Leo ni siku mbaya kabisa katika jiji la Dar es salaam lakini kwa jiji la watu zaidi ya milioni tano pengine hawajui kumetokea nini.Leo makub...
Leo ni siku mbaya kabisa katika jiji la Dar es salaam lakini kwa jiji la watu zaidi ya milioni tano pengine hawajui kumetokea nini.Leo makubwa mawili ya asubuhi chapchap yametokea.
Moja ni wazee wastaafu ambao hawajalipwa fedha zao za kiinua mgongo sijui au malipo gani yalabi, manake hii shida wakati mwingine hata hujui malipo gani hayajalipwa manake yapo mengi, walijilaza pale Salenda bridge na kuzuia magari yote yanayotoka mjini na kuingia mjini katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi.Mishe mishe hiyo ilianza saa 12 na nusu na wakaja kuondolewa kwa nguvu na polisi majira ya saa mbili, foleni ya magari ni mpaka
mwenge utajaza.
Tukio la pili ni la Mv Kigamboni kuparamia gati.
Kutokana na Mv Kigamboni kuparamia hilo gari majira ya asubuhi, maelfu ya wakazi wa
Kigamboni, Kibada,Mji mwema, Ungindoni, Kongowe na wanaotumia kivuko wakitokea maeneo ya Mbagala Kijichi, Mbagala Kiburugwa, MbagalaKuu MbagalaRangi Tatu ambao wanashindwa
kutumia barabara ya Kilwa kutokana na kuharibika kwa kipande cha barabara ya Kilwa
eneo la msikitini hadi katika Mto kizinga kwenye deviation ya daraja walijikuta wanapambana
kuwahi kazini kwa kutumia Mv Alina.
Haikuwezekana maofisa wanaokatisha tiketi kudhibiti watu ilibidi maa MP yaani wale polisi wa jeshi na Polisi wenyewe tena wenye ngazi za maofisa kuanza pilikapilika za kudhibiti wananchi hasa baada ya kujikuta wakilazimika kusaidia wakazi walitumbukia katika maji katika
patashika za kuwania kivuko.
Pamoja na crude way waliyotumia kuzuia watu, manake kila mtu anataka kuingia katika kivuko
bila mpangilio,kuwapo kwao kulisaidia kumantain aina fulani ya oda.
Muda mrefu niliokuwa pale hakuna mtu anayeeleza kwa ufasaha nini
hasa kimesibu MV Kigamboni.Kila mmoja naasema lake na nadhidha hakuwa tayari kuongea.
Pamoja na kutotaka kuzungumza mtu wa kawaida unajiuliza hivi inakuwaje hasa kivuko
kinapoparamia gati?
Juzi niliongea na mtu mmoja kumuuliza MV Kigamboni ina matatizo gani
hasa? Hii ilitokana na ukweli kuwa nilicheza rumba nayo saa tatu usiku. Tukiwa tunatokea
mjini kabla ya kupiga gati, tukaona tunapelkwea kwanza kaskazini kisha haoo tukarejea
kusini kama tunataka kwenza Zenj baadaye Magharibi na dakika 15 baadaye wuuuhh ndio tukapiga nanga.
kama mazingira hayol ya juzi hayakupewa jibu ndio leo najikuta lazima nitumie utaratibu wa
kujitumbukiza katikati ya watu nifanikiwe kuvuka.
Mke wangu wakati tupo katikati ya mamia ya watu alisema angalia jiwe, sasa utaonaje jiwe manake kivuko kimefika na wtau wote wanajisukuma kwa mbele , nikachana kiatu manake nilipiga teke jiwe katika harakati za kujizuia nisipelekwe baharini.
Naam, hayo ni baada ya kuangalia MV Kigamboni ambayo inaonekana kama muda si muda itaishiwa principle ya kuelea ya displacement manake ina matundu fulani ambayo sidhani kama ni ya meli ya makusudi halafu ukitazama ule ulaji wa kutu ahh yaani hata kama ndio meli lazima iwe na kutu hivi upana wa chuma bado upo kweli au ndio maana kinatembea pooooolepole, kuna mtu wa marine anaweza kuelezea mambo haya sijui.
Huku mvua zimeanza barabara ya Kilwa ikiwa tete ipo siku tutasikia kitu kibaya Kigamboni,
Mungu atunusuru na tuhurumie kwa kufikiria vibaya, lakini scientifically something bad is
about to happen, watch out!!! eti hivi vivuko vina miaka mingapi?
Halafu nashindwa kuamini hivi ni kweli lakini, nadhani unafahamu nashindwa kuamini nini.Bahati mbaya sikuwa na kamera manake misele ya asubuhi wakati mwingine
hata vya kuazima mtu unasahau.
Moja ni wazee wastaafu ambao hawajalipwa fedha zao za kiinua mgongo sijui au malipo gani yalabi, manake hii shida wakati mwingine hata hujui malipo gani hayajalipwa manake yapo mengi, walijilaza pale Salenda bridge na kuzuia magari yote yanayotoka mjini na kuingia mjini katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi.Mishe mishe hiyo ilianza saa 12 na nusu na wakaja kuondolewa kwa nguvu na polisi majira ya saa mbili, foleni ya magari ni mpaka
mwenge utajaza.
Tukio la pili ni la Mv Kigamboni kuparamia gati.
Kutokana na Mv Kigamboni kuparamia hilo gari majira ya asubuhi, maelfu ya wakazi wa
Kigamboni, Kibada,Mji mwema, Ungindoni, Kongowe na wanaotumia kivuko wakitokea maeneo ya Mbagala Kijichi, Mbagala Kiburugwa, MbagalaKuu MbagalaRangi Tatu ambao wanashindwa
kutumia barabara ya Kilwa kutokana na kuharibika kwa kipande cha barabara ya Kilwa
eneo la msikitini hadi katika Mto kizinga kwenye deviation ya daraja walijikuta wanapambana
kuwahi kazini kwa kutumia Mv Alina.
Haikuwezekana maofisa wanaokatisha tiketi kudhibiti watu ilibidi maa MP yaani wale polisi wa jeshi na Polisi wenyewe tena wenye ngazi za maofisa kuanza pilikapilika za kudhibiti wananchi hasa baada ya kujikuta wakilazimika kusaidia wakazi walitumbukia katika maji katika
patashika za kuwania kivuko.
Pamoja na crude way waliyotumia kuzuia watu, manake kila mtu anataka kuingia katika kivuko
bila mpangilio,kuwapo kwao kulisaidia kumantain aina fulani ya oda.
Muda mrefu niliokuwa pale hakuna mtu anayeeleza kwa ufasaha nini
hasa kimesibu MV Kigamboni.Kila mmoja naasema lake na nadhidha hakuwa tayari kuongea.
Pamoja na kutotaka kuzungumza mtu wa kawaida unajiuliza hivi inakuwaje hasa kivuko
kinapoparamia gati?
Juzi niliongea na mtu mmoja kumuuliza MV Kigamboni ina matatizo gani
hasa? Hii ilitokana na ukweli kuwa nilicheza rumba nayo saa tatu usiku. Tukiwa tunatokea
mjini kabla ya kupiga gati, tukaona tunapelkwea kwanza kaskazini kisha haoo tukarejea
kusini kama tunataka kwenza Zenj baadaye Magharibi na dakika 15 baadaye wuuuhh ndio tukapiga nanga.
kama mazingira hayol ya juzi hayakupewa jibu ndio leo najikuta lazima nitumie utaratibu wa
kujitumbukiza katikati ya watu nifanikiwe kuvuka.
Mke wangu wakati tupo katikati ya mamia ya watu alisema angalia jiwe, sasa utaonaje jiwe manake kivuko kimefika na wtau wote wanajisukuma kwa mbele , nikachana kiatu manake nilipiga teke jiwe katika harakati za kujizuia nisipelekwe baharini.
Naam, hayo ni baada ya kuangalia MV Kigamboni ambayo inaonekana kama muda si muda itaishiwa principle ya kuelea ya displacement manake ina matundu fulani ambayo sidhani kama ni ya meli ya makusudi halafu ukitazama ule ulaji wa kutu ahh yaani hata kama ndio meli lazima iwe na kutu hivi upana wa chuma bado upo kweli au ndio maana kinatembea pooooolepole, kuna mtu wa marine anaweza kuelezea mambo haya sijui.
Huku mvua zimeanza barabara ya Kilwa ikiwa tete ipo siku tutasikia kitu kibaya Kigamboni,
Mungu atunusuru na tuhurumie kwa kufikiria vibaya, lakini scientifically something bad is
about to happen, watch out!!! eti hivi vivuko vina miaka mingapi?
Halafu nashindwa kuamini hivi ni kweli lakini, nadhani unafahamu nashindwa kuamini nini.Bahati mbaya sikuwa na kamera manake misele ya asubuhi wakati mwingine
hata vya kuazima mtu unasahau.
COMMENTS