KATIKA hali ambayo haikutarajiwa na wachambuzi wa mambo leo katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa waziri mkuu suala la madaktari ...
KATIKA hali ambayo haikutarajiwa na wachambuzi wa mambo leo katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa waziri mkuu suala la madaktari na posho za wabunge zinazowaumiza vichwa hayakupata nafasi ya kuulizwa.
Waandishi wa habari waliokuwapo katika chumba cha kufuatilia mijadala ya bunge walijikuta wakisemezana imekuwaje baada ya maswali manane kwa waziri mkuu yote kukosa swali kuhusu tatizo la madaktari na posho.
Huenda tatizo la madaktari kwa kuwa linangoja tamko la mawaziri husika, lakini suala la posho bado lingeweza kuulizwa kwa kuwa kuna kutupiana mpira kati ya Ikulu na ofisi ya Spika juu ya kuridhiwa kwa posho hizo.
Maswali aliyoulizwa waziri Mkuu jana mengi hayakuwa ya kisera na kumfanya Spika wa Bunge Anne Makinda kuwakumbusha wabunge kwamba Waziri mkuu anahitaji maswali ya kisera na wala si ya kiutendaji , mambo ambayo yanatakiwa kujibiwa na mawaziri.
Lakini hata kabla spika hajasema hayo Waziri Mkuu Mizengo Pinda naye alisema kiungwana kwamba maswali ambayo ni specific (mahususi) hawezi kuyajibu kwa kuwa yeye atakuwa anajua masuala ya kijumla ambayo yanagusa sera.
Katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo wabunge wengi walizungumzia majimbo yao na matatizo binafsi kuliko masuala ambayo ni ya kitaifa na yenye mwelekeo wa kuchanganua sera zilizopo.
Hata hivyo Waziri Mkuu ambaye alijibu maswali kutoka kwa wabunge wanane kati ya 26 walioomba kupewa nafasi kwa Spika, aligusia tatizo la kuyumba kwa uchumi ambako alieleza ni kwa dunia nzima.
Akijibu swali la mbunge Diana Chilolo (Viti maalum-CCM) kuhusu mkakati wa serikali wa kukabiliana na tatizo la kuharibika kwa uchumi wa nchi Waziri Mkuu alisema taifa lipo katika msukosuko mkubwa unaotokana na mfumuko wa bei unaosababishwa na bei kubwa ya chakula na mafuta.
Aliwatafadhalisha watanzania kutambua kwamba tatizo la kuyumba kwa uchumi si la watanzania pekee bali ni la kidunia ila kinachostahili ni kutekeleza mipango itakayowezesha kuongeza tija na kuboresha uchumi.
Pia alizungumzia uboreshaji wa kilimo ambapo alisema serikali inajitahidi kilimo kuwa chepesi na chenye manufaa ili vijana wasikimbilie mijini na pia kutanua sekta nyingine kwa kuwa na mazao ya kusindika na kuyaongezea thamani.
Alisema ni kweli kuwa ni wajibu wa serikali kuweka mazingira mazuri ya uzalishaji mali lakini pia ni wajibu wa wananchi kuwajibika.
“Serikali imejitahidi kusaidia … tumeshusha bei ya matrekta kutoka India kati ya asilimia 15-30 ili kukiinua kilimo” alisema waziri Mkuu.
Wakati huo huo Waziri Mkuu amesema kwamba mradi wa ujenzi wa mji wa kisasa wa Kigamboni na Kurasini unachelewa kutokana na haja ya wananchi kushirikishwa.
Akijibu swali la Mriam Kisangi (viti maalumu –CCM) aliyetaka kujua miradi hiyo inaanza lini kwa kuwa inawachelewesha wananchi kupata mikopo katika benki kwa kukosa hati, alisema kamati imeundwa ili kuzungukia wananchi.
Akizungumzia suala la fidia Mabwepande, Waziri Mkuu alisema kwamba serikali inajipanga ili wale wanaostahili kulipwa waweze kulipwa fidia zao.
Aidha alisema kwamba mpaka sasa viwanja 300 vipo tayari kwa ajili ya waathirika wa mafuriko na kwamba watu waliokusudiwa ni kaya 500.
Alisema hata hivyo wanachangamoto kubwa ya kuwapatia viwanja wapangaji kama Rais Jakaya Kikwete alivyoelekeza.
Taarifa ya mambwepande ilitokana na swali la mbunge wa Kawe Halima Mdee ( Chadema).
Akizungumzia masuala ya magari ya serikali kuwekewa bima, Waziri Mkuu alisema kwamba kupanga ni kuchagua na kusema zipo sababu kwanini magari yote hayo hayawezi kuwekewa bima. Swali la Bima liliulizwa na mbunge wa Ole, Rajab Mbarouk Mohamed (CUF).
Swali jingine ambalo liliulizwa lilikuwa la wastaafu ambalo nalo lilikuwa mahusisi na Waziri Mkuu kumtaka mbunge awasiliane na waziri wa mambo ya ndani.
Wabunge wengine ambao waliuliza maswali mahsusi ni mbunge wa Vunjo Agustino Mrema (TLP) aliyeulizia soko la Himo,Profesa Kulikoyela Kahigi (Chadema) aliyeuliuzia wastaafu jimboni kwake, mbunge wa Kasulu Mjini Moses Machali (NCCR-Mageuzi) na mbunge wa Kilwa kaskazini, Muntazi Ali Mangungu (CCM).
Waandishi wa habari waliokuwapo katika chumba cha kufuatilia mijadala ya bunge walijikuta wakisemezana imekuwaje baada ya maswali manane kwa waziri mkuu yote kukosa swali kuhusu tatizo la madaktari na posho.
Huenda tatizo la madaktari kwa kuwa linangoja tamko la mawaziri husika, lakini suala la posho bado lingeweza kuulizwa kwa kuwa kuna kutupiana mpira kati ya Ikulu na ofisi ya Spika juu ya kuridhiwa kwa posho hizo.
Maswali aliyoulizwa waziri Mkuu jana mengi hayakuwa ya kisera na kumfanya Spika wa Bunge Anne Makinda kuwakumbusha wabunge kwamba Waziri mkuu anahitaji maswali ya kisera na wala si ya kiutendaji , mambo ambayo yanatakiwa kujibiwa na mawaziri.
Lakini hata kabla spika hajasema hayo Waziri Mkuu Mizengo Pinda naye alisema kiungwana kwamba maswali ambayo ni specific (mahususi) hawezi kuyajibu kwa kuwa yeye atakuwa anajua masuala ya kijumla ambayo yanagusa sera.
Katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo wabunge wengi walizungumzia majimbo yao na matatizo binafsi kuliko masuala ambayo ni ya kitaifa na yenye mwelekeo wa kuchanganua sera zilizopo.
Hata hivyo Waziri Mkuu ambaye alijibu maswali kutoka kwa wabunge wanane kati ya 26 walioomba kupewa nafasi kwa Spika, aligusia tatizo la kuyumba kwa uchumi ambako alieleza ni kwa dunia nzima.
Akijibu swali la mbunge Diana Chilolo (Viti maalum-CCM) kuhusu mkakati wa serikali wa kukabiliana na tatizo la kuharibika kwa uchumi wa nchi Waziri Mkuu alisema taifa lipo katika msukosuko mkubwa unaotokana na mfumuko wa bei unaosababishwa na bei kubwa ya chakula na mafuta.
Aliwatafadhalisha watanzania kutambua kwamba tatizo la kuyumba kwa uchumi si la watanzania pekee bali ni la kidunia ila kinachostahili ni kutekeleza mipango itakayowezesha kuongeza tija na kuboresha uchumi.
Pia alizungumzia uboreshaji wa kilimo ambapo alisema serikali inajitahidi kilimo kuwa chepesi na chenye manufaa ili vijana wasikimbilie mijini na pia kutanua sekta nyingine kwa kuwa na mazao ya kusindika na kuyaongezea thamani.
Alisema ni kweli kuwa ni wajibu wa serikali kuweka mazingira mazuri ya uzalishaji mali lakini pia ni wajibu wa wananchi kuwajibika.
“Serikali imejitahidi kusaidia … tumeshusha bei ya matrekta kutoka India kati ya asilimia 15-30 ili kukiinua kilimo” alisema waziri Mkuu.
Wakati huo huo Waziri Mkuu amesema kwamba mradi wa ujenzi wa mji wa kisasa wa Kigamboni na Kurasini unachelewa kutokana na haja ya wananchi kushirikishwa.
Akijibu swali la Mriam Kisangi (viti maalumu –CCM) aliyetaka kujua miradi hiyo inaanza lini kwa kuwa inawachelewesha wananchi kupata mikopo katika benki kwa kukosa hati, alisema kamati imeundwa ili kuzungukia wananchi.
Akizungumzia suala la fidia Mabwepande, Waziri Mkuu alisema kwamba serikali inajipanga ili wale wanaostahili kulipwa waweze kulipwa fidia zao.
Aidha alisema kwamba mpaka sasa viwanja 300 vipo tayari kwa ajili ya waathirika wa mafuriko na kwamba watu waliokusudiwa ni kaya 500.
Alisema hata hivyo wanachangamoto kubwa ya kuwapatia viwanja wapangaji kama Rais Jakaya Kikwete alivyoelekeza.
Taarifa ya mambwepande ilitokana na swali la mbunge wa Kawe Halima Mdee ( Chadema).
Akizungumzia masuala ya magari ya serikali kuwekewa bima, Waziri Mkuu alisema kwamba kupanga ni kuchagua na kusema zipo sababu kwanini magari yote hayo hayawezi kuwekewa bima. Swali la Bima liliulizwa na mbunge wa Ole, Rajab Mbarouk Mohamed (CUF).
Swali jingine ambalo liliulizwa lilikuwa la wastaafu ambalo nalo lilikuwa mahusisi na Waziri Mkuu kumtaka mbunge awasiliane na waziri wa mambo ya ndani.
Wabunge wengine ambao waliuliza maswali mahsusi ni mbunge wa Vunjo Agustino Mrema (TLP) aliyeulizia soko la Himo,Profesa Kulikoyela Kahigi (Chadema) aliyeuliuzia wastaafu jimboni kwake, mbunge wa Kasulu Mjini Moses Machali (NCCR-Mageuzi) na mbunge wa Kilwa kaskazini, Muntazi Ali Mangungu (CCM).
COMMENTS