari za tukio hilo mpaka alipokuwa amewasili Ikulu ya Mbeya.

Na alipopata habari hizo alitoa maelekezo maalum kuwa zisije zikachukuliwa hatua za kipolisi kusumbua kijiji kizima na kutaka upelelezi wa suala hilo ufanyike kwa uangalifu mkubwa bila jabza.

Magari yaliyotupiwa mawe ni yale yaliyokuwa nyuma katika sehemu ya pili ya msafara, yaani nje ya sehemu kuu ya msafara. Na mpaka Rais anaondoka Mbeya jana, ni watu watano tu walikuwa wametiwa mbaroni, tofauti na habari za kubuni za magazeti kuwa wamekamatwa watu 60.

Rais anaamini kuwa tukio hilo la kijiji cha Kanga ni tukio la uharifu. Kamwe haiwezi kutokea Rais Kikwete asisumbuliwe na tukio lolote la uharifu katika nchi yetu. Hili ni tuko lililomkera, lakini kama alivyoeleza jana kazi hiyo waachie polisi waendelee nayo.

Muhimu kusisitiza hapa ni kwamba tukio hilo siyo tukio linalowakilisha taswira ya wananchi wa Mkoa wa Mbeya ambao wameonyesha mapenzi makubwa kwa kiongozi wao mkuu. Ni makosa kwa kuuchukulia mkoa mzima wa Mbeya kama mkoa wa waharifu kwa sababu ya tendo lililotendwa na watu wachache katika kijiji kimoja tu.


Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

19 Oktoba, 2008

COMMENTS

Name

Anga,12,Arusha,27,batiki,1,Burudani,447,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,287,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,3,Habari,7054,habari dodoma,39,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,23,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,6,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,739,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,376,muziki na fasheni,20,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,9,SAYANSI ANGA,12,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,17,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Ikulu yalalamikia coverage ya vyombo vya Habari Mbeya
Ikulu yalalamikia coverage ya vyombo vya Habari Mbeya
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2008/10/ikulu-yalalamikia-coverage-ya-vyombo.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2008/10/ikulu-yalalamikia-coverage-ya-vyombo.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy