KITUO CHA MAENDELEO CHA KANDA YA KUSINI MASHARIKI MWA TANZANIA CHAFUNGULIWA

TANZANIA SOCIAL SUPPORT FOUNDATION OFISI YA MKURUGENZI MKUU TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI YAH: KUFUNGULIWA RASMI KWA KITUO CHA...



TANZANIA SOCIAL SUPPORT FOUNDATION OFISI YA MKURUGENZI MKUU

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH: KUFUNGULIWA RASMI KWA KITUO CHA MAENDELEO CHA KANDA YA KUSINI MASHARIKI MWA TANZANIA.
1.0       UTANGULIZI.
Ndugu Wanahabari, kwa niaba ya bodi ya Utawala wa Shirika la Kusaidia Jamii Tanzania ambalo kwa kiingereza linaitwa “Tanzania Social Support Foundation” ninayo heshima kubwa mbele yenu kwanza kumshukuru Mwenyenzi Mungu aliyetujaalia uzima na nguvu za kuweza kufika hapa tulipo, pamoja na afya njema, vitu ambavyo vimetufanya leo hii tuweze kutekeleza majukumu yetu kwa ufanisi, kila mmoja kwa nafasi yake katika jamii. Pia Shirika linawashukuru sana kwa kuwa mmekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa mnaihabarisha jamii na hivyo kuutekeleza wajibu wenu vyema na kwa ufanisi Mkubwa.
2.0       KITUO CHA MAENDELEO CHA KANDA YA KUSINI MASHARIKI MWA TANZANIA.
Kituo Cha Maendeleo Cha Kanda ya Kusini Mashariki Mwa Tanzania (Centre for Development in South – Eastern Tanzania [CDSET]) ni Taasisi ya Shirika la Kusaidia Jamii Tanzania ambayo imeanzishwa kwa ajili ya kuwaandaa wananchi wa Mkoa wa Mtwara, Lindi, na Ruvuma ili waweze kuzitumia vyema fursa za kiuchumi ambazo zinapatikana katika mikoa ya Lindi, Mtwara, na Ruvuma.
            Mtakumbuka kwamba mnamo Desemba 2012 mpaka sasa kumekuwepo na sintofahamu mbalimbali kati ya Wananchi wa Kanda ya Kusini Mashariki mwa Tanzania (hasa mikoa ya Lindi na Mtwara) na Serikali kuhusiana na namna ambavyo wananchi watanufaika na rasilimali za gesi na mafuta ambazo zilivumbuliwa hivi karibuni. Serikali kwa upande wake imekuwa  ikitoa nyaraka mbalimbali za kuonyesha kuwa ni kwa namna gani wananchi wa Mikoa ya Lindi na Mtwara watavyonufaika na rasilimali zilizovumbuliwa hivi karibuni lakini kwa bahati mbaya sana hakuna hatua muhimu na za haraka ambazo zimechukuliwa ili kuwawezesha wananchi katika kujiandaa vyema ili hatimaye waweze kunufaika na hizo rasilimali.
            Ni kwa sababu hiyo sasa Shirika la Kusaidia Jamii Tanzania (Tanzania Social Support Foundation) limefungua Kituo Cha Maendeleo Cha Kanda ya Kusini Mashariki mwa Tanzania ambacho makao yake makuu yapo katika Ofisi za makao makuu ya Shirika la Kusaidia Jamii Tanzania (Tanzania Social Support Foundation) ambapo ofisi za Shirika zipo katika Ploti Na. 164 Block “H”, Barabara ya TANU, Karibu na Ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mtaa wa Rahaleo Chini, Kata ya Rahaleo, Manispaa ya Mtwara Mikindani, Mkoani Mtwara.
            Kituo Cha Maendeleo Cha Kanda ya Kusini Mashariki Mwa Tanzania kitahudumia mikoa ya Lindi, Mtwara, na Ruvuma na kitakuwa na Majukumu yafuatayo;-
(i)            Kuwawezesha wananchi kwa kuwapa elimu itakayowajengea uwezo wa kutambua, kubaini, kuanzisha na kuendeleza fursa za uzalishaji ili kuweza kujipatia kipato na hivyo kujikwamua kiuchumi. Katika hilo ni vyema wananchi wakafahamu kwamba, ujasiriamali siyo kufungua biashara ndogondogo tu bali ujasirimali ni zaidi ya kufanya biashara. Katika jambo hili, Kituo kitawafundisha wananchi  katika vikundi vidogo vidogo kuhusiana na namna ya kupanga mipango pamoja na kuendesha shughuli mbalimbali za uzalishaji.
(ii)          Kituo Kitatoa elimu kwa wananchi kuhusiana na namna ya kuanzisha vikundi vidogo vidogo vya ujasiriamali, kuboresha vikundi vilivyopo kama vile VICOBA, SACCOS, na asasi za kiraia sanjari na kutoa elimu ya kutatua migogoro katika vikundi na asasi za kiraia ili ziweze kuwa endelevu. Mtakuwa mshahidi wa TSSF kwamba, vikundi vingi vya uzalishaji mali na kukuza kipato ni vya akina mama na kwamba, vikundi hivi vimekuwa vikisambaratika kwa sababu ya migogoro na kutokuelewa hatua stahiki za kuchukuliwa pindi sintofahamu zinapokuwa zimejitokeza katika vikundi husika. Hii ndiyo sababu kubwa inayofanya Kituo hiki kijishughulishe na utoaji wa mafunzo kama ilivyoelezwa hapo juu.
(iii)         Kituo kimeandaa mpango maalum wa kurasimisha asasi za kiraia, mtu mmoja mmoja ambaye yupo katika sekta isiyo rasmi, na vikundi vidogo vidogo vya uzalishaji mali au ujasiriamali ambavyo vipo katika sekta isiyo rasmi, ili kwamba makundi yaliyotajwa hapo juu yaweze kutambulika kisheria na kupata fursa ambazo zitawawezesha kujikwamua kiuchumi. Fursa hizi ni kama vile mikopo, na huduma nyingine za kifedha ambazo zitachangia kuongezeka kwa kiwango cha uwekezaji katika shughuli za kiuchumi na hivyo kuongeza kipato cha mwanachi mmoja mmoja na jamii nzima kwa ujumla.
(iv)          Katika hoja nzima ya kupambana na changamoto ya upatikanaji wa ajira kwa vijana, Kituo kimejipanga kutoa elimu kwa vijana kuhusiana na stadi za maisha, na pia kituo kimeanzisha kanzi data (Database) maalum ambayo inarekodi taarifa za msingi za waombaji wa ajira na hivyo kuwaunganisha na waajiri ambao wanakuwa wametangaza nafasi za kazi pale inapotokea. Zaidi ya hayo, Kituo kinatoa mafunzo rasmi ya elimu ya kujitegemea jambo litakalosababisha vijana kubuni na kuanzisha shughuli mbalimbali ambazo zitawafanya wajiajiri wenyewe na hivyo kutengeneza ajira kwa wao wenyewe na vijana wenzao kuliko kukaa na kuendelea kusubiri kuajiriwa kama ilivyozoeleka hivi sasa.
(v)           Kituo kinatoa huduma za ushauri katika ufanyaji na uandishi wa tafiti mbalimbali, ushauri katika uandishi wa miradi ya maendeleo ya kijamii inayoleta tija kwa wananchi, ushauri katika uandishi wa wazo la kuanzisha biashara, ushauri katika kuanzisha taasisi mbalimbali kama vile, Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali, Vyama vya Kijamii, SACCOS, VICOBA, Makampuni na vikundi vidogo vidogo vya kijasiriamali, kwa mtu mmoja mmoja au kikundi cha watu wanaotaka kuanzisha moja ya taasisi tajwa hapo juu.
(vi)          Elimu ya Uraia na kujitambua ni sehemu ya mafunzo yanayotolewa na Kituo Cha Maendeleo Cha Kanda ya Kusini Mashariki Mwa Tanzania kwa Wananchi.
(vii)        Katika kuandaa kizazi cha sasa na vijavyo, Kituo kimeanza kutekeleza mkakati wa kuboresha elimu katika shule za msingi na sekondari zilizopo katika kanda ya kusini mashariki mwa Tanzania ili kuhakikisha kwamba, elimu inayotolewa inakuwa na tija kwa wanafunzi pindi wanapohitimu masomo. Mtakumbuka kwamba, elimu siyo kuongeza ufaulu kwamba, mwanafunzi huyu alikuwa na alama “F” katika matokeo ya mitihani yake ya wakati uliopita sasa ana alama “A”. Bali ni kumfanya mwanafunzi aweze kuyatawala mazingira yake baada ya kuhitimu masomo yake na siyo kutawaliwa na mazingira. Hilo ndilo jambo kubwa linaloshughulisha kituo chetu katika muktadha wa elimu.
(viii)       Hakuna maendeleo yanayopatikana bila ya kufanya tafiti zenye tija, zinazoandaliwa katika mrengo wa kati, na zenye manufaa kwa walengwa. Kwa kulitambua hilo, Shirika la TSSF linajishughulisha katika kufanya tafiti ambapo tunda la kwanza la kufanya tafiti ambalo limekuwa ni faida kwa wananchi ni kuanzishwa kwa kituo hiki baada ya kubaini changamoto za kijami zinazoikabili mikoa ya kanda ya kusini mashariki mwa Tanzania kwa sasa.
3.0       Wito wa Shirika la TSSF na Kituo Cha CDSET Kwa Wananchi.
Tunawaomba wananchi wajitokeze kwa wingi ili wanufaike na huduma hizi ambazo zimeletwa karibu na wao na ikumbukwe kwamba, si busara kulalamika na kukumbatia matatizo wakati njia ya kuweza kupata suluhu ya matatizo ipo. Pia haiwezekani kufanikiwa katika maisha bila ya kujishughulisha. Hivyo basi naomba kwa umoja wetu kama jamii tuwajibike na baada ya kutimiza wajibu wetu, tutaweza kutembea kifua mbele katika kuidai haki yetu.
            Nawatakia siku njema na utendaji mwema na asanteni kwa kunisikiliza.

Wenu

Ndg. Donati Salla
Mkurugenzi Mkuu wa TSSF.
 


COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4817,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: KITUO CHA MAENDELEO CHA KANDA YA KUSINI MASHARIKI MWA TANZANIA CHAFUNGULIWA
KITUO CHA MAENDELEO CHA KANDA YA KUSINI MASHARIKI MWA TANZANIA CHAFUNGULIWA
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2014/10/kituo-cha-maendeleo-cha-kanda-ya-kusini.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2014/10/kituo-cha-maendeleo-cha-kanda-ya-kusini.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy