LINI TUTAKUMBUKA KUWEKEZA KWENYE MICHEZO YA WATU WENYE WENYE ULEMAVU? Juzi ilikuwa ni siku ya walemavu duniani. labda uwe na roho ya chum...
LINI TUTAKUMBUKA KUWEKEZA KWENYE MICHEZO YA WATU WENYE WENYE ULEMAVU?
Juzi ilikuwa ni siku ya walemavu duniani. labda uwe na roho ya chuma ndio usingegusswa na yale waliyoyasema. Niliona maadhimisho ya Kibaha kupitia luninga, wakasema hawakumuona kiongozi yoyote yule! Hapa Dar nilimuona Mheshimiwa Margareth Mkanga, Mbunge anayewakilisha watu wenye ulemavu akizindua kitabu chenye Jina la WALIOSAHAULIKA. Nikakumbuka michezo, nikamkumbuka kauli ya Mheshimiwa Bendara aliyoitoa kuhusu michezo kwa wenye ulemavu, nikapata simanzi! Hii ni hoja pana sana.
Nakumbuka siku mpaka tarehe, ilikuwa ni machi, 27 mwaka 2007 wakati Tanzania ilipopokea msaada wa shilingi milioni 26 kutoka Uingereza ikiwa ni sehemu ya ufadhili wa shilingi milioni 61 zilizopangwa kwa ajili ya kuhamasisha na kuendeleza michezo kwa watu wenye ulemavu kwa watu wa njii hii kwa miaka 4 (2006 hadi 2010). Msaada huo umetolewa na Baraza la michezo la Uingereza. British Sports Council. Wenyewe hapa wala habari hatuna.
Nakumbuka pia katika kupokea msaada ule Naibu waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Joel Bendera, (MB) aliishukuru sana Uingereza na kusema kwa msaada ule ungetumika kununulia vifaa vya michezo kwa timu za wenye ulemavu. Hii ni kweli kwa sababu timu nyingi zina ukosefu wa vifaa acha za wenye ulemavu hata za hao walemavu watarajiwa nazo nyingi ziko taabani.
Tunaileta hoja ya umuhimu wa kuwasaidia wanamichezo walemavu kwa kunukuu kauli ya Mheshimiwa Bendera aliyoitoa miaka miwili iliyopita kuwa Watanzania tubadilike tabia na kusaidia au kuwekeza kwenye michezo kwa wasiojiweza. kweli ni nadra sana kupata misaada kama hii. Nakumbuka Mheshimiwa Bendera alisema, sisi (watanzania) mara nyingi kunakwepesha kuingiza fedha zetu kwenye michezo kwa wetu wasiojiweza aghalabu wenye ulemavu. (Hapa niwafundishe kiswahili, neno aghalabu maana yake ni, mara nyingi. Wasukuma wenzangu wa ushirombo wanaposema agalabu huwa wanafikiria wamesema nadra aaah nawasamehe. Kwanza treni zenyewe zimegoma).
Turudi kwenye hoja yetu pana. Pamoja na ukweli kuwa kila mwenye fedha yake anao uhuru wa kuchagua wapi asaidie. Uzoefu unaonesha kuwa wanaosaidia huwa wanatoa misaada ya masharti au kutegemea kitu fulani. Japokuwa huwa haisemwi moja kwa moja lakini ukiangalia kwa hoja pana utaiona tuu! Utaona mathalani mfadhili fulani anadhamini shughuli fulani kwa maganga feruzi ili kesho safu ya hoja irudishe fadhila. Mungu apishie mbali!! Mambo ya posho mbili. Wadhamini kama hao hawawezi kwenda kwa wenye ulemavu kwa sababu wale masikini ya Mungu hawana cha kurudisha zaidi ya dua. Wafadhadili wa aina hiyo wao na mambo ya dua ni mbali mbali. Ashakum kama nimegusa pabaya. Bora iwe hivyo kuliko mguso wa kitabu cha WALIOSAHAULIWA! Kweli tunaweza watanzania wenzangu kuwa tumefika hapa?
Niliwahi wakati fulani kuongea na Komredi Iddi Kibwana, tuliongea kwa njia ya simu. Ilikuwa mwaka 2006 akaniambia mambo mazuri kweli na mipango ambayo Paralyimpics inayo. Paralyimpics ni chama cha michezo kwa wenye ulemavu ambacho ni cha kitaifa lakini kinachofanya shughuli za michezo mpaka ngazi ya mikoa kwa watu wenye ulemavu. Wakati ule aliniambia kuwa walikuwa na mpango wa kuipeleka timu ya taifa Algeria na baadaye akaniambia jinsi michezo ya Kanda inavyoendesha na Waingereza hasa kupeleka michezo mashuleni. Nilifarijika. NILISAHAU?
Zamani pale uwanja wa Uhuru (Taifa zamani) ilikuwa kabla ya mechi ya Ligi kuu kuanza kulikuwa na siku ambapo kulikuwa na mechi za utagulizi kwa watu wenye ulemavu. Ilikuwa mechi nzuri zinazovutia. Alipoondoka kakangu Fred Macha pale, zile mechi zikafa kabisaaa na watu WAKASAHAU. Sasa hivi Fred Macha yupo Wizarani na anaendelea na juhudi za kutafuta wafadhili na misaada kwa ajili ya walemavu. Mara ya mwisho nilipokutana naye ilikuwa ni wakati alipokuwa akitafuta fedha kwa ajili ya michezo kwa watoto wenye mtindio wa ubongo. Sijui kama alifanikiwa. NILISAHAU kumuuliza.
Sitaki kusema mimi binafsi nimefanya nini kuhusu kuchangia au kushauri kuhusu michezo kwa ajili ya wenye ulemavu lakini nimeeleza baadhi ya mambo ambayo nilipaswa kuyafanya lakini NILISAHAU kuyafanya. Wenye ulemavu wanaposema WALIOSAHAULIWA tukubali udhaifu huo lakini tusiwasahau tena! Hii ni kweli.
Hujafa hujaumbika. Hata kama hali hiyo isingekuwepo, bado watu wenye ulemavu ni ndugu, jamaa na rafiki zetu. Wanahitaji faraja na kuburudika kama wanajamii wengine. Mungu asipokupa hili anakupa jingine. Kuna watu wenye ulemavu wana vipaji vikubwa tu katika michezo na wanaweza kuiletea sifa nchii hii. WALISAHAULIWE. Tumengangania kuwekeza kwenye maudhi ya timu zinazofungwa kila siku? Tubadilike. Tuwekeze kwa wale ambao tunajua wanahitaji msaada lakini pengine hawana sauti za kutufikia au hawajui hata kuandika mchanganuo wa mapendekezo na hakuna wa kuwaandikia. Wenye ulemavu wanahitaji fursa tu! Tuwasaidie kwenye michezo kwa ufadili na vifaa ili wafanye mambo.
Machi 12 hadi 21, 2010 dunia itashuhudia michezo ya paralyimpics kwa watu wenye ulemavu itakayofanyika majira ya baridi huko vancourver Kanada. Sina uhakika uhakika wa uwakilishi wa Tanzania katika michuano hiyo ikoje au utakuwaje? Au tumeshindwa kwa sababu ya kukosa mambo muhimu?
Kama mashirika na makampuni yetu yaliyopo yataamua kutoa kiasi kidogo kwa ajili ya kusaidia michezo kwa ajili ya watu wenye ulemavu, nina uhakika tutakuwa tumepiga hatua kubwa katika kuwainua wanamichezo hawa hapa Tanzania. Niliwahi kushuhudia kupia luninga jinsi watu wenye ulemavu wanavyoweza kutimua mbio kwa kasi ya ajabu hata kushinda wenye miguu na mikono miwili. Nilitamani wanariadha hao kama wangekuwa watanzania.
Michezo ni ajira. Ipo michezo mingi ambayo wenzetu wenye ulemavu wanaweza kuicheza. Kuna kurusha visahani, kurusha vitufe, mikuki, mbio, kunyanyua vitu vizito na kadhalika na kadhalika. Kama Muingereza aliyetutawala bado anakumbuka kutusaidia kwenye hili, seuze sisi ambao sasa ni taifa huru! Inawezekana hoja hii isiwe nzuri sana wala kuvutia lakini habari ndio .magangaferuzi@gmail.com
Juzi ilikuwa ni siku ya walemavu duniani. labda uwe na roho ya chuma ndio usingegusswa na yale waliyoyasema. Niliona maadhimisho ya Kibaha kupitia luninga, wakasema hawakumuona kiongozi yoyote yule! Hapa Dar nilimuona Mheshimiwa Margareth Mkanga, Mbunge anayewakilisha watu wenye ulemavu akizindua kitabu chenye Jina la WALIOSAHAULIKA. Nikakumbuka michezo, nikamkumbuka kauli ya Mheshimiwa Bendara aliyoitoa kuhusu michezo kwa wenye ulemavu, nikapata simanzi! Hii ni hoja pana sana.
Nakumbuka siku mpaka tarehe, ilikuwa ni machi, 27 mwaka 2007 wakati Tanzania ilipopokea msaada wa shilingi milioni 26 kutoka Uingereza ikiwa ni sehemu ya ufadhili wa shilingi milioni 61 zilizopangwa kwa ajili ya kuhamasisha na kuendeleza michezo kwa watu wenye ulemavu kwa watu wa njii hii kwa miaka 4 (2006 hadi 2010). Msaada huo umetolewa na Baraza la michezo la Uingereza. British Sports Council. Wenyewe hapa wala habari hatuna.
Nakumbuka pia katika kupokea msaada ule Naibu waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Joel Bendera, (MB) aliishukuru sana Uingereza na kusema kwa msaada ule ungetumika kununulia vifaa vya michezo kwa timu za wenye ulemavu. Hii ni kweli kwa sababu timu nyingi zina ukosefu wa vifaa acha za wenye ulemavu hata za hao walemavu watarajiwa nazo nyingi ziko taabani.
Tunaileta hoja ya umuhimu wa kuwasaidia wanamichezo walemavu kwa kunukuu kauli ya Mheshimiwa Bendera aliyoitoa miaka miwili iliyopita kuwa Watanzania tubadilike tabia na kusaidia au kuwekeza kwenye michezo kwa wasiojiweza. kweli ni nadra sana kupata misaada kama hii. Nakumbuka Mheshimiwa Bendera alisema, sisi (watanzania) mara nyingi kunakwepesha kuingiza fedha zetu kwenye michezo kwa wetu wasiojiweza aghalabu wenye ulemavu. (Hapa niwafundishe kiswahili, neno aghalabu maana yake ni, mara nyingi. Wasukuma wenzangu wa ushirombo wanaposema agalabu huwa wanafikiria wamesema nadra aaah nawasamehe. Kwanza treni zenyewe zimegoma).
Turudi kwenye hoja yetu pana. Pamoja na ukweli kuwa kila mwenye fedha yake anao uhuru wa kuchagua wapi asaidie. Uzoefu unaonesha kuwa wanaosaidia huwa wanatoa misaada ya masharti au kutegemea kitu fulani. Japokuwa huwa haisemwi moja kwa moja lakini ukiangalia kwa hoja pana utaiona tuu! Utaona mathalani mfadhili fulani anadhamini shughuli fulani kwa maganga feruzi ili kesho safu ya hoja irudishe fadhila. Mungu apishie mbali!! Mambo ya posho mbili. Wadhamini kama hao hawawezi kwenda kwa wenye ulemavu kwa sababu wale masikini ya Mungu hawana cha kurudisha zaidi ya dua. Wafadhadili wa aina hiyo wao na mambo ya dua ni mbali mbali. Ashakum kama nimegusa pabaya. Bora iwe hivyo kuliko mguso wa kitabu cha WALIOSAHAULIWA! Kweli tunaweza watanzania wenzangu kuwa tumefika hapa?
Niliwahi wakati fulani kuongea na Komredi Iddi Kibwana, tuliongea kwa njia ya simu. Ilikuwa mwaka 2006 akaniambia mambo mazuri kweli na mipango ambayo Paralyimpics inayo. Paralyimpics ni chama cha michezo kwa wenye ulemavu ambacho ni cha kitaifa lakini kinachofanya shughuli za michezo mpaka ngazi ya mikoa kwa watu wenye ulemavu. Wakati ule aliniambia kuwa walikuwa na mpango wa kuipeleka timu ya taifa Algeria na baadaye akaniambia jinsi michezo ya Kanda inavyoendesha na Waingereza hasa kupeleka michezo mashuleni. Nilifarijika. NILISAHAU?
Zamani pale uwanja wa Uhuru (Taifa zamani) ilikuwa kabla ya mechi ya Ligi kuu kuanza kulikuwa na siku ambapo kulikuwa na mechi za utagulizi kwa watu wenye ulemavu. Ilikuwa mechi nzuri zinazovutia. Alipoondoka kakangu Fred Macha pale, zile mechi zikafa kabisaaa na watu WAKASAHAU. Sasa hivi Fred Macha yupo Wizarani na anaendelea na juhudi za kutafuta wafadhili na misaada kwa ajili ya walemavu. Mara ya mwisho nilipokutana naye ilikuwa ni wakati alipokuwa akitafuta fedha kwa ajili ya michezo kwa watoto wenye mtindio wa ubongo. Sijui kama alifanikiwa. NILISAHAU kumuuliza.
Sitaki kusema mimi binafsi nimefanya nini kuhusu kuchangia au kushauri kuhusu michezo kwa ajili ya wenye ulemavu lakini nimeeleza baadhi ya mambo ambayo nilipaswa kuyafanya lakini NILISAHAU kuyafanya. Wenye ulemavu wanaposema WALIOSAHAULIWA tukubali udhaifu huo lakini tusiwasahau tena! Hii ni kweli.
Hujafa hujaumbika. Hata kama hali hiyo isingekuwepo, bado watu wenye ulemavu ni ndugu, jamaa na rafiki zetu. Wanahitaji faraja na kuburudika kama wanajamii wengine. Mungu asipokupa hili anakupa jingine. Kuna watu wenye ulemavu wana vipaji vikubwa tu katika michezo na wanaweza kuiletea sifa nchii hii. WALISAHAULIWE. Tumengangania kuwekeza kwenye maudhi ya timu zinazofungwa kila siku? Tubadilike. Tuwekeze kwa wale ambao tunajua wanahitaji msaada lakini pengine hawana sauti za kutufikia au hawajui hata kuandika mchanganuo wa mapendekezo na hakuna wa kuwaandikia. Wenye ulemavu wanahitaji fursa tu! Tuwasaidie kwenye michezo kwa ufadili na vifaa ili wafanye mambo.
Machi 12 hadi 21, 2010 dunia itashuhudia michezo ya paralyimpics kwa watu wenye ulemavu itakayofanyika majira ya baridi huko vancourver Kanada. Sina uhakika uhakika wa uwakilishi wa Tanzania katika michuano hiyo ikoje au utakuwaje? Au tumeshindwa kwa sababu ya kukosa mambo muhimu?
Kama mashirika na makampuni yetu yaliyopo yataamua kutoa kiasi kidogo kwa ajili ya kusaidia michezo kwa ajili ya watu wenye ulemavu, nina uhakika tutakuwa tumepiga hatua kubwa katika kuwainua wanamichezo hawa hapa Tanzania. Niliwahi kushuhudia kupia luninga jinsi watu wenye ulemavu wanavyoweza kutimua mbio kwa kasi ya ajabu hata kushinda wenye miguu na mikono miwili. Nilitamani wanariadha hao kama wangekuwa watanzania.
Michezo ni ajira. Ipo michezo mingi ambayo wenzetu wenye ulemavu wanaweza kuicheza. Kuna kurusha visahani, kurusha vitufe, mikuki, mbio, kunyanyua vitu vizito na kadhalika na kadhalika. Kama Muingereza aliyetutawala bado anakumbuka kutusaidia kwenye hili, seuze sisi ambao sasa ni taifa huru! Inawezekana hoja hii isiwe nzuri sana wala kuvutia lakini habari ndio .magangaferuzi@gmail.com
COMMENTS