CHAMA cha Maalbino Tanzania, jana kilitoa kilio chake cha ongezeko la mauaji ya albino nchini mbele ya Rais Jakaya Kikwete na kumuomba aunde...
CHAMA cha Maalbino Tanzania, jana kilitoa kilio chake cha ongezeko la mauaji ya albino nchini mbele ya Rais Jakaya Kikwete na kumuomba aunde tume ya kukomesha mauaji hayo ambayo yameanza kuiondolea sifa ya amani Tanzania.
Akisoma risala kwa niaba ya maalbino wenzake jana mara baada ya maandamano ya kupinga vitendo vya mauaji ya albino, Mratibu wa maandamano hayo, Josephat Torner, alisema hali ya mauaji kwa sasa ni tishio kwa jamii ya albino kiasi cha wengine kufikia hatua ya kufikiria kukimbia nchi, kukimbilia mijini na wengine kuacha shule.
“Athari za mauaji haya kwa sasa ni kubwa. Watoto wetu wengi jamii ya albino wameacha kabisa shule na wengine wamekimbia kabisa vijijini kwenda mijini, wapo wanaolindwa na polisi kama madini ya tanzanite,” alisema Torner.
Alisema jamii hiyo inazidi kudharauliwa kwani kila maalbino wanapopita imekuwa kawaida kuitwa ‘dili’ hali ambayo inazidi kuwatia hofu.
Naye Rais Kikwete alisema pamoja na juhudi zinazofanywa na serikali kupitia vyombo vyake vya dola na asasi zisizo za serikali katika kupambana na mauaji hayo, bado iko haja kwa elimu juu ya albino kusambazwa kwa jamii ili iweze kuachana na mila potofu na ushirikina. “Nimepokea mapendekezo yenu na ninawaahidi nitayapitia na kuyafanyia kazi, lakini ni muhimu wote kutambua kuwa chanzo kikubwa cha mauaji haya ni ushirikina na mila potofu walizonazo wananchi juu ya albino,” alisema Kikwete.
“Hata ukikata mikono ya albino wote nchini kama huwajibiki ipasavyo na kujituma huwezi kuwa tajiri, acheni ujinga hawa waganga wanawadanganya zindukeni sasa na mtambue kuwa wajinga ndio waliwao,” alisema.
Alisema serikali katika kutoa adhabu na kusimamia haki za wananchi wake haina ubaguzi na kwamba muuaji yeyote atakayekamatwa adhabu yake ni kifo awe ameua albino au la.
“Najua wanaharakati wanapinga adhabu hii ya kifo na wanataka ifutwe najua wananilaani lakini ndio sheria iliyopo kwa sasa,” alisema.
Alisema katika harakati za kupambana na mauaji hayo tayari watu 47 wamekamatwa wakihusishwa na mauaji ya maalbino, kati yao 17 wamekamatiwa Mwanza ambako ndiko kunakoongoza kwa mauaji hayo, sita Mara, wawili Kagera, mmoja Shinyanga na wawili Mbeya.
Naye Rais Kikwete alisema pamoja na juhudi zinazofanywa na serikali kupitia vyombo vyake vya dola na asasi zisizo za serikali katika kupambana na mauaji hayo, bado iko haja kwa elimu juu ya albino kusambazwa kwa jamii ili iweze kuachana na mila potofu na ushirikina. “Nimepokea mapendekezo yenu na ninawaahidi nitayapitia na kuyafanyia kazi, lakini ni muhimu wote kutambua kuwa chanzo kikubwa cha mauaji haya ni ushirikina na mila potofu walizonazo wananchi juu ya albino,” alisema Kikwete.
“Hata ukikata mikono ya albino wote nchini kama huwajibiki ipasavyo na kujituma huwezi kuwa tajiri, acheni ujinga hawa waganga wanawadanganya zindukeni sasa na mtambue kuwa wajinga ndio waliwao,” alisema.
Alisema serikali katika kutoa adhabu na kusimamia haki za wananchi wake haina ubaguzi na kwamba muuaji yeyote atakayekamatwa adhabu yake ni kifo awe ameua albino au la.
“Najua wanaharakati wanapinga adhabu hii ya kifo na wanataka ifutwe najua wananilaani lakini ndio sheria iliyopo kwa sasa,” alisema.
Alisema katika harakati za kupambana na mauaji hayo tayari watu 47 wamekamatwa wakihusishwa na mauaji ya maalbino, kati yao 17 wamekamatiwa Mwanza ambako ndiko kunakoongoza kwa mauaji hayo, sita Mara, wawili Kagera, mmoja Shinyanga na wawili Mbeya.
Pichani Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na baadhi ya watoto wenye ulemavu wa ngozi,Maalbino ,wakati alipopokea maandamano ya kulaanani ukatili na mauaji ya maalbino,yaliyofanyika katika viwanja vya ukumbe wa Karimjee jijini Dar es salaam jana asubuhi.
picha nyingine ni Mbunge wa kuteuliwa anayewakilisha maalbino, Al Shaimaa John Kwegyir
akiteta jambo na Rais Jakaya Kikwete wakati wa hafla ya kuzindua nakuichangia taasisi ya Goodhope Star Foundation ambayo itatetea na kutoa huduma kwa maalbino nchini,iliyofanyika
katika hoteli ya Movenpick jijini Dar es Salaam jana jioni.Katika harambee hiyo iliyoendeshwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete zaidi ya shilingi 16.3/m zilikusanywa.Rais Kikwete alitoa
jumla ya shilingi milioni mbili na nusu 2.5/m kama mchango wake kwa taasisi
hiyo.
akiteta jambo na Rais Jakaya Kikwete wakati wa hafla ya kuzindua nakuichangia taasisi ya Goodhope Star Foundation ambayo itatetea na kutoa huduma kwa maalbino nchini,iliyofanyika
katika hoteli ya Movenpick jijini Dar es Salaam jana jioni.Katika harambee hiyo iliyoendeshwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete zaidi ya shilingi 16.3/m zilikusanywa.Rais Kikwete alitoa
jumla ya shilingi milioni mbili na nusu 2.5/m kama mchango wake kwa taasisi
hiyo.
Picha ya mwisho baadhi ya wakereketwa wa kupigani haki za maalbinoo wakiandamana jijini
Dar es Salaam jana .Maandamano hayo yaliishia katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam na kupokelewa na Rais Jakaya Kikwete.Picha zote na Freddy Maro.
Dar es Salaam jana .Maandamano hayo yaliishia katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam na kupokelewa na Rais Jakaya Kikwete.Picha zote na Freddy Maro.
COMMENTS