NCHI ZILIZOJITOLEA KUWAHUKUMU MAHARAMIA WA KISOMALI ZISAIDIWE-UN

Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa limetakiwa kutoziachia mzigo mzito nchi ambazo zimejitolea kutekeleza kwa niaba ya jumuia ya Ki...

Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa limetakiwa kutoziachia mzigo mzito nchi ambazo zimejitolea kutekeleza kwa niaba ya jumuia ya Kimataifa, jukumu la kuwapokea, kuwahukumu na kuwafunga maharamia na majangili ya kisomali yanayoendesha uhalifu wao katika pwani ya Somalia na maeneo mengine.
Ushauri huo ambao umeungwa mkono na mataifa mengi, umetolewa na mwakilishi wa serikali ya Uingereza katika Umoja wa Mataifa, Bw. Mark Lyall Grant wakati wa mkutano wa Baraza Kuu la Usalama uliokuwa ukijadili ripoti na mapendekezo yaliyotolewa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban ki Moon, kuhusu namna gani jumuia ya kimataifa itakavyoweza kuboresha na kuongeza kasi ya kuwafikisha mbele ya mkono wa sheria maharamia wa kisomali.
“ Kazi ya kuwahukumu, kuwafunga na kuwahifadhi maharamia na majangili wa kisomali, ni kazi kubwa na nzito, ni mzigo ambao nchi hizo hazitakiwa kuubeba peke yake, Baraza Kuu la Usalama na Jumuia ya Kimtaifa tunapaswa kuwasaidia ni jukumu letu sote” akasema balozi huyo.
Akasema kuwa hadi sasa Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanayoshughulikia dawa za kurevya na uhalifu (UNODC) na lile linaloshughulika Maendeleo (UNDP), kwa pamoja yamefanya kazi nzuri ya kuzisadia nchi kadhaa zilizo katika ukanda wa bahari ya Hindi kuboresha na kuzifanyia marekebisho sheria zake ili ziweze kubebe jukumu hilo la kuwahukumu wahalifu wa kisomali, kwa kuzingatia sheria za kimataifa kuhusu haki za binadamu.
“ ili juhudi hizo ziwe endelevu nchi hizi na nyingine zinatakiwa kupewa msaada wa kutosha wa hali na mali na nchi yangu ( Uingereza ) iko tayari kusaidia wale wote waliotia sahihi mfumo wa kanuni wa Djibouti kuhusu sheria za kuwahukumu maharamia”.
Baadhi ya nchi hizo zipatato 10 ni pamoja na Kenya, Seychelles, Tanzania, Mauritius na Somali yenyewe. Ingawa Tanzania imerekebisha baadhi ya sheria zake, bado haijaanza rasmi utekelezaji wa jukumu hilo kama ilivyo kwa Kenya na Seychelles.
Karibu kila mjumbe aliyezungumza katika mkutano huo, akiwamo mwakilishi kutoka Tanzania,alitilia mkazo wa kusaidiwa kwa nchi hizo na nyingine zitakazojitokeza kwa kile walichosema athari zitokanazo na uharamia huo ni tishio kwa jumuia yote ya kimataifa.
Aidha baadhi ya wazungumzaji, walibainisha kwamba ni vema pia jumuia ya kimataifa, ikajielekeza katika kutafutia ufumbuzi vyanzo au sababu zinazowafanya baadhi ya wananchi wa Somalia kujihusisha na utekaji wa meli na ujangili wa kutumia silaha bahari.
Wanavitaja vyanzo hiyo kuwa ni hali ngumu na duni kiuchumi na kimaendeleo inayowakabilia wananchi wa Somalia, kutokuwapo kwa dola yenye mamlaka na nguvu na kutokuwapo kwa hali ya amani, usalama na utulivu.
Awali kabla ya katibu Mkuu, Ban Ki Moon kuwasilisha ripoti yake, wajumbe wa Baraza la Usalama walisimama kwa dakika moja kuwakumbuka wahanga wa mlipuko wa bomu uliotokea katika hoteli ya Muna huku Somalia na kuua watu kadhaa wakiwamo wabunge.
Akizungumzia tukio hilo, Katibu Mkuu amesema waliotekeleza uhalifu huo katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, siyo tu kwamba wamewaua raia wasio na hatia, lakini pia wamewakosea na kuwadharirisha waislam na watu wote wenye kupenda amani. Akasema Umoja wa Mataifa unalaani vikali tukio hilo kwa nvugu zake zote.
Akiyataja mapendekezo yake saba ambayo anasema yakitekelezwa yanaweza kusukuma mbele utekelezaji wa kisheria dhidi ya maharamia na majangili ya kisomali. Ban Ki Moon anaeleza kuwa katika kipindi cha miezi saba iliyopita kumekuwa na matukio 136 yanayohusishwa na vitendo vya kiharamia, huku meli zipatazo 30 zilitekwa nyara wakati meli 17 zikiwa na wafanyakazi 450 zilikuwa zimeshikiliwa na maharamia hao wakitaka wapewe mamilioni ya fedha.
Katibu Mkuu alizishukuru jitihada za kimataifa za kupambana na uharamia katika pwani ya Somalia, huku akisisitiza kwamba ingawa matukio ya kiharamia yanaelekea kama kupungua, lakini jumuia ya kimataifa inatakiwa kuongeza juhudi za kupambana na wahalifu hao.
Mapendekezo saba ambayo Ban ki Moon aliyawasilisha mbele ya baraza Kuu ni : baadhi ni kuundwa kwa mahakama ya Somalia, lakini itakayokuwa ikiendesha shughuli zake katika nchi ya tatu itakayokubali kuwa mwenyeji wa mahakama hiyo. kuwapo kwa chemba maalum katika mfumo wa sheria za nchi moja au nchi kadhaa za ukanda wa pwani ya Somalia na pembe ya afrika kwa kushirikiana au kutoshirikiana na Umoja wa mataifa na , kuundwa kwa mahakama ya kikanda kwa kuzingatia makubaliano ya nchi kadhaa huku kukiwa na ushiriki wa Umoja wa mataifa.
Mapendekezo mengine ni, kuundwa kwa mahakama ya Kimataifa kwa kuzingatia makubaliano kati ya nchi itakayojitolea kuwa mwenyeji wa mahakama hiyo kwa kushirikiana na Umoja wa mataifa, na kuwapo kwa mahakama ya kimataifa itakayoundwa na Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kuzingatia ibara ya VII ya katiba ya Umoja wa Mataifa.
Pamoja na mapendekezo hayo, ripoti hiyo pia inajadili faida na hasara zitakazotokana na utekelezaji wa mapendekezo hayo ambayo karibu nchi zote ziliyaunga mkono.
SOURCE:UBALOZI WA TANZANIA NEW YORK

COMMENTS

Name

Anga,12,Arusha,27,batiki,1,Burudani,447,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,287,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,3,Habari,7058,habari dodoma,39,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,23,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,6,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,739,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,376,muziki na fasheni,20,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,9,SAYANSI ANGA,12,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,17,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: NCHI ZILIZOJITOLEA KUWAHUKUMU MAHARAMIA WA KISOMALI ZISAIDIWE-UN
NCHI ZILIZOJITOLEA KUWAHUKUMU MAHARAMIA WA KISOMALI ZISAIDIWE-UN
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2010/08/nchi-zilizojitolea-kuwahukumu-maharamia.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2010/08/nchi-zilizojitolea-kuwahukumu-maharamia.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy